Pre GE2025 Kuhusu kupokea fedha za Abdul, kutoka kwa Lissu kuna ukweli kidogo na uongo mwingi

Pre GE2025 Kuhusu kupokea fedha za Abdul, kutoka kwa Lissu kuna ukweli kidogo na uongo mwingi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hapana Mkuu.

Lissu ni mtu bold sana. Lissu ni mtu muwazi sana. To a fault.

Angetaka kumfukuza Abdul pale angemfukuza bila mbinu yoyote.

Lissu ni kati ya wanasiasa wachache Tanzania wanaoweza kusema ukweli mchungu bila kuremba, kasema ukweli mchungu wa kuki expose chama chake mwenyewe kwenye rushwa.

Huyo mtoto Abdul, Lissu anamuogooa kwa kipi mpaka atumie mbinu kumtoa?

Lissu alitaka favor kweli.
kuna kusema ukweli na kuropoka ukweli.

ila lisu ni mropokaji tena muongo
 
Lissu anapata faida isiyo ya haki kwa sababu anaruka mstari wa process halali ya kupata fidia yake ya haki. Anatumia nafasi yake ya kisiasa kama mpinzani mahiri kujipatia faida binafsi ambayo wananchi wa kawaida hawawezi. Hapo hakuna usawa wala haki. Kuna mchezo wa kupeana fadhila kwa kujuana.

Abdul alitaka kumhonga Tundu Lissu oesa ili Tundu Lissu asimsakame rais Samia. Lissu akakataa pesa, lakini akakubali rushwa ya fadhila. Abdul bado alikuwa na expectations kuwa akitimiza upande wake, Lissu naye atatimiza upande wake kuacha kumsakama sana Samia. Suala la oesa au fadhula ni namna tu ya malipo, ila rushwa bado iko pale pale.

Kuna wazee wengi wanadai fidia zao, mafao yao, wamekaa kwenye mstari miaka mingi. Hawajuani na Abdul wala Samia, si wanasiasa. Wanasota.

Tundu Lissu akitakiwa kupigania haki kwa wote, atatue matatizo ya kimfumo.

Tundu Lissu kutaka kutatua tatizo lake yeye tu, kwa fadhila za Abdul na Samia kuruka mfumo rasmi, tena baada ya Abdul kutaka kumhonga pesa ili Tundu Lissu asimseme mama yake Abdul rais Samia vibaya, ni kukubali rushwa ya fadhila.

Tundu Lissu alikataa rushwa ya oesa, akakubali rushwa ya fadhila za Abdul.

Rushwa si lazima iwe ya pesa, hata fadhila ya kukurusha mstarini ili kukurahisishia kupata haki yako ni rushwa.

Fadhila hii ingempa Tundu Lissu advantage ambayo watu wasiojuana na Abdul na Samia hawana.

Hili ni tatizo kubwa Tanzania. Kika mtu anataka awe na mtu wake kwenye kika ofisi iki mambo yaende, hakuna mtu anayetaka kutatua natatizo ya kimfumo ili watu waoate huduma kwa haki bila hata ya kujuana na mtu.

Tundu Lissu kama mtu anayesimamia haki na usawa, alitakiwa ajue kuwa kutumia fadhika za Abdul ili arahisishiwe kuoata haki yake ni rushwa.
Aya ya pili kutoka mwisho ndio tatizo kwa watanzania walio wengi.
Na imekuwa ndio norm na inakuwa vigumu sana kuwaelewesha watanzania kwamba fadhila ili mambo yaende nje ya utaratibu ni rushwa.
 
kuna kusema ukweli na kuropoka ukweli.

ila lisu ni mropokaji tena muongo
Weka mfano mmoja hapa, ikiwezekana kwa ushahidi wa audio au video, tuuchambue kwa kina, kimantiki, kwa kupima neno kwa neno, tujue ukweli uko wapi.
 
Aya ya pili kutoka mwisho ndio tatizo kwa watanzania walio wengi.
Na imekuwa ndio norm na inakuwa vigumu sana kuwaelewesha watanzania kwamba fadhila ili mambo yaende nje ya utaratibu ni rushwa.
Naam, kweli mkuu.

Watanzania wengi washazoea hii rushwa ya fadhila mpaka hawaioni kama rushwa.

