kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Sio kila kinacholiwa kinaweza kuliwa wakatiti wowote. Leo nitawapeni kwa uchache elimu kuhusu ulaji wa vyakula.
Vyakula vimegawanyika katika makundi makuu 6 ya kutia nguvu, kujenga mwili, kulinda mwili, kutia joto, madini na maji.
1. Katika kundi la Vyakula vya kutia nguvu (carbohydrates) viko mahindi, ubwabwa, uwele, ulezi, ngano, mihogo, mtama, viazi, maharage, kunde, n.k. Usagaji na ufyonzwaji mwilini wa kundi hili la vyakula unahitaji vimeng'enyo vinavyohitaji mazingira yasiyokuwa na acid kali, yaani vinahitaji alkaline environment kuanzia mdomoni hadi tumboni na kwenye utumbo.
2. Katika kundi la vyakula vya kujenga mwili (proteins) viko nyama za aina zote, mayai, maziwa. Usagaji wa vyakula hivi vinapoliwa unahitaji vimeng'enyo (enzymes) vinavyohihitaji kufanyakazi kwenye mazingira ya uchachu (acid) mwingi tumboni. Yaani kwenye alkaline environment nyama, maziwa, mayai havisagwi na kufyonzwa vizuri mwilini.
Ushauri: Kuhusu kula vyakula vya Carbohydrates na Protini: Usichanganye kwa wakati mmoja makundi haya mawili ya vyakula kwenye mlo mmoja li kuurahisishia mfumo wako wa chakula katika kusaga chakula ulichokula.
Kama utavichanganya pamoja mwili wako utavyonza sumu nyingi kutoka tumboni zinazotokana na kuoza (ferment) kwa chakula ambacho kinachelewa kusangwa tumboni, pia unaweza kupata kansa ya tumbo na utumbo. unashauriwa Kula ugali/ubwabwa na maharagwe,
nyegele, choroko, dengu, n.k badala ya kula ugali/ubwabwa pamoja na nyama, mayai au maziwa ili kusaidia tumbo kusaga chakula haraka. Kula nyama, maziwa au mayai masaa 3 kabla au baada ya mlo wenye vyakula vya kutia nguvu.
3. Katika kundi la vyakula vinavyolinda mwili yapo matunda na mboga za majani. Matikiti maji ni miongoni mwa matunda yanayopendwa duniani kote yenye madini mengi hasa mbegu zake,
LAKINI sasa tikiti maji na nyanya (oxalate) vina tabia mbaya ya kuzuia usagaji na ufyonzwaji wa aina nyingine za vyakula na virutubisho (madini na vitamins) na kuukosesha mwili rutuba na kusababisha vyakula kukaa sana tumboni.
Matikiti maji yanapoliwa na vyakula vingine kwa wakati mmoja yanaweza kusababisha hali ya kujisikia kichefuchefu pia.
Ushauri:
a) Kuhusu tikitimaji: tikiti maji liliwe masaa 3 kabla au baada ya kula vyakula vingine.
b) Usile chakula pamoja na nyanya mbichi, nyanya ina kemikali (oxalate) inayozuia virutubisho vingine kufyonzwa haraka mwilini.
c) Kula vyakula vya carbohydrates na proteins pamoja na mboga za majani (greens) ili kuboresha usagaji na ufyonzwaji wake.
d) Maji yana tabia ya kupunguza kasi ya kusaga na kumeng'enya chakula tumboni, hivyo usinywe maji wakati wa kula, kunywa maji saa 1 baada au kabla ya mlo.
e) Kuchanganya nafaka (mahindi, mchele, mtama, ulezi, ngano, n.k) kwenye mlo mmoja hakuleti faida yoyote ya kiafya mwilini, aina moja tu ya nafaka ambayo haikukobolewa sana inaleta faida inayokusudiwa. epuka gharama zisizo za lazima kwa kuchanganya aina nyingi za nafaka au proteins (mayai, nyama, maziwa, samaki) kwa wakati mmoja kwenye mlo mmoja, hakuna faida kiafya kufanya hivyo.
