Kuliko Bilion 34 kujenga soko Kariakoo bora soko lihamishwe

Kuliko Bilion 34 kujenga soko Kariakoo bora soko lihamishwe

Kama issue ni kuwaweka wamachinga mahali pazuri basi tuhamishe kiwanda cha urafiki na hata ile millenia business park, tujenge kariakoo kubwa ya kutisha ya ghorofa hata nne majengo makubwa kwa ajili ya wamachinga. Na tuweke miundo mbinu ya usafiri wa umma, kuingia na kutoka.

Hata mwekezaji mchina ameshajenga fremu hapo kiwandani, amewapangisha wamachinga
Wamachinga hawafuati sheria wanafuata vibe la biashara. Palipo na msongamano wa watu na wao utawakuta ila sio uwapeleke sehemu wasubirie kufuatwa na wateja hiyo hawatokubali. Wao wanafuata wateja wanapokwenda.

Ndio maana maeneo yao ni pembezoni mwa barabara, pembezoni mwa vituo vya daladala, kwenye masoko makubwa, nje na ndani ya stand.

So machinga kimsingi wanafanya biashara katika mazingira ambayo kisheria si rasmi na yanavuruga utaratibu.

Say NO kwa MACHINGA. Tufanye biashara rasmi.
 
Ya ubungo bilioni 200 ,hii itakuwa trilioni 4 tunaweza
Trillion 4 ni pesa ndogo sana. Hivi unajua pesa nyingi sana inatumika kwenye mawizara na taasisi za serikali na impact ni sifuri.

Hiyo pesa tukiokota okota huko tunapata zaidi ya 4 trillions na ni ndani ya maiaka miwili tu.
 
Umesema vitu vya maana sana aseee..tatizo la nchi hii linajulikana sikuzote..ni viongozi wa ccm.

#MaendeleoHayanaChama
Nashindilia hapo shida ni wazee wa CCM na watoto wao na wapambe wao. Hawa inabidi watoke.
 
Wamachinga hawafuati sheria wanafuata vibe la biashara. Palipo na msongamano wa watu na wao utawakuta ila sio uwapeleke sehemu wasubirie kufuatwa na wateja hiyo hawatokubali. Wao wanafuata wateja wanapokwenda.

Ndio maana maeneo yao ni pembezoni mwa barabara, pembezoni mwa vituo vya daladala, kwenye masoko makubwa, nje na ndani ya stand.

So machinga kimsingi wanafanya biashara katika mazingira ambayo kisheria si rasmi na yanavuruga utaratibu.

Say NO kwa MACHINGA. Tufanye biashara rasmi.
urafiki pana vibe sana. kumbuka kuna soko la ndizi na mazao mengine pale kuelekea mabibo. ni kwa vile serikali nayo imeelekeza akili zake kariakoo tu. wangepaendeleza pale, pange vaibika kinoma
 
Una chuki na wamachinga eh!!?

Nchi ni yetu sote, nenda Hong Kong kawaulize wanapumlia wapi halafu uliza maendeleo yao then njoo na porojo zako.
Unadhani Hongkong hawana parks? Sha Tin Park? Hamna mji wa maana usio na park. Hata jirani zetu wana Uhuru Park acha Central Park ya New York. Shida yetu tunadhani tukijana maghorofa ndio tutaheshimiwa. Ka Botanical garden ketu kamebanwa mpaka kamekosa pumzi.

Amandla...
 
Inaonekana watu wa mipango miji wamelala na viongozi wetu akili zimeganda. Nimeona leo kwamba soko la k'koo litajengwa upya kwa Billion 34, leo siyo mwaka 1970 jamani kwanini pesa zote zitumike kujenga soko tena eneo lenye tatizo la msongamano wa watu badala ya kulihamisha soko pembezoni mwa mji? Au wazanzibari wao kila kitu wanataka kiwe karibu na feri ili wakitoka Zanzibar wasipate usumbufu[emoji23]? Maana naskia tena kuna mradi mwingine wa soko la jangwani[emoji26][emoji26].

