KUMBUKIZI: Mada maalum ya kumuenzi Munga Tehnan na kazi zake

KUMBUKIZI: Mada maalum ya kumuenzi Munga Tehnan na kazi zake

Ukiweka ahadi lazima uitimize..Ukiweka nadhiri ni lazima uitangue la sivyo itakutesa kifikra na kudai utanguzi.

Mwaka wa jana kwenye post moja, tukiwa na mjadala, tulimjadili gwiji wa falsafa maizi Hayati Munga Tehnan na nikaahidi kuna na mada maalum kwa ajili yake kumuenzi. Naomba sasa nitangue nadhiri na ahadi yangu hii kupitia mada hii.

Kwa wengi wasiomfahamu ndio alikuwa Mmiliki wa gazeti la utambuzi liitwalo JITAMBUE na MSHAURI. Humo ndani kulijaa madini tupu ya falsafa kindakindaki, saikolijia, mambo ya kiroho kijamii hata utani na simulizi za kufurahisha sana.

Mimi ni mmoja wa shabiki na mwanafunzi wake mkubwa... Wengine ninaoweza kuwakumbuka kwa haraka ni pasco na Mtambuzi ..Natambua list ni ndefu na kila mmoja atakuja na mchango wake

Uzi utakuwa updated kutokana na kadiri maudhui yatakavyokuwa yanapatikana ili hatimaye tuwe na mada iliyoshiba kumhusu Munga Tehnan.

Naamini kati yetu kuna wanaojua historia yake, maana mtandaoni haupatikani.

Ombi kwa Moderator Kama kuna uwezekano wa kuziweka mada zake pamoja kwenye mada moja kuu, zile zenye maudhui ya kufanana.

Ombi kwa wana JF kama kuna mwenye hard copy ya kazi zake kupitia JITAMBUE pls share.
Kaka mbona sukuwahi kuona huu Uzi !? wakati nipo humu yangu 2014?
 
Munga alifundisha njia mbalimbali ikiwa kupitia katika Gazeti la Jitambue, vipindi vya Televisheni vilivyorushwa kupitia kituo cha TBC 1 wakati huo ikijulikana kama TVT.
Pale ilipo KIBO PARK karibu na Kimara kona/ROMBO , ndipo ilipokuwa Nyumba ya utambuzi,ilikuwa karibu na barabara ikavunjwa wakati wanajenga njia ya mwendokasi.
 
Back
Top Bottom