Kumbe mfumuko wa bei siyo kitu kibaya

Kumbe mfumuko wa bei siyo kitu kibaya

Of course sio kila mara Mfumuko wa Bei (Inflation) ni mbaya ingawa sio kitu kizuri kukientertain. Mfumuko wa bei unakuwa mzuri tu kwa kuvutia wawekezaji ambapo wanakuja na fedha zao za kigeni ambazo zina purchasing power kubwa katika nchi yenye mfumuko wa bei.
... nimekuelewa; wakati ninyi hela yenu ya ndani inahitajka magunia ya fedha kununua mkate, mwekezaji akija na a few dollars ananunua kijiji kizima!
 
Watanzania bhana!!! Kila kitu wanajua wao! Elimu ya uchumi ina watu wake,

Ona Sasa mnavochangia utopolo!!

Wachumi njooni upande huu, okoeni jahazi.
 
Mkuu, ulichokitolea hapa ni just a basic principle of demand and supply. The rarer the dearer. Hata maji ya kunywa yakiadimika, chupa ya 500 leo inaweza uzwa kwa sh 2500 kesho, na sababu kubwa sio mfumuko wa bei but demand and supply. Tueleze mfumko wa bei unawezaje kuchangamsha uchumi?
Mwalike somebody Kayoza
 
Wewe umechanganya kuongezeka kwa bei na mfumuko wa bei.

Mfumuko wa bei ni simply kupanda bei kusiko fuata taratibu halali za soko lakini pia kukiuka miiko ya kifedha ambayo hupelekea kuua thamani ya pesa au kuifanya pesa kukosa nguvu yake kama tool ya purchasing power.

Mifano ya mambo yanayochangia mifumuko ya bei ni kama ifuatavyo:

1. Ufisadi/Wizi/Udokozi wa pesa za serikali
Wizi wa pesa hufanya pesa zinazoprintiwa na serikali kutoka benki kuu kupita katika mianya au maeneo ambayo yatazifanya zisiwe traced na hatiamae kufika katika uchumi na sekta zake na kufanya manunuzi bila kukusanywa kodi wala kufanya malengo yaliyokusudiwa. Mfano watendaji wa serikali wanapokwiba mabilioni wanakuja kitaa wanatumia kwa kujiachia,eneo husika kutatokea mfumuko wa bei sababu wahusika watakuwa tayari kulipa kiasi chochote bila hofu sababu wamepata pesa bila kutoa jasho na kutumia ni bila uoga.


2. Pesa bandia.
Noti bandia huwa zinachangia sana mfumuko wa bei sababu wahusika wanazisambaza katika uchumi na kuongeza kiasi cha pesa ambacho huwa si halali na hakijawa recorded na BOT.

3. Uzembe wa mamlaka kufuatilia mfumuko wa bei.
Mamlaka zetu kwa kiasi kikubwa hazina meno ya kudhibiti bei za bidhaa sababu ya aidha kuingiliwa kimamuuzi na watendaji wenye masilahi na kupandisha bei na kadhalika. Lakini pia ni kwa kukosa bajeti na nguvu ya kufuatilia na kubana bei.

4. Mrundikano wa tozo na kodi kwa wafanyabiashara.

Hili ni tatizo kubwa sana. Kuna gharama zitokanazo na tozo ambazo hawa viongozi wadangaji wanaziweka nyuma ya pazia na kufanya maisha yawe magumu sana kwa raia. Wafanyabiashara hupandisha bei ili kulinda mitaji yao na kupata faida sababu hawafanyi baishara ili wauze sura.
So hapa mchawi ni serikali.

5. Asilimia kubwa ya bidhaa na huduma hutolewa nje ya mfumo rasmi wa uchumi yaani kuna biashara nyingi zipo nje ya mfumo rasmi na kusoma mzunguko wa fedha. Imagine wafanyabiashara ambao hawawezi pesa benki, ambao huuziana vitu bila mamlaka yoyote kuhusishwa hawa wote huleta shida sana katika uchumi na kuchangia mfumuko wa bei kwenye uchumi.