Wamekuwa ni kama samaki aliyezaliwa na kuishi kwenye maji maisha yake yote, hata hajui kwamba anaishi katika maji, kwa sababu hajui maisha nje ya maji!

Nilitegemea mtu kama Lissu awe anatufundisha kitu tofauti, lakini utamaduni huu ni mgumu sana kuuvunja hata yeye kaingia kwenye mtego huo.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Lete ushahidi kuwa Abduli hakuzipeleka Nyaraka za Abduli katika ngazi husika!

Maana ili rais asaini pesa za Lissu zitoke lazima ziwepo signatures nyingi za watu wa chini kila mtu kwa nafasi yake kwa mujibu wa sheria!

Hata kama Abduli atabeba nyaraka za Lissu na kuzipeleka Ikulu ofisini kwa mama yake hawezi kuzisaini mpaka watu wote wanaotakiwa kusaini wasaini. Na ikifanyika hivyo maana yake utaratibu utafuatwa tu.

Kumbuka, Rais (kwa kuvunja sheria) anaweza kuamuru Lissu alipwe bila hata kupeleka nyaraka yeyote, ikifanyika hivyo hayo madai yako yanapata uhalali kwa mbaaali. Lakini as long as Abduli atabeba nyaraka na kuzipeleka katika ngazi husika hatua kwa hatua mpaka zifike kwa mama yake, hiyo sisi tunaita bahati ya Lissu kupata tarishi wa kumfanyia kazi yake kwa ufanisi!
Abdul mwenyewe si ngazi husika.

Abdul kushika nyaraka za Lissu tu ni favor, ni fadhila, bila kujali Abdul anazipeleka ngazi husika ama la.

Abdul anatumika kama mtoto wa rais kuweka pressure ili Tundu Lissu alipwe pesa zake. Abdul hahusiki na process hiyo, hiyo ni fadhila ya kisiasa kutumia jin ala mtoto wa rais na ofisi ya rais ili kumpa Tundu Lissu fadhila.

Tundu Lissu hakutakiwa hata kumpa Samia madai ya haki zake binafsi za mafao na kupewa pasipoti mpya, alikosea tangu alipompa madai hayo Samia Ubelgiji.

Pasipoti ikipotea, kuna mchakato wa kuomba mpya ubalozini. Mambo ya mafao yana mchakato wake serikalini. Michakato hii haimhusishi rais.

Lissu amejiingiza katika mtego wa kupewa fadhila na Samia katika sehemu ambayo Samia hahusiki.

Mchakato w akupata passport haupiti kwa Samia. Mchakato wa mbunge kulipwa pesa zake haupitii kwa Samia.

Lissu ametumia influence peddling kupata fadhila.

"In·flu·ence ped·dling

The use of position or political influence on someone's behalf in exchange for money or favors."

Hiki ndicho alichofanya Tundu Lissu.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Naam.

Tufikirie kidhahania.

Muandishi wa habari ukienda kudai haki yako ofisi ya mafao yenye mstari mrefu kwa karani, ukaambiwa na meneja kuwa uache kumuandika vibaya, atakupa hela, ukakataa hela, ila ukasema akusaidie upate fadhila uruke mstari mrefu ili upate mafao yako haraka bila kufuata mstari, hapo hata kama unapata mafao ambayo ni haki yako, ukitumia fadhila ya kuruka mstari inayokupa unfair advantage, hiyo fadhila ni kinyume cha maadili. Ni influence peddling. Ni rushwa.

Lissu namkubali kwenye mengi, moja ya jambo alilosema alitaka watu wam challenge, wamfanyie constructive criticism iki aweze kujifunza mengi na kufanya vizuri zaidi.

Hapa alipotaka kufanya influence peddling ni kitu kibaya, angeweza kufanya vizuri zaidi.

Lissu alitakiwa kukataa pesa za Abdul na kukataa fadhila yoyote. Fadhila nayo ni hongo, hata kama ni fadhila katika kupata haki yako.

Hii hapa ni definition ya influence peddling.

Influence peddling - the use of position or political influence on someone's behalf in exchange for money or favors.
kupewa haki yako ni fadhila?
 
Kwenye ushahidi ni vigumu kujua kwa uhakika.

