Hii ni hoja ya kisiasa tuvutane tushawishiane? tumshawishi nani, kwanini, inasaidia nini?Kwanini unampangia mwandishi namna ya kuandika mskala yake?
Kwanini unataka mwandishi aandike vile unavyopenda wewe?
Unaposema Bollen amefanya uchokonozi wa hoja, ni sawa na hilo ndilo lengo kuu la mwandishi, nami nimelipenda, sasa kila mmoja aanze kuvutia upande wake kama nilivyofanya mimi mbele ya safari.
Msipende kutafuniwa kila kitu nyie kazi yenu iwe ku "like" tu, hao walio "like" upande wa CCM waache wa "like", nawe "like" upande wa upinzani ukitaka, but lazima bongo zenu mzikomaze kwa ku prove wrong or right makala ya mwandishi.
Msipende kukimbilia kurusha mateke tu na kunyooshea wengine vidole, hatuwezi kufanana wote mawazo kila saa na kila siku, jengeni hoja zenu kutetea mnachoamini, hilo ndio lengo kuu la mwandishi.
Paragraph yako ya kwanza ya maswali umeonesha ulivyo tawaliwa na emotions, ukiwa hivyo utashindwa kutetea hata ukweli ulio wazi, utashindwa kesi kirahisi sana hata kama haki iko upande wako, rilaxx.Hii ni hoja ya kisiasa tuvutane tushawishiane? tumshawishi nani, kwanini, inasaidia nini?
Usiassume tu kuwa sote humu hatuelewi anachojaribu kukifanya Boleni.
Hili ni suala la uhai wa mtu kuondolewa vs makosa ya wenye mamlaka, tukijadili na kuchokonoa mada inawasaidia akina nani? Kwamba leads zinatoka humu? kwamba wachunguzi hawaelewi chochote wategemee sisi humu tuwape clue? brother.
Bole anafanya damage control kwa malengo anayoyajua yeye, mimi na wenzangu tumekataa na ni kwasababu tunamjua vizuri.
Maswali anayouliza yako wazi anamuuliza nani? narration anazofanya ziko wazi ananarrate nini?
Naungana na mdau aliyesema tumeuchoka uandishi wa Kipascal mayala.
Well Noted Mkuu... Mzee BUTIKU jana kaeleza vizuri sana misingi ya Katiba juu ya huu UNYAMA uliotendeka hawa wengine wanatumwa kwa bahasha....hili jambo linapakuanzia....Majuzi Mbowe alianika hili kundi wazi kabisa .....cha ajabu huyu mwandishi hata hili hakuliona na muunganiko wake katika hili Tukio la KINYAMAHii ni hoja ya kisiasa tuvutane tushawishiane? tumshawishi nani, kwanini, inasaidia nini?
Usiassume tu kuwa sote humu hatuelewi anachojaribu kukifanya Boleni.
Hili ni suala la uhai wa mtu kuondolewa vs makosa ya wenye mamlaka, tukijadili na kuchokonoa mada inawasaidia akina nani? Kwamba leads zinatoka humu? kwamba wachunguzi hawaelewi chochote wategemee sisi humu tuwape clue? brother.
Bole anafanya damage control kwa malengo anayoyajua yeye, mimi na wenzangu tumekataa na ni kwasababu tunamjua vizuri.
Maswali anayouliza yako wazi anamuuliza nani? narration anazofanya ziko wazi ananarrate nini?
Naungana na mdau aliyesema tumeuchoka uandishi wa Kipascal mayala.
Angalau wewe hujaweka mihemko ktk maelezo yako.Hakuna mwenye upeo finyu kama unavyofikiri, Boleni ameandika kikasuku na andiko linazua taharuki zaidi badala ya kuleta tafakuri.
Hili andiko pengine limesomwa na wenye uelewa mkubwa wakaelewa, na pengine limesomwa na wenye uelewa mdogo wakameza mambo kama yalivyo.
Ukitaka kujua hili andiko litaeleweka ndivyo sivyo, Kuna wana CCM wataona amewatetea, (angalia waliolike) na kuna wapinzani wataona Boleni anajaribu kufanya uchokonozi wa hoja! Hiki ndiko mwandishi alichodhamiria na amefanikiwa.
Kivyovyote vile waandishi wana motives wanapozitumia kalamu zao, kwa kaliba yao waandishi wa hii nchi, alichokikusudia Boleni “pengine “ kimefanikiwa kwa 70% isipokuwa kwa watu wachache.
