Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
Baadhi ya Wanachadema hawafahamu kuwa, Kulikuwa na jaribio la Mapinduzi ndani ya @ChademaTz chini ya Kikundi kinachojiita Sauti ya Watanzania ambacho ndani yake kuna Wanaharakati wa ndani wakiongozwa na Dr Slaa mwanaccm ambae ndie alikuwa akiongoza mikutano ya hadhara, Mwabukusi ambae ni Mwanachama wa NCCR Mageuzi, mitandaoni yuko Maria Sarungi mwanachama hai wa CCM na baadhi ya Watz waishio nje (Diaspora) jaribio hilo lililotokea kipindi cha kupinga DP World, Bahati nzuri tulilizima jaribio hilo kwa nguvu kubwa na kuwazuia wasitumie jukwaa la Chadema kufanya mikutano yao.
Sasa wamekuja kwa mlango wa nyuma wamevamia Uchaguzi wa Chadema, wakijiegemeza kwa Tundu Lissu na kufanikiwa kumjaza maneno na fitina kubwa nae akajaa kwenye 18 zao, nyuma yao kuna CCM chini ya Msigwa, na Systeam inayosukuma kete kwa mbali sana na kwa uangalifu mkubwa sana hadi uwe na jicho la tatu ndio utabaini hilo, pia na baadhi ya Wanachadema walioshindwa katika chaguzi za ndani ya chama kuanzia kanda, mikoa na Wilaya ambao kimsingi sio Wapiga Kura bali wapiga kelele. Lengo wakipore chama kwa wanadema na kukidhibiti mikononi mwa ccm na mfumo. Wanachadema msiruhusu chama chenu kiporwe kwa Twita/X na Wasap kisha kukiua chama hiki kwa faida ya ccm.
Tutawashinda, zimefanyika juhudi kadhaa za kumweleza ukweli Lissu kwamba kundi ulilonalo ni kundi linalokwenda kukuua kisiasa na kukupoteza kabisa, lakini ameshupaza shingo tukaamua ikiwa busara imefeli sasa ngoja demokrasia ikaamue, Lissu ataanguka vibaya katika uchaguzi huu yaani akipata kura 100 anatakiwa akafanye sherehe kubwa sana kwao Ikungi. Don't test your master!
Na tutavuka chama kikiwa salama mikononi mwa wanachadema wenyewe! Lakini naomba niweke wazi jambo muhimu ambalo kila mwanachadema anatakiwa kufahamu ni kuwa baada ya uchaguzi huu, Chadema itabadilika na Siasa za nchi hii zitabadilika kwa 100%. Tuwe tayari kwa mabadiliko hayo. Hata ccm wanaoinjinia uchaguzi huu wafahamu kwamba wanaitengeneza Chadema mpya ambayo watakabiliana nayo ikiwa na nguvu ambayo hawatakuja kuiamini maishani mwao! Mfano tu (si rasmi) nani ataamini 2025 akija kuona Jaji Joseph Warioba ndie Mgombea wa Chadema, nasema ni mfano tu usikomaze fuvu. Zingatieni mnacheza na mabingwa wa karata za siasa Afrika, huu ndio utofauti wa harakati na siasa duniani.
Na Yericko Nyerere
Sasa wamekuja kwa mlango wa nyuma wamevamia Uchaguzi wa Chadema, wakijiegemeza kwa Tundu Lissu na kufanikiwa kumjaza maneno na fitina kubwa nae akajaa kwenye 18 zao, nyuma yao kuna CCM chini ya Msigwa, na Systeam inayosukuma kete kwa mbali sana na kwa uangalifu mkubwa sana hadi uwe na jicho la tatu ndio utabaini hilo, pia na baadhi ya Wanachadema walioshindwa katika chaguzi za ndani ya chama kuanzia kanda, mikoa na Wilaya ambao kimsingi sio Wapiga Kura bali wapiga kelele. Lengo wakipore chama kwa wanadema na kukidhibiti mikononi mwa ccm na mfumo. Wanachadema msiruhusu chama chenu kiporwe kwa Twita/X na Wasap kisha kukiua chama hiki kwa faida ya ccm.
Tutawashinda, zimefanyika juhudi kadhaa za kumweleza ukweli Lissu kwamba kundi ulilonalo ni kundi linalokwenda kukuua kisiasa na kukupoteza kabisa, lakini ameshupaza shingo tukaamua ikiwa busara imefeli sasa ngoja demokrasia ikaamue, Lissu ataanguka vibaya katika uchaguzi huu yaani akipata kura 100 anatakiwa akafanye sherehe kubwa sana kwao Ikungi. Don't test your master!
Na tutavuka chama kikiwa salama mikononi mwa wanachadema wenyewe! Lakini naomba niweke wazi jambo muhimu ambalo kila mwanachadema anatakiwa kufahamu ni kuwa baada ya uchaguzi huu, Chadema itabadilika na Siasa za nchi hii zitabadilika kwa 100%. Tuwe tayari kwa mabadiliko hayo. Hata ccm wanaoinjinia uchaguzi huu wafahamu kwamba wanaitengeneza Chadema mpya ambayo watakabiliana nayo ikiwa na nguvu ambayo hawatakuja kuiamini maishani mwao! Mfano tu (si rasmi) nani ataamini 2025 akija kuona Jaji Joseph Warioba ndie Mgombea wa Chadema, nasema ni mfano tu usikomaze fuvu. Zingatieni mnacheza na mabingwa wa karata za siasa Afrika, huu ndio utofauti wa harakati na siasa duniani.
Na Yericko Nyerere