Kwa sababu, mtu anapotaka kuja kukupa rushwa, hakuambii kwamba anakuja kukupa rushwa ili ujiandae kuchukua ushahidi. Hakuandikii hundi na kuiwekea label ya "Rushwa" na kuiwekea saini ili uje uitumie kama ushahidi.

Kuna maneno yamesemwa, kwamba Lissu, Wenje, David Djumbe na Abdul walikutana.

Hili Abdul hajalikanusha.

Lissu kasema Abdul alitaka kumpa pesa ili Lissu asimsakame mama yake Abdul. Hili Abdul hajalikanusha.

Lissu kasema alikataa pesa za Abdul, akamtaka Abdul amsaidie kupata pesa zake za kihalali.

Katika kanuni za habari, habari potofu ikitolewa, anayeona hiyo habari si sahihi ana haki na wajibu wa kuisahihisha.

Na habari isiyopingwa inachukuliwa kuwa ni ya kweli.

Kama Tundu Lissu kasema uongo, Abdul ajitokeze tu na kutupa upande wake tuusikilize.
Hapo kuna mtego unaitwa Abdul tangu haya mambo yaanze hajawahi kuongea hata hayo mambo ya malipo ya Lisu hajaongea kwamba aliyapata kwa soft copy.Hapa ni mtu anatukana sufuria lillilompa chakula na kulitoboa kwa kutumia mtego wa Abdul.
 
kupewa haki yako ni fadhila?
Swali zuri, hapa naona kuna watu wengi hawaelewi.

Kupewa haki yako si fadhila.

Lakini, kumtumia mtoto wa rais ili uruke mstari halali wa kupata haki yako ni kupewa fadhila na huyo mtoto.

Umeelewa?

Yani inawezekana kuna dirisha la kupewa haki yako, kuna mstari wa watu 100 wamekutangulia kufika disrishani kupata haki zao.

Ukija wewe unajuana na mkurugenzi wa hiyo sehemu akakurusha huo mstari upate haki yako bila kufuata mstari, kukurusha huo mstari ni fadhila, hata kama unaruka mstari ili kupata haki yako.

Ushaelewa?
 
Hapo kuna mtego unaitwa Abdul tangu haya mambo yaanze hajawahi kuongea hata hayo mambo ya malipo ya Lisu hajaongea kwamba aliyapata kwa soft copy.Hapa ni mtu anatukana sufuria lillilompa chakula na kulitoboa kwa kutumia mtego wa Abdul.
Kanuni rahisi ni kwamba tuhuma zinatakiwa kujibiwa, zisipojibiwa zinachukuliwa kama kweli.

Kama Abdul kasingiziwa, akanushe tu tuhuma na kutupa upande wake.
 
Kupewa haki yako si fadhila.

Lakini, kumtumia mtoto wa rais ili uruke mstari halali wa kupata haki yako ni kupewa fadhila na huyo mtoto.

Umeelewa?

Yani inawezekana kuna dirisha la kupewa haki yako, kuna mstari wa watu 100 wamekutangulia kufika disrishani kupata haki zao.

Ukija wewe unajuana na mkurugenzi wa hiyo sehemu akakurusha huo mstari upate haki yako bila kufuata mstari, kukurusha huo mstari ni fadhila, hata kama unaruka mstari ili kupata haki yako.

Ushaelewa?
Lisu hakumfuata Abduli. Abduli ndiye alienda kwa Lisu kumhonga, Lisu akamwambia sitaki pesa zako hizo, nataka pesa zangu halali. Nimeshafuata taratibu zote zaidi ya mara mbili bila mafanikio. Kamwambie mama yako anipe pesa zangu. Sitaki hizi zako CHAFU

hapo kuna kuomba fadhila hapo? kuna kuruka foleni hapo?

acha hizo diaspora

kule kwa shamgazi "kiranga" ni jembe lile la kulimia kwa mkono.
 
