Kulazimisha vijana wawe wajasiriamali/ wajiajiri ni kuzidi kuwapoteza zaidi. Sio wote wanaweza

Kulazimisha vijana wawe wajasiriamali/ wajiajiri ni kuzidi kuwapoteza zaidi. Sio wote wanaweza

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Naandika kwa masikitiko makubwa sana ikiambatana na huzuni. Hili tatizo la ajira ni karibu dunia nzima kwa sasa hasa Afrika. Ila tunachotofautiana ni namna ya kukabiliana na tatizo. Nchi nyingi za Afrika tunatumia mbinu za hovyo kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana.

Wanasiasa, viongozi wa dini na public figures wengine kila mara wamejitokeza hadharani na kuwataka vijana wajiajiri ili kujikwamua kwenye hali ngumu. Mimi naona hizo ni porojo ambazo zimewachosha kabisa vijana. Kwanza kudhani kila mtu anaweza kuwa mfanyabiashara ni kosa kubwa mno. Kudhani kuwa kijana akipata mtaji na kujiajiri atafanikiwa ni dharau kubwa kwa ujasiriamali na biashara kwa ujumla. Biashara ni zaidi ya mtaji. Wengi hawana vipaji wala mbinu za kudumu kwenye biashara wanazoanzisha ambapo matokeo yake ni kufeli vibaya kisha kijana kupata stress. Wakati kijana kafeli hupokea lawama kutoka kila kona na mwisho wa siku madhara mengine huanza.

Mimi nadhani serikali ingefikiria upya kuhusu mikopo inayotolewa kwa vijana kupitia 10% ya mapato ya halmashauri kama ina tija au la. Binafsi najua ile mikopo ipo kisiasa sana na mara nyingi huwa haileti matokeo yoyote kwa vijana. Ni ngumu sana kundi la watu zaidi ya 10 wakawa na vision moja ya biashara. Hata kama vision itakuwa moja ni ngumu kuwa pamoja wakati wa mchakato wa kutimiza ndoto.

Mimi nadhani serikali ingetoa mikopo isiyo na riba kuwawezesha wale vijana ambao tayari wameshaanza biashara na zinaonyesha kukua ili ziwe kubwa na kuajiri vijana wenzao. Kwa mfano serikali inaweza toa Tsh 20m kwa biashara ya kijana wa kitanzania ambayo tayari imeshaanza na inafanya vizuri ikiwa pamoja na kulipa kodi. Tsh 20m kwa vijana 10000 ni kama bilioni 200 kitu ambacho serikali hii inaweza. Na hizo bilioni 200 wapewe benki kama NMB au CRDB kuzifuatilia. Yaani wawe mawakala. Au Takukuru wawe mawakala wa hiyo mitaji. Hapo hela zitarudi na vijana watapambana.

Kuna vijana wanaofanya vizuri sana kwenye biashara za kilimo, sanaa, ufugaji, ufundi na fani zingine ila mitaji midogo. Hawa wawezeshwe baada ya kutoa hela kwa makundi ambayo hujiunga tu ili kupata hela za halmashauri na kuzitumia hovyo. Serikali ikalitazame na hili.
 
Pumzi ya moto kwa serikali yako wacha tuone huko mbele
 
IMG_20220922_233329.jpg
 
Sio serikali tu, watu wengi sana hudhani kwamba kila mtu anaweza kufanya biashara. Ndio maana ata humu utasikia mara nyingi watu wakilaumu walioajiriwa kazi za mishahara midogo eti kwanini wasifanye biashara?
Jamani, biashara ni kipaji kama vilivyo vipaji vingine!
 
Sio serikali tu, watu wengi sana hudhani kwamba kila mtu anaweza kufanya biashara. Ndio maana ata humu utasikia mara nyingi watu wakilaumu walioajiriwa kazi za mishahara midogo eti kwanini wasifanye biashara...
Kweli mkuu. Biashara ni kipaji na inahitaji uzoefu mkubwa wa muda mrefu hasa wa nje ya darasa. Mtu kama Vunjabei, Mo na watanzania wengi wenye asili ya Asia kuanzia utoto wao wanajifunza biashara hivyo kufanikiwa ni rahisi sana.

Tatizo mtu alikuwa na ndoto zake za kuwa daktari mara ghafla baada ya kumaliza chuo anaambiwa awe mchuuzi wa nguo kwa hoja ya kujiajiri. Matikeo yake ni kuchanganyikiwa tu.
 
Takukuru ndio taasisi inayoongoza kwa rushwa Tanzania yaani ukisikia kesi yoyote au kitu chochote wanafuatilia takukuru jua hakuna majibu watakayokuja nayo watapigwa hela wanakaa kimya.
 
Nakushukuru mama kwa kusoma huu uzi wangu na kuona nimeshauri jambo la maana. Hakika tumepata Rais anayeheshimu mawazo ya kila mtanzania. Kiukweli benki zikipewa hizo hela watazifuatilia na hazitapotea.
 
Naandika kwa masikitiko makubwa sana ikiambatana na huzuni. Hili tatizo la ajira ni karibu dunia nzima kwa sasa hasa Afrika. Ila tunachotofautiana ni namna ya kukabiliana na tatizo. Nchi nyingi za Afrika tunatumia mbinu za hovyo kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana.