6. Madalali uchwara.

Hawa mabwege sidhani kama kuna haja ya kuwazungumzia na serikali inabidi waje na sheria kali sana za kuwatokomeza haww madubwana.

Sawa wanatusaidia sana kupata mahitaji yetu ila ufala wao wa kuongeza sifuri una madhara makubwa sana katika uchumi kwa kusababisha bei kupandishwa bila sababu za msingi.

Leo kuna maeno yana hadhi ya kawaida kabisa ila nyumba za kupanga zimekuwa bei ya juu sababu ya hawa takataka.

So ndugu mleta mada, Kimsingi unaposema mfumuko wa bei una umuhimu katika uchumi ni simply unasema kuwa hizi sababu nilizokupa hapa ziwe ni sababu positive katika uchumi na zikubalike.

Yaani ni sawa na mwanaume ambaye ana mke anae danga huko nje kisha anakuja na hizo pesa za udangaji analipa bili za nyumba na kumpatia na mumewe za matumizi halafu mumewe aseme udangaji ni jambo zuri sana kwa familia sababu linasaidia kuongeza kipato cha familia na kumpa uwezo mke kuhudumia familia kama mumewe.
 
Moja ya kitu kinasababisha mfumuko wa bei ni exportation. Unafikiri inasababishaje? Exportation inaongeza demand. Demand na supply vinaplay part kubwa kwenye mfumuko wa bei, huwezi kuvitenganisha.
Nilidhania utasema importation. Sababu imports huwa zinauwa mambo mengi sana mfano viwanda, lakini pia bei zinakuja kwa thamani ya pesa ya kigeni hivyo inasababisha kuongezeka matumizi.

So mfano malumalu, na vifaa vya ujenzi kipindi cha nyuma tulikuwa tunachukua sana nje ambapo ukipiga hesabu kuna kodi, tozo, usafiri wa meli ukijumlisha hela inakuwa kubwa sana ila sasa vinatengenezwa hapa hapa tazama bei zilivyoshuka kwa zaidi ya asilimia 70.

Kwa upande wa export ni tofauti export ndio huwa mkombozi wa uchumi wa sisi mataifa ya dunia ya chini.

Korosho bongo naweza uza kilo mwisho 2000 ila nje kilo nitauza 12,000 sasa huoni hiyo income kwa bidhaaa ile ile na hii itasaidia mimi kuongeza uwekezaji wangu uwe imara katika kilimo cha korosho.

So nadhani ungejielimisha kidogo kuhusu kilimo.
 
Binafs natamani kila kitu kipande bei
Maji
Umeme
Kodi
Tozo
Kodi za barabara kwa vyombo vya moto
Mafuta walau Lita diesel au petrol Lita walau 7000
Mafuta ya kula iwe Lita 10000
Vifaa vya ujezi vipande kwa aslimia hata 60
Mama asijal sisi tupo naye hata kama ccm watamkataa
Mama anaupiga mwingi mno

Makanisa na misikiti ilipekodi
Watumishi mshahara inatutosha asihangaike sana
 
Mfano, bei ya samaki wanaovuliwa ikiongezeka basi ujue wengi zaidi wataanza kuvua, na wale waliokuwa wanavua watawekeza zaidi. Bei ya ufuta au mbaazi ikiwa juu basi fahamu kuwa wengi watalima na kujiajiri kwenye hiyo sekta.

Unafikiri kwanini watu wanaacha kulima kahawa, ni ajira ngapi zimepotea? Ni kwa sababu bei haipandi kabisa. Unafikiri wangapi wamekimbia kulima mahindi sababu ya bei ndogo? Nafikiri wewe ndiyo unatakiwa kutumia common sense.
Ndio maana nikakwambia wewe umeshindwa kuelewa tofauti ya Ongezeko la bei na Mlipuko wa bei. Hebu kajielimishe vema mkuu hapa utatia boko.
 
