Kula ovyo kutakuja kutuathiri sana siku moja

Kula ovyo kutakuja kutuathiri sana siku moja

ERoni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2013
Posts
48,052
Reaction score
104,677
Hello wakuu,
Kuna kitu nimekiona, kipo na mara nyingi najiwazia nakuwa na wasiwasi juu ya afya zetu kama jamii. Hii tabia ya kula kila mahali, mazingira yoyote bila kujua namna chakula kilivyoandaliwa.

Ukipita kwenye mikusanyiko na sehemu zilizochangamka utakuta meza zimewekwa, kuna kila aina ya vyakula, vyakula vya haraka mnaita take away kuanzia chips, ndizi hadi bites kama maandazi, kachori na juice za kutengeneza majumbani.

Najiwazia tu na kuona kabisa hakuna regulations kwenye hivi vyakula, sidhani kama upo usimamizi wowote na hili linanipa wasiwasi hasa ukiangalia namna jamii ilivyoharibika. Unakulaje sambusa mtu anatembeza barabarani? Unamjua huyo mtu, unajua ni nyama gani ameandaa, unajua mazingira aliyopika hizo sambusa? Maswali ni mengi, binafsi nikiona mtu busy ananunua mapaja ya kuku wanaotembezwa na anajilia kwa raha zake namuwazia mengi.

Siku hizi kuna serial killers, mtu anaweza kuamua tu kuua watu kwa namna anavyotaka, iwe kuweka sumu kwenye chakula au vyovyote vile na kwa namna wanavyouza, ni ngumu kujua nani alifanya hilo tukio. Huwa nikishuka pale mbezi mwisho na kuona watu wanavyokula kachori, supu ya pweza nk najisemea moyoni kweli nchi bado imejaa ujamaa.

Tujihadhari sana hasa kula vyakula ambavyo hatujui mazingira yake ya maandalizi.
 
Ukiangalia binadamu kila tunapotembea tupo kwenye hatari ya kudhurika au hata kufa kabisa. Wanasema kutembea na kifo.

Ukiacha chakula ulichoandaa mwenyewe basi vingine vyote hata kama ni vya wapi vinaweza kuwa hatari kwetu. Lakini tutafanyaje? Hauwezi kuandaa kila siku kila wakati chakula chako kuna wakati inabidi ununue tu. Na kwenye kununua inategemea , uchumi wako ndio utaamua ule vya barabarani ambavyo ni hatari au ule vya hotelini ambaovyo ni hatari pia.

Sisi tunasema “ If we die, we die”.
 
Ni kweli mkuu, kuna case nyingi hasa kwenye usafiri wa mabasi, unakuta abiria yupo stendi anatokea mtu from nowhere anakaa nae pale kumbe anamlia timing anapiga nae story zikinoga anatoa msosi anamkaribisha "karibu chakula ndugu yangu" bila kujua abiria anabugia kumbe zimetiwa dawa/viambata abiria anasinzia usingizi wa nusu kifo anakuja kushtuka yupo hospital vitu vyake vyote vishaporwa.
...
Hata ndani ya bus the same unapewa msosi na mtu uliekaa nae kumbe ni mwizi, kasafiri ili akuibie unasinzia unakuja kuamshwa na wenye bus, huna kitu ushalizwa.
Kula kwa tahadhari
 
Ni kweli mkuu, kuna case nyingi hasa kwenye usafiri wa mabasi, unakuta abiria yupo stendi anatokea mtu from nowhere anakaa nae pale kumbe anamlia timing anapiga nae story zikinoga anatoa msosi anamkaribisha "karibu chakula ndugu yangu" bila kujua abiria anabugia kumbe zimetiwa dawa/viambata abiria anasinzia usingizi wa nusu kifo anakuja kushtuka yupo hospital vitu vyake vyote vishaporwa.
...
Hata ndani ya bus the same unapewa msosi na mtu uliekaa nae kumbe ni mwizi, kasafiri ili akuibie unasinzia unakuja kuamshwa na wenye bus, huna kitu ushalizwa.
Kula kwa tahadhari
Hiyo ni case tofauti na mleta uzi alicholenga mkuu, huyo anaepokea pokea vyakula toka kwa asiowajua ni mlafi tu na hilo pigo ni stahiki yake.

Kula mahali ambapo unajua uandaaji wake ni changamoto, labda kwa hawa mama ntilie wetu mtaani ndio utaona anapika vipi ila huko mahoteliji kunakoaminika kwa usafi hata jiko hulioni.
 
Ni kweli mkuu, kuna case nyingi hasa kwenye usafiri wa mabasi, unakuta abiria yupo stendi anatokea mtu from nowhere anakaa nae pale kumbe anamlia timing anapiga nae story zikinoga anatoa msosi anamkaribisha "karibu chakula ndugu yangu" bila kujua abiria anabugia kumbe zimetiwa dawa/viambata abiria anasinzia usingizi wa nusu kifo anakuja kushtuka yupo hospital vitu vyake vyote vishaporwa.
...
Hata ndani ya bus the same unapewa msosi na mtu uliekaa nae kumbe ni mwizi, kasafiri ili akuibie unasinzia unakuja kuamshwa na wenye bus, huna kitu ushalizwa.
Kula kwa tahadhari
Mtu wa hivi ni mlaku, yaani anakula popote akikaribishwa? Ujamaa unatusaidia sana ila tuchukue tahadhari. Watu wanaanza kuharibika taratibu.
 
Ukiangalia binadamu kila tunapotembea tupo kwenye hatari ya kudhurika au hata kufa kabisa. Wanasema kutembea na kifo.

Ukiacha chakula ulichoandaa mwenyewe basi vingine vyote hata kama ni vya wapi vinaweza kuwa hatari kwetu. Lakini tutafanyaje? Hauwezi kuandaa kila siku kila wakati chakula chako kuna wakati inabidi ununue tu. Na kwenye kununua inategemea , uchumi wako ndio utaamua ule vya barabarani ambavyo ni hatari au ule vya hotelini ambaovyo ni hatari pia.

Sisi tunasema “ If we die, we die”.
Unaweza kula mapaja ya kuku yanatembezwa na mtu hata humjui? Najua kifo kipo na tunatembea nacho ila muhimu kuchukua tahadhari, huwezi kuvuka barabara kizembe eti kwa vile kifo kipo na tunatembea nacho.
 
We mkuu kweli haupo serious na maisha,watu wanadiriki kula manii ambazo hawajui hata mtu yupo na magonjwa mangapi aliyoambukizwa au ya kurithi...unasema msosi!?

Watameza dawa bhana
 
Asilimia kubwa watu wamedhurika tayari, karibu 80% ya watanzania wana vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na bacteria wa h pylori ,ambao njia moja wapo ya kuwapata ni kula mavyakula yasio salama.
Mtani, watanzania tunakula ovyo sana. Popote na mazingira yoyote tunakula tu, hatuangalii kitu zaidi ya kushibisha matumbo yetu. Hatari sana hii.
 
Back
Top Bottom