Kuhusika kwa Jeshi la Polisi vifo vya vijana wawili, tunataka uchunguzi huru

Kuhusika kwa Jeshi la Polisi vifo vya vijana wawili, tunataka uchunguzi huru

Hao vijana wanafichwa na wazazi wao coz huwa wanagawana na wazazi wao vitu wanavyoiba, but kiukweli wamesababishia watu wasokuwa na hatia maumivu makali sana.
 
Hamumfahamu vyema Camillius Wambura.

Sisemi kaua bali nasema hamumjui vyema walah

Mwenye akili na afahamu
Kiboko ya wanaojiita majambazi....yeye ni kuua tu bdio style yake.....Saa 100 alimuulizia yuko wapi yule kiboko ya majambazi wakamjibu yuko Dodoma.......
 
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya maafisa wa Jeshi la Polisi kuhusishwa na vifo vya vijana wawili ambao ni Bakari Ismail (21) na Shomari Kucheuka (22) waliokuwa wakiishi Vingunguti Dar es Salaam. Taarifa zinaeleza kuwa vijana hao walikamatwa kwa nguvu na Askari Polisi wakiwa nyumbani kwao mnamo Desemba 27, 2023.

Jambo la kusikitisha baada ya kukamatwa haikujulikana walipelekwa wapi kwa kuwa jitihada za ndugu na jamaa kufuatilia kwenye vituo vya Polisi takribani siku sita hazikufanikiwa kuwapata vijana hao. Vilevile, hawakuweza kuwapata kwenye hospitali hadi ilipofika tarehe 28 Desemba walipo taarifiwa kuwa miili ya vijana hao ipo Hospitali ya Amana iliyofikishwa na askari Polisi.

ACT Wazalendo tunaona kwamba zipo hoja zinazoonyesha kuhusika kwa Jeshi la Polisi kwenye mauaji haya. Mosi, kutajwa kwa Askari Polisi wakati wa ukamataji na baadaye tena kwenye kufikishwa miili ya vijana hao katika Hospitali ya Amana.

Pili, sio kawaida ya Jeshi la Polisi kuokota miili ya watu halafu ikaipeleka hospitali wakati tayari kuna taarifa ya watu walioulizia kuhusu ndugu zao. Tatu, hakuna taarifa za Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi ili kubaini nani aliyehusika na mauaji ya miili waliyoikota.

Kutokana na kujirudia kwa matukio na tuhuma za askari polisi kuhusishwa kwenye mauaji ni wazi taswira ya Jeshi la Polisi inaendelea kuchafuka na kushusha imani ya wananchi.

ACT Wazalendo tunarudia wito kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liunde Tume ya kuchunguza mauaji yote ya raia ili kujiridhisha na hatua zilizofanywa na Jeshi la Polisi.

Pili, kwa hatua za awali tunamtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuchukua hatua ya kumfuatilia wanaotajwa kuhusika kwenye tukio hili la vijana.

Mwisho, tunaendelea kusisitiza mageuzi ya Jeshi la Polisi kutoka kuwa chombo cha mabavu na kuwa huduma ili liwe linatekeleza wajibu na majukumu yake kwa weledi na kufuata sheria.
Imetolewa na;

Wakili Bonifasia Aidan Mapunda
Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani ya nchini
31 Desemba, 2023
Rudia unacho type kabla ya kubandika.

Wamekamatwa tarehe 27 Desemba halafu wametafutwa kwa siku 6 wakakutwa hospitali ya Amana tarehe 28 Desemba?
 
Kiboko ya wanaojiita majambazi....yeye ni kuua tu bdio style yake.....Saa 100 alimuulizia yuko wapi yule kiboko ya majambazi wakamjibu yuko Dodoma.......
Siyo kila anayemuua ni jambazi
 
Mdogo wangu Shomari Salehe Kacheuka mtoto wa Salehe Shomari Kacheuka ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya GS Group Limited inayoingiza na kuuza pikipiki aina ya Haujue eneo lake la kazi likiwa mtaa Nyamwezi na Msimbazi ameuawa na polisi siku ya Jumatano, Desemba 27. Shomari nilikuwa naye katika eneo la kazi mpaka ofisi ilipofungwa mida ya saa kumi na mbili kama na robo hivi. Aliondoka Kariakoo majira ya hayo kuelekea nyumbani kwake Vingunguti Kiembembuzi. Muda wa kama dakika 40 baadae kaka yake anaietwa Omary Salehe Kacheuka alipiga simu kusema Shomari anashambuliwa na Polisi. Kwa maelezo ni kwamba Shomari alipaki pikipiki akaingia ndani na kutoka muda huohuo. Alipotoka akakutana na watu waliojitambulisha kama askari waliotaka kuondoka naye. Alipowauliza kulikoni wakamtolea bastola. Punde kuna kijana wa Car wash ya jirani anaejishughulisha na kuosha pikipiki alikuwa akipita. Akahoji kulikoni wakampiga risasi ya mguu. Katika hali ya sintofahamu na taharuki wakampiga risasi ya goti Shomari. Wakawaburuza kutoka nyumbani mpaka barabarani. Barabarani wakaendelea kumshambulia Shomari na kumfyatulia risasi kadhaa. Wakamburuta mpaka kwenye defender na yule waliempiga risasi ya mguu wakampakiza kwenye IST na kutokomea kusikojulikana.

Kama familia tulianza kumtafuta kuanzia majira hayo. Tunaruhusu kufuatilia mawasiliano yetu yote kuanzia saa moja ya siku mpaka sasa. Tulifika vituo vyote vya polisi bila mafanikio. Tulimpigia mkuu wa kituo Buguruni kwenye namba yake hii 0787668306 tuliyopatiwa na msamalia mida ya saa mbili usiku. Akasema bado hajapata taarifa ila ataifanyia kazi. Tuluripoti vituo kadhaa vya polisi ikiwemo Tabata, Vingunguti, Stakishari, Msimbazi, Central, lakini tuliambiwa hata taarifa hizo hazijawafikia. Tulifika Buguruni polisi usiku ule na alfajiri hakukuwa na taarifa. Tukaenda Selander Bridge tulipotoka Buguruni na kufuatilia Muhimbili bila mafanikio. Tukipotoka Muhimbili tukapita Msimbazi na kwenda Amana hospital. Amana hakukuwa na rekodi za kupata majeruhi wala miili ya watu wa tukio aina hiyo. Hivyo kama familia tukaamua kurudi Buguruni kufungua jalada. Buguruni tukakabidhiwa Askari aliejulikana kwa jina la Sylvanus baada ya kuzunguushwa mara kadhaa ili atufungulie jalada. Namba ya Afande Sylvanus ni hii 0755329211. Afande Sylvanus akatuambia kwasababu tukio limetokea majira ya saa moja kasoro usiku inatubidi tuvute subira yafike masaa 24 ndio tufungue jalada. Mimi nikamwambia hatukuja kufungua jalada la kupotelewa na ndugu. Tumekuja kufungua jalada la ndugu kutekwa na wasiojulikana. Tena wakiwa wamepigwa risasi miguuni. Na pamoja na jitihada zetu kama familia kufika sehemu zote ambazo tungesaidia mmeshindwa kutusaidia kutuma hata askari kwenda eneo la tukio. Lakini akiongozwa na askari mwenzake mwenye kama suzua kadhaa ukubwa wa zabibu na ndimu changa kichwani walitugomea kabisa kutufungulia jalada. Ikabidi tutoke nje tuanze kujadiliana. Pembeni yetu tukiwa na askari wawili wanaosikiliza maongezi yetu ambapo tukisema maadamu Polisi wameshindwa kutusaidia basi twende kwa Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama wa Mkoa ambaye pia ni mkuu wa mkoa. Tukaachana ambapo wengine wakarudi kwanza nyumbani. Tunafika nyumbani tunakutana na Mwenyekiti wa serikali ya mtaa nadhani ambaye anasema amepigiwa simu kuwa vijana wale wawili wapo Amana hospital hali zao ni mbaya. Baadhi ya wana familia wakarudi Amana ambako bado wakasema hakuna majeruhi wa risali wala maiti zilizoingia. Mwishoni tukajaribu kwenda moja kwa moja Mortuary kuulizia. Ndio mtu wa Mortuary akasema leo asubuhi kuna miili miwili ililetwa na askari imeokotwa maeneo ya Vingunguti labda mkaangalie. Kuangalia ndio tukatambua kuwa ni wale vijana wetu tuliokesha tukiwatafuta bila mafanikio zikiwa na majaraha mengi ya risasi.

