Kukamatwa Juzi kwa Kato Rasta Muuaji wa Afande Muna Kawe ni jibu tosha kuwa huwezi Kuikimbia popote pale Jamhuri kama ikikutaka

Kukamatwa Juzi kwa Kato Rasta Muuaji wa Afande Muna Kawe ni jibu tosha kuwa huwezi Kuikimbia popote pale Jamhuri kama ikikutaka

Kwa akili zako,mlinzi atategeshea tochi inawaka! Imekuwa taa? Mlinzi wa tochi,uwezo huo hana. Na akifanya hivyo ujue punguani.
Mbona yupo mlinzi wa hivyo.
Akakamata wezi alikuwa analinda maduka ya spare.

Kwamba mlinzi wa tochi hawezi fanya hivyo? Kwanini awezi?
 
Simple tricks from my own knowledge


Ckuzote cmu huonyesha mahali ulipo, especially tz you can escape easily mtego wa kukamatwa na PT/ TISS

First switch VPN
You can buy new phone
Or
Change cmu card while your phone on vpn through WiFi
Then communicate through internet call (chat & call through telegram )

Pesa zote ziamishie binance uwe na crypto currency tuu USDT , huduma zote lipa kwa mfumo huo

Usijarbu ku withdrawal pesa bank au kwa agent kwakutumia details zako
Unajidanganya bure kabisa.
 
Tunatakiwa tufahamu kuwa duniani kote mhalifu anayetafutwa (hata mimi na wewe ikitokea ,Mungu aepushe ) hukumbwa na vitu viwili vikuu ambavyo ni :

1) Hofu (Fear): ni hali ya wasiwasi inayompata mtu au mnyama mbele ya mwingine au kingine kisichompendeza au kuhatarisha usalama wake.


2) Woga (Paranoia/ Anxiety) (Naomba nirekebishwe): ni tabia ya kupatwa na hofu kupita kiasi inayokuwa ndani ya binadamu juu ya kitu au vitu fulanifulani.

Hivyo vitu viwili hupelekea kufanya makosa ya kimkakati ambayo vyombo vya dola huvitumia kama faida kwao! Ukiwa na hivyo vitu ni lazima narudia tena ni lazima utafanya makosa.

Moja ya mafunzo ya kijasusi na machache kwa vyombo vya dola ni kukuondolea hivyo vitu vikuu viwili na kukupa vitu vipya! Baada ya kuondolewa hivi vitu huwa wanaweza kuhimili hali zote! Mimi na wewe hatuwezi!

Mfano 1: mwangalie Kikwete na marehemu Magufuli reaction zao kuhusu jambo lolote, utagundua mmoja amekasirika mwingine anatabasamu.

Unaweza kuona huyu aliyekasirika ni jasiri kumbe ni kinyume chake! Mwingine ana hisia mwingine anaigiza hisia!

Mfano 2: Mwangalie Putin na Kim wa Korea Kaskazini, namaanisha kampe taarifa Kim kuwa wanajeshi wako 1000 wamekufa halafu nenda kwa Putin kampe hiyo taarifa!

Nb: 1) Hisia hupelekea kufanya makosa!

Nb 2) Mhalifu siku zote huwa mwoga!

Nb 3) Dola halina hisia ila watu wake wana hisia!

Ni mtazamo wangu!


"The escape man is still human, he is still afraid, Fear becomes paranoia, paranoia ultimately psychosis. I bring this up because in one hundred and forty years, the fundamental mind of the escape man has not changed "- FBI Special Agent Alexander Mahone (Prison Break)
Hapo mmoja anacheka na mwingine anakasirika ni tabia za Introvert na Extrovert people.

1. * Extrovert people huwa ni rahisi sana kumuelewa akiwa amekasirika au amecheka, amefurahi au amehuzunika sababu huwa mara nyingi wakl free/open minded ndiyomaana wako hujichanganya popote duniani au katika jamii yoyote.

* Extrovert people pia huwa ni wepesi sana kusamehe na ikiwa wamekwazwa hawaoni shida kutafuta suluhisho hata kushirikisha Mtu/Watu apate ushauri.

* Extrovert huwa hawapendi kukaa kipekee pekee bali hujichanganya katika Jamii na rahisi sana kufiti katika nyanya yoyote haswa kibiashara, utangazaji, usanii, ushawishi n.k.

