Tatizo ndugu zangu waislam hawajiamin na din yao, sasa kama waislamu wa saudia nao wanalalamika kunyanyaswa, nan awasaidieView attachment 1173754
Nimemjua Prof. Kighoma Ali Malima katika siku zake za mwisho wa maisha yake na nilijifunza mengi kutoka kwake kuhusu hali ya Waislam toka tupate uhuru mwaka wa 1961.
Nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes kitabu hiki katika utangulizi nilikitoa kama tabaruku na kumbukumbu kwa Prof. Malima.
Inafaa siku kama ya leo kutafakari ingekuwaje iwapo kama Prof. Malima angeishi na akawa ni mmoja wa viongozi wa vyama vya siasa vilivyopo hivi sasa na Prof. Malima akiwa na agenda ya kuleta usawa wa kweli katika jamii hii yetu.
Prof. Malima aliamini kuwa njia pekee ya kuleta haki na usawa kwa wote ni kwake kupigania hili nje ya CCM na kwa ajili hii alijitoa kwenye chama hicho.
Mkutano wake wa kwanza wa hadhara na ndiyo alioutumia kujitoa CCM aliufanya Tabora Viwanja Vya Uyui.
Kishindo chake kilikuwa kikubwa.
Mkasa mkubwa ulitokea pale vyombo vya habari ambavyo vyote kwa sababu za wazi vilikuwa vikimpiga vita Prof. Malima toka akiwa CCM na katika Baraza la Mawaziri vilipoandika kuwa Prof. Malima atajitoa CCM ndani ya msikiti Tabora.
Sheikh Issa Mavumbi sheikh wa BAKWATA alitumika bila kujijua katika propaganda hizi na alipata fedheha kubwa kutoka kwa umma wa Waislam wa Tabora pale alipoletwa na polisi msikitini Tabora kuja kutahadharisha kuwa msikiti ule usimruhusu Prof. Malima kufanya siasa msikitini na kujitoa CCM akiwa ndani ya msikiti.
Vurugu kubwa ilitokea msikitini pale na msikiti siku ile ya Ijumaa ulikuwa umejaa hadi nje kwa ile propaganda iliyokuwa imezagaa kote kuwa Prof. Malima atajitoa CCM ndani ya msikiti ule.
Ilikuwa katika taharuki hii hapo ndipo aliposimama mwanasiasa mkongwe na muasisi wa TANU na harakati za kudai uhuru Mzee Bilal Rehani Waikela kutuliza hali ile.
Mzee Waikela akamuuliza Sheikh Mavumbi habari za Prof. Malima kuja msikitini kujitoa CCM yeye kapewa na nani?
Sheikh Mavumbi hakuwa na majibu.
Mzee Waikela akawauliza Waislam kama kuna mtu yeyote mle ndani ameomuona Prof. Malima ndani ya msikiti ule.
Prof. Malima hakuwapo Tabora siku ile achilia mbali kuwa ndani ya msikiti ule.
Sheikh Mavumbi alitolewa kwa haraka pale msikitini na polisi wale wale waliomleta mara ya kwanza huku kivumo cha, ''Takbir,'' kikitanda ndani na nje ya msikiti.
Sheikh Mavumbi ilimdhihirikia kuwa kasababisha vurugu ndani ya msikiti pasi na sababu yoyote.
Hii ilikuwa katika sala ya Ijumaa na baada ya Sheikh Mavumbi na askari kuondoka khutba ya Ijumaa ikaanza na Waislam wakakamilisha ibada kwa utulivu.
Hii ndiyo ilikuwa fungua pazia la Prof. Malima pale alipojitoa CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uyui.
Ghafla joto la siasa nchi nzima lilipanda vibaya sana.
Harakati za chinichini za miaka mingi zilikuwa zimewatayarisha Waislam kusimama na kuuliza nini kimetokea kuwafanya wao juu ya mchango wao mkubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika leo wamekuwa raia daraja la pili?
Waislam walitegemea Prof. Malima sasa akiwa nje ya CCM ataiweka agenda hii uwanjani peupe ijadiliwe na ufumbuzi upatikane.
