Kumekucha, hatimaye lango la mwisho limefunguliwa rasmi

Kumekucha, hatimaye lango la mwisho limefunguliwa rasmi

Natumaini wote ni wazima wadau wa huku.

Lengo la kuleta uzi huu kwenu ni kutoa taarifa ya furaha na kuwaamsha usingizini kuwa ule msimu wa mwisho wa dunia tayari umeshafunguliwa na lango lake lipo wazi. Tuanze, miaka 2000 iliyopita waliokuwepo walishuhudia lango la pili kutoka mwisho likifunguliwa. Lango lililokuwa likubwa sana lilipelekea mifumo yote ya dunia kubadilika kabisa ikiwemo kuporomoka kwa mataifa yenye nguvu, kuzalishwa kwa zana mpya za kilimo, kivita na hatimaye baadhi ya mataifa yasiyo tarajiwa kupata nguvu.

Lengo langu si kuelezea lango hilo lililopita maana mambo yatakuwa mengi sana. Mimi nataka ufahamu kuwa unaposoma uzi huu shukuru Mungu wako kwanza kwa kupata neema kubwa namna hii ya kushuhudia hili lango la mwisho kufunguliwa na hatimaye upo msimu mpya. Pia, kama ulikuwa na mpango wa kujiua nakuomba acha kwanza na kama unawasiwasi kuwa miaka yako ya kuishi hapa duniani inakaribia kuisha omba Mungu wako akuongezee japo miaka michache ili uone na kushuhudia yafuatayo;

Moja, nakutaarifu kuwa nchi zote tajiri na matajiri mmoja mmoja dunia nzima wametikiswa sana na bado wanatikiswa na lengo ni kuibuka kwa nchi mpya na watu wapya watakaokuwa matajiri katika msimu huu mpya. Hao watu na hizo nchi ni mimi na wewe na nchi yetu ya Tanzania kama tutapata watu wenye akili za kutambua majira na nyakati lazima tuwe "superpower".

Pili, katika msimu huu wa mwisho wa dunia tutashuhudia vita sana, njaa sana, ukame, ukosefu wa viongozi wenye maono, malalamiko sana, watu wengi kukata tamaa, nyumba za ibada zitajaa watu, nyumba za waganga wa kienyeji zitajaa watu na vyuo na mashuleni kujaa wanafunzi. Kwanini iwe hivi!? Ni kwa sababu huu ni msimu wa mwisho na hivyo mifumo yote ya mfumo wa zamani inaachwa kwa kushindwa kutatua matatizo ya huu msimu mpya wa dunia.

Yaani wote duniani tumerudishwa kituo "A" (mwanzo) ili tuanze wote safari ya huu msimu mpya, ndiyo hivyo kama ulikuwa hujui changamka sasa na nchi nayo ichangamke. Ukitaka kufeli na kuachwa katika msimu huu jaribu kutumia mbinu za zamani, hizo hazipo tena na ukitaka kufaulu kirahisi tumia mbinu mpya za huu msimu.

Ukitaka kuelewa vizuri tafuta habari ya Nuhu na ngarika usome. Kwa ufupi ni kuwa dunia nzima iliangamizwa kwa maji na akabakia Nuhu,mkewe na watoto wao watatu na wake za watoto wao tu. Baada ya maji kukauka Nuhu alitoka ndani ya safina na huku watu wake wote wakiwa wanamtegemea na kumsikiliza yeye. Sasa ndiyo tupo hapo leo (ndiyo kama tumetoka ndani ya safina wote) na watu wote wanakutegemea wewe!,pambana sasa uwasaidie maana lango lipo wazi.

Mwisho, tunapata hizo changamoto tu hapa mwanzoni wa lango ili kutulazimisha kutumia akili zetu vizuri na baada ya muda tutaishi maisha mazuri sana kwa faida ya watakaoweza kutumia akili zao vizuri za nyakati na majira. (Wao na nchi zao zitakuwa mabilionea wapya)
Nimekuelewa sana maono yako ndo maono yangu. China ndo inaenda kuwa nchi yenye nguvu
 
Nimekuelewa sana maono yako ndo maono yangu. China ndo inaenda kuwa nchi yenye nguvu
Ongezea hapo!

