Kuiba Misalaba, Mashada ya Maua Makaburini ni Laana

Kuiba Misalaba, Mashada ya Maua Makaburini ni Laana

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
373
Reaction score
829
  1. KWA miaka ya hivi karibuni kuna kukithiri kwa wizi wa mashada ya maua makaburini, na ung'oaji wa misalaba unaofanywa na baadhi ya wananchi kwa Malengo tofauti tofauti.
  2. Katika baadhi ya makaburi ambayo hayalindwi, kumekuwa na aina hiyo ya wizi hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Arusha, lakini kwa sasa hali imeendelea kuwa mbaya, safari hii jiji la Mwanza limekumbwa na kadhia hiyo.
  3. kutokana na hali hiyo, hivi sasa baadhi ya ndugu wanalazimika kuweka alama za mawe kwenye makaburi ya wapendwa wao waliofariki, au misalaba ya mbao ambayo wanadai imekuwa ikiliwa na mchwa na kukosa uimara
  4. Inatusikitisha sana kutokana na vitendo hivyo ambavyo ni sawa na udhalilishaji wa ndugu waliokufa kwa kuibiwa alama zao, ambazo ni muhimu kwa kumbukumbu kujua walikozikwa.
  5. Hali imekuwa ikusishwa na Biashara ya chuma chakavu ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo imesababisha kukithiri kwa biashara hii, ambapo mbali na kung'oa misalaba. wamekuwa wakijihusisha katika biashara ambazo sio rasmi
 
Kwaiyo Na wewe kwa Akili zako ndogo unaamimi hela wanazopata zinaendesha maisha Yao
Watu wanadhani kula na kunywa bila kujali kinachonunua kimetokana na nini ndiyo maisha.

Na watu kama hawa ndiyo wale wakienda magengeni wanaiba nyanya muuzaji akigeuka upande wa pili wakifika nyumbani familia ikala kesho watoto wawili wanaamkia hospital matumbo yanauma akipewa bill Tsh 40,000/= analipa asijue ile nyanya moja ya Tsh 100/= aliyoiiba jana ndiyo imegeuka fimbo yake.
 
Kwaiyo Na wewe kwa Akili zako ndogo unaamimi hela wanazopata zinaendesha maisha Yao
Wanaoiba misalaba ili wauze chuma chakavu mara nyingi ni mateja wasiojiweza.
Akiuza akapata 5,000 hiyo inamtosha kuendesha maisha yake kwa siku hiyo.
Siko hapa kuwatetea ila najaribu kukupa kitu wewe mwenye akili kubwa
 
  1. KWA miaka ya hivi karibuni kuna kukithiri kwa wizi wa mashada ya maua makaburini, na ung'oaji wa misalaba unaofanywa na baadhi ya wananchi kwa Malengo tofauti tofauti.
  2. Katika baadhi ya makaburi ambayo hayalindwi, kumekuwa na aina hiyo ya wizi hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Arusha, lakini kwa sasa hali imeendelea kuwa mbaya, safari hii jiji la Mwanza limekumbwa na kadhia hiyo.
  3. kutokana na hali hiyo, hivi sasa baadhi ya ndugu wanalazimika kuweka alama za mawe kwenye makaburi ya wapendwa wao waliofariki, au misalaba ya mbao ambayo wanadai imekuwa ikiliwa na mchwa na kukosa uimara
  4. Inatusikitisha sana kutokana na vitendo hivyo ambavyo ni sawa na udhalilishaji wa ndugu waliokufa kwa kuibiwa alama zao, ambazo ni muhimu kwa kumbukumbu kujua walikozikwa.
  5. Hali imekuwa ikusishwa na Biashara ya chuma chakavu ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo imesababisha kukithiri kwa biashara hii, ambapo mbali na kung'oa misalaba. wamekuwa wakijihusisha katika biashara ambazo sio rasmi
Kuiba msalaba uliopo kaburini na kuiba fedha zilizotolewa na wafadhili kununua dawa, na watu wakafariki kwa kukosa dawa zilizopaswa kununuliwa, ni kipi chenye laana zaidi?
 
Watu wanadhani kula na kunywa bila kujali kinachonunua kimetokana na nini ndiyo maisha.

Na watu kama hawa ndiyo wale wakienda magengeni wanaiba nyanya muuzaji akigeuka upande wa pili wakifika nyumbani familia ikala kesho watoto wawili wanaamkia hospital matumbo yanauma akipewa bill Tsh 40,000/= analipa asijue ile nyanya moja ya Tsh 100/= aliyoiiba jana ndiyo imegeuka fimbo yake.
Magonjwa kwa watoto yapo tu mkuu! Na wala haihusiani na wizi wa mzazi.
Jisomee hapa chini jamaa kaeleza vizuri
Kuiba msalaba uliopo kaburini na kuiba fedha zilizotolewa na wafadhili kununua dawa, na watu wakafariki kwa kukosa dawa zilizopaswa kununuliwa, ni kipi chenye laana zaidi?
Saint Anno II
 
Inaumiza sana, familia imejipanga kujenga kaburi la mpendwa wao kwa gharama kubwa lakini baada ya siku kadhaa wezi wanaenda kuvunja kila kitu. Wakishindwa kuiba marumaru au chochote basi watavunja kaburi lote. Ni laana mbaya sana.
 
