Kama picha tuu inadhibitisha ugonjwa wa mtu, basi ile picha ya Jangwani na kule Mwanza ya kupiga mweleka ndiyo ungekuwa udhibitisho mahsusi wa ugonjwa. Tena ule ambao watu wanakatazwa kusogelea jikoni.Ukisoma huelewi basi hata picha huoni?
Lowassa ameonewa kabisa,huyu bwana anafanya siasa za kimataifa kabisa kama marekani,tunaona wagombea wa urais marekani wanaanza harakati zao ndani ya chama muda mrefu sana na kujiandaa vyema...lakini kwa ccm siyo.yaani unamtaka yule ambaye atawafumbia macho....katika kundi hilo waote pale maamuzi yao yanatabirika....lowasa pekee ndiye alikuwa maamuzi magumu ambayo wakuu wa ccm hawapendi.....
Namshauri Lowassa.....nenda upinzani hasa Ukawa maana wana fremwork saffi.....ushinde urais...utapata kura za kumwaka ambazo watashindwa kuiba.
Masikini Mr. President
Wanabodi,
CC ya CCM, imefanya kazi yake, imelikata jina la kipenzi cha wengi, Edward Ngoyai Lowassa!.
Jee kukatwa huku ndio mwisho wa ile safari ya matumaini, au ndio mwanzo wa safari ya kweli ya matumaini, kwa kipenzi cha watu, kuanza rasmi safari ya ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, kwa kuipeleka rasmi CCM kaburini?
Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, aliwahi kusema, upinzani wa kweli, utatoka CCM. Jee hiki ndio kipindi cha upinzani huu?
Kwa miaka 50 sasa, Watanzania tumelogwa na jinamizi la CCM kiasi cha kuamini mgombea wa CCM ndie automatically atakuwa rais wa Tanzania!. Wanaopiga kura sio CCM bali ni Watanzania!. Kama Lowassa ndie chaguo la watu, CCM wakaamua kumkata, jee sisi ambao ndio watu, tumchukue Lowassa, kupitia chama kingine chochote tumuingize ikulu?
Jee Lowassa tuliombatiza jina la mwamba, ataliishi hilo jina la mwamba kwa kuonyesha umwamba wake kwa kutokubali kuchinjwa na kufanywa mbuzi wa shughuli, au lile jina la mwamba, tulimpachika tuu, ila in reality kumbe sii mwamba lolote wala chochote, bali ni kichuguu tuu?
Mimi bado ni muumini wa andiko hili lisemalo "Jiwe Walilolikataa Waashi, Litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni!", jee Watanzania tuendelee kuwatumainia hawa waashi wa CCM kuamua hatma yetu na taifa letu, au tumchukue mtu wetu na kusindikiza ikulu nje ya CCM?
Nauliza tena, jee huu ndio mwisho wa safari, au mwanzo wa safari ya kweli ya matumaini kwanza kwa kuingoa CCM na kuikomboa Tanzania?
Pasco!
Pasco
Najiuliza;
Yaliyotokea Kenya yanaweza kutokea Tanzania?
Daniel arp Moi alimpiga panga Makamu wake, Emilio Mwai Kibaki, akamteua Uhuru Kenyatta.
Mwai Kibaki akajiuliza; kulikoni?
Akajiengua KANU, akawaachia Moi na Kenyatta chama chao..
Akaunganisha nguvu na wapinzani,na wakawashinda Rais Moi, Kenyatta na KANU kwenye sanduku la kura.
Hali hiyo yaweza kuja Tanzania?
Edward Ngoyai Lowassa aungane na UKAWA kuiangusha CCM?
HAKIKA, UTABIRI WA BABA WA TAIFA UTAKUWA UMETIMIA[/QUOTE
Natamani iwe hivyo
Kwani itaisha saa ngapi ama lini ili na mimi niagize maji ya kandoro na mahindi ya kuchoma ya kutosha pamoja na ndimu na chumvi ya pilpili.
Kichwa cha habari hapo juu chahusika!
1. Andaa mkutano wa hadhara hapo JANGWANI, Kwenye huo mkutano hakikisha Unamwaga MBOGA, UGALI, MAJI YA KUNAWA NA yA KunYWA! mwaga kila kitu usibaki hata kimoja!
2. Hakikisha Unawaomba radhi na kutubu madhambi yote mliyowafanyia "watanzania" tangu uhuru ilipokuwa ccm!
3.Hakikisha Unaongozwa sala ya toba na hapo hapo uwanjani na mchungaji yeyote utakayemwandaa kwa ajili ya tukio hilo(hili ni muhimu sana ili kuzawaliwa upya baada ya kumtumia shetani(ccm) kwa muda mrefu!
4.Baada ya kukamilisha taratibu hizo hapo juu OMBA UKAWA WAKUPOKEE KWA MIKONO MIWILI na UPEWE KADI AMA YA CDM/CUF/NCCR-MAGEUZI/NLD!
5.Baada ya hiyo no4 sasa washukuru UKAWA na wananchi kwa ujumla na utangaze msimamo wa KUMUUNGA MKONO MGOMBEA WA UKAWA!
Mwisho, baada ya hatua zote hizo hakika utakuwa kiumbe KIPYA NA hakuna wa kukuita KUBWA LA MAFISADI TENA!
KARIBU UKAWA-SAFARI YA UHAKIKA KUELEKEA WHITE HOUSE MAGOGONI.
Walioimba ufisadi wa Lowassa ni CCM.
Mara kuvua gamba, n.k.
Sikumbuki popote Wapinzani walipomtaja Lowassa kuwa ni fisadi.
Ufisadi ndani ya Chama cha Mapinduzi ni MFUMO RASMI.
UKAWA wasipompokea Lowassa, maana yake ni kwamba hawataki kuuondoa madarakani mfumo wa ufisadi.
Tatizo letu ni mfumo, siyo watu au majina ya watu.
Kama kweli Ukawa wanaitakia mema nchi yetu, basi naamini wako kwenye kikao na Lowassa hivi sasa.
Mungu ibariki Tanzania.
by Mmawia;
Hilo pia neno mkuu
Mkuu Mmawia nakushukuru sana kamanda!
Mamvi kama anataka kujiunga na jeshi la ukombozi lazima atubu na amwage yote!
Huu ndio muda wa maamuzi MAGUMU Anayosemaga yeye ni mzee wa maamuzi magumu!
Ha ha ha ha kweli mkuu halafu huenda yakanipa shida wakati wa kushusha mzigo.Hii ni Tamthilia mkuu siyo picha la kawaida lenye part 1 & 2, hayo maji ya Kandoro na mahindi ya kuchoma yatakuumiza tumbo bure, maana mwisho wa hii movie haujulikani. Hii ni kama ISIDINGO!!!
Nimejikuta nacheka tu
Kwa kuwa Slaa ni Padre, hiyo kazi ya kumbandikia mikono na kumsalisha sala ya toba angeifanya yeye