Kuikosoa Serikali ukiwa madarakani ni kazi ngumu mno

Kuikosoa Serikali ukiwa madarakani ni kazi ngumu mno

Kufupisha Uzi nitatoa mfano!

Chukulia ukiwa na njaa Kali, umepigika, jua kali halafu ukapewa lifti ya gari na dreva ambaye katika safari yenu kuna sehemu akakosea!

Kama huwezi kumsema vibaya dereva wako au kumkosoa kwa uderevawake mbovu! Ndivyo ilivyo vigumu kuikosoa serikali inayokulipa mshahara!

Serikali ni tamu sana ukiwa madarakani! Kwanza watu wakilalamika na kuponda unawaona kama mashetani mbele ya malaika!
Ni mfumo wa hovyo sn wanafaidi wachache wengi wanaumia
 
Nilishakua kwenye hari unayoisema, nipo Dodoma naenda Singida, Dereva Mwanamke, anaendesha IT akiitoa Bandalini Dar anaipeleka Rwanda, Akanibeba pale njia Panda, hajalala vya kutosha toka atoke Dar jana yake, saa 8 mchana anaanza kusinzia Barabarani njia nzima anatembea yeye, mara ya kwanza nikamshtua, coz tulikua tunatembea njia isiyo yetu, mara pili akalala tena, nikamwambia mimi nimefanya kazi za Night shift, najua Uchovu ulivyo, nikamwambia paki pembeni ulale hata Dakika 15 tu ukiamka, usingizi utakata.

Akanisikiliza akapaki pembeni akalala kidogo, alivyoamka kawa mpya tukaendelea na safari, akinishukuru!

So ukiwa upo ndani ya Serikali badala ya kuikosoa kuna njia ya kuishauri kupitia Vikao, na isiposikia Ushauri, njia bora ni kujiuzuru.
Tanzania hii wa kujiuzulu atafutwe kwingine
 
Kifupi Watanzania wameshakubaliana na haya maisha, mambo ya viongozi wao hayawahusu sana kikubwa usiwanyime udaku/umbea na mpira...
 
Kufupisha Uzi nitatoa mfano!

Chukulia ukiwa na njaa Kali, umepigika, jua kali halafu ukapewa lifti ya gari na dreva ambaye katika safari yenu kuna sehemu akakosea!

Kama huwezi kumsema vibaya dereva wako au kumkosoa kwa uderevawake mbovu! Ndivyo ilivyo vigumu kuikosoa serikali inayokulipa mshahara!

Serikali ni tamu sana ukiwa madarakani! Kwanza watu wakilalamika na kuponda unawaona kama mashetani mbele ya malaika!
Ni sahihi, nani anakupinga.
 
Kifupi Watanzania wameshakubaliana na haya maisha, mambo ya viongozi wao hayawahusu sana kikubwa usiwanyime udaku/umbea na mpira...
Haha ndiyo maana Mange akabadili gia angani
 
Back
Top Bottom