Kumbukumbu Kutoka Maktaba 1989 Askofu Mkuu Marko A Mgulunde, Pd. W. Slaa na Mama Getrude Mongela

Kumbukumbu Kutoka Maktaba 1989 Askofu Mkuu Marko A Mgulunde, Pd. W. Slaa na Mama Getrude Mongela

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1732186468343.jpeg

Mhashamu Askofu Mkuu Marko A Mgulunde akimpongeza Mama Getrude Mongela mara baada ya kutoa mada yake iliyohusu uhusiano wa kanisa na serikali kwenye warsha ya Caritas; huku Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Pd. W Slaa (kushoto) akiangalia. [PICHA Pd. Anthony Chilumba].

Kiongozi Toleo la Kwanza December 1989

Lakini kupata picha kamili tambua na uelewe kuwa Pd. W. Slaa huyo hapo juu pichani akiwa nje ya uongozi wa kanisa alichaguliwa na chama chake CHADEMA kugombea urais wa Tanzania akipambana na Jakaya Mrisho Kikwete wa CCM mwaka wa 2010.

(Picha hiyo hapo juu inatoka katika ''scrap book'' yangu ambayo sasa ina umri wa miaka 46 ingawa imeacha kufanya kazi kwa miaka mingi.

Imestaafishwa na computer).​
 
Ungesema unachotaka kusema mzee wangu with plain words. Hamna haja ya kupinda pinda. Nyosha rula. Weka mpira kati Wagaratia na Wavaa kobazi mtoane ngeu humu.
Umtama...
Nakuwekea picha nyingine kutoka ''scrap book.'':

1732187807181.png
BI. TITI MOHAMED NA RAIS ALI HASSAN MWINYI IKULU SIKU YA EID EL FITR 1989

Picha hiyo ya Bi. Titi Mohamed na Raid Ali Hassan Mwinyi nimeitoa kwenye "scrap book" yangu yenye umri wa miaka 44.

Tabia hii nimetokanayo mbali toka udogoni labda Nina miaka 10.
Wanetu leo hawajui nini "scrap book" kwa kuwa simu zao zinahifadhi kila kitu hata vile asivyopenda.

Hatuwezi kuwalaumu.

likuwa siku ya Eid El Fitr 1989 na picha hii ilitoka ukurasa wa mbele wa Daily News la tarehe 8 May.

Rais Mwinyi aliwaalika Ikulu Viongozi wa Chama na Serikali, Watu Maarufu wa Mjini na Masheikh asubuhi kuja kustaftahi pamoja na yeye Ikulu.

Picha hiyo inamuonyesha Rais Mwinyi akimkaribisha Bibi Titi Ikulu.
 
Unavyopenda udini utafikiri una hatimiliki ya huko akhera.. siwezi kushangaa nikisikia unafuga majini km wazee wenzio wa kiswahili..
Yoso,
Hakika Uislam naupenda mno.

Huu ni mwaka wa 26 toka nilipoandika kitabu changu cha kwanza: ''The LIfe and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika.''

Kitabu hiki kimebadili maisha yangu na kimebadili historia ya uhuru wa Tanganyika na kimebadili pia historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Jina la kitabu liliwashtua wengi.

Kama kupenda Uislam kuna uhusiano na kufuga majini mimi nimekuwa hivi toka udogoni na kuwa hivi ni malezi yetu.

Kufuga majini ni ilm maalum nimeelezwa watu wanajifunza.

Majini ni viumbe kama sisi wameumbwa na Allah.
Nilipokuwa mtoto nilimfahamu Sheikh mmoja jina lake Mwalimu Bakari.

Mwalimu Bakari alikuwa mtu maarufu mitaa ya Gerezani akiishi Mtaa wa Livingstone na Kirk Street (Lindi Street).

Mwalimu Bakari walimpa jina lingine wakazi wa Dar es Salaam.
Walimwita Mwalimu Bakari ''Sethabari.''

Maana ya hili jina lingine ni kuwa mjuzi wa yale ambayo hayaonekani na macho.

Mimi alitokea kunipenda kwa kuwa nilikuwa nimefiwa na mama yangu nikiwa na umri wa miaka minne.

Akiniona alikuwa ananishika kichwa na kuniombea dua na kunifariji kwa kunipa fedha.

Hii ilikuwa kawaida yake.

Mwalimu Bakari watu wakihadithia mengi kuhusu yeye kuwa alikuwa anaweza kuzungumza na majini na kuwatuma kazi na wakamtii.

Kwa hakika ni ilm ambayo sijakutana na mtaalamu akanieleza hasa undani wake.

Wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika katika Baraza la Wazee wa TANU alikuwa Sheikh Issa Nasr kutoka Bagamoyo.

