Kulipa kodi ni maendeleo

Francis fares Maro

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2021
Posts
1,227
Reaction score
1,339
Ndugu wanabodi,

Nimefwatilia Kwa kina mijadala hii ya Tozo na Kodi ya majengo

Niseme machache!

Tulipe kodi kwasababu Kodi ndio msingi wa maendeleo yetu,bila Kodi nchi Itakua ngumu sana hii,hizi Kodi ndio tunaona mabarabara, vituo vya Afya, watumishi kupandishwa madalaja, madarasa, Elimu Bora, madawa hospitalini, tunapunguza vifo vya mama wajawazito, maji safi na salama nchi nzima.

Bila Kodi maana yake Sisi kama nchi tutaendelea kuwa tegemezi,tutataka tufanyiwe kila kitu na wahisani, tutashindwa kujiendesha, tutashindwa kupanga na kufanya maendeleo yetu, tunaweza kusema Tozo Sawa lakini zimekua kubwa lakini wakati wa kutoa maoni tulikua wapi?

Tunapenda uongo na umbea tunaacha mijadala ya maana na msingi ya kujenga nchi tunaenda kushadadia vitu vya kipumbavu kabisa!

Awamu ya Tano

JPM aliweka wazi kabisa lazima tulipe Kodi ili tujitegee tuache kusubiria misaada kutoka magharibi na uchina huko ambayo inatunyonya sana!

Nadhani ni wakati Ndugu zangu tufunge mikanda tulipe Kodi tujiendeshe wenyewe, tuweze kufanya hata tafiti zetu, vijana wetu tuwapatie mikopo wajiajiri kwa namna hii Mama zetu tuwatue Ndoo, tupate umeme huko vijijini, barabara zitengenezwe, reli ya SGR, bwawa la Nyerere, watoto wetu waache kukaa chini,walimu walipwe madeni yao,wastafu nao asiachwe namna hii lakini vitu vyote hivi ni msingi wa kulipa Kodi.

TULIPE KODI KWA MAENDELEO YETU
 
Tatizo siyo kulipa kodi.
Kodi zetu ziko salama kiasi gani
Utasikia mtu kapiga trilion alafu safi tu maisha yanaendelea si kuumizana huku nani anaweza kumuwajibisha mtu serikali hii

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Sheria zetu na wanasheria hii ni shida kubwa!!.. Tulipe Kodi Kwa Maendeleo yetu
 
Mzalendo ni lazima kulipa kodi ili taifa lako liendelee, ila kazi ya kodi ionekane na sio kwa manufaa ya wachache kwa kupiga dili. Kama kazi ya kodi inaonekana kama wakati wa JPM,mzalendo yupo tayari kutoa taarifa kwa anaekwepa kodi kwani anazuia maendeleo ya Taifa.
 
Mzalendo ni lazima kulipa kodi ili taifa lako liendelee, ila kazi ya kodi ionekane na sio kwa manufaa ya wachache kwa kupiga dili. Kama kazi ya kodi inaonekana kama wakati wa JPM,mzalendo yupo tayari kutoa taarifa kwa anaekwepa kodi kwani anazuia maendeleo ya Taifa.
Mshahara wa Rais unakatwa kodi au yeye siyo mzalendo?
 
Sheria zetu na wanasheria hii ni shida kubwa!!.. Tulipe Kodi Kwa Maendeleo yetu
Bora umekiri kwamba tunatatizo, hata sasa sio kwamba watu hawalipi kodi au hawataki kulipa, shida ni pale inapotapanywa na kufujwa nje ya kufanya kile kilichokusudiwa.

Hapo ndio maana watu wanalalamika. Wangeanza kwanza kushughulikia mianya na upotevu wa pesa zinazokusanywa sasa hivi.
 
Tubadilishe katiba, kwa mzalendo wa kweli kila mmoja anapaswa kuchangia katika ujenzi wa nchi. Kuanzia mkuu wa nchi hakuna anaesamehewa kodi.
 
Kodi ilipwe lakini isiwe ya kuwaumiza wananchi, kumrundikia mwananchi tozo ya miamala ya simu, luku kulipia majengo yasiyo yao, mbolea, bei ya mafuta imepanda, wakati wanasiasa maposho yao hayaguswi, ni unyonyaji na utumwa mamboleo.
 
Back
Top Bottom