Kujiajiri: Wazo sahihi, wakati sahihi, sehemu sahihi na uwepo wa rasilimali sahihi

Kujiajiri: Wazo sahihi, wakati sahihi, sehemu sahihi na uwepo wa rasilimali sahihi

miamiatz

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2017
Posts
505
Reaction score
941
Katika harakati za kujiajiri kuna mambo manne ambayo endapo yataweza kukutana kwa pamoja basi suala la kujiajiri na kukua kijasiriamali litakuwa kama baraka kwako. Mambo hayo ni:

a. Wazo sahihi
b. Wakati sahihi
c. Sehemu sahihi
d. Uwepo wa rasilimali sahihi

Wazo sahihi la biashara ni hatua namba moja ya kufikia mafanikio katika suala la ujasiriamali.

Ila wazo sahihi lililopatikana wakati usio sahihi basi linakuwa sio wazo sahihi tena. Ila pia kama wazo lenyewe limezaliwa wakati sahihi ila sehemu yenyewe sio sahihi basi wazo hilo pia huwa si sahihi tena mpaka litapopelekwa sehemu sahihi.

Kila wazo la kijasiriamali huhitaji rasilimali fedha na rasilimali nyenginezo kutekelezwa. Bila kuwa na rasilimali sahihi basi wazo hubaki kuwa fikra tu.

Kwa wale wanaopambana kujiajiri katika ujasiriamali itakuwa wamewahi jikuta katika mtego huu. Kuna wakati una wazo zuri na linahitaji ulifanye sehemu flani afu unahangaikia kupata ofisi ama fremu katika eneo hilo madalali wanahangaika wanakosa ofisi katika eneo hilo na wanakupeleka mtaa mwingine.

Kama ilivyo shida kupata nyumba ya kuishi sehemu unayoitaka yenye kiwango unachokitaka kwa bajeti uliyojiwekea ndivyo pia ilivyo kwa ofisi ya ujasiriamali.

Kuna wakati unaweza jikuta una mtaji na una wazo zuri na ni wakati mzuri ila sehemu unayopaswa kuliweka wazo lako unaikosa badala yake unapata sehemu nyengine ambayo haifai kwa wazo hilo.

Sasa nini cha kufanya kutatua changamoto hii? Maoni yenu ni muhimu wadau wote wenye uzoefu wa kukumbana na jambo hili. Kwa uzoefu wangu nimejifunza mambo kadhaa wakati wa kutafuta wazo sahihi la biashara:

Kwanza inabidi kuwa na mawazo kadhaa badala ya kuwa na wazo moja hata kama una mtaji mkononi.

Pili mawazo yako ya biashara yanapaswa kuzaliwa katika field yaani katika pita pita zako mitaani badala ya mawazo hayo kuzaliwa ukiwa chumbani ama ofisini kwako. Wazo linalozaliwa katika field ni wazo ambalo unapita sehemu unaona fursa na unaona eneo linalofaa kuweka ofisi yako na unauliza unaambiwa linaweza kupatikana.

Tatu yafaa kujua kila kiasi cha pesa chaweza kuwa mtaji tosha ama kisiwe mtaji tosha kulingana na namna unavyoliunda wazo lako. Kuna ambao kwao laki ni mtaji hali ya kuwa kwa mwingine hata milioni kumi anaona bado sio mtaji bali ni senti.

Nasubiri mawazo yenu wadau mnashauri nini cha kufanya kukabiliana na jambo hili.
#KukuzaMaarifa #KuongezaUstawi #miamiatz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatu yafaa kujua kila kiasi cha pesa chaweza kuwa mtaji tosha ama kisiwe mtaji tosha kulingana na namna unavyoliunda wazo lako. Kuna ambao kwao laki ni mtaji hali ya kuwa kwa mwingine hata milioni kumi anaona bado sio mtaji bali ni senti.



Sent using Jamii Forums mobile app[/QUOTE]
Kiasi utakacho kuwa nacho wakati husika ni bora uangalie mazingira pia sahihi ya biashara ambayo unayoweza kufanya wakati huo tumia hicho kiwango ulichonacho, hii ya kuendelea kuhifadhi ili ufikishe kiasi flani ndo uanze jambo flan wakati mwingine waweza jikuta hata icho kidogo umekutumia, au shida zimetokea ukatumia, then malengo yako ya kuanzisha jambo Fulani nayo uishia hapo
 
