Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

[emoji1787][emoji1787][emoji1787] nijenge wapi bwana hata ya matope sina. Kwanza electronics unamaanisha vitu kama simu na vifaa vyake? Au vifaa vya umeme wa nyumbani? Sijuagi kutofautisha mwenzio

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
Mimi nauza simu na vifaa vyake.

Kumbe mjengo badobado! ukimaliza unifanye kiben 10 basi..
 
Hapa Tanzania watu wengi huchukulia kujenga na kumili nyumba ni hatua kubwa ya mafanikio katika miasha. Wafanyakazi wengi hukopa na kuishi na madeni ya viwanja na nyumba maisha yao yote ili tu wasikae katika nyumba za kupanga.

Pia wafanyakazi wengi wako tayari wasiwe na chanzo kingine chochote cha kipato kwa kuelekeza pesa yao yote wanayoipata katika ujenzi wa nyumba badala ya uwekezaji unaoleta fedha ili tu waishi katika nyumba zao wenyewe.

Katika muktadha wa utaalamu wa kifedha ni sahihi hasa kwa vijana kuelekeza nguvu na pesa zote katika ujenzi badala ya kuwekeza pesa katika biashara ambazo zitazalisha pesa zaidi na baadaye ndipo suala la ujenzi wa nyumba lifikiriwe baada ya kuwa na uhakika wa mtiririko mzuri wa kipato cha uhakika?
Kwa mimi ninavyoona, biashara inahitaji utulivu na maarifa zaidi namna ya kutengeneza faida kupitia hiyo biashara husika sasa utakuta vijana wanawekeza pesa na nguvu kwenye kujenga nyumba zao ili wakiwa huko wapate utulivu kwanza wa akili na mawazo.

Ukikaa kwa nyumba za kupanga kuna muda utulivu wako utakuwa unaondoka kutokana na usumbufu kwa either mmiliki wa nyumba kwani anaweza akajitokeza mtu mwenye kipato zaidi anahitaji nyumba uliyopanga kwa matumizi mengine na mwenye nyumba akakupa notice.

Huwezi kutulia kwenye biashara na kutengeneza faida kama unakuwa mtu wa kuhama hama utakuta faida unayoitengeneza kwenye biashra unaitumia kuwalipa wamiliki w nyumba na ukashindwa kujenga.
 
Aisee bora kujenga kwanza nilijiaminisha kujenga ni uoga wa maisha nikafungua biashara. Ulipita upepo kidogo nikaona nitakosa vyote nikahamia kujenga kwasababu ukiwa na nyumba hata mambo yaende vibaya namna gani nyumba haiwezi kuyumba ila biashara ikiyumba unaweza kuchanganyikana

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Biashara inataka roho ngumu

Kupoteza ni sehemu ya game ila unafanya tena na tena mpaka unatoboa.
 
SASA KITEndo cha nyumba kuwa ni hitaji kuu ndio kinafanya tusianze na ujenzi kwa sababu hata kula ni lazima lakini hakuna anayeenda kukopa pesa benki ili awe anakula tu au yupo ?

Kuoa ni hitajio la muhimu lakini je mtu akienda kukopa benki ili aoe tutamuona mjinga sio ?

KUpumua ni hitaji la muhimu lakini je mtu akienda kununua mitungi ya oksijeni akaiweka ndani ili imsaidie endapo atakosa pumzi tutamuonaje kama sio ni mpuuzi ?,lakini why tumuone mpuuzi ?

Jawabu ni kwamba katika haya maisha hatutakiwi kujikalifisha kwa ajili ya mambo ya lazima,mambo ya lazima yatakuja tu,kwanza tufanye mambo ya hiari alafu yale ya lazima yatajiseti baadae.

Biashara ndio jambo la msingi kwanza
Nakupa maua yako mkuu,
Tatizo ni Woga
Sisi watanzania ni waoga mno,
Hii inachangiwa pia na kujifungia ndani (Tanzania) hatutoki kujifunza wenzetu wanafanyaje biashara, wanaishije, wanapambanaje, wanakabiliana vipi na changamoto.

Tumejifunga mno na tunakatishana tamaa wenyewe kwa wenyewewenyewe na ndio maana uchumi wetu umeshikiliwa na wageni (Wahindi na waarabu)
 
Bora kujenga kwanza kuliko kuanza biashara ambayo hujui hatma Yake itakuwaje.
 
Punguza mikwara, mm nazungumzia gharama za vifaa vya ujenzi sio vyanzo vya pesa vya mtu yaan ata ujengee lwa pesa ya chumajlete bado gharama ya vifaa vya ujenzi bongo ni ghali ..umeelewa hoja yangu ?
HOja yako ni gharama ya vifaa vya ujenzi.