Siku zote nimekuwa naamini kuwa mfumuko wa bei ni kitu kibaya hadi juzi kati nilipoona kinyume chake kwenye kitabu kimoja. Kabrasha hilo linasema kuwa mfumuko wa bei hadi wa 20 percent unasaidia kukuza uchumi.

Huu unasaidia kutengeneza ajira na kuchangamsha shughuli za kiuchumi. Linaendelea kudai kuwa mfumuko hadi wa 40% hauna athari zozote mbaya kwenye uchumi. Ila Aidi ya hapo ndipo kunakuwa na hyperflation ambao ni sumu kwa uchumi.

Muandishi anashauri kuwa nchi maskini zinatakiwa kumantain mfumuko wa bei hadi wa 20% ili kukuza uchumi wao. Anatoa ni mifano wa nchi ambazo ziliona ukuaji mkubwa wa uchumi wakati zina mfumuko mkubwa na jinsi ukuaji ulivyoshuka baada ya kudhibiti mfumuko.

Hii ni tofauti kabisa na IMF wanavyozilazimisha nchi maskini kuwa na mfumuko wa bei wa single digit. Unakuta hadi serikali zinajisifu kuwa mfumuko wa bei ni 5%, au 4%.

Anasema kuwa watu pekee ambao huathirika na mfumuko wa bei wa hadi 40% ni watu ambao wana kipato fixed kama waajiriwa, lakini anasema kuwa hata nao wanaweza kufaidika kwa ukuaji wa uchumi.

Kumbe mfumuko wa bei ni kitu kizuri!
Wewe umeamini hayo makala uliosoma??????????????
 
Bado nakusaidia mkuu, bei ya mbaazi ikiongezeka na wakulima wengi zaidi wakakimbilia julian mbaazi, bado inaangukia kwenye demand and supply. Wakulima kukacha kilimo cha kahawa au mahindi kwa sababu tu bei zimeporomoka bado kunakurudisha pale kwenye demand and supply. Na nikukumbushe tu kuwa demand and supply siyo the only factor inayopelekea mfumuko wa bei, ziko factor nyingine nyingi.

Nikurudishe sasa kwenye swali la msingi, je mfumuko wa bei kwa kiwango cha 20-30% unasaidiaje kuchangamsha uchumi?
Ukiangalia factors zinazosababisha mfumuko wa bei zote utazikuta zinakuleta kwenye demand and supply. Hatuwezi kuelewana sababu unalazimisha kutenganisha mfumuko wa bei na supply and demand.
 
Wewe umechanganya kuongezeka kwa bei na mfumuko wa bei.

Mfumuko wa bei ni simply kupanda bei kusiko fuata taratibu halali za soko lakini pia kukiuka miiko ya kifedha ambayo hupelekea kuua thamani ya pesa au kuifanya pesa kukosa nguvu yake kama tool ya purchasing power.

Mifano ya mambo yanayochangia mifumuko ya bei ni kama ifuatavyo:

1. Ufisadi/Wizi/Udokozi wa pesa za serikali
Wizi wa pesa hufanya pesa zinazoprintiwa na serikali kutoka benki kuu kupita katika mianya au maeneo ambayo yatazifanya zisiwe traced na hatiamae kufika katika uchumi na sekta zake na kufanya manunuzi bila kukusanywa kodi wala kufanya malengo yaliyokusudiwa. Mfano watendaji wa serikali wanapokwiba mabilioni wanakuja kitaa wanatumia kwa kujiachia,eneo husika kutatokea mfumuko wa bei sababu wahusika watakuwa tayari kulipa kiasi chochote bila hofu sababu wamepata pesa bila kutoa jasho na kutumia ni bila uoga.


2. Pesa bandia.
Noti bandia huwa zinachangia sana mfumuko wa bei sababu wahusika wanazisambaza katika uchumi na kuongeza kiasi cha pesa ambacho huwa si halali na hakijawa recorded na BOT.

