Kumnyima upadre anayestahili kunaleta maumivu makubwa sana. Ya Prof Maghway ni ushuhuda

Kumnyima upadre anayestahili kunaleta maumivu makubwa sana. Ya Prof Maghway ni ushuhuda

Mungu aliwakabidhi binadamu jukumu la kuchagua binadamu wa kufanya kazi ya Mungu. Changamoto inakuja pale wale binadamu waliopewa jukumu hilo wanapotumia ubinadamu wao kuwapata watumishi wa Mungu.
Mungu atamsaidia huyo mtu kuepuka vichawishi na vikwazo katika njia iliyowekwa na binadamu.

Kama hajaweza this means that Mungu amemuongoza katika njia nyingine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaah! Makosa ya dingi nahukumiwa mtoto!!! Si sawa kabisa
Yaani ilikuwa hivyo, aliukosa jamani, watu wakamshauri yule Mzee aligoma kabisa, zamani kijana anayezaliwa nje ya ndoa ilikuwa ngumu sana kwenda seminary, lazima atoke familia yenye maadili kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
si kweli, wanaoamua ni wanadamu na mara nyingine wanakosea sana
RC wanajua siri nyingi uongozi wao upo mpaka chini kabisa hivyo waumini wanawafahamu vizuri sana, hata wewe unaweza kuwa na jirani yako usimfahàmu mambo yake lakini Padri wako/ wake anayafahamu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RC wanajua siri nyingi uongozi wao upo mpaka chini kabisa hivyo waumini wanawafahamu vizuri sana, hata wewe unaweza kuwa na jirani yako usimfahàmu mambo yake lakini Padri wako/ wake anayafahamu

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanajua siri zipi? Mbona kuna mtu alikuwa anafahamika na wenzie huko seminarini kuwa ni shoga lakini kapewa upadri? Waseminari wenzie walimjua lakini hakuna aliyethubutu kumsema kwa sababu pale utakapotakiwa kutoa ushahidi inaweza kuwa mwisho wako, ukafukuzwa wewe akabaki huyo unayemtuhumu. Au hata akifukuzwa, inabakia historia pale kuwa wewe ndiwe uliyemfukuzisha, wenzio wanakuchukia na kukuundia zengwe la kufa mtu, hautaishi kwa amani. Matokeo yake waseminari wenyewe ni mabingwa wa kufichiana dhambi.
Chanzo cha bifu kati ya padre Privatus Karugendo (ameshaachishwa) na aliyekuwa askofu wake Severini Niwemugizi ni dhambi walizokuwa wanafichiana walipokuwa seminari Segerea, na huyu Karugendo alipoasi akaamua kuzimwaga hadharani. Kwa hekima yake, askofu aliamua kutokumjibu, kwahiyo kashfa akabaki nazo Karugendo hadi leo.
Kwa ujumla jambo likishategemea akili za binadamu pekee haliwezi kuwa na ukamilifu mbele za Mungu.
 
Hata IGP wa sasa Simon Sirro aliachishwa upadri akiwa anakaribia sana kuupata, na kama mnavyomwona ni mtu timamu sana na mweledi, na ana familia. Hizo hadithi nyingine wanazolishana watu ni uzushi tu.
Alifikia levo ipi ?unaposema kukaribia ndio kupi huko?
 
Wanajua siri zipi? Mbona kuna mtu alikuwa anafahamika na wenzie huko seminarini kuwa ni shoga lakini kapewa upadri? Waseminari wenzie walimjua lakini hakuna aliyethubutu kumsema kwa sababu pale utakapotakiwa kutoa ushahidi inaweza kuwa mwisho wako, ukafukuzwa wewe akabaki huyo unayemtuhumu. Au hata akifukuzwa, inabakia historia pale kuwa wewe ndiwe uliyemfukuzisha, wenzio wanakuchukia na kukuundia zengwe la kufa mtu, hautaishi kwa amani. Matokeo yake waseminari wenyewe ni mabingwa wa kufichiana dhambi.
Chanzo cha bifu kati ya padre Privatus Karugendo (ameshaachishwa) na aliyekuwa askofu wake Severini Niwemugizi ni dhambi walizokuwa wanafichiana walipokuwa seminari Segerea, na huyu Karugendo alipoasi akaamua kuzimwaga hadharani. Kwa hekima yake, askofu aliamua kutokumjibu, kwahiyo kashfa akabaki nazo Karugendo hadi leo.
Kwa ujumla jambo likishategemea akili za binadamu pekee haliwezi kuwa na ukamilifu mbele za Mungu.
Acha uongo karugendo hakusoma segerea kasoma kipalapala tabora.. stori ya kuunga
 
Hii hapa mojawapo ya propaganda za padre Karugendo dhidi ya askofu wake baada ya urafiki wao kugeuka uadui: Wakati wa Kubadili fikra ni huu: Askofu akumbushwa Mwanae

Mwenye kumwandikia baruapepe hii Askofu Severini ameniambia niiweke kwenye blogu ili watu wengine wasome kwamba "Baba Askofu" ana mtoto huko Arusha.

Date:
Wed, 15 Feb 2006 02:00:45 -0800 (PST)
From:
"Antiparth Martin"
Subject:
Mkunde!
To:
niwemugizi@iwayafrica.com
CC:
nunzio@cats-net.com, nyumba@cats-net.com, tec@cats-net.com
HTML Attachment [ Download File Save to Yahoo! Briefcase ]

Mtumishi wa Mungu, Askofu Severine Niwemugizi, Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge na Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.
Tumsifu Yesu Kristu.