2. * Introvert people wako kinyume na tabia hizo zote hapo juu za Extrovert.

* Introvert people wanaweza wakakwazwa na usiwajue kabisa maana huwa ni Watu wa kuficha hisia zao na huwa hawaishiwi visasi na maamuzi yao huwa ni ya kibabe maana huwa hawaombi ushauri kabla ya vitendo.

* Introvert ni hard workers, risk takers, innovators, hawaaminigi kabisa kuna kushindwa katika kutimiza ndoto zao wako radhi kugharamika kwa namna yoyote ile.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Angedakwa tu. Simple scenario ingekuwa hivi; lazima angekuja kukatiza mahali penye public CCTV kama stendi au benki; in a matter of seconds, picha yake ingekuwa compared against picha zake zilizo kwenye kanzidata tofauti including NIDA, mitandao ya simu, etc. Ingejulikana day fulani alikuwa mahali fulani na nguvu ingeelekezwa huko.

Kwa dunia ya leo ya teknolojia, vijana waache usela mavi! Wawe raia wema wala hutaona ukifautiwa na yeyote. Ukileta ujinga; siku zako wala sio nyingi - utaishi kwa tabu, mateso, na hofu sana duniani humu.
Nakataa, PT hawajafikia level hiyo ya kutumia facial recognition technology kubaini wahalifu Kwa kutumia CCTV cameras ahilia mbali tu kutumia fingerprint kubaini wahalifu.

Ni sehemu ngapi Zina CCTV camera za mitaani huko mikoani?

Yani askari wa bongo wanafika kwenye crime scene lakini hakuna forensic investigation yoyote inafanywa. Kiufupi jeshi la poilisi Tanzania bado Wana safari ndefu mara nyingi wanakisia tu
 
Huyu mwamba alifia angani alivyoruka mkuu according to FBI.
FBI hawana proof ya Hilo ,ni wazushi .Huo mwili wake waliuona ?
Au zile pesa alizochukua ?
Au parachute alilolitumia kuruka toka kwenye ndege ?
FBI hawana majibu ya hivyo vitu mpaka leo
 
PT hawa hawa walioshindwa kuwakamata washambuliaji wa Lissu?
Hawa hawa ninaowajua mimi?
Intel mbovu za PT, Tiss, na Jw mpaka majasus ya Rwanda yanaingia nchini yanateka na kuondoka na watu 5 wa familia moja?
Usipime taasisi za serikali kwenye mambo ya siasa mdogo wangu. Kwenye siasa, akili, weledi na imani vinakaa pembeni.

Kuhusu Rwanda wala sio ajabu, unajua intel yetu inawafanya nini kwao?

Anyway, tufanye Kagame ni noma, so kama anaingia na kuua Marekani, SA nk sisi ni nani?
 
Acha ujuaji WA kijinga , kuna Kato mnyiramba ?
Unajua maana ya kina Kato kwa kihaya na luganda ?
Halafu huyo kijana si alikuwa ameshakamatwa kitambo ?
Si wewe uliwahi kusema humu kuwa ameshakamatwa alipokuwa anaenda kufuatilia pikipiki yake iliyoibiwa huko Mwenge ?
Kaka Hivi KKK ulihitimu vizuri
 
Hata asingetumia simu kama bado alikuwa ndani ya nchi angekamatwa tu. Pia idea ya kukimbilia kijijini ni idea mbovu kwasababu wanakijiji wote wanajuana na akitokea tu mgeni wanaanza kuulizana. Hakuna namna ambayo serikali ya Tanzania ikutake halafu isikupate ukiwa ndani ya nchi. Na hata ukitorokea nchi nyingine wanaweza shirikisha interpol ukakamatwa.
 
Kuna kuishiwa pesa unapiga simu nyumbani usaidiwe nauli.....hela kula ...unaweza kujikuta uko mganga miezi 6 umeishiwa oohhh
Unabadili location kama Osama.... yaani mfano upo singida mjini basi unaenda hadi shelui kupiga simu tena ya maelekezo tu kuwa wakutumie pesa. Unaenda itolea Kiomboi alafu unarudi hadi Ikungi!! Ukienda zig zag hivyo na ukatumia mtu wa pili kuongea na mtu wa pili wa ndugu yako basi hawakudaki.