3. Uzembe wa mamlaka kufuatilia mfumuko wa bei.
Mamlaka zetu kwa kiasi kikubwa hazina meno ya kudhibiti bei za bidhaa sababu ya aidha kuingiliwa kimamuuzi na watendaji wenye masilahi na kupandisha bei na kadhalika. Lakini pia ni kwa kukosa bajeti na nguvu ya kufuatilia na kubana bei.

4. Mrundikano wa tozo na kodi kwa wafanyabiashara.

Hili ni tatizo kubwa sana. Kuna gharama zitokanazo na tozo ambazo hawa viongozi wadangaji wanaziweka nyuma ya pazia na kufanya maisha yawe magumu sana kwa raia. Wafanyabiashara hupandisha bei ili kulinda mitaji yao na kupata faida sababu hawafanyi baishara ili wauze sura.
So hapa mchawi ni serikali.

5. Asilimia kubwa ya bidhaa na huduma hutolewa nje ya mfumo rasmi wa uchumi yaani kuna biashara nyingi zipo nje ya mfumo rasmi na kusoma mzunguko wa fedha. Imagine wafanyabiashara ambao hawawezi pesa benki, ambao huuziana vitu bila mamlaka yoyote kuhusishwa hawa wote huleta shida sana katika uchumi na kuchangia mfumuko wa bei kwenye uchumi.

6. Madalali uchwara.

Hawa mabwege sidhani kama kuna haja ya kuwazungumzia na serikali inabidi waje na sheria kali sana za kuwatokomeza haww madubwana.

Sawa wanatusaidia sana kupata mahitaji yetu ila ufala wao wa kuongeza sifuri una madhara makubwa sana katika uchumi kwa kusababisha bei kupandishwa bila sababu za msingi.

Leo kuna maeno yana hadhi ya kawaida kabisa ila nyumba za kupanga zimekuwa bei ya juu sababu ya hawa takataka.

So ndugu mleta mada, Kimsingi unaposema mfumuko wa bei una umuhimu katika uchumi ni simply unasema kuwa hizi sababu nilizokupa hapa ziwe ni sababu positive katika uchumi na zikubalike.

Yaani ni sawa na mwanaume ambaye ana mke anae danga huko nje kisha anakuja na hizo pesa za udangaji analipa bili za nyumba na kumpatia na mumewe za matumizi halafu mumewe aseme udangaji ni jambo zuri sana kwa familia sababu linasaidia kuongeza kipato cha familia na kumpa uwezo mke kuhudumia familia kama mumewe.
Mfumuko wa bei siyo kitu cha ajabu au tofauti na kuongezeka kwa bei. Inflation ni kuongezeka kwa bei kulikopimwa kwa muda fulani. Mara nyingi hupimwa kwa mwaka. Unaweza pima ongezeko la bei kwa miaka kumi, miaka miaka mia nk. So mfumuko wa bei ni kasi ya kuongezeka kwa bei. Kuna kasi ambayo ni nzuri kwa uchumi(hadi 20%) kuna kasi isiyo na athari hasi kwa uchumi(hadi 40%) na kuna mfumuko mbaya ambao ni kuanzia 40% kwenda juu.

Hata bei ikiongezeka kwa asilimia 1% kwa mwaka. Huo ni mfumuko wa bei wa asilimia moja. Kama hutaki mfumuko wa bei(inflation)maana yake unataka bei ibaki vilevile miaka yote.
 
Nilidhania utasema importation. Sababu imports huwa zinauwa mambo mengi sana mfano viwanda, lakini pia bei zinakuja kwa thamani ya pesa ya kigeni hivyo inasababisha kuongezeka matumizi.

So mfano malumalu, na vifaa vya ujenzi kipindi cha nyuma tulikuwa tunachukua sana nje ambapo ukipiga hesabu kuna kodi, tozo, usafiri wa meli ukijumlisha hela inakuwa kubwa sana ila sasa vinatengenezwa hapa hapa tazama bei zilivyoshuka kwa zaidi ya asilimia 70.

