Kukalia kimya uhalifu ni kutotekeleza jukumu la kiraia

Kukalia kimya uhalifu ni kutotekeleza jukumu la kiraia

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
TUSIUKALIE KIMYA UHALIFU 1.jpg


Watu wengi wanaamini kwamba kupambana na uhalifu ni jukumu la vyombo vya usalama pekee. Lakini ukweli ni kwamba vyombo hivyo haviwezi kudhibiti uhalifu peke yao. Ushiriki wa wananchi katika kupambana na uhalifu ni jukumu muhimu la kiraia na kizalendo.

Miongoni mwa mipango inayoweza kutumika katika kuzuia/kupunguza uhalifu katika jamii ni pamoja na ulinzi shirikishi, mabaraza ya usalama wa raia kwenye mitaa, kuripoti uhalifu kwa siri n.k. Serikali nyingi duniani zinatoa wito kwa raia wake kuripoti uhalifu kwa mamlaka husika. Watoa taarifa za uhalifu na mashahidi ni sehemu muhimu ya uchunguzi wa polisi.

Hata hivyo, pamoja na umuhimu wa kufichua uhalifu katika maeneo yetu, bado kuna mambo mbalimbali yanayowafanya wananchi kutoripoti uhalifu pindi unapotokea au wanapogundua mipango ya utekelezaji wa uhalifu.

Baadhi ya watu huwa na hofu ya kulipizwa kisasi kwa kuripoti uhalifu unapotokea katika maeneo yao au wanapoathiriwa na uhalifu huo moja kwa moja. Kwa mfano, wanaoathirika na unyanyasaji wa kijinsia mara nyingi hupata hofu ya kulipiziwa kisasi na hivyo kulazimika kunyamaza.

Pia, watu ambao wana imani ndogo na mfumo wa haki, wakiamini kuwa haufanyi kazi au hautafanya kazi vizuri, wana uwezekano mdogo wa kuripoti uhalifu. Lakini pia kuna wengine huwa wanapata uzito kuripoti uhalifu kwakuwa wanawafahamu wahalifu na hivyo wanawalinda kutokana na ukaribu au mahusiano yaliyopo kati yao.

Hata hivyo, kwa sababu yoyote ile, si sawa kunyamazia uhalifu unaotekelezwa kwa wengine kwani mhalifu akimalizana na mhanga mmoja kuna siku anaweza kukufikia mwenyewe au watu wako wa karibu. Kutoripoti uhalifu unaotekelezwa kwako moja kwa moja ni hatari kwani anayekutendea hatoacha na kuna hatari ya kuwaathiri wengine.

Ukiogopa kuitwa "snitch" kwenye jambo linaloweza kusababisha hatari au hasara kwa wengine, basi wengine nao watakaa kimya kwenye jambo linalokuhusu na uhalifu utaendelea kushamiri. Ikiwezekana ni vema kutafuta namna ya siri kuripoti.

Ni nuhimu kujijengea utamaduni wa kuwa sehemu ya mabadiliko chanya katika jamii zetu kwa kuhakikisha kuwa hatukalii kimya matendo maovu tunayoyashuhudia au kuyasikia. Hili ni jukumu la kiraia na linapaswa kutekelezwa na kila mmoja wetu. Haijalishi ni nini kilitokea au ni lini, uhalifu wote ni mbaya na unaweza kuacha makovu yasiyofutika katika jamii.
 
"Imani ndogo kwa mfumo wa haki" Rushwa, Rushwa, Rushwa. Baada ya siku mbili mhalifu yupo mtaani kuja kumalizana na wewe.
 
Unaenda kuripoti, Afu afande anamwambia, mhalifu kuwa aliyekuripoti ni fulani, kesho unapigwa chuma unaondoka
 
Polisi ndio chanzo cha uhalifu nchini bila Polisi hakuna uhalifu, nadhani mtanishangaa!

Iko hivi, Polisi hasa hawa wa vituoni askari anatoka depo leo kesho anataka kuendesha mark x crown au subaru anataka starehe zote za dunia hii apate yeye sasa huyu akimpata mhalifu atamchukulia hatua wakati anampea pesa ya kuishi anavyotaka?

Kuna wakati huwa nawaza wale askari wa kwenye Biblia waliokuwa wanasemwa na Bwana Yesu wote hao wapo hapa Tanzania! Maana hawatosheki na mishahara yao wanakula rushwa, wanabambika kesi ni waongo na hatimaye mauaji ya wasio na hatia na kisha kuwabambikia kesi na kuchukua silaha kwenye maghara ya vidhibiti kwamba wameua jambazi mwenye silaha wakati ukweli ni kwamba wamedhulumiana mgao wa deal!

Raia nasisi tunaunga mkono uhalifu wa polisi kwa kuamini hawakosei taarifa inasema wameua jambazi raia tunalipongeza jeshi la polisi bila hata kujua ukweli wa walichotangaza.

Tunangojea mabadiliko makubwa kwenye idara hiyo ndipo tutoe ushirikiano na si vinginevyo.
 
Polisi ndio chanzo cha uhalifu nchini bila Polisi hakuna uhalifu, nadhani mtanishangaa!

Iko hivi, Polisi hasa hawa wa vituoni askari anatoka depo leo kesho anataka kuendesha mark x crown au subaru anataka starehe zote za dunia hii apate yeye sasa huyu akimpata mhalifu atamchukulia hatua wakati anampea pesa ya kuishi anavyotaka?

Kuna wakati huwa nawaza wale askari wa kwenye Biblia waliokuwa wanasemwa na Bwana Yesu wote hao wapo hapa Tanzania! Maana hawatosheki na mishahara yao wanakula rushwa, wanabambika kesi ni waongo na hatimaye mauaji ya wasio na hatia na kisha kuwabambikia kesi na kuchukua silaha kwenye maghara ya vidhibiti kwamba wameua jambazi mwenye silaha wakati ukweli ni kwamba wamedhulumiana mgao wa deal!

Raia nasisi tunaunga mkono uhalifu wa polisi kwa kuamini hawakosei taarifa inasema wameua jambazi raia tunalipongeza jeshi la polisi bila hata kujua ukweli wa walichotangaza.

Tunangojea mabadiliko makubwa kwenye idara hiyo ndipo tutoe ushirikiano na si vinginevyo.
Huko ndio kumeoza kabisa na hata kunuka
 
Wahalifu wanajulikanaga kila eneo ni vilee tu wanawaogopa una uhakika wewe unayesoma comment hii hauwajui vibaka wapolaji mtaani kwenu au hauwajui wauza unga mtaani kwenu ni vile tu mnawaogopa; natuma salamu kwa chinja chinja wezi cha kitongoji changu; maliza hao wote naona washaanza kujiachia sasa wamesahau
 
Back
Top Bottom