Mtumishi wa Mungu,
Pole sana kwa kazi nyingi ya kuchunga kondoo. Bwana akubariki na kukuzidishia moyo mkuu. Ninakuandikia ujumbe huu kukumbusha jambo moja:

Unakumbuka siku chache kabla ya kuchaguliwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge, ulizaa mtoto na Consolata Kyala, dada yake na Padri..... wa Jimbo Kuu la Dar-es-salaam. Padri huyo alikutunzia siri, na sisi tukanyamaza! Mtoto wako Mkunde, anaendelea kukua na sasa anasoma shule Maji ya Chai Arusha.

Ili Consolata Kyala, akae kimya, ulimjengea nyumba kule Maji ya Chai Arusha. Sasa hivi anaishi kwenye nyumba hiyo na mme wake Antiparth Martin. Hapo hapo anaendesha biashara ya Bar ijulikanayo kwa jina la Holiday Inn.

Tumesikia tetesi kwamba hivi karibuni utateuliewa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Tabora. Tunafikiri ni jambo la muhimu na la lazima, viongozi wa Kanisa kufahamu kwamba wewe una mtoto. Ofisi ya Askofu Mkuu ni kubwa na yenye kudai maadili ya Kanisa Katoliki.

Viongozi wa kanisa wanaweza kupuuzia jambo hili. Nawe pia unaweza kupuuzia jambo hili. Kwa vile siku hizi sayansi imepiga hatua, tutasisitiza ipimwe DNA yako na ya mtoto Mkunde. Tunataka watanzania wajue ukweli huu na ulimwengu ujue ukweli huu.

Ni matumwaini yetu kwamba utaupokea ujumbe huu na kuwajibika ipasavyo.
Tunakutakia moyo mkuu.

Kwa niaba ya waumini wenye upendo na kanisa katoliki wa Maji Chai-Arusha.
Ni, wako katika Upendo wa Kristu.
Antiparth Martin.
 
PROFESA mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Josephat Maghway (65) jana aliamua kufunga nadhiri za daima za maisha ya utawa katika Kanisa Katoliki la Salvatorian la Chuo Kikuu cha Jordan mkoani Morogoro.

Taarifa ambazo gazeti hili lilizipata jana kupitia marafiki wa karibu wa Profesa huyo, zilieleza kuwa, kabla ya kuingia utawa na kufunga nadhiri hizo, aligawa vitu vyote ikiwamo nyumba, magari na mashamba kwa taasisi za dini.

“Leo (jana) ndio amefunga nadhiri za daima za maisha ya utawa ambapo amekula kiapo cha kuishi maisha ya kujitolea kwa ajili ya watu maskini kwa kuuza kila alicho nacho na kuwagawia maskini na yeye kuamua kuishi maisha ya nadhiri ya ufukara, utii, na usafi wa moyo,” alisema Faraja Chrysostom ambaye ni rafiki wa karibu.

Alisema ingawa Profesa Maghway anapenda kuishi kitawa lakini shirika lake likitaka linaweza kumpatia upadri.

Akielezea tukio hilo la kuweka nadhiri, alisema Profesa huyo aliungana na watawa wengine wanne wa shirika la Mtakatifu Francis wa Assizi wa Kapuchini walioko Kola, Morogoro kufanya agano hilo.

Profesa Maghway alistaafu kufanya kazi UDSM akiwa na miaka 60 mwaka 2010 na inaelezwa hakuwahi kuoa wala hana watoto.

Profesa Maghway alipongezwa na watu mbalimbali wakiwamo marafiki zake ambao waliandika katika mtandao wa Whatsapp.

Miongoni mwa waliompongeza ni Dk. Vincensia Shule wa kitengo cha Sanaa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye aliandika katika kundi moja la mtandao wa Whatsapp kuwa;

“Kwa namna ya kipekee kabisa napenda kumpongeza Prof. Josephat Baran Maghway kwa kuweka nadhiri ya kudumu ya Utawa…amefanya mengi kwenye taaluma akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Department of Foreign Languages & Linguistics (kitengo cha lugha) sasa ameamua kuendelea kumtumikia Mungu kwa next level (hatua nyingine mbele), Inshallah atakamilisha safari ya upadre”.

HABARI NI YA MWAKA 2017 LAKINI NIMEIONA LEO MTANDAONI.
NIMEIWEKA HAPA KWA SABABU NAMFAHAMU PROF MAGHWAY BINAFSI, ALIKUWA MWALIMU WANGU MLIMANI.
ALINYIMWA UPADRI AKIWA KIJANA, BAADA YA KUSOMA SEMINARINI HADI HATUA YA USHEMASI AKIMALIZA PHILOSOPHY NA THEOLOGY KAMA IPASAVYO. LAKINI KWAKUWA HUO HASA NDIO ULIKUWA WITO WAKE, ALIUISHI HADI UZEENI JAPO ALINYIMWA UPADRE!
MUNGU AZIDI KUMTIA NGUVU.

MAASKOFU NA WENGINE MNAOHUSIKA MUWE MAKINI SANA NA OMBENI UONGOZI WA MUNGU KATIKA TAFAKARI ZENU MNAPOLETEWA MAPINGAMIZI YA KUNYIMA SHEMASI UPADRI, MUNGU AWAONGOZE KATIKA KUTAMBUA WENYE WITO HALISI NA KUWALINDA NA KUWAJENGA.
Hongera kwake.
 
Back
Top Bottom