Kumshambulia Hayati Magufuli kunaweza ligawa Taifa na kupunguza nguvu ya CCM kanda ya Ziwa

Kumshambulia Hayati Magufuli kunaweza ligawa Taifa na kupunguza nguvu ya CCM kanda ya Ziwa

Manelezu

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2015
Posts
1,908
Reaction score
2,774
Nianze moja kwa moja kutoa maoni yangu kwa hali ya kisiasa nayoiona. Kifo cha Rais Magufuli kimeacha pengo kubwa sana kwenye taifa. Kwa wale wasiopenda kusikia jina la magufuli niseme tu, Hayati alikuwa na wafuasi wengi kifo chake kimedhihirisha hivyo na atakumbukwa siku zote kwa mambo mazuri aliyolifanyia taifa hili.

Niseme tu wazi si kila jambo alilolifanya hayati ni baya kwenye taifa hili. Ameacha alama kubwa sana. Licha ya kuwa na matatizo ya moyo alijitolea usiku na mchana kulipigania taifa lake.

Najua akili ni nywere na kila mtu ana zake. Watu wanaodai magufuli alikuwa fisadi unashindwa kuelewa jinsi walivyo na kumbukumbu ndogo ya aina ya ufisadi tuliyopitia kwenye taifa hili kabla ya magufuli kuingia madarakani. Kumbukeni ufisadi wa TEGETA ESCROW, EPA, BOMBA LA GAS MTWARA. Sote tunajua viongozi wa Afrika wakiiba pesa wanapeleka wapi. Wanakimbiza nchi za magharibi..kama Hayati aliiba hayo mabillioni yako wapi? Matrillion yako wapi?

Ameanzisha ujenzi wa reli kwa gharama ndogo sana uki compare na majirani zetu tena ya kutumia umeme.

Magufuli anatoka kanda yenye nguvu kiasiasa. Ukweli ni kwamba magufuli ameumiza sana watu wa kanda hiyo na taifa kwa jumla. Kitendo cha kuendelea kumshambulia kwa tuhuma ambazo watu wenye akili za kawaida kabisa wanajua zina malengo ya kisiasa nikutengeneza mgawanyiko mkubwa huko mbeleni.

Kuna kitu magufuli kaacha kwenye mioyo ya watanzania, nacho ni uzalendo. Wamejua kuhusu ukoloni mamboleo na jinsi baadhi ya viongozi wanavyotumika na nchi za magharibi kuhujumu mataifa yao either kwa ufisadi, mikataba mibovu etc.

Nimalizie kwa kusema, magufuli hakuwa malaika. Binafsi kuna mambo kadhaa niliyapinga kwenye utawala wake lakini niseme tu ni kiongozi mzalendo hili taifa kuwahi kupata.

Kama mnataka tuamini huo ufisadi mtueleze MAGUFULI KAFICHA HELA WAPI? Alizibeba kwenye sandarusi? Ana account ya pesa ulaya? MUNGU ATAMLIPA KIUMBE WAKE. KAKIKA KILA NAFSI ITAONJA MAUTI.

Mwisho kabisa kabla haujaendelea na mkakati ovu wa kumshambulia magufuli labda ujiulize. MAUAJI YA ALBINO YAKO WAPI? UFISADI MKUBWA UKO WAPI? UJAMBAZI UKO WAPI? KUKATIKA UMEME JE? AU TUMESAHAU JINSI MAJENERETA YALIVYOKUWA YANATUUMIZA MASIKIO?

Hakika MUNGU ATAMLIPA JPM kwa kutetea wanyonge na watu wasiokuwa na nguvu. Miaka 100 ijayo utakuwepo? Basi jifunze na beba mema ya hayati JPM mabaya muachie Mungu wake atamuhukumu.

Daudi alimwaga damu lakini Mungu alimkumbuka.
 
Kwani Magufuli alikuwa raisi wa kanda ya Ziwa?
Kagera ni kanda ya Ziwa pia lakini aliwafanyia kitu kisicho cha ubinadamu kipindi cha tetemeko kwa hiyo sioni ni kwa namna gani wakazi wa Kagera wanaweza kumaindi Magufuli akichambuliwa unyama wake
Nashangaa unatusemea watu wa Kagera...mbona sisi hayo hatuyajui?
 