Lisu hakumfuata Abduli. Abduli ndiye alienda kwa Lisu kumhonga, Lisu akamwambia sitaki pesa zako hizo, nataka pesa zangu halali. Nimeshafuata taratibu zote zaidi ya mara mbili bila mafanikio. Kamwambie mama yako anipe pesa zangu. Sitaki hizi zako CHAFU

hapo kuna kuomba fadhila hapo? kuna kuruka foleni hapo?

acha hizo diaspora

kule kwa shamgazi "kiranga" ni jembe lile la kulimia kwa mkono.
Nani kamfuata nani ni irrelevant, unaweza kumfuata Abdul kwake akakupa rushwa, mnaweza kukutana hotelini akakupa ruswa, anaweza kuja kwako akakupa rushwa.

Kwa hiyo habari ya nani kamfuata nani ni irrelevant.

Lissu angeweza kumwambia Abdul sitaki pesa zako ondoka kwangu.

Hakufanya hivyo.

Lissu alimtaka Abdul amfanyie fadhila ya kumsaidia kupata haki yake, fadhila ya kutumia jina la rais ili Lissu apate haki yake kirahisi.

Hii fadhila ni rushwa ya fadhila.

Hii rushwa ya kutumia influence yako ili kupata urahisi kinyume na mifumo rasmi iliyotumika hapa inaitwa "influence peddling".

in·flu·ence ped·dling

the use of position or political influence on someone's behalf in exchange for money or favors.

Jadili hoja, usimtukane mtoa hoja. Kumtukana mtoa moja ni dalili ya kukosa hoja.

Ni logical fallacy inaitwa ad hominem.
 
Lissu hakukataa hongo.

Alikataa hongo ya pesa akakubali hongo ya fadhila ya Abdul kumsaidia apate mafao yake.

Kwa maneno yake mwenyewe.

That was influence peddling.

Lissu should do better than that.
Mtu akiwa muongeaji sana kuna mahali anajikanyaga kwenye maelezo yake.
Lissu ameongea mengi kiasi cha kujiweka kwenye hatia ya yeye kutaka kupokea rushwa ya gharama za matibabu.
Ameruka moto akakanyaga maji ya moto.
Nikitoka nje ya mada kidogo, naona Mbowe imefika wakati anastahili kuachia mtu mwingine nafasi ya uongozi CDM.
 
Mtu akiwa muongeaji sana kuna mahali anajikanyaga kwenye maelezo yake.
Lissu ameongea mengi kiasi cha kujiweka kwenye hatia ya yeye kutaka kupokea rushwa ya gharama za matibabu.
Ameruka moto akakanyaga maji ya moto.
Nikitoka nje ya mada kidogo, naona Mbowe imefika wakati anastahili kuachia mtu mwingine nafasi ya uongozi CDM.
Lissu kaongea sana mpaka kajikanganya kwenye maelezo yake.

Lakini kujikanganya kwenye mazungumzo mara nyingine kunaonesha mtu anasema ukweli. Ukiona mtu anatoa story imenyooka kila kitu, hapo inabidi upate shaka kujiuliza kama kuna vitu vinafichwa.

Mimi nimefurahia uwazi wake, Lissu hapa kasema kama mtoto ambaye hawezi kudanganya, anasema mambo mpaka yale yanayoweza kumuumiza yeye mwenyewe.

Ila pia, Tanzania tuna standards ndogo sana, pengine kwake yeye anaona hili si tatizo, na kama mwanasheria pengine anaangalia the legal standard, which is a very low standard kwa sababu kuna rushwa nyingine zipo kisheria kabisa na mtu mwenye moral compass anatakiwa kuzikataa.

Ndiyo maana CCM ilipotaka kuhalalisha takrima, kuna watu wengi walipinga wakisema wameipa rushwa chafu jina jipya tu.

Wanasheria wana tabia ya kusema mengi huku wakiamini kuwa hata wakibanwa wanaweza kujitetea kisheria.

Tatizo uongozi wa jamii si suala la kisheria tu, kuna mambo mpaka ya maadili pia.
 
m
Naam.

Tufikirie kidhahania.

Muandishi wa habari ukienda kudai haki yako ofisi ya mafao yenye mstari mrefu kwa karani, ukaambiwa na meneja kuwa uache kumuandika vibaya, atakupa hela, ukakataa hela, ila ukasema akusaidie upate fadhila uruke mstari mrefu ili upate mafao yako haraka bila kufuata mstari, hapo hata kama unapata mafao ambayo ni haki yako, ukitumia fadhila ya kuruka mstari inayokupa unfair advantage, hiyo fadhila ni kinyume cha maadili. Ni influence peddling. Ni rushwa.