Inatosha kwa Prof. Malima akakumbukwa kwa hili.
Wacha uongo. Malima hajawahi kumnyonga mtu.Ni mengi na wala si ya kuambiwa. Alikuwa anapendelea kiuwazi waislam na kuwanyongelea mbali ambao si waislam. Usinichokoze nitoe vidhibiti hata kutaja mengine. Tuishie hapo mtetezi wa uislam
Nahisi "lecturer" wako alikuwa anakujaza ujinga.*..Waislam kusimama na kuuliza nini kimetokea kuwafanya wao juu ya mchango wao mkubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika leo wamekuwa raia daraja la pili?'*
Nikiwa chuo lecturer wetu wa Historia aligusia kua, waislamu kupitia chama chao waliwaomba wakoloni wasiachie kwanza madaraka kwakua waislamu wengi hawakua wamepata elimu na hawana nafasi za juu katika TANU.
Kama historia inasema hivi, na huu uzi umesema vingine. Je hii inamaanisha kulikua na kundi la waislamu lililopigania uhuru na kundi jingine likizuia uhuru usitolewe kwanza?
Mama yangu hata kama ulipotokea kuna moto ukifika kwenye kisima hauna sababu ya kuhisi bado upo kwenye moto.Nahisi "lecturer" wako alikuwa anakujaza ujinga.
Kama hauufahamu mchango wa Waislam kuhusu kudai Uhuru wa Tanganyika ngoja tumuombe mwanahistoria Allama Mohamed Said aje kutupa darsa kidogo kuhusu hayo.
Allama tunakuomba utusaidie kujibu hili swali.
Castr,*..Waislam kusimama na kuuliza nini kimetokea kuwafanya wao juu ya mchango wao mkubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika leo wamekuwa raia daraja la pili?'*
Nikiwa chuo lecturer wetu wa Historia aligusia kua, waislamu kupitia chama chao waliwaomba wakoloni wasiachie kwanza madaraka kwakua waislamu wengi hawakua wamepata elimu na hawana nafasi za juu katika TANU.
Kama historia inasema hivi, na huu uzi umesema vingine. Je hii inamaanisha kulikua na kundi la waislamu lililopigania uhuru na kundi jingine likizuia uhuru usitolewe kwanza?
Nahisi "lecturer" wako alikuwa anakujaza ujinga.
Kama hauufahamu mchango wa Waislam kuhusu kudai Uhuru wa Tanganyika ngoja tumuombe mwanahistoria Allama Mohamed Said aje kutupa darsa kidogo kuhusu hayo.
Allama tunakuomba utusaidie kujibu hili swali.
Kiranga,Rest in Protons Dr. Malima.
Wazee waliokula ice cream za Princeton Junction hao.Nakumbuka kipindi chake Mipango na Uchumi tumekula sana lunch boxes za fish and chips na chicken and chips za Kilimanjaro Hotel.
Mohamed Said
Umemsoma Francis Fukuyama katika kitabu chake kipya "Identity: The Demand For Dignity And The Politics of Resentment" ?
Nimekisoma kimenikumbusha wewe sana.
Identity
The New York Times bestselling author of The Origins of Political Order offers a provocative examination of modern identity politics: its origins, its effects, and what it means for domestic and international affairs of stateIn 2014, Francis Fukuyama wrote that American institutions were in...books.google.ca
Ni kweli nimekusudia AMNUT. Nilisema "chama chao" kwakua hiki kiliundwa kutetea maslahi ya Waislamu.Castr,
Naomba nami nikuulize swali na nakutaka radhi sana kwa kuwa wajibu wangu
ni mimi kukujibu si kukuulza swali.
Nipe kwa mukhasari hicho, ''chama chao ni kipi?''
Ikiwa unakusudia AMNUT hicho hakikuwa ''chama chao.''
Chama cha Waislam kilikuwa TANU.
Ningependa kujua kama mwalimu alifundisha historia hii.
Weka rejea wacha porojo za kisimani.Mama yangu hata kama ulipotokea kuna moto ukifika kwenye kisima hauna sababu ya kuhisi bado upo kwenye moto.
