Kujihisi kuchelewa imefanya wengi wachague bila utulivu na hatimaye kujichelewesha zaidi

Kujihisi kuchelewa imefanya wengi wachague bila utulivu na hatimaye kujichelewesha zaidi

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
Kuchelewa sio nadharia bali kupo ila inatakiwa udhibiti hisia za kuchelewa ili usijipoteze zaidi


Zipo sababu nyingi zinafanya watu wachelewe ila bila kujali kuwa ulicheleweshwa au ulijichelesha ni muhimu kuwa na utulivu zaidi hasa pale unapojiona kuchelewa.

Kushindwa kudhibiti hisia za kuchelewa kumefanya watu wengi wakurupukie gari lolote hata kama haliwafikishi waendapo na yote hii ni hofu inayoletwa na HISIA ZA KUCHELEWA.


Watu wengi hasa wakike wameamua kuolewa na yoyote ilimradi mwanaume kwa sababu tu wamejiona kuchelewa na ile hofu imewasukuma wavamie yoyote hali inayoleta majuto baadaye kwa wengi.


Usipodhibiti hisia za kuchelewa utajikuta unakosea zaidi kwenye maamuzi kwa sababu utachagua kwa pupa ukidhani usipofanya hivyo utakosa tena na hapo utajikuta kwenye chaguo baya zaidi.

Unapojiona tayari umechelewa kwanza kubali huo ukweli kisha tulia ili katika maamuzi yako yasikufanye uchelewe tena zaidi.


#Mwanasayansi Saul Kalivubha.
#Fikia Ndoto Zako
 
Kuchelewa sio nadharia bali kupo ila inatakiwa udhibiti hisia za kuchelewa ili usijipoteze zaidi


Zipo sababu nyingi zinafanya watu wachelewe ila bila kujali kuwa ulicheleweshwa au ulijichelesha ni muhimu kuwa na utulivu zaidi hasa pale unapojiona kuchelewa.

Kushindwa kudhibiti hisia za kuchelewa kumefanya watu wengi wakurupukie gari lolote hata kama haliwafikishi waendapo na yote hii ni hofu inayoletwa na HISIA ZA KUCHELEWA.


Watu wengi hasa wakike wameamua kuolewa na yoyote ilimradi mwanaume kwa sababu tu wamejiona kuchelewa na ile hofu imewasukuma wavamie yoyote hali inayoleta majuto baadaye kwa wengi.


Usipodhibiti hisia za kuchelewa utajikuta unakosea zaidi kwenye maamuzi kwa sababu utachagua kwa pupa ukidhani usipofanya hivyo utakosa tena na hapo utajikuta kwenye chaguo baya zaidi.

Unapojiona tayari umechelewa kwanza kubali huo ukweli kisha tulia ili katika maamuzi yako yasikufanye uchelewe tena zaidi.


#Mwanasayansi Saul Kalivubha.
#Fikia Ndoto Zako
Walipokuwa kwenye hoe phase walirunga basi Haina budi kuhitaji mwanaume anaepumua tu wakishachakaa
 
Hao waliochelewa ni dead balls, hiyo kwetu wakata ufuta ni mipira ya kutenga, hainaga ghasighasi ni kusubiri kipyenga cha Arajiga tu.
 
Back
Top Bottom