Kukosa mishahara sekta binafsi: Ni muda wa Social Security Funds kutoa hata 30% ili watu wajikimu

Kukosa mishahara sekta binafsi: Ni muda wa Social Security Funds kutoa hata 30% ili watu wajikimu

Kulingana na yanayotokea kwa watu kukosa mishahara mfano shule binafsi kama tusiime, st Anne Marie na zingine nyingi ilhali watumishi hao wanachangia vizuri tu nssf. Serikali aioni haja ya kuruhusu watu wachukue sehemu ya asilimia 30 tu ya mafao yao ili kujilinda kipindi hiki cha janga la covid19. Lengo kuu la mifuko hii in kuihifadhi jamii.

Na ni dhahiri kwa hali ilivyo wanahitaji hifadhi nyakati hizi kwani waajiriwa hawana fedha na waajiri hawana fedha za kuwalipa ni vyema wapewe walizokuwa wanatunza nssf ili nazo ziwatunze na ndio malengo. Au kama kuna watu wamezitafuna basi wanachama waambiwe. Kama kweli hii ni serikali ya wanyonge lazima italifanyia kazi suala hili tofauti na hapo itakuwa ni kuigiza tu kujali wanyonge.

Na fedha zitoke ndani ya wiki au sikutatu kulingana na hali ya dhalura iliyopo.

WABUNGE MKO WAPI? HIZI NDIO ZILIKUWA HOJA ZA DHARURA KUJADILIWA BUNGENI SIO UPINZANI KUWAZA KUPINGA TU KILA KITU NA WA CHAMA TAWALA KUSIFIA MPAKA UJINGA.
Fanyieni kazi haya
Mpaka sasa Malipo ya mkupuo kwa wastaafu chini ya mfuko wa nssf ni asilimia 25 tu ya mafao yako. Kwa hiyo kusema upewe kwa sasa kiasi ambacho hata wastaafu hawapewi ni ndoto za mchana. Huko nssf ni kilio!! Kile kikokotoo kilichopigiwa kelele, huko nssf ndicho kinachotamba! Hata zoezi LA kuwahamishia PSSSF watumishi wa umma waliokuwa NSSF halijasaidia maana mtumishi huyo akistaafu bado nssf ndio wanaohusika kumlipa mafao yake kwa kikokotoo hicho hicho ambacho kililalamikiwa na rais akakisitisha! Eti wanasema nssf ndiko alikolipia michango yake mingi!!
Ninayajua haya kwa kuyapitia! Hivi sasa nimestaafu na wamenipigia mahesabu ya hicho kikokotoo kandamizi japo hata hicho kidogo sijakipata nikiwa nimestaafu kwa zaidi ya miezi 5.
 
Hilo ni swala lingine, angalau bado wanachochote cha kuwalipa Wastaafu ambao wameshachangia kwa miaka mingi klk huyu ambaye hajachangia sana na bado hajastaafu kutaka kulipwa.
Kama unayoyaongea ni ya ukweli basi hii mifuko haina maana kabisa.. Yaani mstaafu anakosa pesa ya kulipwa anasubiri mpaka wanachama wachange ndio apewe? Kwani michango take aliyokuwa anachanga inakuwa imeenda wapi wakati huo mpaka asubiri ya wengine? Kufiria kwa makini hapo utaona eidha hueleweki au hujielewi ama kuelewa vizuri unachokiongea
 
Kama unayoyaongea ni ya ukweli basi hii mifuko haina maana kabisa.. Yaani mstaafu anakosa pesa ya kulipwa anasubiri mpaka wanachama wachange ndio apewe? Kwani michango take aliyokuwa anachanga inakuwa imeenda wapi wakati huo mpaka asubiri ya wengine? Kufiria kwa makini hapo utaona eidha hueleweki au hujielewi ama kuelewa vizuri unachokiongea

Labda wewe ndio hauelewi jinsi hii mifuko inavyofanya kazi, siyo kwamba unachokiweka ndicho unachokipata hiyo siyo Benki kwanza hata Benki yenyewe ukiweka laki watakukata kiasi.

Jielimishe kwanza jinsi mifuko inavyofanya kazi ndio uongee.
 
Labda wewe ndio hauelewi jinsi hii mifuko inavyofanya kazi, siyo kwamba unachokiweka ndicho unachokipata hiyo siyo Benki kwanza hata Benki yenyewe ukiweka laki watakukata kiasi.

Jielimishe kwanza jinsi mifuko inavyofanya kazi ndio uongee.
Labda nieleweshe unaelewa inafanyaje kazi kiasi cha kukosa mafao ya kumlipa mstaafu na kutegemea michango wa wanachama wapya.? Ni michango ya mstaafu anayedai inakuwa imepotelea wp?
 
Labda nieleweshe unaelewa inafanyaje kazi kiasi cha kukosa mafao ya kumlipa mstaafu na kutegemea michango wa wanachama wapya.? Ni michango ya mstaafu anayedai inakuwa imepotelea wp?

Kwa kifupi ndivyo ilivyo wewe unavyokatwa analipwa anayestaafu kwa sasa, nimerasihisha lkn ni muelekeo huo, ukipenda kuelewa zaidi watembelee Wataalamu wao watakuelewesha ili uelewe kwa maana kama ni Mfanyakazi na unakatwa inakuhusu na ni muhimu kuelewa, ...
 
Kipi bora, upate 30 % now ikusaidie kununua barakoa, sanitizers na lishe bora kwa familia yako au ufe na hiyo pesa usikie ukiwa kaburini??

Sent using Jamii Forums mobile app


Ukifa kabla ya kustaafu nafikiri Mke/Mme aliyebakia atalipwa, sina uhakika hapo, isitoshe siyo swala la kipi bora bali jinsi hiyo Mifuko inavyofanya kazi na ni Dunia nzima, ni kwa ajili ya watu waliochangia kwa miaka kadhaa 15-20 ambao hulipwa baada ya kustaafu.
 
Kwan unachoweka si akiba yko au unawawekea na wengine???
Mifuko haiendeshwi kwa hisia na matakwa binafsi, bali kwa Mahesabu, kwamba ukipewa sasa hivi 30% ukistaafu kutakuwa hakuna hela ya kukupa kwa maana ulishaichukuwa nikimaanisha kama kila mtu akitaka apewe 30% sasa hivi, wanaostaafu watakosa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hivi hawa wanyonge huwa hawaishagi?kila awamu ikija madarakani inajifanya kuwajali wanyonge ni wakina nani hawa wanyonge jamani!!!!!
serikali inapaswa kufanya kitu kwa hawa sekta binafsi ambao pia ni wa lipa kodi wazuri tuu wakati huu wa hili janga la corona.
 
Back
Top Bottom