Unalalamikaje vitu bei kali wakati bei hupangi wewe ndugu yangu.

Anayepanga bei ni mfanya biashara kutokana na anavyoiona biashara yake.

Unapolalamika bei ya vifaa vya ujrnzi ni ghali maana yake una bei zako mfukoni ambazo haziendani na bei za wenzio wanaouza vifaa hivyo.

My point ni kwamba hakunaga kitu bei kali,ni kwamba hatunaga hela tu.

Nadhani nawewe umenipata mkuu.😄
 
Sio kila mtu anaweza kufanya biashara,na sio kila mtu ana muda wa kufanya biashara.
Pia,sio kila mtu anaweza kupata ajira, sio kila mtu anakopesheka.
Upepo wako ulipo ndilo chaguo utakaloamua kufanya.
Huwezi kufanya kila kitu na huwezi kuwa na kila kitu.
Ova!
 
NIMEKWAMA NAUZA ENEO LANGU KIBAHA KWA MFIPA.

LIKO SEHEMU NZURI HUDUMA MUHIMU ZIPO.
NGUZO MBILI ZA UMEME MPAKA SAITI.
MCHANGA UKO HAPO HAPO
TOFARI MAPAKA SITE TSH. 750
MAJI YAPO JIRANI TUPO KWENYE MCHAKATO WA KUYAINGIZA
KUTOKA MAIN ROAD KM. 1.5

Square mita 300
Bado sijapata mteja sahihi.
NATAKA MIL. 1.5

0685223804
 
Hapa Tanzania watu wengi huchukulia kujenga na kumiliki nyumba ni hatua kubwa ya mafanikio katika miasha. Wafanyakazi wengi hukopa na kuishi na madeni ya viwanja na nyumba maisha yao yote ili tu wasikae katika nyumba za kupanga.

Pia wafanyakazi wengi wako tayari wasiwe na chanzo kingine chochote cha kipato kwa kuelekeza pesa yao yote wanayoipata katika ujenzi wa nyumba badala ya uwekezaji unaoleta fedha ili tu waishi katika nyumba zao wenyewe.

Katika muktadha wa utaalamu wa kifedha ni sahihi hasa kwa vijana kuelekeza nguvu na pesa zote katika ujenzi badala ya kuwekeza pesa katika biashara ambazo zitazalisha pesa zaidi na baadaye ndipo suala la ujenzi wa nyumba lifikiriwe baada ya kuwa na uhakika wa mtiririko mzuri wa kipato cha uhakika?
Woga wa maisha ndio unapelekea maskini kujenga badala ya kuwekeza wawe na cash flow.
 
Sio kila mtu anaweza kufanya biashara,na sio kila mtu ana muda wa kufanya biashara.
Pia,sio kila mtu anaweza kupata ajira, sio kila mtu anakopesheka.
Upepo wako ulipo ndilo chaguo utakaloamua kufanya.
Huwezi kufanya kila kitu na huwezi kuwa na kila kitu.
Ova!
Sasa kama huwezi kufanya biashara si unawapa hizo fedha wenye kujua biashara wakuletee gawio.
Nunua hisa DSE, nunu vipande UTT, nunua bondi BOT.
Tatizo maskini mmekariri umaskini.
 
Sasa kama huwezi kufanya biashara si unawapa hizo fedha wenye kujua biashara wakuletee gawio.
Nunua hisa DSE, nunu vipande UTT, nunua bondi BOT.
Tatizo maskini mmekariri umaskini.
Sio lazima kila mtu kufanya biashara!
Na sio wote wafanye biashara moja!
 
Nyumba ni asset kama ukiipangisha but ni liability kama ukiishi wewe.

All in all it's all about your dreams and plans and your priorities.
Labda upangishe kwa Foreigners hasa Wazungu, ukipangisha kwa Mswahili Rental Income=Maintenance Costs.
 