Pia mnatumia calls sio SMS, ni rahisi ku intercept messages kuliko calls unless wawe guaranteed utapiga. Sasa unaweza tumia namba geni ukapiga namba ya dukani kwa mangi jirani na kwenu apeleke simu uongee na ndugu yako. Hapo hawakudaki hata iweje maana sidhani polisi wana database ya number zote hadi street level, data analysts wenyewe hawazidi 10 ndio sembuse kutrack number za mtaa mzima?
 
FBI na utabe wao kwenye issue za criminal investigation ,walishindwa kumnasa The legendary Dan Cooper mpaka leo
Sometimes vyombo vya dola hupata changamoto sababu michoro yote na namna ya upenyo hunajisiwa na wasio waaminifu miongoni mwao.

Mfano ile misheni ya benki ya Brazil kuibwa pesa na Majambazi unadhani ni akina nani haswa waliotoa ramani hadi wakachimba chini Kwa chini wakatokea benki?

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Apo mmoja anacheka na mwingine anakasirika ni tabia za Introvert na Extrovert people.
Ngoja nikuulize swali.

Kati ya Kikwete (jasusi) na marehemu Magufuli unahisi nani anaweza kumuiga mwenzake halafu usoni usione mabadiliko?

Yaani wote wacheke, wakasirike, walie n.k. Namaanisha hivi hapa kuna mmoja amefundishwa kuishi kulingana na mazingira na hali fulani, huyu mwingine huendeshwa kihisia zaidi!

Kumbuka jasusi hana hisia kwani huambiwa kuwa hisia huiondoa akili katika kufanya maamuzi sahihi! Hisia anatakiwa kuwa nazo raia na siyo dola!
 
Tatizo la Rasta katumia simu na ukitumia simu kwenda kwa mnara ulio karibu ya eneo aliopo.

Sasa hapa polisi ndio wanajua Rasta yupo eneo gani nao wanatuma picha yake kwa polisi wa eneo husika.

Kama Rasta ange wacha wapigia simu watu wake wa karibu mbona asinge patikana milele.
Hili ndio jibu walimpataje ukifanya any network connections with your buddy shughuli ingekwisha angesepa zake hata msumbiji or malawi and change all his identity wasingeweza tena possible masela wake ndio waemchoma kwa mwela
 
Ukitaka upotee unapotea na hakuna wa kukukamata. Hata ulaya leo hii watu wanafanya matukio na wanapotea na hawajulikani walipo na wako hai sembuse Tanzania.

Vijana wanafanya makosa, wanatumia simu kuwasiliana na ndugu na jamaa zao na kuwapa location wako wapi wanafanya nini inakua ni rahisi kukufuatilia.

Ukitaka upotee kwanza achana na vifaa vya kielektroniki. Acha kuwasiliana na ndugu na jamaa wasijue uko wapi na unafanya nini. Ndugu zako wasiliana nao kwa facebook tu na sio normal call.

Kaa miezi kadhaa watafte kwa simu ya mtu mwingine wajulishe uko hai na siku hiyo hiyo hama hilo eneo ama mkoa.

Njia ya pili ni kupotelea nchi jirani. Kwa mfano kwa Tanzania kimbilia Kenya ndio rahisi. Potelea huko kabisa.
Nakubali mwamba.
 
Unabadili location kama Osama.... yaani mfano upo singida mjini basi unaenda hadi shelui kupiga simu tena ya maelekezo tu kuwa wakutumie pesa. Unaenda itolea Kiomboi alafu unarudi hadi Ikungi!! Ukienda zig zag hivyo na ukatumia mtu wa pili kuongea na mtu wa pili wa ndugu yako basi hawakudaki.

Pia mnatumia calls sio SMS, ni rahisi ku intercept messages kuliko calls unless wawe guaranteed utapiga. Sasa unaweza tumia namba geni ukapiga namba ya dukani kwa mangi jirani na kwenu apeleke simu uongee na ndugu yako. Hapo hawakudaki hata iweje maana sidhani polisi wana database ya number zote hadi street level, data analysts wenyewe hawazidi 10 ndio sembuse kutrack number za mtaa mzima?
Dah; kwa "ujanja" ulioeleza hapo utadakwa mapema sana. Uhusishe wote hao hadi akina Mangi uwe salama? Hamna kitu kama hiko.
 
Back
Top Bottom