Kwanini aandike overstatements na parables kama tuko wakati wa yesu? Huoni kama kuna majambo yamefanyiwa “amplifications” bila sababu za msingi? au hili ni andiko la kifasihi?
JokaKuuAngalau wewe hujaweka mihemko ktk maelezo yako.
Yaonekana umemuelewa kiasi.
Bollen ameweka clue za kutosha kuonesha nani prime suspect wa hilo tukio. Nani walikuwa na 'ugomvi' au tuite most 'probable cause' ya kufanya vile kwa marehemu?
Bollen kajiwekea kinga ile kitu inaitwa 'plausible deniability' akiitwa aweze kukana sikumtaja mtu au taasisi.
Bollen siyo mjinga aitaje taasisi au mtu fulani 'explicitly' kwamba ndiyo muuwaji. Wewe pia wala wengi wetu humu JF au mitaani ndani ya TZ hatuwezi vinginevyo tutaishia jela.
Tanzania tunahitaji kusajiri huduma ya wapelelezi binafsi kuweza kuwabaini na kushitaki watuhumiwa kesi kama hizi zenye maslahi na ........
Muandishi amewasaidia kuweka baadhi ya matukio na sehemu zingine dot au dash kwenye sequence ya matukio, sisi wananchi tuhukumu (hukumu ya umma) au wenye kuweza kushitaki wajaze nafasi wazi kuunganisha hiyo sequence waende mahakamani.
Kadiri watu wanavyo jadili na kuweka clue wanawaweka hadharani wahusika na kutoa msukumo kwa mamlaka yenye kuwawajibisha ifanye hivyo.Kwamba leads zinatoka humu? kwamba wachunguzi hawaelewi chochote wategemee sisi humu tuwape clue? brother.
ni ipi hukumu ya muhaini au gaidi kwa mujibu wa sheria? kutekwa? kupigwa na kumwagiwa tindikali? kuuwawa kinyama? kama haijakufika au katika familia yako bhs huwezi elewa utabaki kuandika makala ya ajabu kama hayaC&P from Face Book.
KUTEKWA, KUTESWA, KUUAWA KWA ALLY KIBAO, TUSAIDIANE KUTAFAKARI
Na Bollen Ngetti
SOMA lakini kwa tafakuri pana labda tukajua ukweli walau kidogo si wote katika giza hili lililofunika kutekwa, kuteswa na hatimaye kuuawa kikatili Mzee Ally Muhammed Kibao al-maarufu MeD.
Niharakishe kusema ukweli kwamba hakuna uhusiano mzuri baina na kati ya CCM na Chadema kimkakati, kisiasa na hata kimtazamo na kimaadili. Niharakishe pia kusema kama ilivyo kwa vyama vyote kongwe ni hayawani pekee anayeweza kutenganisha chama-tawala na dola. Kwamba dola inaishi kwa hisani ya chama-tawala na kwa mantiki hiyo dola ina wajibu mkubwa wa kukilinda chama kwa gharama yoyote.
Sasa twende. Siku za karibuni Jeshi la Polisi lilitoa taadhari kwa umma mpana kwamba lina taarifa za kijasusi zisizo na chembe ya shaka kwamba Chadema inapanga makundi ya vijana yapatayo 20 ambayo yatavamia vituo vya polisi jijini Dar es salaam kwa wakati mmoja.
Kwa mujibu wa Polisi intelijensia ilionesha kikao kilichokuja na uamuzi huo mgumu ulifanyika kupitia mtandao wa ZOOM. Hata hivyo Polisi haikusema lengo la kuvamia vituo hivyo ni nini hasa? Kuvichoma moto? Kuwapiga Polisi? Kuwafungulia huru maabusu? Kukwapua silaha? Kwenda kuvitumia wapi? Endelea kutafakari.
SASA tujiulize haya maswali ya msingi. Hakuna mtu wa kawaida mwenye uwezo wa kuvamia kituo cha polisi akijua fika ni eneo salama iliyosheheni silaha za kivita. Mtu huyo anaweza tu kama naye ana mafunzo mahsusi ya masuala hayo ama ni jambazi mzoefu. (Rejea kuvamiwa kwa kituo cha Polisi Stakishari Ukonga).
Tembea na neno "taarifa zisizo na SHAKA" kichwani.
