Kumlinda sana mtoto (overprotective) ni kumlemaza na kumjengea mazingira magumu kwenye maisha yake ya kujitegemea

Kumlinda sana mtoto (overprotective) ni kumlemaza na kumjengea mazingira magumu kwenye maisha yake ya kujitegemea

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
Njia nzuri ya kumlinda mtoto ni kumkomaza ajue kukabiliana na maisha pale atapoanza kujitegemea ama ukitoweka kwa kifo na ulinzi wako kwake ukawa haupo tena.

Sina maana ya kusema mtoto umlee maisha magumu tu, NO! Njia sahihi ni kumlea kivugu vugu, raha azijue na shida nazo ajue namna ya kukabiliana nazo (sio kuzijua tu bila kujua namna ya kuzitatua)

aina hii ya wazazi over protective huwa wana nia ya kuwalinda Watoto wao lakini aina hii ya malezi haiwafai watoto wao katika uhalisia wa dunia hii hasa ukizingatia watoto nao wakiwa wakubwa watajitegemea,

Wazazi wa aina hii mara nyingi humuanda mtoto aje kuwa aina mtu wasiemtaka ama kuja kuwa katika hali wasiyoitaka.

Mzazi hataki mtoto wake apitie shida alizopitia, anaanza kumpa pesa na kila anachohitaji, mtoto hajui hata hio fedha na vitu namna gani vinavyopatikana, yeye anajua kupewa tu, mzazi akitoweka ama mtoto akianza Maisha ya kujitegemea bila back up anaweza kurudi kuishi maisha ya chini maana hajui fedha alizopewa jinsi zinavyotafutwa kwa jasho.

Mzazi hataki mtoto awe mchafu, house girl anamfulia nguo na kumfanyia kila shughuli ya usafi mtoto, matokeo yake mtoto hawezi kujifanyia usafi, akianza maisha ya kujitegemea bila house girl anakuwa mchafu.


Mzazi anamfungia ndani mtoto wake geti kali, yani ile mtoto kuleta rafiki zake wacheze nae kwake hataki, mtoto kwenda kucheza kwa jirani nyumba ya pili ama tatu chini ya uangalizi hataki, mtoto anakosa kujifunza mbinu za kuishi na jamii independently na matokeo yake anaweza kuwa mtu wa kupenda kuishi kivyake akaona ni kawaida, mtoto anaweza kuonewa kirahisi sana akiwa kivyake bila mzazi, n.k.

Bruce Lee aliwahi kusema "usiombee kuja kuishi maisha mepesi, Omba upewe uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha".


Hatujui kesho yetu tunaweza kuanguka na ikawa hatari kwa watoto wetu, Tujaribu angalau kuwalea watoto wetu kulingana na maisha ya kiuhalisia watayokutana nayo pindi tukiwa hatupo ama nao wakianza maisha yao ya kujitegemea.
 
Ni kuwafanya kuja kuwa wazembe wazembe sana baadae.
Kuwaweka watoto geti kali sana si afya. waache wajichanganye huko nje wacheze cha ndimu, sarakasi etc. muhimu kila jambo kwa kiasi akizurura nje kuanzia saa 11 then saa moja usiku akarudi ndani inatosha.
 
Ni kuwafanya kuja kuwa wazembe wazembe sana baadae.
Kuwaweka watoto geti kali sana si afya. waache wajichanganye huko nje wacheze cha ndimu, sarakasi etc. muhimu kila jambo kwa kiasi akizurura nje kuanzia saa 11 then saa moja usiku akarudi ndani inatosha.
Ni kweli, tahadhari nayo iwepo kujua mtoto yupo wapi na kumuwekea mipaka asiende mbali sana,, shida inakuja mzazi akiona tu habari kuna mtoto kafanyiwa ubaya anakuwa very over protective kwa mtoto wake anampigia kufuli ,,, mtoto anashinda ndani kucheki katuni ambazo hazina uhalisia kwenye ulimwengu wa kweli.

Tukumbuke kwamba hata ndani kinaweza kutokea kitu kibaya.
 
Familia nyingi haswa za kitajiri na kipato cha kati wana tabia hizi unakuta mtoto yupo chuo hawez hata kusonga ugali au kuchangamana na wenzake.
 
Familia nyingi haswa za kitajiri na kipato cha kati wana tabia hizi unakuta mtoto yupo chuo hawez hata kusonga ugali au kuchangamana na wenzake.
Mzazi akifariki, kufukuzwa kazi, kwenda jel, kufilisika, n.k. watoto inabidi waanze kujifunza from scratch
 
Okay sawa kesho ntaawacha wakacheze na rama kamongo
Hizi ni kauli za mzazi overprotective, jambo dogo inalikuzaa mpaka basi ili upate justification ya kumbana mtoto kwa kivuli cha ulinzi.

Kama mzazi inabidi ujue kumwekea mipaka mtoto wako huku huathiri uhuru wake.

Unaweza kumruhusu acheze na watoto wa majirani hata nyumbani kwako ama kwa jirani ama sehemu za karibu ambazo ni salama huku ukimuwekea utaratibu wa kuaga na kukwambia yupo wapi.

Simple like that, wala hakuna haja ya ku complicate...
 
Utafiti nchini Marekani unaonyesha kuwa watoto wanaolelewa katika mazingira masafi sana wamakosa natural immunity against certain diseases.
 
Back
Top Bottom