Kumbe mfumuko wa bei siyo kitu kibaya

Kumbe mfumuko wa bei siyo kitu kibaya

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Siku zote nimekuwa naamini kuwa mfumuko wa bei ni kitu kibaya hadi juzi kati nilipoona kinyume chake kwenye kitabu kimoja. Kabrasha hilo linasema kuwa mfumuko wa bei hadi wa 20 percent unasaidia kukuza uchumi.

Huu unasaidia kutengeneza ajira na kuchangamsha shughuli za kiuchumi. Linaendelea kudai kuwa mfumuko hadi wa 40% hauna athari zozote mbaya kwenye uchumi. Ila Aidi ya hapo ndipo kunakuwa na hyperflation ambao ni sumu kwa uchumi.

Muandishi anashauri kuwa nchi maskini zinatakiwa kumantain mfumuko wa bei hadi wa 20% ili kukuza uchumi wao. Anatoa ni mifano wa nchi ambazo ziliona ukuaji mkubwa wa uchumi wakati zina mfumuko mkubwa na jinsi ukuaji ulivyoshuka baada ya kudhibiti mfumuko.

Hii ni tofauti kabisa na IMF wanavyozilazimisha nchi maskini kuwa na mfumuko wa bei wa single digit. Unakuta hadi serikali zinajisifu kuwa mfumuko wa bei ni 5%, au 4%.

Anasema kuwa watu pekee ambao huathirika na mfumuko wa bei wa hadi 40% ni watu ambao wana kipato fixed kama waajiriwa, lakini anasema kuwa hata nao wanaweza kufaidika kwa ukuaji wa uchumi.

Kumbe mfumuko wa bei ni kitu kizuri!
 
Mona hujaeleza kwa mifano jinsi hiyo nadharia inavyofanya kazi? Kwa mfano, maji ya kunywa yanayouzwa Tsh 500 leo yatasababishaje kuchangamsha uchumi kama yatauzwa kwa Tsh 3000 next week? Au kwa mfano wa mbolea alioutolea mchangiaji no 1?

Lakini je? Unataka kutuaminisha kwamba wanauchumi wetu wabobezi Hawaii chochote kuhusu hasara na faida za kudhibiti mfumuko wa bei ubakie chini?
 
Of course sio kila mara Mfumuko wa Bei (Inflation) ni mbaya ingawa sio kitu kizuri kukientertain. Mfumuko wa bei unakuwa mzuri tu kwa kuvutia wawekezaji ambapo wanakuja na fedha zao za kigeni ambazo zina purchasing power kubwa katika nchi yenye mfumuko wa bei.
 
Mona hujaeleza kwa mifano jinsi hiyo nadharia inavyofanya kazi? Kwa mfano, maji ya kunywa yanayouzwa Tsh 500 leo yatasababishaje kuchangamsha uchumi kama yatauzwa kwa Tsh 3000 next week ? Au kwa mfano wa mbolea alioutolea mchangiaji no 1?

Lakini je? Unataka kutuaminisha kwamba wanauchumi wetu wabobezi Hawaii chochote kuhusu hasara na faida za kudhibiti mfumuko wa bei ubakie chini ?
Mfano mzuri ni mayai ya kware. Yalipoongezeka bei mara mia kadhaa (kutoka kutojulikana hadi kuwa mayai ya bei ghali) watu wakaanza kufuga, kununua na kuuza. Hili lilichangamsha uchumi. Songwe wanalima maharage wanaita mwasipenjele, yalipanda bei sababu walikuwa wanaexport South. Kila mtu alianza kuchangamkia kuyalima. Hili linazalisha ajira na kuchangamsha uchumi. Mifano ni mingi.
 
Mfumuko wa bei unashusha thamani ya pesa, pesa ikishuka thamani na uchumi unashuka Sana.
Hii ni hatari sana kwa nchi zetu hizi ambazo tununua sana nje kuliko kuuza
Upo sahihi, lakini research zinaonyesha kuwa mfumuko wa bei wa hadi asilimia 40 hauna athari kwenye uchumi. Na mfumuko wa hadi 20% unafaida kwenye uchumi. Shida ipo kuanzia 40% kwenda juu.
 