Lissu namkubali kwenye mengi, moja ya jambo alilosema alitaka watu wam challenge, wamfanyie constructive criticism iki aweze kujifunza mengi na kufanya vizuri zaidi.

Hapa alipotaka kufanya influence peddling ni kitu kibaya, angeweza kufanya vizuri zaidi.

Lissu alitakiwa kukataa pesa za Abdul na kukataa fadhila yoyote. Fadhila nayo ni hongo, hata kama ni fadhila katika kupata haki yako.

Hii hapa ni definition ya influence peddling.

Influence peddling - the use of position or political influence on someone's behalf in exchange for money or favors.
mimi kimtazamo wangu kuhusu ombi la lisu kusaidiwa na abdul kupata stahiki zake si jambo baya ,maana kama tunavyojua abdul si mtu wa wizara husika inayoshughulikia maadai ya lisu ila ni mtu wa connection ambae ana influence kubwa kwa watu wa maamuzi hivyo aliamini kwa kupitia yeye basi jambo lake lingapata msukumo wa moja kwa moja kutoka kwa mama mtu na mama abdul akatoa comand kwa wahusika wafuate sheria inavyosema,kwa kutengua vikwazo vinavyominya stahiki za lisu kupatikana,kwa hisia zangu zinakuja kuwa abdul nae alitoa conditions za kufanikisha hilo,au kwa lugha nyingine quid pro quo ilihitajika au kula uliwe hapo ndipo lisu aliona huu mtego ,lisu aliona hawa watu wanataka kumziba mdomo ili siku nyingine asiweze tena kukemea rushwa akaona potelea pote sihitaji tena msaada wenu nendeni zenu.abdul kwa sasa ni kama dalali ukitaka jambo lako liwe la kisheria lisiwe la kisheria liende haraka basi muone hilo limeisha kama unavyojua system za kiafrika zpo kwa ajiri ya kuweka ugumu ili ufanikishe unachohitaji ,sio kama wenzetu system zpo kurahisisha maisha,.
 
m

mimi kimtazamo wangu kuhusu ombi la lisu kusaidiwa na abdul kupata stahiki zake si jambo baya ,maana kama tunavyojua abdul si mtu wa wizara husika inayoshughulikia maadai ya lisu ila ni mtu wa connection ambae ana influence kubwa kwa watu wa maamuzi hivyo aliamini kwa kupitia yeye basi jambo lake lingapata msukumo wa moja kwa moja mama mtu na mama abdul akatoa comand kwa wahusika wafuate sheria inavyosema,kwa kutengea vikwazo vinavyominya stahiki za lisu kupatikana,kwa hisia zangu zinakuja kuwa abdul nae alitoa conditions za kufanikisha hilo,au kwa lugha nyingine quid pro quo ilihitajika au kula uliwe hapo ndipo lisu aliona huu mtego ,lisu aliona hawa watu wanataka kumziba mdomo ili siku nyingine asiweze tena kukemea rushwa akaona potelea pote sihitaji tena msaada wenu nendeni zenu.abdul kwa sasa ni kama dalali ukitaka jambo lako liwe la kisheria lisiwe la kisheria liende haraka basi muone hilo limeisha kama unavyojua system za kiafrika zpo kwa ajiri ya kuweka ugumu ili ufanikishe unachohitaji ,sio kama wenzetu system zpo kurahisisha maisha,.
Hiyo habari nzima ya kutumia connection ya Abdul kupata fadhila ili madai ya Lissu yapate msukumo ndiyo tatizo lilipo hapo.

Tundu Lissu kama msimamia haki alitakiwa kusimamia kupata haki yake bila kutegemea fadhila ya mtu.

Kutegemea fadhila ya Aabdul ni tatizo kwa sababu.

1. Kimsingi ni rushwa ya fadhila. Abdul alitaka kumpa Lissu rushwa ya pesa, Lissu akakataa rushwa ya pesa, akamtaka Abdul amfanyie fadhila kupata pesa zake, hii fadhila ni rushwa pia.