Kwa upande wa export ni tofauti export ndio huwa mkombozi wa uchumi wa sisi mataifa ya dunia ya chini.

Korosho bongo naweza uza kilo mwisho 2000 ila nje kilo nitauza 12,000 sasa huoni hiyo income kwa bidhaaa ile ile na hii itasaidia mimi kuongeza uwekezaji wangu uwe imara katika kilimo cha korosho.

So nadhani ungejielimisha kidogo kuhusu kilimo.
Kila mtu akianza kuuza korosho nje kwa Tsh 12,000 kwa kilo utashangaa aotomatically hata hapa bongo haiwi 2,000 tena kwa kilo. Itafika hata elfu nane na zaidi huko. Kama ndani ya mwaka bei imeongezeka kutoka 2000 hadi elfu nne maana yake una mfumuko wa bei ya korosho kwa asilimia 100. Hivyo ndivyo exportation inasababisha mfumuko wa bei.

Unafikiri kwanini serikali inakataza kuuza mahindi nje? Inajua kuwa mahindi yakianza kuwa exported nje kwenye bei kunwa, bei ya ndani nayo automatically itapanda. Hivyo ndivyo exportation inavyosababisha inflation. Usichambue hili jambo kwa namna uliyokariri kuwa mfumuko wa bei ni dubwana baya.
 
Ndio maana nikakwambia wewe umeshindwa kuelewa tofauti ya Ongezeko la bei na Mlipuko wa bei. Hebu kajielimishe vema mkuu hapa utatia boko.
Huwezi kutenganisha kuongezeka kwa bei na mfumuko wa bei(inflation). Mfumuko wa bei ni kipimo cha ongezeko la bei kwa muda fulani.

Na huo mlipuko wa bei ndiyo nini?
 
Kila mtu akianza kuuza korosho nje kwa Tsh 12,000 kwa kilo utashangaa aotomatically hata hapa bongo haiwi 2,000 tena kwa kilo. Itafika hata elfu nane na zaidi huko. Kama ndani ya mwaka bei imeongezeka kutoka 2000 hadi elfu nne maana yake una mfumuko wa bei ya korosho kwa asilimia 100. Hivyo ndivyo exportation inasababisha mfumuko wa bei.

Unafikiri kwanini serikali inakataza kuuza mahindi nje? Inajua kuwa mahindi yakianza kuwa exported nje kwenye bei kunwa, bei ya ndani nayo automatically itapanda. Hivyo ndivyo exportation inavyosababisha inflation. Usichambue hili jambo kwa namna uliyokariri kuwa mfumuko wa bei

Kila mtu akianza kuuza korosho nje kwa Tsh 12,000 kwa kilo utashangaa aotomatically hata hapa bongo haiwi 2,000 tena kwa kilo. Itafika hata elfu nane na zaidi huko. Kama ndani ya mwaka bei imeongezeka kutoka 2000 hadi elfu nne maana yake una mfumuko wa bei ya korosho kwa asilimia 100. Hivyo ndivyo exportation inasababisha mfumuko wa bei.

Unafikiri kwanini serikali inakataza kuuza mahindi nje? Inajua kuwa mahindi yakianza kuwa exported nje kwenye bei kunwa, bei ya ndani nayo automatically itapanda. Hivyo ndivyo exportation inavyosababisha inflation. Usichambue hili jambo kwa namna uliyokariri kuwa mfumuko wa bei ni dubwana baya.
Ushindani wa biashara kwa hapa nchini hauko kwenye kuuza kwa wingi bali umejikita kibei kabla ya kuangalia usambazaji,,,kuna bidhaa zinazalishwa na kuwa na bei shindani lakin figisu zinafanywa vibaya sana ili kukwamisha uzalishaji wa bidhaa moja na ingine kisa bei hazilingani
Na kwa nchi yetu hatuangalii ubora tumejikita katika bei
 
Mfano mzuri ni mayai ya kware. Yalipoongezeka bei mara mia kadhaa (kutoka kutojulikana hadi kuwa mayai ya bei ghali) watu wakaanza kufuga, kununua na kuuza. Hili lilichangamsha uchumi. Songwe wanalima maharage wanaita mwasipenjele, yalipanda bei sababu walikuwa wanaexport South. Kila mtu alianza kuchangamkia kuyalima. Hili linazalisha ajira na kuchangamsha uchumi. Mifano ni mingi.