Embu tafuta eneo itisha mkutano na wananchi uwaambie hii "elimu" yako uone kitakachotokea!

Vitu vingine ni obvious,havihitaji kusoma sana makabrasha.

Embu toa mfano wa nchi ambayo ilisaidiwa na mfumuko wa bei wa 40%
 
Mfumuko wa bei ni kitu kibaya sana kwa Uchumi wa Mlaji na wa Nchi.
Hivyo ndivyo tulivyoaminishwa. Lakini hizo hizo nchi tajiri uchumi wao ukidorora huwa wanaweka pesa kibao mtaani na kushusha riba. Kushusha riba na kuongeza money supply ni njia za kuongeza mfumuko wa bei.
 
Hivyo ndivyo tulivyoaminishwa. Lakini hizo hizo nchi tajiri uchumi wao ukidorora huwa wanaweka pesa kibao mtaani na kushusha riba. Kushusha riba na kuongeza money supply ni njia za kuongeza mfumuko wa bei.

Unaweza kuwa umeelewa vibaya, anyway hebu tupe mfano hai mmoja.
 
Imagine unampango wa kwenda kukopa bank, dhamana nyumba yako ambayo thamani yake tsh 300 million.

Mkopo umechukua 70% ya thamani ya Nyumba tsh 210 million.

Mwaka unaofuata kutokana na inflation nyumba imepanda thamani tsh 350 million; ina maana 70% inakuwa 245 million.

Maana yake nini kuna ‘future value’ ya 35 million ambayo bank imepoteza kwenye thamani ya mkopo.

Sasa banks are not stupid kuhakikisha hela wanayokupa leo inaweza nunua kitu kile kile kesho kwenye mkopo utakuta interest ya faida ni 5%, kama inflation ya nyumba 17% as in our example basi total interest ya mkopo wako inaweza kuwa 22% (profit interest 5% + 17% inflation).

Na karibu kila mfanyabiashara anakopa bank sasa kila kitu kikipanda interest za mikopo zinaweza shuka kweli?

Inflation is not good in generally speaking na inflation kwenye high value assets is even worst.

Ndio maana inflation has to be controlled kwa sababu interest za mikopo zikiwa juu na bidhaa zinapanda and this creates the vicious circle ya bank interst, inflation and prices; something has to be controlled.
 
Mfano mzuri ni mayai ya kware. Yalipoongezeka bei mara mia kadhaa(kutoka kutojulikana hadi kuwa mayai ya bei ghali)watu wakaanza kufuga, kununua na kuuza. Hili lilichangamsha uchumi. Songwe wanalima maharage wanaita mwasipenjele, yalipanda bei sababu walikuwa wanaexport South. Kila mtu alianza kuchangamkia kuyalima. Hili linazalisha ajira na kuchangamsha uchumi. Mifano ni mingi.
Mkuu, ulichokitolea hapa ni just a basic principle of demand and supply. The rarer the dearer. Hata maji ya kunywa yakiadimika, chupa ya 500 leo inaweza uzwa kwa sh 2500 kesho, na sababu kubwa sio mfumuko wa bei but demand and supply. Tueleze mfumko wa bei unawezaje kuchangamsha uchumi?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mkuu, ulichokitolea hapa ni just a basic principle of demand and supply. The rarer the dearer. Hata maji ya kunywa yakiadimika, chupa ya 500 leo inaweza uzwa kwa sh 2500 kesho, na sababu kubwa sio mfumuko wa bei but demand and supply. Tueleze mfumko wa bei unawezaje kuchangamsha uchumi?
Moja ya kitu kinasababisha mfumuko wa bei ni exportation. Unafikiri inasababishaje? Exportation inaongeza demand. Demand na supply vinaplay part kubwa kwenye mfumuko wa bei, huwezi kuvitenganisha.
 