Na wachina watakuja wengi Africa HASA Bongo tutawazalisha na kupata wabongo wa kichina wenye akili sana na ndio kizazi bora hicho kitaleta maziwa na asali hapa NCHINI!

Nimeshaanza kujifunza kichina ili nijue kutongoza kichina China!

Mkuu changamkia FURSA Hiyo!!
 
Siamini kama wanyonge watanzania watakua matajiri na hao wanaoitwa mapapa wawe ombaomba!!!

Serikali za ulaya eti zije kuomba msaada wa kibajeti kwa hizi nchi ombaomba zilizojaza walarushwa,wafujaji mali za umma,wezi,wanyanganyi nk ndani ya miaka mitano ijayo?

Tutafakari kwa kina zaidi
 
Unabii ni unabii tu, ni kosa kuupinga wala kuukataa.hata kama ni utabiri.
Ni kweli,chakufanya ni mtu kwenda kwa Mungu wake yeyote anayemwabudu na kumuuliza tupo msimu gani?(kuthibitisha),kama anauwezo wa kusikia sauti ya Mungu wake awe na uhakika jibu litakuwa ni ndiyo.Hakijibiwa hapana arudi hapa.
 
Kwahiyo Mama la Mama, Mama SaSHa anatupeleka katika nchi ya ahadi?

Au umemuona nani mwingine?
Sukuma gang wametoboa?
Anapaswa kujua kuwa amepata bahati ya kipekee kwa lango la msimu mpya kufunguliwa akiwa ameshika hatamu (mwenzake aliishia langoni kwa sababu maalumu). Akitumia akili vizuri na kupata watu makini wenye akili za kujua majira na nyakati hizi zinahitaji nini Tanzania tunaenda kung"aa duniani.( watu hao wapo wengi sana sema si rahisi kuwajua kutokana na kufichwa na mfumo kwani kila nchi ipo makini kupambana na hali yake).
 
Siyo huyo!

Inasemekana huyu atamalizia nyakati hizi chungu za zamani halafu YUPO mwenye maono kesha andaliwa NDANI ya chama atasimama Hapo mbeleni!YUPO top ten ya NEC pale!
Asante kwa nyongeza yako,kama watu wa ndani ndani wameshatambua nyakati hizi na kuanza kuandaa watu wakuendana nazo ni jambo zuri sana hili.
 
Siamini kama wanyonge watanzania watakua matajiri na hao wanaoitwa mapapa wawe ombaomba!!!

Serikali za ulaya eti zije kuomba msaada wa kibajeti kwa hizi nchi ombaomba zilizojaza walarushwa,wafujaji mali za umma,wezi,wanyanganyi nk ndani ya miaka mitano ijayo?

Tutafakari kwa kina zaidi
Inawezekana sana tu,inategemea na namna nchi zilivyojipanga na si lazima waje kuomba msaada wa kifedha huku,hata sisi kama nchi kujitegemea tu na kuishi maisha ya hali nzuri na watoto wetu itatutosha sana. Cha msingi nafasi hii ya dhahabu tusiichezee.
 
Nyongeza;Hili ndilo lango la msimu wa mwisho wa watu wema na waovu kuchanganyika,linalofuata soon litawatenga watu wema na waovu na hapo fujo yake itakuwa ya kutisha sana!.(naomba tuliache kwanza hilo tulipambanie hili).
 
Anapaswa kujua kuwa amepata bahati ya kipekee kwa lango la msimu mpya kufunguliwa akiwa ameshika hatamu (mwenzake aliishia langoni kwa sababu maalumu). Akitumia akili vizuri na kupata watu makini wenye akili za kujua majira na nyakati hizi zinahitaji nini Tanzania tunaenda kung"aa duniani.( watu hao wapo wengi sana sema si rahisi kuwajua kutokana na kufichwa na mfumo kwani kila nchi ipo makini kupambana na hali yake).
Sawa kiongozi
Ila hujatoa hatma ya sukuma gang
 
Back
Top Bottom