Kumbe mtandao wa Twitter unaweza kuhatarisha usalama endapo utatumika vibaya, ndio maana huwa unafungwa!

Kwa sababu ndio umeamka kutoka usingizini fahamu kwamba Twitter imekuwa inafungia watumiaji ambao wanakiuka sheria zake za uendeshaji, hata hao wanaharakati wengine wamewahi kufungiwa na Twitter. Twitter imeonyesha weledi wa hali ya kumfungia hata mtu mkubwa kama Trump. Zaidi fahamu Twitter ni kampuni binafsi ya watu, sio chombo cha serikali.
 
No!Twitter ya Tanzania imefungiwa na serekali lakini kule Marekani account ya twitter ya Trump imefungiwa na kampuni ya twitter baada ya trump kuvunja policy za twitter.Sasa wewe hapa unalinganisha vitu viwili tofauti kabisa!
Sijalinganisha ndio maana nimetoa mifano mitatu!
 
Mbona fb Na insta huzitaji?
Hata simu yako inaweza kuhataridha.
Kila myu ni hatari.
Hata meko alimpoteza ben saanane
 
Wakati mwingine ukiangalia angle ya mwandishi unabaki unacheka tu!Uwezo wa kujenga hoja kwa watanzania wengi ni tatizo kubwa!
Naomba niishie hapo!
 

Sababu za kufungia mtandao wa Twitter kwa Tanzania ni ili chama tawala kiibe uchaguzi. Na sababu ya kufungia akaunti ya Trump kwenye mtandao wa Twitter, ni kumzuia kupotosha umma na kuhamasisha mapingamizi uchwara dhidi ya serikali halali baada ya kushindwa.
 
Wakati mwingine ukiangalia angle ya mwandishi unabaki unacheka tu!Uwezo wa kujenga hoja kwa watanzania wengi ni tatizo kubwa!
Naomba niishie hapo!
Hahahaaaa...... Wewe endelea kunywa mbege na kisusio bwashee!

Haya mambo waachie akina Halima James Mdee na mama Kaboyoka wa Kilimanjaro mpya!
 
Sasa kuna tofauti kati ya uchochezi wa Antipas na Trump?
The difference is very clear, kule Marekani Twitter wamefunga akaunti ya mtu mmoja Trump, wakati serikali ya Tanzania imezuia matumizi ya twitter kwa watanzania wote wenye hatia na wasio na hatia.
 
The difference is very clear, kule Marekani Twitter wamefunga akaunti ya mtu mmoja Trump, wakati serikali ya Tanzania imezuia matumizi ya twitter kwa watanzania wote wenye hatia na wasio na hatia.
Trump kazuiwa asiteme sumu na watanzania wamezuiwa wasinywe sumu.

Kitu ni kile kile!
 
Hata kalamu yako inaweza ila wanashindwa kutunyang'anya.
 
Unachanganya mambo. Huko Marekani, Rais Trump, mbaguzi, kaburu, dikteta na asiyejali maslahi ya taifa la Marekani, kafungiwa akaunti yake binafsi ya Twitter, baada ya kuitumia kufanya vitendo vilivyosababisha vifo, kuhujumu vyombo vya demokrasia, vya kikatiba vya taifa, na kusababisha vurugu kubwa.

Serikali ya Tanzania iliagiza "kuzimwa" huduma nzima ya Internet ikiwemo Facebook, Twitter, Whattsap, Web, nk. Kipindi cha uchaguzi na baada ya hapo, kinyume na katiba, ili kuminya uhuru wa mawasiliano halali. Kwa kifanyavhivyo, serikali ilihujumu, kama alivyofanya Trump, vyombo vya demokrasia.

Na wala si kwamba vurugu zingetokea, bali serikali ilihofia vitendo vyake vya wizi wa kura vingeanikwa wazi.

Tofautisha akaunti moja ya mtu anayehatarisha amani, tena tayari keshahatarisha amani, inafungwa, dhidi ya huduma nzima ya Twitter kufungwa.

Mtu yeyote ana uhuru kamili wa kufunga akaunti yake, kama alivyofanya Kenyatta. Hapo wala hajamfungia yeyote bali yeye mwenyewe. Unalinganishaje hayo na huu ujinga uliofanywa na serikali ya Magufuli?
 
Trump kazuiwa asiteme sumu na watanzania wamezuiwa wasinywe sumu.

Kitu ni kile kile!
Watanzania wamefungiwa na serikali inayoua watu, inayozuia maelfu wasigombee, kwa kuwaengua. Yote hiyo ni hofu ya kushindwa. Hakuna tofauti kati ya Trump na Magufuli. Kinachomdhibiti Trump ni mifumo imara ya Marekani. Magufuli wetu anajifanyiavatakavyo
 
Sio kufungwa twitter, twitter haijawahi kufungwa ila mtu fulani akionekana na ulimwengu anaweza kusababisha hali ya taharuki kama Donald Trump hapo Jumatano iliyopita ilifungwa account yake kwa saa 24 tu.
 
No!Twitter ya Tanzania imefungiwa na serekali lakini kule Marekani account ya twitter ya Trump imefungiwa na kampuni ya twitter baada ya trump kuvunja policy za twitter.Sasa wewe hapa unalinganisha vitu viwili tofauti kabisa!
Vp kama twitter wameifunga account ya DT kwa kuongozwa na serikali nyuma ya pazia
 
Sasa kuna tofauti kati ya uchochezi wa Antipas na Trump?
Hakuna tofauti ila wapanua midomo wa ufipa wanaona kuna tofauti. Tangu maandanano yaanze ya kuvamia bunge na mauaji ya watu kadhaa kutokea sijaona kauri au tamko lolote kutoka kwa Lissu, Bagonza au Mwamba wa ufipa.
 
Kilakitu duniani kinaweza kusababisha uvunjifu wa amani, ni ajabu kwa umri wako huo kutolijua hilo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…