Wanasiasa, viongozi wa dini na public figures wengine kila mara wamejitokeza hadharani na kuwataka vijana wajiajiri ili kujikwamua kwenye hali ngumu. Mimi naona hizo ni porojo ambazo zimewachosha kabisa vijana. Kwanza kudhani kila mtu anaweza kuwa mfanyabiashara ni kosa kubwa mno. Kudhani kuwa kijana akipata mtaji na kujiajiri atafanikiwa ni dharau kubwa kwa ujasiriamali na biashara kwa ujumla. Biashara ni zaidi ya mtaji. Wengi hawana vipaji wala mbinu za kudumu kwenye biashara wanazoanzisha ambapo matokeo yake ni kufeli vibaya kisha kijana kupata stress. Wakati kijana kafeli hupokea lawama kutoka kila kona na mwisho wa siku madhara mengine huanza.

Mimi nadhani serikali ingefikiria upya kuhusu mikopo inayotolewa kwa vijana kupitia 10% ya mapato ya halmashauri kama ina tija au la. Binafsi najua ile mikopo ipo kisiasa sana na mara nyingi huwa haileti matokeo yoyote kwa vijana. Ni ngumu sana kundi la watu zaidi ya 10 wakawa na vision moja ya biashara. Hata kama vision itakuwa moja ni ngumu kuwa pamoja wakati wa mchakato wa kutimiza ndoto.

Mimi nadhani serikali ingetoa mikopo isiyo na riba kuwawezesha wale vijana ambao tayari wameshaanza biashara na zinaonyesha kukua ili ziwe kubwa na kuajiri vijana wenzao. Kwa mfano serikali inaweza toa Tsh 20m kwa biashara ya kijana wa kitanzania ambayo tayari imeshaanza na inafanya vizuri ikiwa pamoja na kulipa kodi. Tsh 20m kwa vijana 10000 ni kama bilioni 200 kitu ambacho serikali hii inaweza. Na hizo bilioni 200 wapewe benki kama NMB au CRDB kuzifuatilia. Yaani wawe mawakala. Au Takukuru wawe mawakala wa hiyo mitaji. Hapo hela zitarudi na vijana watapambana.

Kuna vijana wanaofanya vizuri sana kwenye biashara za kilimo, sanaa, ufugaji, ufundi na fani zingine ila mitaji midogo. Hawa wawezeshwe baada ya kutoa hela kwa makundi ambayo hujiunga tu ili kupata hela za halmashauri na kuzitumia hovyo. Serikali ikalitazame na hili.
Kujiajiri ni kazi ngumu sana.Nakuunga mkono kwa hoja yenye mashiko..Wawezeshwe wachache iji nao wawaajiri wengine.
 
Naandika kwa masikitiko makubwa sana ikiambatana na huzuni. Hili tatizo la ajira ni karibu dunia nzima kwa sasa hasa Afrika. Ila tunachotofautiana ni namna ya kukabiliana na tatizo. Nchi nyingi za Afrika tunatumia mbinu za hovyo kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana.

Wanasiasa, viongozi wa dini na public figures wengine kila mara wamejitokeza hadharani na kuwataka vijana wajiajiri ili kujikwamua kwenye hali ngumu. Mimi naona hizo ni porojo ambazo zimewachosha kabisa vijana. Kwanza kudhani kila mtu anaweza kuwa mfanyabiashara ni kosa kubwa mno. Kudhani kuwa kijana akipata mtaji na kujiajiri atafanikiwa ni dharau kubwa kwa ujasiriamali na biashara kwa ujumla. Biashara ni zaidi ya mtaji. Wengi hawana vipaji wala mbinu za kudumu kwenye biashara wanazoanzisha ambapo matokeo yake ni kufeli vibaya kisha kijana kupata stress. Wakati kijana kafeli hupokea lawama kutoka kila kona na mwisho wa siku madhara mengine huanza.

Mimi nadhani serikali ingefikiria upya kuhusu mikopo inayotolewa kwa vijana kupitia 10% ya mapato ya halmashauri kama ina tija au la. Binafsi najua ile mikopo ipo kisiasa sana na mara nyingi huwa haileti matokeo yoyote kwa vijana. Ni ngumu sana kundi la watu zaidi ya 10 wakawa na vision moja ya biashara. Hata kama vision itakuwa moja ni ngumu kuwa pamoja wakati wa mchakato wa kutimiza ndoto.

Mimi nadhani serikali ingetoa mikopo isiyo na riba kuwawezesha wale vijana ambao tayari wameshaanza biashara na zinaonyesha kukua ili ziwe kubwa na kuajiri vijana wenzao. Kwa mfano serikali inaweza toa Tsh 20m kwa biashara ya kijana wa kitanzania ambayo tayari imeshaanza na inafanya vizuri ikiwa pamoja na kulipa kodi. Tsh 20m kwa vijana 10000 ni kama bilioni 200 kitu ambacho serikali hii inaweza. Na hizo bilioni 200 wapewe benki kama NMB au CRDB kuzifuatilia. Yaani wawe mawakala. Au Takukuru wawe mawakala wa hiyo mitaji. Hapo hela zitarudi na vijana watapambana.

Kuna vijana wanaofanya vizuri sana kwenye biashara za kilimo, sanaa, ufugaji, ufundi na fani zingine ila mitaji midogo. Hawa wawezeshwe baada ya kutoa hela kwa makundi ambayo hujiunga tu ili kupata hela za halmashauri na kuzitumia hovyo. Serikali ikalitazame na hili.
Hiyo inawezekana ila hawataki tu wameamua.
 
Unafahamu ccm inataka matatizo sio mafanikio waendelee kutumia hayo matatizo kuombea kuchaguliwa kwa nguvu
 
Back
Top Bottom