Hii maana yake ni kwamba wavamizi watarajiwa wa vituo vya polisi kutoka Chadema wana uwezo, mafunzo, ujasiri juu ya maswala ya usalama na kwa mantiki hiyo wasingekwenda kujaribu bali kutekeleza. Swali lingine linanijia kichwani maana taarifa ya Polisi ina ukweli "usio na shaka". Kwamba vijana hawa wa Chadema wamepata mafunzo hayo wapi na lini? Maana si majambazi kwa mujibu wa Polisi.
Vyuo vya usalama nchini vinajulikana kuanzia Polisi, Magereza, TISS, JWTZ. Wao wamepata mafunzo wapi? Chadema ina chuo cha mafunzo ya silaha kiasi cha kuvamia vituo vya Polisi kulikosheheni bunduki za kila aina?
Kama hawa chuo kama hicho ndani au nje ya nchi, basi tujiulize kusumbua bongo zetu. Nani aliwapa mafunzo wakaiva na hivyo kuwa na uwezo, ujuzi na ujasiri wa kuvamia vituo vya polisi ? Kwani Red Brigade wanafunzwa kuvamia vituo vya Polisi? Usichoke kutafakari....
SASA, moja ya sifa tuliyoambiwa Marehemu Ally Kibao anayo ni kwamba ni Mwanajeshi mstaafu aliyefika katiko vyeo vya juu si kabisa. Kibao alikuwa ni Mjumbe wa Sekretariat ya Chadema lakini pia tunaambiwa kuwa ndiye alikuwa ni "strategist" wa chama na ndio hakufahamika sana majukwaani maana alikuwa "nyuma ya kamera ".
Sijui viapo vya JWTZ vinasemaje ila Kibao baada ya kustaafu alijiunga na CCM na kuwa Mwenezi Mkoa wa Tanga na baadaye kutimkia Chadema hadi alipotekwa, kuteswa., kuuawa na mwili wake kutupwa vichakani huko Ununio (Dar es salaam).
Swali fikirishi! Je, ni huyu (Kibao), strategist, JWTZ mstaafu ndiye aliwapika vijana wa kuvamia vituo vya Polisi? Je, uratibu huu ulikuwa ukiendelea na tuseme Polisi waliamua kujihami kabla ya uvamizi kwa usemi, "mpige mchungaji na kondoo wote watatawanyika"? Haya yote ni kuwaza maana ripoti ya uchunguzi juu ya waliomuua Kibao ni kina nani hasa licha ya alama zote kuonesha ni watu wenye kumiliki pingu ama wa ndani au nje ya nchi. Yote yawezekana.
Je, polisi iko katika operesheni maalum kuzuia wavamizi kabla ya kuvamiwa? Swali linalogonga vichwa ni kwamba kama taarifa za kijasusi zilionesha kuwa MeD ndiye alikuwa "chuo" cha kuwaandaa wavamizi ndiyo auawe badala ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria? Sina jibu....wauaji wana majibu.
Nawaacha na swali hili! Kwa tusiamini kuwa nyuma ya vitendo vya utekaji Chadema haiko nyuma yake kisiasa? Kwa nini hutaki kuamini na kwa nini uamini. Nawatakia tafakuri njema na jadidi. Alamsiki.
PIA SOMA
- TANZIA - Dar: Ally Mohamed Kibao, kiongozi wa chadema auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana
Huyo mwandishi wa mada ametumia tumbo kufikiri.Mwandishi anajaribu kuonyesha CHADEMA ATI wanauwezo Mkubwa huku akidharau uwezo wa Vyombo vya Dola kwamba havijui, havina uwezo, havitambui wajibu wake n.k.
Mwandishi kadharau serikali kimantiki ingawaje Kwa umbo la nje ameonyesha kuitetea Kwa namna Moja ama ñyiñgine.
Mwandishi amejisahaulisha kuwa siô jukumu la CHADEMA, Kulinda raia WA nchi hii.
Mwenye jukumu Hilo ndîo anakuwa wakwanza kubeba lawama, fedheha Kwa kushindwa kutimiza wajibu
Muulize Godbless Lema kilichomfanya akimbie kwenda kanada ni nini baada ya uchaguzi .Kwani walitaka kufanya nini?Hili la kuvamia vituo walisema polisi wenyewe wiki kama mbili zilizopita
Duu ndio maana tunaenda kuzika. MtumeeeeC&P from Face Book.