Mhh haya ndo Yale Yale ya kilimo cha matikitimaji

Sent using Jamii Forums mobile app
hahaha,inaweza ikawa kweli, japokuwa maarifa pia katika biashara ni muhimu sana, waweza ukawa na capital na kila kitu kama huna maarifa ya swala unalotaka lifanya waweza dondoka mda wowote, Mali bila daftar huisha bila habari( kwaiyo ukijumuisha experience yako ya biashara uliyonayo mtaani plus maarifa mbali mbali unayoyapata either kwenye vitabu, ama majarida ya watu waliofanikiwa kabla yako Mara nyingi hutujenga mkuu). Japokuwa ulisemalo lipo waandishi wengi wa makala za uchumi unakuta yeye binafsi hajawahi jaribu biashara ya aina yeyote ile zaidi ya kuwa motivate wafuasi wengine mahubiri hewa ambayo yeye binafsi hajuwi kama yatatekelezeka ama la
 
hahaha,inaweza ikawa kweli, japokuwa maarifa pia katika biashara ni muhimu sana, waweza ukawa na capital na kila kitu kama huna maarifa ya swala unalotaka lifanya waweza dondoka mda wowote, Mali bila daftar huisha bila habari( kwaiyo ukijumuisha experience yako ya biashara uliyonayo mtaani plus maarifa mbali mbali unayoyapata either kwenye vitabu, ama majarida ya watu waliofanikiwa kabla yako Mara nyingi hutujenga mkuu). Japokuwa ulisemalo lipo waandishi wengi wa makala za uchumi unakuta yeye binafsi hajawahi jaribu biashara ya aina yeyote ile zaidi ya kuwa motivate wafuasi wengine mahubiri hewa ambayo yeye binafsi hajuwi kama yatatekelezeka ama la
Kabisa mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe umeajiriwa au umejiajiri.
Hebu tupe full na ya ukweli experience yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimeajiriwa na nimejiajiri ila kuajiriwa kulikoma mwaka jana september baada ya maradhi kunikubili kwa muda mrefu ambayo mpaka sasa bado napambana nayo. Kiukweli waajiri ni wanyanyasaji sana. Nilipata ajali nikidrive kutokea job kwenda home afu madhara yakawa ndani kwa ndani kwenye uti wa mgongo maeneo ya shingo afu madokta wakasema nipumzike kwa muda mrefu ila mwajiri alikuwa hata nikijaza fomu ya likizo ananuna badala ya kusaini. Kuajiriwa na private companies nako kuna changamoto nyingi sana.

Najuta kuajiriwa na muajiri huyo wakati biashara zangu zilikuwa zikienda hata kabla hajaniajiri.

Nilitaka kufata historia ya Mengi. Miaka kadhaa ambayo mzee huyu alikuwa anaendesha IPP na kadhalika pia alikuwa akitumikia ajira kama Director kwenye baadhi ya taasisi nyenginezo.

Bahati mbaya ajira kwangu ilinidhoofisha na kunijeruhi si kama yeye ilimneemesha na kumuimarisha.

Nahisi mengine ni privacy labda iwe person to person.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeajiriwa na nimejiajiri ila kuajiriwa kulikoma mwaka jana september baada ya maradhi kunikubili kwa muda mrefu ambayo mpaka sasa bado napambana nayo. Kiukweli waajiri ni wanyanyasaji sana. Nilipata ajali nikidrive kutokea job kwenda home afu madhara yakawa ndani kwa ndani kwenye uti wa mgongo maeneo ya shingo afu madokta wakasema nipumzike kwa muda mrefu ila mwajiri alikuwa hata nikijaza fomu ya likizo ananuna badala ya kusaini. Kuajiriwa na private companies nako kuna changamoto nyingi sana.

Najuta kuajiriwa na muajiri huyo wakati biashara zangu zilikuwa zikienda hata kabla hajaniajiri.

Nilitaka kufata historia ya Mengi. Miaka kadhaa ambayo mzee huyu alikuwa anaendesha IPP na kadhalika pia alikuwa akitumikia ajira kama Director kwenye baadhi ya taasisi nyenginezo.

Bahati mbaya ajira kwangu ilinidhoofisha na kunijeruhi si kama yeye ilimneemesha na kumuimarisha.

Nahisi mengine ni privacy labda iwe person to person.

Sent using Jamii Forums mobile app


Pole..hujaumia ubongo lakini..hilo ndo jambo jema!
 