Sheikh Issa Nasr nimeambiwa alikuwa ujuzi mkubwa wa ilm ya majini.

Katika utafiti wangu wa kitabu cha Abdul Sykes nilifahamishwa kuwa Sheikh Issa Nasr alikuwa mmoja wa ''walinzi maalum' wa Mwalimu.

Wanasema popote alipokuwa Nyerere yeye atakuwa karibu yake na mpashaji habari wangu anasema hapo yuko na ''askari'' zake ambao hawaonekani.

Huyu aliyekuwa akinipa taarifa hizi ameniambia yeye akimjua Sheikh Issa Nasr toka udogoni kwake Bagamoyo na wao walipokuwa watoto wakimuona Sheikh Nasr amekaa nje ya nyumba yake walikuwa wanabadilisha njia kwa kumuogopa.

Mimi nikaamua kufanya utafiti kuangalia picha za Nyerere kama nitamuona Sheikh Issa Nasr karibu ya Mwalimu akipiga doria na jeshi lake la askari maalum.

Niliweza kuona picha mbili na zote tawire.
Sheikh Issa yuko pembeni ya Mwalimu Nyerere.

Picha ya kwanza ni ile ya Baraza la Wazee wa TANU iliyopigwa mwaka wa 1957.

Angalia picha hiyo hapo chini Sheikh Issa Nasr ni huyo aliyechutama miguuni kwa Nyerere na fimbo begani.

Picha ya pili ni ya mwaka wa 1961 siku Ian Macleod Waziri wa Makoloni alipotoa siku ya uhuru wa Tanganyika Karimjee Hall mwaka wa 1961.

Angalia picha hiyo utamuona Nyerere kabebwa mabegani na Sheikh Issa Nasr yuko pembeni yake.

1732189790611.jpeg

Sheikh Issa Nasr huyu chini ya Mwalimu Nyerere ni wa pili kushoto baada ya aliyevaa koti jeusi
1732190066364.png

Kulia ni Sheikh Issa Nasr​
 
Mhashamu Askofu Mkuu Marko A Mgulunde akimpongeza Mama Getrude Mongela mara baada ya kutoa mada yake iliyohusu uhusiano wa kanisa na serikali kwenye warsha ya Caritas; huku Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Pd. W Slaa (kushoto) akiangalia. [PICHA Pd. Anthony Chilumba].

Kiongozi Toleo la Kwanza December 1989

Lakini kupata picha kamili tambua na uelewe kuwa Pd. W. Slaa huyo hapo juu pichani akiwa nje ya uongozi wa kanisa alichaguliwa na chama chake CHADEMA kugombea urais wa Tanzania akipambana na Jakaya Mrisho Kikwete wa CCM mwaka wa 2010.

(Picha hiyo hapo juu inatoka katika ''scrap book'' yangu ambayo sasa ina umri wa miaka 46 ingawa imeacha kufanya kazi kwa miaka mingi.

Imestaafishwa na computer).​
Nini hasa lengo la bandiko lako hili??
Linatufundisha nini hasa?
 
Mohamed Said Babu Natamani kujua machache kuhusu John Okelo field marshal .

Nini kilimkuta baada ya mapinduzi ya Zanzibar?

Kwanini hakupata wadhifa wowote baada ya mapinduzi.
Aliondoka kwa kupenda au walimtimua?

Alihongwa chochote?
Dume...
Ingia Google kuna mengi kuhusu Okello.
 
Mhashamu Askofu Mkuu Marko A Mgulunde akimpongeza Mama Getrude Mongela mara baada ya kutoa mada yake iliyohusu uhusiano wa kanisa na serikali kwenye warsha ya Caritas; huku Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Pd. W Slaa (kushoto) akiangalia. [PICHA Pd. Anthony Chilumba].

Kiongozi Toleo la Kwanza December 1989

Lakini kupata picha kamili tambua na uelewe kuwa Pd. W. Slaa huyo hapo juu pichani akiwa nje ya uongozi wa kanisa alichaguliwa na chama chake CHADEMA kugombea urais wa Tanzania akipambana na Jakaya Mrisho Kikwete wa CCM mwaka wa 2010.

(Picha hiyo hapo juu inatoka katika ''scrap book'' yangu ambayo sasa ina umri wa miaka 46 ingawa imeacha kufanya kazi kwa miaka mingi.

Imestaafishwa na computer).​
Unapoaandika haya, mawazo yako yapeleke BUGANDO,KCMC, ST .FRANCIS IFAKARA, ITIGI, IKONDA MAKETE ,NDANDA, na nyingine nyingi ...halafu kunywa maji upoze kichwa ukalale ! Kaa huna usingizi fungua TV uangalo kinachoendelea Gaza,Lebanon , ...na kwa msisitizo usisahau SUDAN!
 
Back
Top Bottom