Maneno matupu nisingeyapokea. Maneno yenye rejea zake ni nitayapokea. Nilichoandika hapo hata yeye hakukitoa hewani alitoa kwenye vitabu.
Na swali langu halijasema waislamu hawana mchango. Soma vizuri tena.
Niliyemuuliza amejua hajataka rejea. Kwakua haujui kaa tulia ujifunzeWeka rejea wacha porojo za kisimani.
NdioNasikia ndio muasisi wa kuweka mfumo wa namba badala ya majina katika mitihani, majina yalikuwa yanakuja kujulikana baada ya matokeo kuwa tayari na kutolewa public.
Castr,Ni kweli nimekusudia AMNUT. Nilisema "chama chao" kwakua hiki kiliundwa kutetea maslahi ya Waislamu.
Kwa kadri ninavyojua TANU ilikua inaundwa na wote, waislamu kwa wakristo. Na hakikujisema kama kinatetea maslahi ya watu fulani pekee.
Ila hata kama TANU nayo ilikua ni ya waislamu watupu bado swali langu lina maana.
Nimesoma historia rasmi. Kuna majina umeyataja na kusema ukweli ndiyo nayasikia hapa.Castr,
AMNUT waasisi wake walitoka TANU ukitoa Ramadhani Mashado Plantan hao wengine kama Hamisi Hunde na Abdulkarim Abdulwahid walikuwa watu wasio na nguvu yoyote katika ulingo wa siasa.
Kwa kiwango chochote hawa hawawezi kuwa ndiyo wawakilishi wa Waislam wa Tanganyika walipenda TANU.
Bahati mbaya Sheikh Hassan bin Ameir amefutwa katika historia rasmi kama alivyofutwa Abdul Sykes na miamba mingine katika historia ya uhuru.
Hawa kwa kuwataja wachache ndiyo walikuwa viongozi ambao laiti wangesimama kumpinnga Nyerere athari yake ingeonekana.
Ningependa kufahamu ulisoma historia ipi ni hii ya kweli au ile historia rasmi?
Wacha porojo, sema huna tu rejea.Niliyemuuliza amejua hajataka rejea. Kwakua haujui kaa tulia ujifunze
Castr,Nimesoma historia rasmi. Kuna majina umeyataja na kusema ukweli ndiyo nayasikia hapa.
Ndiyo kusema AMNUT lengo lao haswa lilikua ni uhuru usitolewe kwa TANU kwakua hiyo ingepelekea TANU kujiimarisha? Na hii inamaanisha kua sababu zilizotajwa, za kuzuia uhuru kisa waislamu kukosa nafasi za juu TANU, ni sababu za kupikwa?
Kumbe ni lengo lako na ulikuwa unazuwa tu kuwa ni "lengo lao"! Maana umekiri hata majina mengine hujapata kuyasikia. Hayo majina ni yepi ulioanza kuyasikia "hapa tu"?Nimesoma historia rasmi. Kuna majina umeyataja na kusema ukweli ndiyo nayasikia hapa.
Ndiyo kusema AMNUT lengo lao haswa lilikua ni uhuru usitolewe kwa TANU kwakua hiyo ingepelekea TANU kujiimarisha? Na hii inamaanisha kua sababu zilizotajwa, za kuzuia uhuru kisa waislamu kukosa nafasi za juu TANU, ni sababu za kupikwa?
Sijakutana na mtu anapenda ugomvi kama wewe.Kumbe ni lengo lako na ulikuwa unazuwa tu kuwa ni "lengo lao"! Maana umekiri hata majina mengine hujapata kuyasikia. Hayo majina ni yepi ulioanza kuyasikia "hapa tu"?
Naona juu hapo umeanza kupata darsa na linaanza kukuingia tartiibu.
Hayo majina ambayo hujawahi kuyasikia awali sasa umeyasikia na elewa kuwa hao ni wazee wetu.
Allama Mohamed Said mwaga darsa kaka yangu, aliyesema hatujui kitu tutulie kumbe hata majina ndiyo kaanza kuyasoma "hapa".