Mimi nazani tuachane na hili soko la kariakoo tena serikali ingetumia opportunity hii kujenga mradi wa kuwezesha kariakoo kupumua kwa kubomoa lile soko na kupanda miti eneo lile na kutengeneza city park yenye bustani na benchi za watu kupumzika. Itungwe sheria iundwe mamlaka ya City park Authority ya kusimamia mambo haya kwenye miji yetu ipendeze. Tuache fikra kwamba kila eneo lazima lijengwe mji ule hauna hata sehemu ya kupumzika, mtalii akienda k'koo leo hii hakuna hata sehemu ya kupumzika labda ale chips sehemu ambayo imejaa joto la moshi wa jiko la mkaa na hewa ya mafuta ya kukaanga.

Kwanini bado serikali inakaa na kuwaza kujenga jenga sehemu yenye msongamano hata parking za magari hakuna badala ya kujenga miradi ya kuboresha changamoto za mji kama kujenga jengo la parking pale kwenye soko japo mimi ningetamani pasijengwe chochote ipandwe miti tu pale mji upumue.

Leo tunataka kufanya makosa yaleyale ya kujenga mwendokasi jangwani kwa kujenga soko jingine pale la wamachinga badala ya kujenga daraja flyover la kutoka magomeni kwenda faya au interchange ya kutoka magomeni kwenda faya kwenda salender kwenda karume na kupanda miti mirefu ya misitu jangwani ili kusaidia joto la mji kupungua.

Ukizingatia eneo la jangwani ndiyo aneo peke kwenye mji wa dar es salaam lenye unapana wa kutosha ndani ya jiji lenye kutosha kujenga 4 tier interchange ambazo kwa Africa ziko mbili tuu, moja iko Ghana na nyingine iko South Africa.

Yani pale inasukwa interchange moja matata sana kono moja linaenda faya kono jingine linaenda magomeni, kono jingine linasambaa hadi salender , kono jingine linasambaa hadi mitaa ya ilala karume, kono jingine linakatiza hadi kinondoni studio au nyuma yake pale.

Hela tunazo invest kwenye mavitu yasiyo na kichwa (madege, ma dreamliner) tunaweza tukatoa kitu cha maana sana pale jangwani chenye kupunguza changamoto nyingi sana za mji na kutujengea heshima kubwa sana kama jiji.

N:B Yani kwa asiyeelewa umuhimu wa misitu katikati ya mji ni kwamba binadamu tunazalisha kiwango kikubwa sana cha Co2 gases kwa tunavyopumua na moshi wa magari na viwanda, pia majiko tunayopikia ya mkaa sasa jiji linakuwa na hewa chafu sana ya co2 sasa wenzetu kama hongkong wamezungusha misitu kwenye jiji lao ili kuthibiti kiwango kikubwa cha Co2 gases kwa sababu misitu inanyonya gesi za Co2 na ku release gases za Oxygen hivyo kusaidia mji kuwa Na hewa safi na kusaidia ubongo kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. Kinyume chake ni sisi hapa.
View attachment 1999008
Hongera mkuu...UMEWAZA
 
Ukizingatia eneo la jangwani ndiyo aneo peke kwenye mji wa dar es salaam lenye unapana wa kutosha ndani ya jiji lenye kutosha kujenga 4 tier interchange ambazo kwa Africa ziko mbili tuu, moja iko Ghana na nyingine iko South Africa

Yani pale inasukwa interchange moja matata sana kono moja linaenda faya kono jingine linaenda magomeni, kono jingine linasambaa hadi salender , kono jingine linasambaa hadi mitaa ya ilala karume, kono jingine linakatiza hadi kinondoni studio au nyuma yake pale.

Hela tunazo invest kwenye mavitu yasiyo na kichwa (madege, ma dreamliner) tunaweza tukatoa kitu cha maana sana pale jangwani chenye kupunguza changamoto nyingi sana za mji na kutujengea heshima kubwa sana kama jiji.

View attachment 1999009
Uko sawa kabisa ila watu wanakupinga bure Tu. Btw kupinga kuunga hoja ni haki ya ya MTU
 
Uko sawa kabisa ila watu wanakupinga bure Tu. Btw kupinga kuunga hoja ni haki ya ya MTU
Fikiria tumeagiza ndege mpya nne kwa $700 million. Hizo pesa tungejenga ma interchange kama hayo mawili au zaidi. Ila watu wanashobokea ndege ambazo hata hawajui zinaruka wapi. Ila madaraja hayo kila mtu angepita kuwahi foleni ya kwenda kwao mida mibovu.
 
Back
Top Bottom