Moja ya kitu kinasababisha mfumuko wa bei ni exportation. Unafikiri inasababishaje? Exportation inaongeza demand. Demand na supply vinaplay part kubwa kwenye mfumuko wa bei, huwezi kuvitenganisha.
Mkuu, jaribu hata kutumia common sense. Kwa sasa kuna mfumuko mkubwa wa bei kwenye vifaa vya ujenzi. Je, umesababishwa na export? Je kuna shortage ya vida vya ujenzi tofauti na mwaka jana au juzi iliyopelekea bei kupanda? Na he huku kupanda kumechangamsha vipi uchumi wa nchi? Kukusaidia tu, though mini sijagusa kabisa course yoyote ya uchumi zaidi ya Macro-economics analysis, ungetuambia na CONDITIONS / ASSUMPTIONS under which the theory might work, ungeeleweka. Vinginevyo, the theory, na wewe uliyeileta hamueleweki
 
Mkuu, jaribu hata kutumia common sense. Kwa sasa kuna mfumuko mkubwa wa bei kwenye vifaa vya ujenzi..... je umesababishwa na export? Je kuna shortage ya vida vya ujenzi tofauti na mwaka jana au juzi iliyopelekea bei kupanda? Na he huku kupanda kumechangamsha vipi uchumi wa nchi? Kukusaidia tu, though mini sijagusa kabisa course yoyote ya uchumi zaidi ya Macro-economics analysis, ungetuambia na CONDITIONS / ASSUMPTIONS under which the theory might work, ungeeleweka. Vinginevyo, the theory, na wewe uliyeileta hamueleweki
Mfano, bei ya samaki wanaovuliwa ikiongezeka basi ujue wengi zaidi wataanza kuvua, na wale waliokuwa wanavua watawekeza zaidi. Bei ya ufuta au mbaazi ikiwa juu basi fahamu kuwa wengi watalima na kujiajiri kwenye hiyo sekta.

Unafikiri kwanini watu wanaacha kulima kahawa, ni ajira ngapi zimepotea? Ni kwa sababu bei haipandi kabisa. Unafikiri wangapi wamekimbia kulima mahindi sababu ya bei ndogo? Nafikiri wewe ndiyo unatakiwa kutumia common sense.
 
Upo sahihi, lakini research zinaonyesha kuwa mfumuko wa bei wa hadi asilimia 40 hauna athari kwenye uchumi. Na mfumuko wa hadi 20% unafaida kwenye uchumi. Shida ipo kuanzia 40% kwenda juu.
Kila kitu kina pande mbili. Unachomaanisha kuwa upande wa faida ya mfumuko wa bei ni nyingi zaidi ya upande wa hasara?
 
Scholary books husomi kama novels what is your take? Unakubaliana nae ama? Under what conditions inflation ya hadi 20% ni nzuri?
 
Mfano, bei ya samaki wanaovuliwa ikiongezeka basi ujue wengi zaidi wataanza kuvua, na wale waliokuwa wanavua watawekeza zaidi. Bei ya ufuta au mbaazi ikiwa juu basi fahamu kuwa wengi watalima na kujiajiri kwenye hiyo sekta.

Unafikiri kwanini watu wanaacha kulima kahawa, ni ajira ngapi zimepotea? Ni kwa sababu bei haipandi kabisa. Unafikiri wangapi wamekimbia kulima mahindi sababu ya bei ndogo? Nafikiri wewe ndiyo unatakiwa kutumia common sense.
Bado nakusaidia mkuu, bei ya mbaazi ikiongezeka na wakulima wengi zaidi wakakimbilia julian mbaazi, bado inaangukia kwenye demand and supply. Wakulima kukacha kilimo cha kahawa au mahindi kwa sababu tu bei zimeporomoka bado kunakurudisha pale kwenye demand and supply. Na nikukumbushe tu kuwa demand and supply siyo the only factor inayopelekea mfumuko wa bei, ziko factor nyingine nyingi.

Nikurudishe sasa kwenye swali la msingi, je mfumuko wa bei kwa kiwango cha 20-30% unasaidiaje kuchangamsha uchumi?
 
Back
Top Bottom