My hair my crown
JF-Expert Member
- Feb 5, 2016
- 898
- 2,478
Hiyo ya kuachisha mtoto shule ili mahari ipatikane ni ya wapi tena? anayeoa ndo anayetakiwa atafute mwenyewe mahari. Sasa kama mahari mpaka wadogo zako waachishwe shule ndo ipatikane, utaweza kweli kimuhudumia mkeo? na kulipiwa mahari na wazazi sio sawa maana ni kuruhusu wao baadae waje kuingilia maamuzi kwenye ndoa yako maana hutakuwa na sauti utabaki kukumbushwa tu tulikuolea huyo mke.Ni kumdhalilisha mwanamke ndio maana wazazi wengine wanamwachisha mtoto masomo ili tu wapate mahari . Kama mwanamke ananipenda kama ni mahari tutatafuta pamoja ili tuwape wazazi wetu (pande zote) zawadi kwa kutulea
kwa hiyo sisi tuliozaa mnatuchukua kama mizoga eti?Swali chokozi,km mdada kaisha zalishwa na MTU mwingine unamlipia mahari ?
Au mwanamke yupi anayestahili mahari,aliyetayari na mtoto au bado?
Vipi kwani
HahahaMillion 8 labda awe bikra
Vipi tenaHahaha
Sasa hapo kwenye ml8 unafikikili uta bargain million moja au laki tano tuwe makini mdogo wangu ashawai kutajiwa ngombe saba mbuzi kumi na mbili na ml5 kisa tu kaenda na gari ya mjomba yake kuepusha zile purukushani za usafi yeye alijua atatajia laki tano atoe nusuMahari ni zawadi na sio udhalilishaji, ila kinacho wabana ni ile hali ya familia ku panga kiasi cha mahari, ingekua sawa kama wanaume wangekua wana jipangia wenyewe, lakini asioe bila kutoa mahari. Hii ya familia kupanga ndo inayopelekea wanaume kukimbia maana wanatajiwa kiasi kikubwa na familia zingine wamegeuza mahari ndo pakupatia mtaji.
Na sio ukitajiwa tu unakimbia hata mahari huwa wana bargain bwana, unamoenda mtu si unaomba upunguziwe.
Kwaiyo kwenye 8 yeye atoe 4?Tamaduni tuliyojiwekea waafrika..na ni kama ahsante kwa wazazi wa mwanamke
Ila binafsi mwanaume wangu ajikakamue hata kutoa nusu yake tu
Haha..kama ingekua yafika 8 angetoa tuKwaiyo kwenye 8 yeye atoe 4?
Sasa wewe mwanamke kuna watu hawaoni shida kulipa ila wako rough mpaka utaomba mahari ilejeshweUdhalilishaji huo vipiii unataka kuoa binti wa watu lipa mahari hakuna cha bure
My side sitalipa mahari sababu najua mzigo nilionao ni mkubwa kuliko hiyo mahariHaha..kama ingekua yafika 8 angetoa tu
Bahati nzuri kwetu haifiki hyo 8