Kukuza mtaji wa biashara ya kompyuta

Kukuza mtaji wa biashara ya kompyuta

King snr

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2015
Posts
1,165
Reaction score
1,470
Habari wakuu,
Hongereni kwa majukumu ya hapa na pale nimekuja kwenu kupata mawazo na ushauri hasa katika kukuza mtaji.
Biashara yangu Ni uuzaji wa laptop, desktop and accessories.

Nilianza biashara hii mtandaoni kwa kuwa napost bidhaa ambazo sina mteja akihitaji naenda kumchukulia changamoto ya hii biashara Ni kuaminiwa na watu maana wengi wameshapigwa Sana online Sasa inapelekea kupoteza wateja wengi.

Nilijitahidi nikafanikiwa kupata frem na Sasa kidogo wateja wanaweza kufika dukani na kuangalia mzigo.

Changamoto ninayopata saizi sio changamoto mbaya Sana maana Nina wateja wengi lakini wakija dukani hawakuti bidhaa za kutosha na hii Ni kutokana na kukosa mtaji wa kuwa na pc zangu mwenyewe hapa dukani wengine wanataka wakija dukani wachukue mzigo waondoke nao na sio stori za kuwaambia lipia hii nakuagizia.

Natamani nipate japo kiasi Cha 10M nichukue mzigo biashara ichangamke maana wateja Nina uhakika ninao wa kutosha,branding na marketing zote ziko vizuri.

Nawasilisha kwenu Kama Kuna ambaye anaweza kunishauri kwa chochote.

Karibu.
 
Andika mchanganuo wa biashara Kisha omba mkopo Benki kama una asset Hata kiwanja itakuwa rahisi. Pia unaweza ukatafuta duka Kubwa uwe unaenda kuchukua mzigo Kwa Mali kauli endapo watakuamini.
Uwezo wa kulipa mkopo ninao kabsa Ila sifa za kupata mkopo bank Sina
Sina asset yoyote ya kuwapa
 
Andika mchanganuo wa biashara Kisha omba mkopo Benki kama una asset Hata kiwanja itakuwa rahisi. Pia unaweza ukatafuta duka Kubwa uwe unaenda kuchukua mzigo Kwa Mali kauli endapo watakuamini.
Kuomba mzigo nimejaribu maeneo baadhi Ila sijafanikisha
 
Hebu weka mpango wa biashara yako hapa, ni vipi unapata faida

Hasara zinakuwaje,

bidhaa unanunuwa utoka wapi (unaagiza nje, au unashirikiana na wafanyabiashara wengine mnaagiza kwa pamoja/au supplier wa hapa kwenye godauni.

Mtaji wako ,kuendesha biashara na bidhaa, fremu jumla kiasi gani?

Kwanini unahisi unahitaji 10mil?, kwanini isiwe 5mil, 3mil au zaidi ya 10mil?
 
Ama hata milion moja tu,ama hata laki 5. Yeye anakimbilia mtaji mkubwa kwa haraka
 
Mimi nafanya biashara hiyo nilianza na mtaji mdg saana kama laki 3, Kwa sasa nina kijiofisi changu alhamdullah, Kamtaji kanakua kdg kdg. Japo naendelea kujifunza zaidi jinsi ya kutunza fedha za faida ili mtaji ukue.
PXL_20221202_161645268.jpg
 
Mimi nafanya biashara hiyo nilianza na mtaji mdg saana kama laki 3, Kwa sasa nina kijiofisi changu alhamdullah, Kamtaji kanakua kdg kdg. Japo naendelea kujifunza zaidi jinsi ya kutunza fedha za faida ili mtaji ukue.View attachment 2437572

Kweli mwanzo mkuu kiongozi,hongera sana kwa kuthubutu maana kwenye biashara hakuna mtaji unaotosha,ila vijana wengi wanataka kuanza biashara na milioni 50 ,gari ya kuwapeleka dukani watasubiri sana [emoji28]na kuanza kuponda serikali
 
Kweli mwanzo mkuu kiongozi,hongera sana kwa kuthubutu maana kwenye biashara hakuna mtaji unaotosha,ila vijana wengi wanataka kuanza biashara na milioni 50 ,gari ya kuwapeleka dukani watasubiri sana [emoji28]na kuanza kuponda serikali
🤣🤣🤣🤣🤣
 
Uwe unanunua bidhaa kwenye maduka kama mawili au matatu, jitahidi force mzunguko wako .
Mwenye duka akiona unakwenda kila siku kununua pc 2 kila siku atapata imani ya kukukopesha na cha nyongeza ukiwa mwaminifu utakataa mwenyewe mizigo
 
Mimi nafanya biashara hiyo nilianza na mtaji mdg saana kama laki 3, Kwa sasa nina kijiofisi changu alhamdullah, Kamtaji kanakua kdg kdg. Japo naendelea kujifunza zaidi jinsi ya kutunza fedha za faida ili mtaji ukue.View attachment 2437572
Nimetafakari laki3 frame ulilipiaje? mtaji wa operation ulikuaje yaan jaman tuweni wakweli ata kma ungepata frame kwa elanya chini 50k ni sawa na laki3 kwa miezi 6.. haya hiyo fram ulikuwa unaifanyia nini maana mtaji umelipa kodi..
 
Embu mwenye kawazo kazuri cha biashara ya mtaji w 1.5milion anisaidie .. nimewaza tangu mwezi wa9 mpaka sasa mtaji umepungua kwenye kula, kutoka 2milion mpaka sasa nina 1.5m

Sasa nasoma comment watu wanasema inabidi mtu uwe na milion 10 ndio uanze biashara kochwa kina zidi niuma.

ila.uzi huu naona kama kuna shughuda za mitaji midogo.. nipeni wazo la kuwa na kaframe napenda sana biashar yenye adress.. elimu ya ngu ni degree, umri 30. niko dar tegeta.

asanten sana
 
Back
Top Bottom