Sisi kama familia tuliamini labda kijana alipita eneo lisilo sahihi katika muda huo na kupelekea kufananishwa na mtu fulani. Tuliamua kumshitakia Mungu tukampumzisha Marehemu ili maisha yasonge. Mengine tumemwachia Mungu. Lakini kilichotusikitisha ni ripoti iliyotolewa na Kamanda Murilo kwa kuwabatiza uhalifu na kuwahusisha na tukio la panya road lililotokea majira ya saa mbili huko Vingunguti huku likiwahusisha vijana hao. Bila haya wala hofu ya Mungu akawabatiza na majina mabaya. Kama familia tunatoa ruhusa kwa mamlaka kufuatilia mawasiliano yetu wote wana familia kuanzia saa moja usiku ili kuonesha ni namna gani jeshi letu lilivyowafanyia udhalimu vijana hawa. Pia tunaomba serikali ifuatilie mtaani alipoishi Shomari nyumba kwa nyumba kujua alikuwa na tabia zipi na kama ashawahi hata kulala ndani kwa kukaa tu kijiweni ama kuzurula. NB. Hakuna jirani anaemjua Marehemu kwa jina la Shomari. Toka mchanga anajulikana kwa jina moja tu la Babuu. Shomari ni jina analotumia kwenye documents tu na shuleni.
Naomba taarifa hii imfikie Mheshimiwa Raisi huenda akatia mkono wake na ukweli ukabainika na ikawa faraja kwa familia.
Natanguliza shukran.
Mungu asimame na wote wenye kuisimamia na kuiishi Haki
🙏🙏🙏🙏
 
Polisi ni panya road waliopewa silaha,magari na sare
 
Hilo ni muhimu maana tumeshaona polisi wakiuwa watu bila hatia.

polisi haruhusiwi kuua mtu yeyote kwa hatia/bila hatia.

kinachofanyika huwa wanapunguza matatizo mtaani,hasa yale yaliyowashinda wazazi,ndugu na jamaa.
 
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya maafisa wa Jeshi la Polisi kuhusishwa na vifo vya vijana wawili ambao ni Bakari Ismail (21) na Shomari Kucheuka (22) waliokuwa wakiishi Vingunguti Dar es Salaam. Taarifa zinaeleza kuwa vijana hao walikamatwa kwa nguvu na Askari Polisi wakiwa nyumbani kwao mnamo Desemba 27, 2023.

Jambo la kusikitisha baada ya kukamatwa haikujulikana walipelekwa wapi kwa kuwa jitihada za ndugu na jamaa kufuatilia kwenye vituo vya Polisi takribani siku sita hazikufanikiwa kuwapata vijana hao. Vilevile, hawakuweza kuwapata kwenye hospitali hadi ilipofika tarehe 28 Desemba walipo taarifiwa kuwa miili ya vijana hao ipo Hospitali ya Amana iliyofikishwa na askari Polisi.

ACT Wazalendo tunaona kwamba zipo hoja zinazoonyesha kuhusika kwa Jeshi la Polisi kwenye mauaji haya. Mosi, kutajwa kwa Askari Polisi wakati wa ukamataji na baadaye tena kwenye kufikishwa miili ya vijana hao katika Hospitali ya Amana.

Pili, sio kawaida ya Jeshi la Polisi kuokota miili ya watu halafu ikaipeleka hospitali wakati tayari kuna taarifa ya watu walioulizia kuhusu ndugu zao. Tatu, hakuna taarifa za Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi ili kubaini nani aliyehusika na mauaji ya miili waliyoikota.