Kwani uraiani nako watu wanamchukia Magufuli kama ilivyo kwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Twitter na Ufipa?

Bado naamini Rais Magufuli alikuwa anaungwa mkono na idadi kubwa ya watu walio wengi.

Na watu hao walituma ujumbe wao kipindi cha msiba wake.
 
Nyie mnaotaka huyo Magufuli aonekane mungu mtu ndio wajinga sana mbona Kikwete alisemwa sana tena akiwa hai na magufuli tena wazi wazi kwa vijembe mbona mlikaa kimya?

Nyie wasukuma tuondoleeni upuuzi wenu huyo mtu wenu kama mnaona ni malaika nendeni kaburini kwake mkamtukuzie huko huko tuondoleeni upumbavu wenu.

Mtu asiye taka kukaguliwa anafunga watu midomo watu wasiseme mapungufu yake sasa watu wameyakusanya maovu sasa wamepata nafasi ya kuyaongea sasa wanayaongea mnalalamika nini sasa.
 
Kanda ya nyonyo wenyewe wanamkataa na hawajawahi kuwa nae isipokuwa wale wapenda mtelezo waliojipendekeza kupata vyeo iweje taifa ligawanyike kwa kushambuliwa kwake?
Wewe ni Kichaa tumchukie Hayati mtu aliyetufumbua macho dhidi ya tabia chafu ya Kanda ya SHASHI mtu ambaye hatoki Kanda yao ni mbaya Magufuli lala salama daima tutakuenzi daima kwa kuelezea mazuri uliyofanya kizazi na kizazi.
 
Kwani uraiani nako watu wanamchukia Magufuli kama ilivyo kwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Twitter na Ufipa?

Bado naamini Rais Magufuli alikuwa anaungwa mkono na idadi kubwa ya watu walio wengi.

Na watu hao walituma ujumbe wao kipindi cha msiba wake.
Walio mpenda magufuli ni wale watanzania wajinga wajinga ambao uelewa wao upo chini sana na ndio maana walikuwa alipo kuwa anatukana watendaji wake wachini, na alipo kuwa anagawa vihela hovyo hovyo ili kutafuta cheep politics walikuwa wanamshangilia sana.

Lakini wenye akili wote wanao kuchuja mambo hawawezi kuungana na utawala wa magufuli pamoja na mambo yake alitumia sana ubabe kuliko maarifa.
 
1.5 tirion ilipotea kipindi cha nani?
Na usituchanganye kabisa , Kikwete aliruhusu watu kujadiri Wizi kwenye Nchi yao, yeye hata Kukopa alikuwa anakopa kwa siri

Uchumi wa Gizani

Yaani maufisadi yoooote ya Kipindi cha Kikwete uliyoyasema , tuliyajua kwasababu Kikwete mwenyewe alitaka tuyajue, angetaka kuficha angeweza na angetoka madarakani bila kuwa na rekodi unazosema,

Kuficha tatizo, haina maana kwamba hakuna tatizo, limefichwa
 
Nianze moja kwa moja kutoa maoni yangu kwa hali ya kisiasa nayoiona. Kifo cha Rais Magufuli imeacha pengo kubwa sana kwenye taifa. Kwa wale wasiopenda kusikia jina la magufuli niseme tu, Hayati alikuwa na wafuasi wengi kifo chake kimedhirisha hivyo na atakumbukwa siku zote kwa mambo mazuri aliyolifanyia taifa hili...
Unaongelea CCM kuna watu wengi hawana vyama. Walikuwa wamenyamaza tu muda wote
 
Walio mpenda magufuli ni wale watanzania wajinga wajinga ambao uelewa wao upo chini sana na ndio maana walikuwa alipo kuwa anatukana watendaji wake wachini, na alipo kuwa anagawa vihela hovyo hovyo ili kutafuta cheep politics walikuwa wanamshangilia sana.

Lakini wenye akili wote wanao kuchuja mambo hawawezi kuungana na utawala wa magufuli pamoja na mambo yake alitumia sana ubabe kuliko maarifa.
Hayo ni maoni yako tu.

Na hao unaowaita Watanzania wajinga na wasio na uelewa nao wanaweza kukuona wewe u mjinga na uliye na uelewa wa chini.

Kujiona una akili haimaanishi kwamba una akili kweli.

Haupo vile ujidhaniavyo.
 
Back
Top Bottom