Kumbe DP World wako mabara yote; Tanzania kuna nini?

Kumbe DP World wako mabara yote; Tanzania kuna nini?

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mwanzoni zilipotoka habari za kuwepo mkataba wa bandari kati ya Tanzania na kampuni ya DP World nilifikiri hii ni kampuni ya kijanja janja inayoanza shughuli zake nchini. Baadae ilipokuja hoja ya kuwa ni kampuni ya waarabu nikajua athari ya elimu zitolewazo Tanzania.

Nilipojaribu kuangalia historia na utendaji kazi wa kampuni hiyo nikaono kumbe ni kampuni kubwa sana, iliyoanza kazi miaka kadhaa nyuma na kwamba inaendesha shughuli za bandari katika mabara yote na katika nchi zilizoendelea kama Marekani na ndio wapakiaji wakubwa wa ngano za Ukraine pia zikaifikia dunia nzima kiurahisi.

Ramani na kupanuka kwa shughuli za DP world kila siku zinaongezeka mpaka kufikia nchi hata zisizokuwa na bahari.

Zaidi ni kuwa makao makuu yake yako kwenye nchi ya kiarabu lakini viongozi wake na teknolojia wanazotumia havina sura ya uarabu jambo ambalo ni hoja kubwa ya wapinzani wake.

Kama kuna watu wanaopinga mkataba huu kwa maoni yangu wabadili hoja zao zielekee kwenye marekebisho penye mapungu na si kupinga au kutumia kipengele cha uarabu. Wakifanya hivyo watadharaulika na hawataaminika katika misimamo yao mingine ya kisiasa.

Kwa upande mwengine wakisikilizwa na kuachwa mkataba huu basi watazifanya bandari za Tanzania ziwe kama zilivyokuwa karne iliyopita. Zitakuwa kama bandari za kusubiria samaki na majahazi,Meli za mizigo zitaelekea nchi nyengine.

1690093375850.png
 
Tatizo si ufanyaji kazi wa hiyo kampuni, tatizo ni makubaliano yaliyomo kwenye huo mkataba.
Siamini kama mikataba yote iliyongiwa kati ya hiyo kampni na hizo nchi inafanana mkataba wa hapa TZ
hoja ya watetezi sio hiyo
 
Tatizo soo Dp world..Tatizo ni mkataba.
Hatuna shida na Dubai..Tuna shifa na viongiz pamoja na serikali yetu walio ridhia terms za kizezeta .
 
Dp world inayoletwa TANGANYIKA ni ya wahuni wanasiasa mafisadi

Kiufupi ni wanasiasa fulani wanashirikiana na waarabu kujiuzia nchi na kumiliki
 
Sema kweli, tatizo wamiliki wake ni Waarabu Waislam .
Hayo ni ya kwako.
Katika comments zangu sijataja uislam wala waarabu. Husilazimishe mtu kufuata unayoyataka ili kumtoa kwenye mada.
JE HIYO MIKATABA ILIYOSAINIWA NA HIZO NCHI ILIKUWA NA MAPUNGUFU KAMA HUU WA TANZANIA?
 
Hayo ni ya kwako.
Katika comments zangu sijataja uislam wala waarabu. Husilazimishe mtu kufuata unayoyataka ili kumtoa kwenye mada.
JE HIYO MIKATABA ILIYOSAINIWA NA HIZO NCHI ILIKUWA NA MAPUNGUFU KAMA HUU WA TANZANIA?
Naam, hayo ni yangu na yanajionesha shahiri shahiri. Hujaona Mapadri na Maaskofu walivyokomaa?

Mkataba upi unauongelea "huu wa Tanzania"? Ambao unataka kulinganisha nayo ni ipi?
 
Hoja za msingi zipo wazi na zimeshajadiliwa sana.kama una akili utakua umeshazisikia na kuzielewa.mengine yanayojadiliwa ni porojo tu za chawa kutaka kuharibu mjadala kwasababu ya njaa au manufaa yao binafsi.
 
Mwanzoni zilipotoka habari za kuwepo mkataba wa bandari kati ya Tanzania na kampuni ya DP world nilifikiri hii ni kampuni ya kijanja janja inayoanza shughuli zake nchini.Baadae ilipokuja hoja ya kuwa ni kampuni ya waarabu nikajua athari ya elimu zitolewazo Tanzania.
Nilipojaribu kuangalia historia na utendaji kazi wa kampuni hiyo nikaono kumbe ni kampuni kubwa sana,iliyoanza kazi miaka kadhaa nyuma na kwamba inaendesha shughuli za bandari katika mabara yote na katika nchi zilizoendelea kama Marekani na ndio wapakiaji wakubwa wa ngano za Ukraine pia zikaifikia dunia nzima kiurahisi.
Ramani na kupanuka kwa shughuli za DP world kila siku zinaongezeka mpaka kufikia nchi hata zisizokuwa na bahari.
Zaidi ni kuwa makao makuu yake yako kwenye nchi ya kiarabu lakini viongozi wake na teknolojia wanazotumia havina sura ya uarabu jambo ambalo ni hoja kubwa ya wapinzani wake.
Kama kuna watu wanaopinga mkataba huu kwa maoni yangu wabadili hoja zao zielekee kwenye marekebisho penye mapungu na si kupinga au kutumia kipengele cha uarabu.Wakifanya hivyo watadharaulika na hawataaminika katika misimamo yao mingine ya kisiasa.Kwa upande mwengine wakisikilizwa na kuachwa mkataba huu basi watazifanya bandari za Tanzania ziwe kama zilivyokuwa karne iliyopita.Zitakuwa kama bandari za kusubiria samaki na majahazi,Meli za mizigo zitaelekea nchi nyengine.
Issue ni vipengele vya mkataba hapa sio uwepo wao
 
Back
Top Bottom