Kukamatwa kwa Mtanzania Kiongozi wa Waasi nchini Msumbiji: Kwanini hakuripotiwi na Vyombo vyetu?

Kukamatwa kwa Mtanzania Kiongozi wa Waasi nchini Msumbiji: Kwanini hakuripotiwi na Vyombo vyetu?

Frustration

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
3,134
Reaction score
4,124
Habarini za Asubuhi Watanzania wenzangu, BBC wameripoti kupatikanika kwa kiongozi wa waasi ambaye ni raia wa Tanzania.

Vikosi vya jeshi la Msumbiji vinasema kuwa vimemkamata kiongozi wa kijihadi, raia wa Tanzania, katika wilaya ya Nangade kaskazini mwa jimbo la Cabo Delgado.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 39, anayejulikana kama Ali, alikamatwa pamoja na wanamgambo wengine wa Kiislamu sita wenye uhusiano na kundi la Islamic State, maafisa wa kijeshi wameeleza.

Amesema alikuwa mmoja wa viongozi wa wanamgambo ambao kazi yao ilikuwa kuajiri wapiganaji na kutekeleza mashambulizi ya moja kwa moja.

Kukamatwa kwake kunakuja huku kukiwa na hali mbaya ya usalama katika wilaya hiyo, na mfululizo wa mashambulizi ya wanajihadi katika siku za hivi karibuni.

_122855448_306b97d8-4542-4095-9cdc-e3e6784f277c.jpg
 
Serikali ilipotumia nguvu kupambana na huu ugaidi kule kibiti,kama kawaida wanasiasa wa upinzani walilitumia tukio lile kama agenda ya kutafutia kick za kisiasa.

Tulifikia mahali Polisi wanavamiwa vituoni mchana kweupe.
Askari wanavamiwa kwenye vizuizi mchana kweupe na kuuwawa kama kuku.

Tukafikia mahali kuwa mwenyekiti wa serikali ya kijiji huko kibiti ni kosa na unauwawa.

Serikali ilipolivalia njuga hili kundi na kufanikiwa kulidhibiti ndio likatimkia huko Mozambique[emoji1174].

Tanzania [emoji1241] kila kitu tunapiga domo, kila kitu ni ujuaji.

Kwa hili tukio kuna la kujifunza hapo kwa jamii yetu.

Na sijui kwa nini Media za Tanzania [emoji1241] zinakuwa na umbeya badala ya kutuletea habari.

Wao wanakaa kudandia lift kwenye magari ya wakubwa kwenda kuwajenga kisiasa kwa kupewa vibahasha vya khaki.

Kisha taarifa za habari zinajaa siasa tupu.

Makonngamano, Warsha, Uzinduzi, Uteuzi na kisha Migogoro ya wakulima na wafugaji.

Hatuoni media kwa mfano ikimtafuta waziri wa Nishati na kumuweka Interview atuambie sababu ya kuzuka ghafla kwa tatizo la umeme nchini?

Lini na nini hatma yake?

Na vitu vingine kama hivyo vyenye kuigusa jamii.

MEDIA Tanzania [emoji1241] ni kanjanja tupu 75%.

Huko online media nako TCRA imepakalia kimya huku kukiwa na madudu tupu.

Wao TCRA wanamuona Polepole tu.
 
Serikali ilipotumia nguvu kupambana na huu ugaidi kule kibiti,kama kawaida wanasiasa wa upinzani walilitumia tukio lile kama agenda ya kutafutia kick za kisiasa...
Something noted here, Paskal atatuambia kwa nini siku hizi tendency ya waandishi habari kuwahoji viongozi wenye dhamana imepungua?
 
Sawa kabisa hata hizo walizoshikilia mikononi nazo ni za ovyo ovyo tu!
Kwamba ni silaha mdebwedo? Technically Africa kivita bado sana na tunatumia mbinu zilezile za UP yaani Ujanja wa Polini. Technique hizi hata mgambo mtaani wanajifunza.
 
Back
Top Bottom