Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Hapa Tanzania watu wengi huchukulia kujenga na kumiliki nyumba ni hatua kubwa ya mafanikio katika miasha. Wafanyakazi wengi hukopa na kuishi na madeni ya viwanja na nyumba maisha yao yote ili tu wasikae katika nyumba za kupanga.

Pia wafanyakazi wengi wako tayari wasiwe na chanzo kingine chochote cha kipato kwa kuelekeza pesa yao yote wanayoipata katika ujenzi wa nyumba badala ya uwekezaji unaoleta fedha ili tu waishi katika nyumba zao wenyewe.

Katika muktadha wa utaalamu wa kifedha ni sahihi hasa kwa vijana kuelekeza nguvu na pesa zote katika ujenzi badala ya kuwekeza pesa katika biashara ambazo zitazalisha pesa zaidi na baadaye ndipo suala la ujenzi wa nyumba lifikiriwe baada ya kuwa na uhakika wa mtiririko mzuri wa kipato cha uhakika?
 
Biashara ni kipaji na ni hobby pia.

Mimi binafsi nikifanya biashara,siwezi pata kiu ya soda halafu mezani kuna buku naiangalia.

Unawezaona ni kwa namna gani biashara sio fani yangu.

Kingine inabidi tushukuru wafanyakazi wa aina hiyo, maana wanawapisha wasio wafanyakazi nao waishi kupitia biashara, vinginevyo itakuwa ni urafi na roho za ubinafsi.
 
Kujenga nyumba yako ni muhimu, ni muhimu kwa sababu unakuwa na uhakika wa makazi na ni moja ya mahitaji ya msingi ya kibinadamu. Kuna biashara kuyumba ukakosa hata fedha ya kodi ya pango,

kingine tunatofautiana vipaumbele, tunaweza kuwa wote tunampango wa kujenga na kuanziasha biashara. Mwingine akaanza na nyumba kwa ajili ya makazi baadaye biashara na mwingine akaanza biashara baadaye makazi tofauti hizi katika vipaumbele vinaweza kuchangiwa na tofauti ya misingi ya uchumi ya mtu mmoja mmoja

kingine siyo Kila mtu anahitaji kuanzisha biashara
 
Hitaji la nyumba bora za kuishi Tanzania ni kubwa mno, si mijini wala vijijini. Kutokana na hitaji kuwa kubwa, kodi za nyumba hasa mijini ni kubwa sana. Kijana anae anza maisha anatumia 3/4 ya kipato chake katika makazi, hii ni pamoja na kodi, umeme na maji.

Vijana wengi wanawaza kujenga ili aepukane na kodi ili miaka inayofuata aweze kuwa na biashara au uwekezaji mwingine.

ili kutatua hili tatizo, affordable homes mijini zinahijika sana. Nyumba self kuanzia laki moja kwa mwezi, zikipatikana hizi mindset ya vijana zitabadilika.
 
Hapa Tanzania watu wengi huchukulia kujenga na kumili nyumba ni hatua kubwa ya mafanikio katika miasha. Wafanyakazi wengi hukopa na kuishi na madeni ya viwanja na nyumba maisha yao yote ili tu wasikae katika nyumba za kupanga.

Pia wafanyakazi wengi wako tayari wasiwe na chanzo kingine chochote cha kipato kwa kuelekeza pesa yao yote wanayoipata katika ujenzi wa nyumba badala ya uwekezaji unaoleta fedha ili tu waishi katika nyumba zao wenyewe.

Katika muktadha wa utaalamu wa kifedha ni sahihi hasa kwa vijana kuelekeza nguvu na pesa zote katika ujenzi badala ya kuwekeza pesa katika biashara ambazo zitazalisha pesa zaidi na baadaye ndipo suala la ujenzi wa nyumba lifikiriwe baada ya kuwa na uhakika wa mtiririko mzuri wa kipato cha uhakika?
Wewe wekeza kwenye biashara nunua hiace ndani ya mwaka imekujengea wewe tuache masikini tukimbilie nyumba tuishi kwa Uhuru kwa kujiachia tukiondoa wazo la kulipa Kodi.
Ada za watt tunajenga nyumba inasomesha watoto. Yaani kila mtt akiwa na nyumba yake unamkabidhi ndio anaiomba hela mie sipendi kuombea hela.
Yaani namuwezesha kila mmoja anasimama kwa miguu yake.
Yaani ukiniomba hela nenda ukachukue kule Kodi nabaki mie naishi kwa Uhuru Tena ndio nawagongea.
 
