Kujenga nyumba ni usumbufu sana

Kujenga nyumba ni usumbufu sana

Tusiwalaumu mafundi tu, hii ni tabia ya watanzania kwa ujumla wetu, huko serikalini ni wizi na ufisadi tu, popote watu wakipata nafasi wanaiba tu.

Muhimu ni, kuwa na ABC za ujenzi, simamia kazi yako mwanzo mwisho, hakikisha unafatilia materials mwenyewe...hii ya kumwambia fundi waambie jamaa walete mchanga fuso moja, waambie washushe tofali 1000 ndio utaanza kuchapwa hapo hapo.
SASA mkuu Kwa wale ambao ubize ni 24/7 inakuwaje?? Yaan hata ukiweka kampuni ya ujenzi inabidi uwepo pia kufuatilia Kama nondo wamelaza Kwa usahihi.

Kuna Ile unafuatilia Ila huna maarifa ya ujenzi haha mafundi wanakutajia vifaa Kwa kingereza mara ringbeam mara sijui vitu gani.....

Kwenye mitaala labda hata na hili somo la mambo ya ujenzi lingekuwepo Kwa sababu katika maisha zaidi ya asilimia 70 ya watu hupitia hatua ya kujenga. Kuliko kujifunza mambo ya mtemi mirambo na chief samore toure

Wenzetu nje wanajengaje?? Hivi wale wakina rashford nawao wanshindaga site kusimamia?? Labda tungejifunza kupitia wenzetu.
 
SASA mkuu Kwa wale ambao ubize ni 24/7 inakuwaje?? Yaan hata ukiweka kampuni ya ujenzi inabidi uwepo pia kufuatilia Kama nondo wamelaza Kwa usahihi.

Kuna Ile unafuatilia Ila huna maarifa ya ujenzi haha mafundi wanakutajia vifaa Kwa kingereza mara ringbeam mara sijui vitu gani.....

Kwenye mitaala labda hata na hili somo la mambo ya ujenzi lingekuwepo Kwa sababu katika maisha zaidi ya asilimia 70 ya watu hupitia hatua ya kujenga. Kuliko kujifunza mambo ya mtemi mirambo na chief samore toure

Wenzetu nje wanajengaje?? Hivi wale wakina rashford nawao wanshindaga site kusimamia?? Labda tungejifunza kupitia wenzetu.

Ukitaka kujenga kwa sasa mkuu ni kukabana site usiibiwe sana(coz kuiba wataiba tu).

Kampuni za ujenzi zina escalate gharama coz kuna mambo mengi kama kampuni wanahitaji kulipa serikalini. So ukiweka kampuni kubaliana na gharama kubwa za ujenzi.

Mafundi wetu sio wabaya kama utawasimamia, lazima ujifunze na kuujua ujenzi, materials, gharama za ufundi, hatua za ujenzi nk.

Ni kweli haya mambo tunayahitaji mashuleni, vijana wafundishwe ABC za ujenzi kuliko historia zisizo na mashiko kwa dunia ya sasa.

Wenzetu serikali zao zinajenga, wewe unapewa mortgage contract utalipia miaka buku haha. Au wale wenye uwezo wanajenga na makampuni, lakini pia swala la weledi na uaminifu kwao ni kila kitu.
 
Ujenzi mgumu sana aiseee sasa material yote yale ununue bado uje kusimamia namna wanavyojenga duh
Tafuta mtu akusimamie, ila ukipata fundi mzuri sio lazima umsimamie. Mara nyingi utasimamia ili vipimo visizidi au vipungue. Mfano jamvi unaeza patana 500k la nchi 5 ila likamiminwa la nchi tatu.
 
Ukiona fundi anakuibia
Ukiona fundi anachelewesha kazi
Ukiona fundi anakudanganya au hafiki site
TAMBUA TATIZO NI WEWE. Wengi mnawanyonya Sana mafundi mnapopatana nao kazi. Boss anaelipa vizuri huwa haibiwi na fundi, boss anaelipa vizuri hawezi kuharibiwa kazi kwasababu fundi ana budget ya kutosha.
Kama unajali maslahi ya fundi Basi nae atajali kazi ya boss.
Sawa Fundi mahiri wa ujenzi
 
Tafuta mtu akusimamie, ila ukipata fundi mzuri sio lazima umsimamie. Mara nyingi utasimamia ili vipimo visizidi au vipungue. Mfano jamvi unaeza patana 500k la nchi 5 ila likamiminwa la nchi tatu.
Huyo wa kusimamia ndo jipu yaani itabidi kabla ujenzi aujaanza mtu upate abc za namna ujenzi unavyokuwa na gharama estimate ya kila material. Ili hata ukimuweka mtu na wewe uwepo aisee
 
Huyo wa kusimamia ndo jipu yaani itabidi kabla ujenzi aujaanza mtu upate abc za namna ujenzi unavyokuwa na gharama estimate ya kila material. Ili hata ukimuweka mtu na wewe uwepo aisee
Toa shaka we tafta fundi muaminifu maana wapo.
 
Juzi kuna fundi nimemuamini nikamuacha sait, kuna mtu nilimuweka aniangalizie. Fundi kamimina shimo kumbe kapunja nondo nyingine kaficha. Nimeshikwa na hasira hapa nina mpango wa kuvunja niongezee nondo nimimine upya. Nimejuta sijawahi kupata hasara mpaka namalizia lakini hii ya sasa hivi kiboko.
 
Juzi kuna fundi nimemuamini nikamuacha sait, kuna mtu nilimuweka aniangalizie. Fundi kamimina shimo kumbe kapunja nondo nyingine kaficha. Nimeshikwa na hasira hapa nina mpango wa kuvunja niongezee nondo nimimine upya. Nimejuta sijawahi kupata hasara mpaka namalizia lakini hii ya sasa hivi kiboko.
Ulimlipa vzr.? 🤣
 
Hii ni mara yangu ya pili kipitia msoto wa ujenzi.Nilipitia hali hii kwa mara kwanza mwaka 2014.

Ni kero sana. Ni kero sana kufanya kazi na mafundi ambao hawako smart. Huyu atakuharibia kazi, huyu atakuibia materials, yule ni muongo kachukua kazi halafu hafanyi. Yaaani kuna kila aina ya kero.

Nimechoka sana. Sasa naelewa kwa nini baadhi ya watu huamua kununua nyumba tu na kuhamia.

Mafundi wengi wanahitaji usimamizi, ukiondoka tu, umepigwa. Wengine huo muda hatuna.
Sijapitia hoi situation lakini ni kweli

Kwa maoni yangu kuna haja na hawa watu kusajiliwa kuwa na ofisi zinazotambulika inakuwa rahisi kuishtaki ofisi kuliko kushtaki mtu mmoja ambaye ni ngumu kumkamata

Hawa watu wengi wao wamekuwa hasa za wizi na uongo , kongole kwa wale waaminifu
 
Hii ni mara yangu ya pili kipitia msoto wa ujenzi.Nilipitia hali hii kwa mara kwanza mwaka 2014.

Ni kero sana. Ni kero sana kufanya kazi na mafundi ambao hawako smart. Huyu atakuharibia kazi, huyu atakuibia materials, yule ni muongo kachukua kazi halafu hafanyi. Yaaani kuna kila aina ya kero.

Nimechoka sana. Sasa naelewa kwa nini baadhi ya watu huamua kununua nyumba tu na kuhamia.

Mafundi wengi wanahitaji usimamizi, ukiondoka tu, umepigwa. Wengine huo muda hatuna.
Nunua appartment , hzi pesa ni makaratasi tuu , NHC , Palm village na kwingineko , ulaya hakuna mtu anayejenga , mashirika yanajenga kazi yako ni kununua ama kupanga ... Ujenzi ni suluba tuuu
 
Mafundi tunadharaulika sana, kwa mujibu wa comment kwenye uzi huu hakuna mtu thamani yake kwenye kazi ni ndogo zaidi ya fundi.
Nashuhudia hilo nikiwa fundi zaidi ya miaka kumi na Tano.

Tunekua watu wakujitoa ili mkae mazingira mazuri na bora sisi mkitupa ujira mdogo, nyie mna baki kwenye nyumba zenu sisi tunaishia kupanga, mnakalia na kulalia furniture nzuri sisi tunalala chini na kukalia vigoda, nyumba zenu zina milango mizuri zetu ni milango ya bati!.

Hela mnazotupa zinaisha kabla ya kazi hata kuisha nyie mna baki kilicho bora sis tunaishia kuwa maskini , hata Asante hakuna mnaishia kututukana na kutubeza!
 
Kutegemea upate fundi ujenzi smart ni sawa na kutafuta bikra wodi ya wazazi!.
Halafu usifanye ujenzi ukawa serious sana utajipa tu stess , we jenga kwa nafasi na kwa ku enjoy, uone how fun it is kushuhudia fundi anaficha mfuko wa cement kwenye rundo la mchanga
Kweli kabisa Mkuu, halafu unakuwa na amani sana ila fundi anajitahidi kufanya kazi vizuri ili asikukwaze.
 
Back
Top Bottom