Kulikoni Mali za KKKT -DKMS kupigwa Mnada?

Sisi tuliambiwa chuo kilikosa vijana kwakua serikali ilikataa kutoa mikopo kwa moja ya vyuo binafsi kikiwepo hicho, kimawa kinajiendesha kwa hasara.

Kama sikosei walikua na management issues nyingi nakumbuka serikali ikashindwa kuwakubali kipindi ile familia ya Mstaafu Askofu imejipa haki miliki ya kutawala chuo… kuna mambo mengi yalienda hovyo mpaka chuo kikapoteza sifa, fitna uzandiki, upigaji, kujuana, lack of creativity etc. At the end washarika walibebeshwa zigo na bakuli kuzunguka! Kuna thread humu nadhani juu ya hicho chuo.
 
Wakatoliki waliona mbali sana waliposema mafather wasioe. Inamaana wao ni familia kubwa inayolinda taasisi yao kwa wivu mkubwa
 
Ooooh imekuwaje tena! shule yangu hio nilisoma hapo kipindi hiko Mwalimu Mkuu wa shule alikuwa Mch. Mwamboza.
 
DKMS iliharibiwa na Munga pamoja na mke wake.
Walifanya ubadhirifu hadi wakaua chuo kikuu.
Nasubiri tamko kutoka kwa Munga na mkewe walioiganya dayosisi kua mali yao binafsi.
I stand to be corrected.
Mshana Jr tia neno.
 
Tuhuma za kutisha za Dr. Munga Askofu KKKT -DKMS | Page 4 Tuhuma za kutisha za Dr. Munga Askofu KKKT -DKMS
 

Dawa ya deni kulipa, nyingine bla bla tu.
 
Kwa hii magamba KKKT walipitisha Sana bakuli makanisani na mimi nilichangia sana tu, nasikia Leo inapigwa mnada tena? Zile pesa zilienda wapi?
Michango ya washarika inapigwa na Viongozi wakubwa wa kanisa..

Unakuta Askofu anazunguka huko ulaya na familia yake bila Tija..

Hulk KKKT-DKMS nina uzoefu nao mkubwa maana hata mimi nawadai pesa nyingi kutokana na kazi niliyowafanyia..lakini mpaka leo sijalipwa.

Zaidi utasikia tu viongozi wakuu wa Dayosisi wamejiongezea mishahara..pia pamoja na kwamba kuna deni benki lkn bado wanajitengenezea mazingira ya kukopa na wanaliweka kanisa kuwa mdhamini wao..

Maaskofu na Viongozi wa Dayosisi wanalala five stars hotels na hata watoto zao na familia KWA ujumla zinalala huko KWA bills za kanisa...

Unakuta mimi nadai milioni mbili tu, ila hawataki kuilipa wakati huo safari za Askofu kwenda Sweden ni milioni 40..na si safari ya lazima..


KWA ufupi Kkkt kuna upigaji wa kufa mtu..
 
Kwa hii magamba KKKT walipitisha Sana bakuli makanisani na mimi nilichangia sana tu, nasikia Leo inapigwa mnada tena? Zile pesa zilienda wapi?
Walichimba madini katika maeneo ya kanisa na mpaka Sasa pesa hazieleweki zilienda wapi...wanadai ati hawakupata kitu wakati tuliokuwepo pembeni tuliona wakitorosha madini na fedha...mkurugrnzi wa uchumi na mipango kapiga fedha ya kufa mtu..🤣🤣🤣..

Kuna mianya mingi ya upigaji kkkt..so dini siku hizi ni machaka ya watu..

So kama mali zitapigwa mnada na watu tutalipwa pesa itakuwa ni Jambo jema
 
Kwani wanadaiwa sh ngapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…