2. Tundu Lissu alipokataa rushwa ya pesa kimsingi alikataa kununuliwa kwa pesa ili asimsakame Samia. Kukataa pesa za Abdul halafu kukubali fadhila zake ni kukubali rushwa vile vile. Abdul akimpa pesa au fadhila bado anategemea Lissu asiendelee kumsema Mama yake Abdul rais Samia.

3. Rushwa ya fadhila inaondoa usawa. Kuna watu wengi sana wana tatizo kama la Lissu lakini hawajuani na Abdul wala Samia. Tundu Lissu akitumia nafasi yake ya kisiasa ya kujuana na Abdul na Samia kutatua tatizo lake, anakuwa kakwepa kutatua tatizo la kimfumo linalowaacha Watanzania wengi wenye tatizo kama lake ambao hawamjui Samia.

4. Tundu Lissu amekosa kuitumia nafasi hii muhimu kuifanya kama cause ya kulazimisha mifumo ifanye kazi vizuri zaidi kwa watu wengi zaidi. Amepewa nafasi ya kufanya kazi ngumu ya kuanzisha mabadiliko haya au kujinufaisha yeye mwenyewe kwa cheo chake na connections za kisiasa, kawasaliti Watanzania maelfu kwa maelfu wenye tatizo kama hili kwa kujipendelea yeye mwenyewe kupata mteremko kwa Abdul bila kushughulikia tatizo la kimfumo.

5. Noblesse oblige. Those who are given much, much shall be required from them. Tundu Lissu amepewa heshima kubwa, matumaini mengi na watanzania wengi. Standard ambayo tunapaswa kuwawekea viongozi wetu nayo inatakiw akuw akubwa.Tundu Lissu alitakiwa kuwa mfano kwa Watanzania wengi ambao hawajui influence peddling ni nini, alikuwa na nafasi ya kuwafundisha kukataa mfumo wa kupata haki kwa kujuana na kuonesha kuwa anaweza kung'ang'ania mfumo halali unaotakiwa kutumiwa mpaka apate halki yake, bila kutumia fadhila ya connections za Abdul na Samia.
 
TUNDU Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Tanzania Bara, alishusha tuhuma kuhusu mtu anayeitwa Abdul, mtoto wa Rais Samia Suluhu Hassan, kwenda nyumbani kwake kumhonga.

Alizungumza kwa mara ya kwanza Iringa Mei 2024 kwenye mkutano wa hadhara. Aliendelea kurejea maneno hayo katika mikutano mingine. Nchi nzima inajua kuwa Lissu alifuatwa kuhongwa fedha na Abdul, akakataa.

Ambacho hakijawahi kusemwa ni kuwa hongo ambayo alitakiwa kupewa lengo lilikuwa nini. Lissu, alishusha tuhuma hizo kipindi ambacho maneno kuwa viongozi wa Chadema “wamelambishwa asali”, yamechukuwa nafasi tangu chama hicho kilipofanya maridhiano ya kisiasa na CCM mwaka 2022.

Mtuhumiwa mkuu wa kulamba asali ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe. Januari 21, 2023, Mbowe akiwa kwenye mkutano wa hadhara, viwanja vya Furahisha, Mwanza, alitetea maridhiano na kueleza kuwa kuna wenzao ndani ya chama hawaungi mkono.

Yupo mtu angeweza kuunganisha alama na kupata majibu kuwa Lissu aliposema alifuatwa na Abdul kuhongwa, akakataa, alitaka kufikisha ujumbe kuwa yeye siyo kama wengine wanaohongeka. Hafanani na “walamba asali”. Ukifika hapo, jina la Mbowe halipo mbali.

Kilichomponza Mbowe ni kuunga mkono maridhiano. Akayavaa kama beji ya heshima. Maridhiano yalifungua milango na madirisha, hivyo kuruhusu hewa mpya kuingia. Kesi za kisiasa zote zilifutwa, mikutano ya hadhara ilifunguliwa, waliokuwa wamekimbia nchi, walirejea. Unawezaje kumsimanga?

Wengi wanasahau. Mbowe alikaa jela miezi saba, kabla ya kuachiwa, hivyo kufungua milango ya maridhiano. Mbowe, alikuwa akikabiliwa na mashitaka ya ugaidi. Alikamatwa Julai 21, 2021 na kuachiwa huru Machi 4, 2022. Je, alilamba asali ili aachiwe huru na kuunga mkono maridhiano?