f) epuka kuchanganya matunda baridi (matango, matikiti, parachichi, ndizi, karoti, n.k) na yale makali (machungwa, passions, ukwaju, mabungo, matofaa, maembe, zabibu, ndimu, limau, n.k) kwenye mlo mmoja au kuyachanganya na sukari. Yaani kula tango tu, au chungwa tu, au tikiti maji tu au ndizi tu kwa wakati mmoja.
g) Vyakula vilivyochachuka kama vile mtindi, kabichi, togwa, mbege, mvinyo vinasadia kusaga chakula haraka tumboni. Ukivipata usiviache.
h) Kunywa maziwa peke yake kwa wakati wa peke yake, angalau nusu saa kabla au baada ya kula milo ya aina nyingine au dawa. Epuka chai za maziwa pia kama unaweza.
Usiku: Usiku mwili unahitaji protein zaidi ili kupata matofali (amino acids) ya kuujenga mwili na kurekebisha sehemu za mwili zilizoharibika na kuumia wakati wa mchana.
Wakati wa kulala mwili hauhitaji chakula kingi cha kutia mwili maana kazi zinazohitaji nguvu nyingi hakuna. Hivyo,
ni marufuku kula sahani ya ugali/ubwabwa na kwenda kupanda kitandani kulala wakati huo huo, maana chakula hakitasangwa vizuri na mwili utatengeneza sumu nyingi sana na kuwa na uwekezano wa kuota ndoto mbayambaya tu usiku kucha.
Asubuhi: Mwili unahitaji chakula cha kutosha cha kutia nguvu, na matunda, juice, siagi, asali, sukari, mkate, kiporo cha ubwabwa ili kuupatia mwili nguvu nyingi za kuendesha mitambo ya mwili inayohitaji nguvu (break fast).
Ianze siku yako kwa mlo wenye rutuba zote na kukutia nguvu nyingi sana.
Kama una swali lolote kuhusu namna ya kuchanganya vyakula uliza ujibiwe! Asalam aleykum.
Vyakula vimegawanyika katika makundi makuu 6 ya kutia nguvu, kujenga mwili, kulinda mwili, kutia joto, madini na maji.
1. Katika kundi la Vyakula vya kutia nguvu (carbohydrates) viko mahindi, ubwabwa, uwele, ulezi, ngano, mihogo, mtama, viazi, maharage, kunde, n.k. Usagaji na ufyonzwaji mwilini wa kundi hili la vyakula unahitaji vimeng'enyo vinavyohitaji mazingira yasiyokuwa na acid kali, yaani vinahitaji alkaline environment kuanzia mdomoni hadi tumboni na kwenye utumbo.
2. Katika kundi la vyakula vya kujenga mwili (proteins) viko nyama za aina zote, mayai, maziwa. Usagaji wa vyakula hivi vinapoliwa unahitaji vimeng'enyo (enzymes) vinavyohihitaji kufanyakazi kwenye mazingira ya uchachu (acid) mwingi tumboni. Yaani kwenye alkaline environment nyama, maziwa, mayai havisagwi na kufyonzwa vizuri mwilini.
Ushauri: Kuhusu kula vyakula vya Carbohydrates na Protini: Usichanganye kwa wakati mmoja makundi haya mawili ya vyakula kwenye mlo mmoja li kuurahisishia mfumo wako wa chakula katika kusaga chakula ulichokula.
Kama utavichanganya pamoja mwili wako utavyonza sumu nyingi kutoka tumboni zinazotokana na kuoza (ferment) kwa chakula ambacho kinachelewa kusangwa tumboni, pia unaweza kupata kansa ya tumbo na utumbo. unashauriwa Kula ugali/ubwabwa na maharagwe,
nyegele, choroko, dengu, n.k badala ya kula ugali/ubwabwa pamoja na nyama, mayai au maziwa ili kusaidia tumbo kusaga chakula haraka. Kula nyama, maziwa au mayai masaa 3 kabla au baada ya mlo wenye vyakula vya kutia nguvu.