Kutokana na kujirudia kwa matukio na tuhuma za askari polisi kuhusishwa kwenye mauaji ni wazi taswira ya Jeshi la Polisi inaendelea kuchafuka na kushusha imani ya wananchi.

ACT Wazalendo tunarudia wito kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liunde Tume ya kuchunguza mauaji yote ya raia ili kujiridhisha na hatua zilizofanywa na Jeshi la Polisi.

Pili, kwa hatua za awali tunamtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuchukua hatua ya kumfuatilia wanaotajwa kuhusika kwenye tukio hili la vijana.

Mwisho, tunaendelea kusisitiza mageuzi ya Jeshi la Polisi kutoka kuwa chombo cha mabavu na kuwa huduma ili liwe linatekeleza wajibu na majukumu yake kwa weledi na kufuata sheria.
Imetolewa na;

Wakili Bonifasia Aidan Mapunda
Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani ya nchini
31 Desemba, 2023
Wazo zuri sana lkn watanzania tuliowengi hatuna imani na ACT maana ni ccm b
 
Naomba kuuliza swali la kizushi kama kuna mwenye historia ya hao vijana aiweke hapa, pia hao vijana hawana rekodi yoyote kufungwa jela?
Kwani mtu ulifungwa jela ndiyo iwe green light ya kifo chako?

Wewe ni manzanita au mhutu?
 
Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya maafisa wa Jeshi la Polisi kuhusishwa na vifo vya vijana wawili ambao ni Bakari Ismail (21) na Shomari Kucheuka (22) waliokuwa wakiishi Vingunguti Dar es Salaam. Taarifa zinaeleza kuwa vijana hao walikamatwa kwa nguvu na Askari Polisi wakiwa nyumbani kwao mnamo Desemba 27, 2023.

Jambo la kusikitisha baada ya kukamatwa haikujulikana walipelekwa wapi kwa kuwa jitihada za ndugu na jamaa kufuatilia kwenye vituo vya Polisi takribani siku sita hazikufanikiwa kuwapata vijana hao. Vilevile, hawakuweza kuwapata kwenye hospitali hadi ilipofika tarehe 28 Desemba walipo taarifiwa kuwa miili ya vijana hao ipo Hospitali ya Amana iliyofikishwa na askari Polisi.

ACT Wazalendo tunaona kwamba zipo hoja zinazoonyesha kuhusika kwa Jeshi la Polisi kwenye mauaji haya. Mosi, kutajwa kwa Askari Polisi wakati wa ukamataji na baadaye tena kwenye kufikishwa miili ya vijana hao katika Hospitali ya Amana.

Pili, sio kawaida ya Jeshi la Polisi kuokota miili ya watu halafu ikaipeleka hospitali wakati tayari kuna taarifa ya watu walioulizia kuhusu ndugu zao. Tatu, hakuna taarifa za Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi ili kubaini nani aliyehusika na mauaji ya miili waliyoikota.

Kutokana na kujirudia kwa matukio na tuhuma za askari polisi kuhusishwa kwenye mauaji ni wazi taswira ya Jeshi la Polisi inaendelea kuchafuka na kushusha imani ya wananchi.

ACT Wazalendo tunarudia wito kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liunde Tume ya kuchunguza mauaji yote ya raia ili kujiridhisha na hatua zilizofanywa na Jeshi la Polisi.

Pili, kwa hatua za awali tunamtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuchukua hatua ya kumfuatilia wanaotajwa kuhusika kwenye tukio hili la vijana.

Mwisho, tunaendelea kusisitiza mageuzi ya Jeshi la Polisi kutoka kuwa chombo cha mabavu na kuwa huduma ili liwe linatekeleza wajibu na majukumu yake kwa weledi na kufuata sheria.
Imetolewa na;

Wakili Bonifasia Aidan Mapunda
Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani ya nchini
31 Desemba, 2023
Dawa ya vibaka na panya road ni risasi tuu na ikiwezekana mabomu yatumike nyie ni wadini tunawajua mmetazama majina mmekuja na waraka…watu wana jeruhi watu halafu waachwe…hao marehemu walipaswa kupigwa mabomu
 
Back
Top Bottom