Nani hakumbuki? Maridhiano yalifanyika wakati wa uongozi wa Rais Samia. Kabla yake, Ikulu alikuwepo Dk John Magufuli, ambaye hakutaka kutazamana na wapinzani wake wa kisiasa kwa tabasamu. Kesi nyingi za kisiasa, mazingira ya kufanya siasa yalifunikwa na giza, wanasiasa walikimbia nchi. Nani wa kubeza maridhiano?

Turejee kwenye fedha za Abdul. Lissu alisema kulikuwa na jaribio la kumhonga. Yupo mtu hakumtaja, ama alimweka kiporo au alimhifadhi kwa sababu zake. Mbio za uenyekiti Chadema zikafanya Lissu amtaje. Ni Ezekia Wenje, Mwenyekiti wa Chadema, Kanda ya Ziwa.

Nilimsikia Lissu akisema: “Aliyemleta Abdul nyumbani kwangu aje kunihonga, ametangaza kugombea umakamu mwenyekiti na amesema kwa maneno yake mwenyewe anaamuunga mkono Mwenyekiti (Mbowe).” Mtajwa ni Wenje.

Neno “afterthought”, hutumiwa sana na wanasheria kwenye mijadala ya kisheria. Lissu ni mwanasheria. Ni kwa nini siku zote Lissu alilihifadhi jina la Wenje? Je, alikaa nalo kama kifungo ili Wenje asiende kinyume naye? Walikuwa na makubaliano ambayo Wenje ameyakiuka? Hakuwa na mpango wa kumtaja ila amekasirika kuona Wenje anamuunga mkono Mbowe dhidi ya yake?

Hutakuwa mbali na ukweli endapo utasema Lissu kumtaja Wenje ni afterthought, yaani fikra zilizofuata baada ya kuona anamuunga mkono Mbowe, ambaye anashindana naye katika mbio za uenyekiti wa Chadema. Yupo anayeamini leo kuwa Wenje na Lissu wana mengi, wakibanwa, wataeleza.

Nilimsikia Wenje akijibu tuhuma dhidi yake. Kwanza hakukataa, isipokuwa amefafanua ukweli upande wake ambao anadai unapindishwa na Lissu. Ukimsikiliza Wenje, unapata jibu moja; hakukuwa na kuhongwa. Habari ya hongo ni tungo nje ya uhalisia.

Wenje anasema kuwa alikutana na Abdul kama bahati kwenye shughuli moja, na baada ya utambulisho, moja kwa moja alimhoji: “Kwa nini Serikali ya mama yako haitaki kumlipa Lissu fedha zake za matibabu?” Lissu alishambuliwa kwa risasi nyingi Septemba 7, 2017.

Ni tukio baya kwa kipimo chochote. Ajabu, uliibuka mvutano wa fedha za matibabu ya Lissu. Sera ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), inaelekeza rufaa ya matibabu kwenda nje ya nchi kutolewa na Hospitali ya Taifa Muhimbili. Lissu alishambuliwa kwa risasi Dodoma, akapelekwa Hospitali ya Mkoa ya Dodoma. Kisha, akasafirishwa kwa ndege ya kukodi hadi Hospitali ya Aga Khan, Nairobi, Kenya. Hakupita Muhimbili.

Sababu za kutompitishia Lissu Muhimbili zilikuwa zinajitosheleza kabisa. Alishambuliwa, waliomshambulia hawakuwa wamepatikana. Nadharia zilikuwa nyingi. Hofu kuwa waliotaka kumuua wangeweza kumfuata Muhimbili, ndiyo ilisababisha apelekwe Nairobi.

Msimamo wa Serikali haukubadilika. Kwa kutambua kuwa Lissu alihitaji matibabu na hakuwa na bima, iliitishwa michango nchi nzima hadi diaspora. Mwitikio ulikuwa mkubwa. Tatizo ni moja, ulikosekana uwazi wa michango ya matibabu ya Lissu. Ukiacha Sh200 milioni zilizotangazwa na Mbowe Septemba 23, 2017, hakuna taarifa nyingine.