3. Katika kundi la vyakula vinavyolinda mwili yapo matunda na mboga za majani. Matikiti maji ni miongoni mwa matunda yanayopendwa duniani kote yenye madini mengi hasa mbegu zake,
LAKINI sasa tikiti maji na nyanya (oxalate) vina tabia mbaya ya kuzuia usagaji na ufyonzwaji wa aina nyingine za vyakula na virutubisho (madini na vitamins) na kuukosesha mwili rutuba na kusababisha vyakula kukaa sana tumboni.
Matikiti maji yanapoliwa na vyakula vingine kwa wakati mmoja yanaweza kusababisha hali ya kujisikia kichefuchefu pia.
Ushauri:
a) Kuhusu tikitimaji: tikiti maji liliwe masaa 3 kabla au baada ya kula vyakula vingine.
b) Usile chakula pamoja na nyanya mbichi, nyanya ina kemikali (oxalate) inayozuia virutubisho vingine kufyonzwa haraka mwilini.
c) Kula vyakula vya carbohydrates na proteins pamoja na mboga za majani (greens) ili kuboresha usagaji na ufyonzwaji wake.
d) Maji yana tabia ya kupunguza kasi ya kusaga na kumeng'enya chakula tumboni, hivyo usinywe maji wakati wa kula, kunywa maji saa 1 baada au kabla ya mlo.
e) Kuchanganya nafaka (mahindi, mchele, mtama, ulezi, ngano, n.k) kwenye mlo mmoja hakuleti faida yoyote ya kiafya mwilini, aina moja tu ya nafaka ambayo haikukobolewa sana inaleta faida inayokusudiwa. epuka gharama zisizo za lazima kwa kuchanganya aina nyingi za nafaka au proteins (mayai, nyama, maziwa, samaki) kwa wakati mmoja kwenye mlo mmoja, hakuna faida kiafya kufanya hivyo.
f) epuka kuchanganya matunda baridi (matango, matikiti, parachichi, ndizi, karoti, n.k) na yale makali (machungwa, passions, ukwaju, mabungo, matofaa, maembe, zabibu, ndimu, limau, n.k) kwenye mlo mmoja au kuyachanganya na sukari. Yaani kula tango tu, au chungwa tu, au tikiti maji tu au ndizi tu kwa wakati mmoja.
g) Vyakula vilivyochachuka kama vile mtindi, kabichi, togwa, mbege, mvinyo vinasadia kusaga chakula haraka tumboni. Ukivipata usiviache.
h) Kunywa maziwa peke yake kwa wakati wa peke yake, angalau nusu saa kabla au baada ya kula milo ya aina nyingine au dawa. Epuka chai za maziwa pia kama unaweza.
Usiku: Usiku mwili unahitaji protein zaidi ili kupata matofali (amino acids) ya kuujenga mwili na kurekebisha sehemu za mwili zilizoharibika na kuumia wakati wa mchana.
Wakati wa kulala mwili hauhitaji chakula kingi cha kutia mwili maana kazi zinazohitaji nguvu nyingi hakuna. Hivyo,
ni marufuku kula sahani ya ugali/ubwabwa na kwenda kupanda kitandani kulala wakati huo huo, maana chakula hakitasangwa vizuri na mwili utatengeneza sumu nyingi sana na kuwa na uwekezano wa kuota ndoto mbayambaya tu usiku kucha.
Asubuhi: Mwili unahitaji chakula cha kutosha cha kutia nguvu, na matunda, juice, siagi, asali, sukari, mkate, kiporo cha ubwabwa ili kuupatia mwili nguvu nyingi za kuendesha mitambo ya mwili inayohitaji nguvu (break fast).
Ianze siku yako kwa mlo wenye rutuba zote na kukutia nguvu nyingi sana.
Kama una swali lolote kuhusu namna ya kuchanganya vyakula uliza ujibiwe! Asalam aleykum.