Hahaha kama nimekosea unanichana tu sio unanisifia uongo hapa. Upo sahihi kamesa na maelezo yako yana-make alot of sense ila mimi kipaumbele changu ni makazi kwa kweli maana nikiangalia kodi inavyonipaga stress hapana kwa kweli. Unapata kadili kadogo unapata kahela badala ufikirie vitu vya maana unamfikiria mwenye nyumba, kodi huwa inaniuma mimi utadhani nampa ya bure
Hasa kama kodi ya nyumba unalipa kila baada ya miezi mitatu au zaidi. Unampelekea mwenye nyumba sh 900,000 kwa miezi 3 inauma sana. Mimi niliwahi kupanga mahali fulani kodi ya nyumba ilikuwa sh 250,000 halafu Mshahara wangu mpaka makato napata sh 900,000 kwa mwezi. Nilikuwa nalipa kodi ya nyumba sh 750,000 kwa miezi 3. Ilikuwa inaniuma sana, ilibidi nimwombe mwenye nyumba niwe namlipa kodi kila mwezi yaani sh 250,000. Nilipojenga nyumba yangu nilifurahi na ninaishi maisha ya raha sana. Sasa nimejikita kwenye Biashara na Kilimo, siwazi tena masuala ya kodi ya nyumba.
 
Ni liability unless haujaingia madeni kuijenga ndipo uishi nitakupa mfano.

Wewe umepata kazi, mshahara wako ni 1milion. Unapanga nyumba lets say tabata. Kazini ni posta. Kodi ya nyumba ni laki 2. So unabakiwa na laki nane kudeal na expenses na utility za nyumba nje ya kodi. Hapo kutoka tabata ni approximately km 12 hadi kazini kwako posta so mafuta ya gari no cheap plus unaenda na mkeo na watoto pengine unawadrop shule.

Sasa ukaamua kufanya ujenzi, possibility ya kupata kiwanja katika eneo la mzingo wa kipenyo kamili cha duara cha ndani ya KM 30 kutokea hapo tabata ni uongo. Yaani ukienda chanika viwanja ni huko zaidi ya KM 20+ hadi 30 kutoka hapa tabata. Ukienda kigamboni ni maeneo ya umbali wa KM kuanzia 30+ ndipo viwanja vilipo, na ukienda upande wa morogoro road na bagamoyo road ni zaidi ya KM 35+ kupata viwanja.

Haya haya maeneo yenyewe ukienda utaambiwa yanaanza kuuzwa kwa bei za ghafla yaani milioni 5. So lazima ujipange na hiyo pesa. Then ukishalipia hivyo shughuli inabakia kuanza ujenzi. So itakubidi uwe na cash ili ujenzi uende chap au ukakope ili upate cash ya kuanza huo ujenzi.

Then ukimaliza inabidi ufanye kuhamia sasa makazi mapya. Of which itabidi watoto kuhamishwa shule, au kama watabakia shule hizo hizo basi itakulazimu kuingia gharama ya kuwapeleka mwenyewe au wakae boarding.

Then kuna swala la umbali sasa kumbuka sasa hivi utakuwa kwa siku unatembea KM zaidi ya 60+ au hata KM 70+ per day ambayo ukija piga kwa mwezi ni zaidi ya laki 6 kwenye usafiri tu.

Plus kule mji mpya kuna vitu vingi sana utakosa maana wakati wa ujana unatakiwa kukaa na vijana wenzako mpange mishe za maisha na utafutaji.

Sasa utarudi nyumbani saa ngapi kukaa na familia na utakaa na wenzako saa ngapi kuyajenga.

Hiyo laki sita ya kila siku plus unadeni la kumalizia kulipa ndio mwanzo wa mateso umehamia kwako ila stress pale pale na kudhoofu juu ndio maana watu wengi wanaohamia nje ya mji nyakati hizi za ujana mambo huwa yanaishia pabaya sana.

Maisha ni sayansi na hesabu. Tengeneza formula yako ambayo variables zake zitakuwa ni vigezo vyako ili uishi vizuri kipindi chako cha ujana ili uzeeke ukiwa na afya nzuri na ukajenga nyumba yako ya uzee ili ukaishi kipindi cha utu uzima kwa utulivu kabisa huko nje ya mji.

Sio unatoka kukwepa kulipa kodi ya tshs laki 2 unaenda kukaa nje ya mji huko ambao gharama za usafiri tu ni zaidi ya laki 6 kwa mwezi na bado nyumba haijaisha plus madeni ya mikopo unatumia miaka mingi unaishi kwa wasi wasi na maumivu. Wakati hiyo laki sita ungelipa kodi na laki nne ingebakia kusapoti usafiri na gharama zingine za familia plus upo karibu na town so gharama zitakuwa chini.

Hapo ni bidii yako tu kupambana na biashara ndogo ndogo ili uweze kuongeza kipato na kusave kiasi cha pesa cha kutosha kuanza ujenzi na kuumaliza bila kutegemea mkopo popote.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Suppose unajenga hapo hapo Tabata karibu na ulipopanga. Gharama zitakuwaje ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom