Uhuru wa kuwa na muda wa kufanya mambo yako nao una umuhimu aisee.
Utamu wa ngoma ingia ucheze, usilewe na maneno matamu ya motivational speakers kujidanganya kwamba kila mtu aliejiajiri anaweza kuamua aamke saa ngapi, aende likizo wiki nzima mbugani, n.k. haya mambo wanaoyaweza ni kundi la watu wachache waliojiajiri, hapa utawakuta kina Mo, Bakhresa, na matajiri wengine walio invest ama kuweza kuajiri watu wa kusimamia miradi yao,
Kiuhalisia huku kwenye kujiajiri kundi kubwa ni day workers, yani hakuna uhuru wa kusema leo nilale hadi saa nne, nipumzike weekend nzima, niende likizo mbugani, n.k. yani kuamka ni almost kila siku asubuhi na kurudi ni usiku, hatupendi lakini inatulazimu
Sisemi kwamba watu waliokoajiri hawana muda huu, la hasha!! wapo watu waliojiajiri na wamefanikiwa katika hili lakini wengi wamejikuta wakiingia katika listi ndefu ya kuwa day workers yani muda wa kuwa huru unakuwa umeminywa sana
Sasa kuna daraja ya kujiajiri ambamo tupo wengi zaidi almaarufu day worker, yani huku stress tupu.
Kujiajiri nako unaweza kuwa mtumwa asikwambie mtu aisee.
Ni mwaka wa tatu huu kwenda ofisini saa moja kurudi saa moja ama mbili ni mwendo mdundo bampa to bampa,
Naweza kusema nna nafuu siku pekee ya kumpumzika ni jumapili tu, nje ya hapo labda krismas na pasaka imeisha hio.
Muda wa kurudi ndio hivyo tena ni usiku yani hata kupata muda wa kuspend na mwanangu unakuwa limited, nikifika mimi nimechoka nae anakaribia kwenda kulala.