  1. KWA miaka ya hivi karibuni kuna kukithiri kwa wizi wa mashada ya maua makaburini, na ung'oaji wa misalaba unaofanywa na baadhi ya wananchi kwa Malengo tofauti tofauti.
  2. Katika baadhi ya makaburi ambayo hayalindwi, kumekuwa na aina hiyo ya wizi hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Arusha, lakini kwa sasa hali imeendelea kuwa mbaya, safari hii jiji la Mwanza limekumbwa na kadhia hiyo.
  3. kutokana na hali hiyo, hivi sasa baadhi ya ndugu wanalazimika kuweka alama za mawe kwenye makaburi ya wapendwa wao waliofariki, au misalaba ya mbao ambayo wanadai imekuwa ikiliwa na mchwa na kukosa uimara
  4. Inatusikitisha sana kutokana na vitendo hivyo ambavyo ni sawa na udhalilishaji wa ndugu waliokufa kwa kuibiwa alama zao, ambazo ni muhimu kwa kumbukumbu kujua walikozikwa.
  5. Hali imekuwa ikusishwa na Biashara ya chuma chakavu ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo imesababisha kukithiri kwa biashara hii, ambapo mbali na kung'oa misalaba. wamekuwa wakijihusisha katika biashara ambazo sio rasmi
Waambie pia wale wanaofukuwa makaburi kuiba vya mfu, viatu, suit, gold, silver na chochote watakachopata. Wale ma pharaohs Misri, makaburi yao mengi yalifukuliwa na watu wakatajarika!
People don't care about the dead, dead people are alone, their time is finished on earth! Watafaidika na nini hivyo vitu?! You're forgotten as soon as you are under six feet deep under!
 
  1. KWA miaka ya hivi karibuni kuna kukithiri kwa wizi wa mashada ya maua makaburini, na ung'oaji wa misalaba unaofanywa na baadhi ya wananchi kwa Malengo tofauti tofauti.
  2. Katika baadhi ya makaburi ambayo hayalindwi, kumekuwa na aina hiyo ya wizi hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Arusha, lakini kwa sasa hali imeendelea kuwa mbaya, safari hii jiji la Mwanza limekumbwa na kadhia hiyo.
  3. kutokana na hali hiyo, hivi sasa baadhi ya ndugu wanalazimika kuweka alama za mawe kwenye makaburi ya wapendwa wao waliofariki, au misalaba ya mbao ambayo wanadai imekuwa ikiliwa na mchwa na kukosa uimara
  4. Inatusikitisha sana kutokana na vitendo hivyo ambavyo ni sawa na udhalilishaji wa ndugu waliokufa kwa kuibiwa alama zao, ambazo ni muhimu kwa kumbukumbu kujua walikozikwa.
  5. Hali imekuwa ikusishwa na Biashara ya chuma chakavu ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo imesababisha kukithiri kwa biashara hii, ambapo mbali na kung'oa misalaba. wamekuwa wakijihusisha katika biashara ambazo sio rasmi
Biblia inasemaje kuhusu kuweka mashada ya maua,misalaba,kuvisha suti,cheni,Pete marehemu?
Unakuta utaratibh wa mtu mweupe munauleta huku uswahilini ambapo 99% ya watu ni masikini wa kutupwa.
Kama vitu havijaainishwa ulazima wake kwenye vitabu vya dini basi sisi tunaovifanya ndio wapimbavu
 
Tujenge misalaba ya tofali maana watu hawana haya hata kwa marehemu.
 
Siku hizi kunawekwa misalaba ya hollow cavity haina vyuma ni vigae tu ila ni ghali, ipo kwenye makaburi ya wenye uwezo mkubwa wa kiuchumi. Nadhani vigae hivyo vinatoka nje ya nchi maana hata maandishi inaonekana yamechapwa nje ya nchi
 
Kule mexico kuna makaburi ya bei ghali, ni ya wauza mihadarati, yamejengewa vijumba na yanalindwa, ulinzi ni mkali hakuna kibaka wala mwizi kuingia eneo hilo kuiba kwenye makaburi hayo
 
Ukiona hata wafu wanaibiwa vyao ujue tumefika pabaya kama jamii. Sungu sungu irudishwe mitaani kuleta amani.
 
Zamani makaburi yaliogopwa sana, hata mchana tu ilikuwa ni ngumu kupita maeneo hayo yalitisha. Siku hizi kuna vinjia vingi vinakatisha makaburini, kuna watu wanazurura makaburini na mifuko ya salfeti wakitafuta vyuma chakavu na takataka zingine kama chupa za plastiki.
 
Back
Top Bottom