Pole..hujaumia ubongo lakini..hilo ndo jambo jema!
Yeap ubongo upo sawa kabisa. Mkanda wa gari na airbag zinasaidia sana. Kikubwa kilitokea wataalam wa afya huita whiplash injury. Na shingo iliathirika sana bila kujijua sehemu ya uti wa mgongo eneo la shingo iliathirika zaidi na kupelekea ubongo kukosa mawasiliano ya uhakika toka mwili ulio chini ya shingo. Hii hupelekea numbness kwa baadhi ya nyakati, loss of energy, na kuanguka wakati mwingine, pia kushindwa kuconcentrate. But napambana na maradhi kwa kasi sana na bila shaka yataisha mana dalili ni njema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yeap ubongo upo sawa kabisa. Mkanda wa gari na airbag zinasaidia sana. Kikubwa kilitokea wataalam wa afya huita whiplash injury. Na shingo iliathirika sana bila kujijua sehemu ya uti wa mgongo eneo la shingo iliathirika zaidi na kupelekea ubongo kukosa mawasiliano ya uhakika toka mwili ulio chini ya shingo. Hii hupelekea numbness kwa baadhi ya nyakati, loss of energy, na kuanguka wakati mwingine, pia kushindwa kuconcentrate. But napambana na maradhi kwa kasi sana na bila shaka yataisha mana dalili ni njema.

Sent using Jamii Forums mobile app


Utapona naamini..nilimanisha had ukaandika nondo nzuri kama hii ww sio mgonjwa kbs..kila kitu kinaanzia kwenye ubongo ukiulisha kuwa ww ndo wakulala tu kitandani ni kweli utalala kitandani ...nimependa umeamua kuwa postive...Mungu mwema..lakini si unafanya mazoez ya viungo!
 
Utapona naamini..nilimanisha had ukaandika nondo nzuri kama hii ww sio mgonjwa kbs..kila kitu kinaanzia kwenye ubongo ukiulisha kuwa ww ndo wakulala tu kitandani ni kweli utalala kitandani ...nimependa umeamua kuwa postive...Mungu mwema..lakini si unafanya mazoez ya viungo!
Asante sana. Mazoezi yes nafanya na namshukuru Mungu naendelea vyema sana baada ya kuachana na muajiri katili. Na ujasiriamali pia unasonga poa sana tu. Mungu ni mwema.

But pamoja na ukatili wake amenifunza practical administration. Kuongoza watu ni kazi kuliko kuongoza viumbe wengine wote waliopo duniani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana. Mazoezi yes nafanya na namshukuru Mungu naendelea vyema sana baada ya kuachana na muajiri katili. Na ujasiriamali pia unasonga poa sana tu. Mungu ni mwema.

But pamoja na ukatili wake amenifunza practical administration. Kuongoza watu ni kazi kuliko kuongoza viumbe wengine wote waliopo duniani.

Sent using Jamii Forums mobile app


Ni kweli mkuu hilo na mm napitia kwenye hyo changamoto tatizo hatuwazi mamoja..unampata kijana yy hawaz muendeleze biashara ikue anawaza kukupiga tu pesa..dah..!naudhika sana na watu wa aina hii..yy muda wot anawaza kukurudisha chini..Hongera sana..!ukivuka hayo ww ushatoka
 
Ni kweli mkuu hilo na mm napitia kwenye hyo changamoto tatizo hatuwazi mamoja..unampata kijana yy hawaz muendeleze biashara ikue anawaza kukupiga tu pesa..dah..!naudhika sana na watu wa aina hii..yy muda wot anawaza kukurudisha chini..Hongera sana..!ukivuka hayo ww ushatoka
Mimi nadhani njia bora ya kudili na vijana wengi ktk biashara wanayofanya kwa niaba yako ni kama ile ya barber shop ama daladala ama bodaboda etc.

Lazima ulete hesabu ya bosi kila ikifika jioni kinachozidi chukua wewe. Hii inawezekana ktk biashara zote. So inakuwa kama rent vile haulipi unafyekwa. Muhimu biashara anayoifanya uwe na ujuzi nayo kiasi.

Hii hupunguza risks haimalizi risks zote za kupigwa ila hupunguza. Pia kuwa tayari kuona mafanikio ya kijana mana anaweza akawa anapata zaidi ya hesabu ya bosi. Akifanikiwa muombee heri nae akasimame awatoe vijana wengine.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nadhani njia bora ya kudili na vijana wengi ktk biashara wanayofanya kwa niaba yako ni kama ile ya barber shop ama daladala ama bodaboda etc.

Lazima ulete hesabu ya bosi kila ikifika jioni kinachozidi chukua wewe. Hii inawezekana ktk biashara zote. So inakuwa kama rent vile haulipi unafyekwa. Muhimu biashara anayoifanya uwe na ujuzi nayo kiasi.

Hii hupunguza risks haimalizi risks zote za kupigwa ila hupunguza. Pia kuwa tayari kuona mafanikio ya kijana mana anaweza akawa anapata zaidi ya hesabu ya bosi. Akifanikiwa muombee heri nae akasimame awatoe vijana wengine.


Sent using Jamii Forums mobile app

sawa sawa
 
Back
Top Bottom