Mfumuko wa bei yaani INFLATION refers to the general price level in an economy na sio kwa bei ya zao moja!!
 
Mfumuko wa bei yaani INFLATION refers to the general price level in an economy na sio kwa bei ya zao moja!!
Lakini huanza kwa kuhesabu bei ya kitu kimoja kimoja kwenye uwiano wake katika uchumi.
 
Lakini huanza kwa kuhesabu bei ya kitu kimoja kimoja kwenye uwiano wake katika uchumi.

Kupanda kwa bei ya maharage sio lazima iathiri bei ya bidhaa nyingine!!! Lakini kupanda kwa bei ya mafuta ya petrol na Diesel kunaweza kuwa chanzo cha mfumuko wa bei wa bidhaa nyingi!!
 
Mfano mzuri ni mayai ya kware. Yalipoongezeka bei mara mia kadhaa (kutoka kutojulikana hadi kuwa mayai ya bei ghali) watu wakaanza kufuga, kununua na kuuza. Hili lilichangamsha uchumi. Songwe wanalima maharage wanaita mwasipenjele, yalipanda bei sababu walikuwa wanaexport South. Kila mtu alianza kuchangamkia kuyalima. Hili linazalisha ajira na kuchangamsha uchumi. Mifano ni mingi.
mfano wako unaendana na nyanya ile mwaka jana uhaba wa nyanya kupanda bei
umefanya wengi wajifunze kuhusu kilimo cha nyanya
na sasa leo hii tunaona faida nyanya zimekuwa nyingi wakulima walokuwa hawafikilii kulima nyanya wameongeza kipato

so mfumuko wa bei wa nyanya mwaka jana umeleta faida kwa sisi walaji na wakulima wapya
 
U
Kupanda kwa bei ya maharage sio lazima iathiri bei ya bidhaa nyingine!!! Lakini kupanda kwa bei ya mafuta ya petrol na Diesel kunaweza kuwa chanzo cha mfumuko wa bei wa bidhaa nyingi!!
Kwahiyo mfumuko wa bei unapimwa kwa mafuta tu?
 
U
Kwahiyo mfumuko wa bei unapimwa kwa mafuta tu?

Mfumuko wa bei hupimwa kwa wastani wa bei za bidhaa nyingi kupanda i; mafuta kama yakipanda bei na kwavile yanatumika kwenye usafirishaji wa bidhaa huchangia katika kupanda kwa bei huko!!
 
Kila mtu akianza kuuza korosho nje kwa Tsh 12,000 kwa kilo utashangaa aotomatically hata hapa bongo haiwi 2,000 tena kwa kilo. Itafika hata elfu nane na zaidi huko. Kama ndani ya mwaka bei imeongezeka kutoka 2000 hadi elfu nne maana yake una mfumuko wa bei ya korosho kwa asilimia 100. Hivyo ndivyo exportation inasababisha mfumuko wa bei.

Unafikiri kwanini serikali inakataza kuuza mahindi nje? Inajua kuwa mahindi yakianza kuwa exported nje kwenye bei kunwa, bei ya ndani nayo automatically itapanda. Hivyo ndivyo exportation inavyosababisha inflation. Usichambue hili jambo kwa namna uliyokariri kuwa mfumuko wa bei ni dubwana baya.
Kwahiyo mkuu na kupanda kwa bei ya bidhaa za chuma kama nondo inamaanisha kuwa kwa sasa tunaexport chuma kwa bei ya juu sana au?

Sent from my M2101K7AG using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom