Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,186
- 7,492
Ripoti mbalimbali za 'World happiness index' zinaonesha kuwa Tanzania ni moja ya nchi zinazoshika nafasi za juu sana kwa watu wake kutokuwa na furaha. Jibu la kwa nini hali inakuwa hivyo halijawahi kuelezwa kwa ufasaha. Leo tutatoa jibu la swali hilo
Asilimia kubwa ya watanzania ni wanafiki vibaya mno. Wanafiki wanaweza kuwa kama 90% hivi ya watu wote. Sasa hawa wote hawawezi kuwa na furaha kwa sababu dhamira, fikra, na matendo yao huwa yanapingana muda wote na ukishajikuta kwenye hali hiyo hakuna namna unaweza kuwa na furaha. Ikumbukwe furaha ni 'State of mind'
Kama 8% hivi wanaweza kuwa sio wanafiki lakini ni watu wasiokuwa na ujasiri wa kusimamia vitu wanavyoamini, kwa hiyo kwa kawaida hawa hawachukui hatua kwenye yale wanayoamini ili kusaidia kubadili hali ya mambo. Hawa husubiria wenzao wafanye vile watakavyofanya. Utasikia wakisema 'sasa kama wao hawajafanya sisi tutatafanya nini? ngoja tuonea kama watafanya". Hawa nao hawana wala hawawezi kuwa na furaha kwa sababu dhamira zinapingana na matendo.
Kama 2% hivi iliyobaki, hawa ni wa kweli, wana dhamira njema na wanasimamia wanayoamini ila nao hawafanikiwi maana ni wachache mno, ni kama tone kwenye bahari. Ijapokuwa hawafanikiwi, hawa angalau wana furaha maana Imani, dhamira na matendo yao yanaendana.Hapa ndio unawakuta kama kina ustadh na wengineo wachache, ustadh nani huyu wanamuita mwenye kigari kidogo dogo!?
Tunazo option mbili tu; Kuchagua kuwa wanafiki au kuwa wakweli, kuwajibika au kila mtu aache akiamini mwenzake ndio anawajibika. Chaguo lolote tunaloamua kufanya lina gharama na faida yake.
Hata hivyo mpaka sasa haifahamiki kwamba ni kwa nini asilimia kubwa ya watanzania wamekuwa wakichagua kuwa wanafiki kuliko wakweli na kuchagua kutokuwajibika badala ya kinyume chake licha ya chaguo hilo kuwa na gharama kuliko faida ikiwemo kutokuwa na furaha,.
Hakuna namna ambayo 'index' ya furaha inaweza kupanda kama hali ya unafiki itabaki kama ilivyo kwa sababu unafiki na furaha ni sawa na shetani na malaika mmoja akiingia mwezake lazima atoke.
Mwisho, maisha bila ya furaha ni maisha yasiyo na maana na hakuna namna unaweza ukawa na furaha kama unaendekeza unafiki au kutokuwajibika hata kama utakuwa na cheo au pesa au kitu kingine chochote kwa kiasi chochote kile.
Asilimia kubwa ya watanzania ni wanafiki vibaya mno. Wanafiki wanaweza kuwa kama 90% hivi ya watu wote. Sasa hawa wote hawawezi kuwa na furaha kwa sababu dhamira, fikra, na matendo yao huwa yanapingana muda wote na ukishajikuta kwenye hali hiyo hakuna namna unaweza kuwa na furaha. Ikumbukwe furaha ni 'State of mind'
Kama 8% hivi wanaweza kuwa sio wanafiki lakini ni watu wasiokuwa na ujasiri wa kusimamia vitu wanavyoamini, kwa hiyo kwa kawaida hawa hawachukui hatua kwenye yale wanayoamini ili kusaidia kubadili hali ya mambo. Hawa husubiria wenzao wafanye vile watakavyofanya. Utasikia wakisema 'sasa kama wao hawajafanya sisi tutatafanya nini? ngoja tuonea kama watafanya". Hawa nao hawana wala hawawezi kuwa na furaha kwa sababu dhamira zinapingana na matendo.
Kama 2% hivi iliyobaki, hawa ni wa kweli, wana dhamira njema na wanasimamia wanayoamini ila nao hawafanikiwi maana ni wachache mno, ni kama tone kwenye bahari. Ijapokuwa hawafanikiwi, hawa angalau wana furaha maana Imani, dhamira na matendo yao yanaendana.Hapa ndio unawakuta kama kina ustadh na wengineo wachache, ustadh nani huyu wanamuita mwenye kigari kidogo dogo!?
Tunazo option mbili tu; Kuchagua kuwa wanafiki au kuwa wakweli, kuwajibika au kila mtu aache akiamini mwenzake ndio anawajibika. Chaguo lolote tunaloamua kufanya lina gharama na faida yake.
Hata hivyo mpaka sasa haifahamiki kwamba ni kwa nini asilimia kubwa ya watanzania wamekuwa wakichagua kuwa wanafiki kuliko wakweli na kuchagua kutokuwajibika badala ya kinyume chake licha ya chaguo hilo kuwa na gharama kuliko faida ikiwemo kutokuwa na furaha,.
Hakuna namna ambayo 'index' ya furaha inaweza kupanda kama hali ya unafiki itabaki kama ilivyo kwa sababu unafiki na furaha ni sawa na shetani na malaika mmoja akiingia mwezake lazima atoke.
Mwisho, maisha bila ya furaha ni maisha yasiyo na maana na hakuna namna unaweza ukawa na furaha kama unaendekeza unafiki au kutokuwajibika hata kama utakuwa na cheo au pesa au kitu kingine chochote kwa kiasi chochote kile.