Wapo wanaosema hilo ni jini. Nasema hayo ni mapepo tu. Yawe majini au majinamizi yote ni mapepo tu. Ndg yangu, iko kiboko ya hayo yoote. Kwanza jaribu kiila utakachoambiwa humu jf na pale utakapoona vimeshindikana hii yangu haitashindwa.
Lipo jina moja tu, jina lipitalo majina yoote. Hilo jina, mwenye hilo jina amepewa mamlaka yote, mbinguni juu na duniani pia. Huyo mwenye hilo jina aliepewa hayo mamlaka yote, hakufanya uchoyo. Ametupa na sisi yaani ametupa hayo mamlaka, ili sisi tukikutana na mateso kama yako tulitumie hilo jina kwa mamlaka aliotupa litusaidie.
Mfano, ukilipwa mafao yako, hawakupi fedha taslimu. Wanakupa karatasi iitwayo cheki. Imeandikwa kiasi na idara iliyokupa hiyo cheki. Ukienda Benki tu, unaitoa kule unangojea kidogo tu. Mtunza fedha wa benki anakupa mamilioni yako una sepa.
Sasa, huyo mwenye hilo jina ametupa sisi wanadamu watakao muamini kuwa anao huo uwezo, ametupa hilo jina tulitumie.
Linaitwa Jina la YESU KRISTO WA NAZARETI. Weye, ukilitaja jina hilo, hata kwa kuwaza tu; HAKUNA nasema HAKUNA pepo atakaye simama. Hutoweka ghafla.
Kabla hujalala sema hivi; YESU WA NAZARETI UNILINDE. Anza leo uone. Tafuta biblia uusome mstari huu; Luka 10 : 19
ni PM kupata simu yangu. Niite saa yeyote nitakuombea hata kwa mbali wala hutaona taabu hiyo tena.