Hapa Tanzania watu wengi huchukulia kujenga na kumili nyumba ni hatua kubwa ya mafanikio katika miasha. Wafanyakazi wengi hukopa na kuishi na madeni ya viwanja na nyumba maisha yao yote ili tu wasikae katika nyumba za kupanga.

Pia wafanyakazi wengi wako tayari wasiwe na chanzo kingine chochote cha kipato kwa kuelekeza pesa yao yote wanayoipata katika ujenzi wa nyumba badala ya uwekezaji unaoleta fedha ili tu waishi katika nyumba zao wenyewe.

Katika muktadha wa utaalamu wa kifedha ni sahihi hasa kwa vijana kuelekeza nguvu na pesa zote katika ujenzi badala ya kuwekeza pesa katika biashara ambazo zitazalisha pesa zaidi na baadaye ndipo suala la ujenzi wa nyumba lifikiriwe baada ya kuwa na uhakika wa mtiririko mzuri wa kipato cha uhakika?
Kwa nchi ambayo mifumo yake ya kodi imejikalia kushoto ni ngumu sana kumshawishi mtu akope million 60 akafanyie biashara kisha ndio ajenge kwa faida!

Biashara ambazo zimenyooka kibongo bongo ni chache sana labda upate business ya ku supply materials au equipments! Au supply ya bidhaa ambazo unalipwa on delivery. Ila kunishawishi nifungue biashara ambayo namsubiria mteja aje kwa kudra za Mungu hilo sahau😅
 
Benki au taasisi za umma zingekuwa zina nyumba nyingi na za aina tofauti za kupanga kwa bei nafuu, kusingekuwa sana na mihemko ya kujenga nyumba kwa kila mtu.
Tatizo watu binafsi wanapangisha bila kuzingatia haki na sheria za kupangisha. matokeo yake ni kunyanyasa wapangaji na mara nyingi kuwadhalilisha mbele ya familia zao. Hiyo ndiyo inayofanya watu wengi wajitahidi wajenge nyumba ingawa wataishi maisha ya tabu.
 
Kwa nchi kama TZ nyumba bora za kuishi ni chache sana, hivyo ni muhimu sana kuendelea kujenga hata kabla ya mishe zingine.

Usilinganishe na nchi za watu ambako nyumba za kupanga zipo kila pale, labda na sisi tutafikia huko lakini sio leo.
 
Binadamu Tuna vipao mbele vinavyo tofautiana.
Na Kuna watu wamekuja Duniani kufanikisha maisha ya watu wengine.
Hatuwezi fanya Biashara wote au kuajiriwa wote au kujenga wote.
Na chochote tufanyacho kinafaida kama sio kwangu basi kwa mwingine
 
Biashara ni kipaji na ni hobby pia.

Mimi binafsi nikifanya biashara,siwezi pata kiu ya soda halafu mezani kuna buku naiangalia.

Unawezaona ni kwa namna gani biashara sio fani yangu.

Kingine inabidi tushukuru wafanyakazi wa aina hiyo,maana wanawapisha wasio wafanyakazi nao waishi kupitia biashara, vinginevyo itakuwa ni urafi na roho za ubinafsi.
Unajielewa
 
Biashara kabla ya ujenzi unatakiwa uwe makini sana, biashara ina sayansi yake. Nashauri jenga kwanza huku unafikiria hiyo sayansi ya biashara. Kumbuka katika mahitaji makuu ya binadamu, nyumba ipo ila biashara haipo, tafakari.
Hiyo sentensi ya mwisho izingatiwe
 
Back
Top Bottom