KUTEKWA, KUTESWA, KUUAWA KWA ALLY KIBAO, TUSAIDIANE KUTAFAKARI
Na Bollen Ngetti
SOMA lakini kwa tafakuri pana labda tukajua ukweli walau kidogo si wote katika giza hili lililofunika kutekwa, kuteswa na hatimaye kuuawa kikatili Mzee Ally Muhammed Kibao al-maarufu MeD.
Niharakishe kusema ukweli kwamba hakuna uhusiano mzuri baina na kati ya CCM na Chadema kimkakati, kisiasa na hata kimtazamo na kimaadili. Niharakishe pia kusema kama ilivyo kwa vyama vyote kongwe ni hayawani pekee anayeweza kutenganisha chama-tawala na dola. Kwamba dola inaishi kwa hisani ya chama-tawala na kwa mantiki hiyo dola ina wajibu mkubwa wa kukilinda chama kwa gharama yoyote.
Sasa twende. Siku za karibuni Jeshi la Polisi lilitoa taadhari kwa umma mpana kwamba lina taarifa za kijasusi zisizo na chembe ya shaka kwamba Chadema inapanga makundi ya vijana yapatayo 20 ambayo yatavamia vituo vya polisi jijini Dar es salaam kwa wakati mmoja.
Kwa mujibu wa Polisi intelijensia ilionesha kikao kilichokuja na uamuzi huo mgumu ulifanyika kupitia mtandao wa ZOOM. Hata hivyo Polisi haikusema lengo la kuvamia vituo hivyo ni nini hasa? Kuvichoma moto? Kuwapiga Polisi? Kuwafungulia huru maabusu? Kukwapua silaha? Kwenda kuvitumia wapi? Endelea kutafakari.
SASA tujiulize haya maswali ya msingi. Hakuna mtu wa kawaida mwenye uwezo wa kuvamia kituo cha polisi akijua fika ni eneo salama iliyosheheni silaha za kivita. Mtu huyo anaweza tu kama naye ana mafunzo mahsusi ya masuala hayo ama ni jambazi mzoefu. (Rejea kuvamiwa kwa kituo cha Polisi Stakishari Ukonga).
Tembea na neno "taarifa zisizo na SHAKA" kichwani.
Hii maana yake ni kwamba wavamizi watarajiwa wa vituo vya polisi kutoka Chadema wana uwezo, mafunzo, ujasiri juu ya maswala ya usalama na kwa mantiki hiyo wasingekwenda kujaribu bali kutekeleza. Swali lingine linanijia kichwani maana taarifa ya Polisi ina ukweli "usio na shaka". Kwamba vijana hawa wa Chadema wamepata mafunzo hayo wapi na lini? Maana si majambazi kwa mujibu wa Polisi.
Vyuo vya usalama nchini vinajulikana kuanzia Polisi, Magereza, TISS, JWTZ. Wao wamepata mafunzo wapi? Chadema ina chuo cha mafunzo ya silaha kiasi cha kuvamia vituo vya Polisi kulikosheheni bunduki za kila aina?
Kama hawa chuo kama hicho ndani au nje ya nchi, basi tujiulize kusumbua bongo zetu. Nani aliwapa mafunzo wakaiva na hivyo kuwa na uwezo, ujuzi na ujasiri wa kuvamia vituo vya polisi ? Kwani Red Brigade wanafunzwa kuvamia vituo vya Polisi? Usichoke kutafakari....
SASA, moja ya sifa tuliyoambiwa Marehemu Ally Kibao anayo ni kwamba ni Mwanajeshi mstaafu aliyefika katiko vyeo vya juu si kabisa. Kibao alikuwa ni Mjumbe wa Sekretariat ya Chadema lakini pia tunaambiwa kuwa ndiye alikuwa ni "strategist" wa chama na ndio hakufahamika sana majukwaani maana alikuwa "nyuma ya kamera ".
Sijui viapo vya JWTZ vinasemaje ila Kibao baada ya kustaafu alijiunga na CCM na kuwa Mwenezi Mkoa wa Tanga na baadaye kutimkia Chadema hadi alipotekwa, kuteswa., kuuawa na mwili wake kutupwa vichakani huko Ununio (Dar es salaam).
Swali fikirishi! Je, ni huyu (Kibao), strategist, JWTZ mstaafu ndiye aliwapika vijana wa kuvamia vituo vya Polisi? Je, uratibu huu ulikuwa ukiendelea na tuseme Polisi waliamua kujihami kabla ya uvamizi kwa usemi, "mpige mchungaji na kondoo wote watatawanyika"? Haya yote ni kuwaza maana ripoti ya uchunguzi juu ya waliomuua Kibao ni kina nani hasa licha ya alama zote kuonesha ni watu wenye kumiliki pingu ama wa ndani au nje ya nchi. Yote yawezekana.
Je, polisi iko katika operesheni maalum kuzuia wavamizi kabla ya kuvamiwa? Swali linalogonga vichwa ni kwamba kama taarifa za kijasusi zilionesha kuwa MeD ndiye alikuwa "chuo" cha kuwaandaa wavamizi ndiyo auawe badala ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria? Sina jibu....wauaji wana majibu.
Nawaacha na swali hili! Kwa tusiamini kuwa nyuma ya vitendo vya utekaji Chadema haiko nyuma yake kisiasa? Kwa nini hutaki kuamini na kwa nini uamini. Nawatakia tafakuri njema na jadidi. Alamsiki.
PIA SOMA
- TANZIA - Dar: Ally Mohamed Kibao, kiongozi wa chadema auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana
Mashaka ya wengi juu ya Bollen na lengo la hili andiko lake yana msingi yasipuuzwe!Angalau wewe hujaweka mihemko ktk maelezo yako.
Yaonekana umemuelewa kiasi.
Bollen ameweka clue za kutosha kuonesha nani prime suspect wa hilo tukio. Nani walikuwa na 'ugomvi' au tuite most 'probable cause' ya kufanya vile kwa marehemu?
Bollen kajiwekea kinga ile kitu inaitwa 'plausible deniability' akiitwa aweze kukana sikumtaja mtu au taasisi.
Bollen siyo mjinga aitaje taasisi au mtu fulani 'explicitly' kwamba ndiyo muuwaji. Wewe pia wala wengi wetu humu JF au mitaani ndani ya TZ hatuwezi vinginevyo tutaishia jela.
Tanzania tunahitaji kusajiri huduma ya wapelelezi binafsi kuweza kuwabaini na kushitaki watuhumiwa kesi kama hizi zenye maslahi na ........
Muandishi amewasaidia kuweka baadhi ya matukio na sehemu zingine dot au dash kwenye sequence ya matukio, sisi wananchi tuhukumu (hukumu ya umma) au wenye kuweza kushitaki wajaze nafasi wazi kuunganisha hiyo sequence waende mahakamani.
Kama akina mdee walikuwa watumishi wa umma ndani ya chama tuseme nini basi sisi tunao ona huu mchezoMashaka ya wengi juu ya Boleni na lengo la hili andiko lake yana msingi yasipuuzwe!
Kuunganisha kwake narration ya viongozi wa CDM kufanya kikao zoom na kifo cha Kibao sio suala la kuchukulia kiwepesi! Anajua anachofanya! Wewe unafanya kikao Zoom? Kila mtu akiwepo kwake akaingia zoom kufanya kikao cha kujadili masuala ya uhalifu mkubwa kama huo na hao polisi wasiwe hata na clip ya sauti?? Hawa polisi wetu ambao weledi wao huwa unaonekana vizuri sana likija jambo la CDM? Sasa hayo yote sio ya msingi lamsingi ni kuwa kwanini Mwandishi amelikoleza wino sana hili jambo?
Hivi ni kweli hamuoni unafiki anaojaribu kuufanya huyu mwandishi? au kisa amewataja kwa kuibua tuhuma kwa polisi pia? Kila mtu amefanya hivyo kipya kipi anafanya Boleni?
Na hiyo paragraph ya mwisho unaona bado ana lengo la kuchokonoa mada?
Uelewa wako ni mdogo sana. Kwani mimi nimekataa kwamba Mahakama si chombo cha juu kwa utoaji haki nchini? Fuatilia kwanza ujue comment yangu hiyo ilikuwa inajibu kitu gani!!Acha ngonjera zako.
Katiba ya JMT 1977 inasema mahakama ndio chombo cha juu kwa utoaji haki nchini.
Hizo story zako za Marekani hapa sio mahala pake.
Staili ya uandishi; sijui kama hii ndiyo inayo kufanya ujisikie vizuri.Nawaacha na swali hili! Kwa tusiamini kuwa nyuma ya vitendo vya utekaji Chadema haiko nyuma yake kisiasa? Kwa nini hutaki kuamini na kwa nini uamini. Nawatakia tafakuri njema na jadidi. Alamsiki.