Zaidi, Watanzania hawakuwahi kuambiwa kama fedha walizochanga, zilitosha kugharamia matibabu ya Lissu au kinyume chake. Hivyo, inaleta ukakasi kuona Serikali bado inadaiwa fedha za matibabu ya Lissu. Je, tafsiri ya ile michango ni ipi? Lissu anataka apewe fedha za matibabu ambayo ameshalipiwa na Watanzania? Zingatia, hata Serikali ikilipa ni fedha za Watanzania.

Tusiondoke kwa Wenje; kwa nini alianzisha mada ya fedha za matibabu ya Lissu baada ya kutambulishwa kwa Abdul? Je, Lissu amewahi kumtuma au alijituma mwenyewe? Nilimsikia Wenje akisema fedha za matibabu ya Lissu zinamhusu kwa sababu naye kuna za kwake. Lissu alichangiwa, ina maana Wenje anataka kurudishiwa fedha alizomchangia Lissu kwa ajili ya matibabu?

Wenje anasema Abdul ni muungwana sana, maana alikubali kuongozana naye mpaka Tegeta, nyumbani kwa Lissu. Naunga mkono. Abdul ni muungwana, maana alipaswa kushangaa suala la matibabu ya Lissu kupelekewa yeye ambaye siyo waziri wa afya, katibu mkuu wa wizara hiyo wala mkurugenzi mkuu wa NHIF.

Mtu mmoja Kariakoo kwenye kijiwe cha kahawa, alisema: “Nashindwa nimwamini yupi, Lissu au Wenje?” Jibu langu ni kuwa mkweli ni yule anayezungumza taarifa na siyo fumbo. Wenje, ama kwa ukweli au kumsingizia Lissu, alichokizungumza ni taarifa (statement). Lissu, hoja yake ilikaa kwenye mabano. Ilihitaji kufumbuliwa. Ndiyo maana anavyofumbua inabeba tafsiri ya afterthought.

Swali la jumla ni je, nani anamsingizia mwenzake? Lissu kaamua kumsingizia Wenje kwa sababu ametofautiana naye katika uchaguzi ndani ya chama? Hata hivyo tuhuma za jaribio la kuhongwa alizitoa kabla ya moto wa uchaguzi ndani ya Chadema. Wenje amechagua kumkaanga Lissu ili kujinasua na kashfa? Wazungu husema “time heals all boo-boos” – “muda hutibu majeraha yote.” Tuwape muda.

Nilitazama mahojiano ya Lissu kwenye kituo cha Star TV. Nilimwona na nikamsikia Lissu akisema alifuatwa na “mwana malkia”, huyo “mwana malkia”, aliahidi kumsaidia kupata fedha za matibabu. Lissu akasema: “Nilimwambia yule mwana-malkia, ukinisaidia kupata hizi fedha utakuwa rafiki yangu.”

Rejea mkutano wa hadhara, Singida Juni 8, 2024, Lissu alisema: “Namfahamu mtoto wake mmoja anaitwa Abdul. Aliniletea rushwa nyumbani kwangu, nikamwambia shenzi. Kahonge wanaohongeka.”

Upande mmoja, Lissu anasema, alimwambia Abdul kuwa angemsaidia kupata fedha za matibabu, wangekuwa marafiki. Upande mwingine, Lissu anasema, alimfukuza, akamwambia ‘shenzi’. Lissu yupi mkweli?

Katika mahojiano Star TV, Lissu alisema “watu wema” ndiyo walimpeleka Abdul nyumbani kwake. Alikataa kuwataja hao watu wema. Baada ya Wenje kutangaza kumuunga mkono Mbowe, Lissu hakungoja kuulizwa, alimtaja moja kwa moja.

Kuna mwana-Chadema kutoka Magu, Mwanza, aliniandikia ujumbe unaosema: “Nahisi Lissu na Wenje walikuwa na makubaliano yao, wamegeukana, sasa wanatajana. Upo ukweli zaidi wa kuuchimba ndani ya vifua vyao. Wanachikitoa sasa kina uongo mwingi kuliko ukweli kwa sababu wanakomoana.”

Credit: Luqman MALOTO
Mtamaliza theories zote lakini ukweli hela za Abdul zimewaumbua Mbowe na genge lake la matapeli hapo Chadema
 
Back
Top Bottom