Kumtegemea Rais kupata majibu ya kila tatizo la nchi ni sawa?

Kumtegemea Rais kupata majibu ya kila tatizo la nchi ni sawa?

Uncalled-for hubris!
Are you sure?FYI iam confident but not over confident.Arrogance?I dont really care!
Back to the point,changia mada na ujibu accordingly,vijembe vipo,unaumizwa sana,i wonder why.Dont bring emotions once again.Hilli si jukwaa lake.
 
Are sure?FYI iam confident but not over confident.Arrogance?I dont really care!
Back to the point,changia mada na ujibu accordingly,vijembe vipo,unaumizwa sana,i wonder why.Dont bring emotions once again.Hilli si jukwaa lake.

We Meku na wewe bana...sasa naumizwa sana na nini au na nani?
 
We Meku na wewe bana...sasa naumizwa sana na nini au na nani?
Unaumizwa watu flani flani wakipigwa vijembe kidogo tu.Ndo jukwaa la siasa hakuna mapenzi humu.Rudi kwenye hoja na unieleze ni kwanini JK hatakiwi kuulizwa issue ya umeme.
 
Jmushi,
My compliments and respect to you as well!


WOS,

First off i do respect you.

However
nadhani una ujuzi zaidi kwenye yale majukwaa mengine.(You know what i am talking about)
Thread yako hii inaonyesha kutokuelewa masuala ya kiutawala na siasa.Soma katiba kidogo utagunduwa ni kwanini the bucks stops with Mkulu/Rais.

Hata hivyo nimesikitika kwa uliyosema na kupitisha hukumu kuwa sielewi siasa au hata Katiba - lol nimecheka hadi machozi yakanitoka!The bolded part ndio imeniacha hoi!Labda ungekuwa more specific Mkuu.

Mada hii haijanikera kwasababu kutokuelewa kwako si kubaya sana,utaweza kueleweshwa tu kwasababu kuna tutakaofanya hivyo.We know you are a smart lady,you just need a little bit of brushin' in this arena.

Is it?? Nitasubiri huo msasa basi ndugu yangu.



Tatizo letu ni kwamba hatuna katiba ya kuwabana.Tunaweza kuweka ultmatum kwamba if you can't fix this problem,then we will fire you right away!Rais ni lazima aulizwe kila kitu,si kazi rahisi kuwa rais wa nchi masikini.Ni dedication,unaweza kufa kwa presha kama kweli umeingia madarakani kwa dhumuni la kuiongoza nchi yetu na kuindoa kwenye umasikini.

Hapo kwenye bold, nadhani ungevuta subira ukanisoma kwenye jibu langu kwa MwanaFalsafa ungeona ndicho i alluded to.

I
menisikitisha wewe kuja na kauli kuwa it is fair enough for the president to say that he is not capable of asking God to provide us with rain.Hii si caliber ya great thinking.Nasikitika kwamba ulianza kuwa defensive na kudai watu wasiweke maneno yasiyo ya lazima.I hope you will be patient and read what you dont like without getting personal.

I believe if you had practiced what you preach basi ungekuwa na subira na wala usingeweza kuwa judgemental. Pls read once more so that you can discover the "mischief" behind the thread!



Narudia tena dada yangu,hii issue si ya vyama vya siasa kama unavyotaka kuiweka.Tafadhali elewa kuwa tatizo si kutokuweza kwa JK kumwuliza Mungu kuhusu mvua(Tafadhali elewa hilo)

R u sure umenisoma na kunielewa au hata umewasoma waliochangia walionielewa?



Wewe unapoamini kuwa rais hatakiwi kuwa na majibu ya kila tatizo,unakuwa kama na wewe una tatizo la kuelewa kuwa issue ya umeme si just "Kila tatizo"

Mkuu, iweje unaniwekea maneno mdomoni? Please exercise your comprehension skills kabla ya ku attack wengine. Usilazimishe uelewa wako kuwa ni universal knowledge/understanding.



Kwa kumalizia,naomba usijali kuhusu baadhi ya maneno niliyoyatumia kama utakuwa hujayapenda
.

Siwezi kujali bali nimekusahihisha pale nilipoona nawe umekosea hivyo nawe take it easy!
 
Unaumizwa watu flani flani wakipigwa vijembe kidogo tu.Ndo jukwaa la siasa hakuna mapenzi humu.Rudi kwenye hoja na unieleze ni kwanini JK hatakiwi kuulizwa issue ya umeme.

Hahahaaaa Meku bana...haya basi naumizwa watu flani flani wakipigwa vijembe.

JK hatakiwi kuulizwa peke yake issue ya umeme kwa sababu there is plenty of blame to go around. Matatizo ya uhaba wa umeme hayajaanza leo. Ni ya muda mrefu sana. Nakumbuka kwenye mwanzoni mwa miaka ya 90 mzee Mwinyi akiwa raisi mgao wa umeme ulikuwepo.

Nakumbuka kwa uzuri kabisa kwa sababu kipindi hicho mimi nilikuwa naishi Chuo Kikuu (la hasha sikuwa mwanafunzi kwa hiyo msianze ku imagine umri wangu lol) na tulikuwa tunapata 'preferential treatment' kwa sababu chuo kikuu kilihesabika kuwa kama moja ya sehemu muhimu ambazo zilistahili kuwa na umeme muda wote na hivyo adha ya mgao hatukuwa tunaipata kama ilivyokuwa kwa wengine. Kwa waliokuwa wakiishi chuo kikuu enzi hizo kama wana kumbukumbu nzuri basi watakubaliana nami kuhusiana na hili.

Sasa kwa mtaji huo utaona kuwa hili tatizo la umeme limekuwa tatizo lililowashinda wengi sana na hivyo haitakuwa haki kumnyooshea kidole mtu mmoja tu na kusema wewe ndiyo sababu ya yote haya yahusianayo na huu umeme wa mgao. Lakini pia naelewa kuwa lawama au pongezi they come and go with the territory kwa hiyo itakuwa vigumu sana kwa Kikwete kama raisi kuepuka kubebeshwa lawama hapa.

Jambo la msingi ni wadau wote (kwa hapa namaanisha wananchi wote) kukuna vichwa vyetu na kuja na ufumbuzi wa tatizo. Tusikilizane na tusibezane. Sote ni wadau kwenye hili. Na kuanza kunyoosheana vidole hakutatatua tatizo. Hebu fikiria mwenyewe, ukianza kunyoosha vidole vya lawama utaanzia wapi na kuishia wapi na mwishowe manufaa yake yatakuwa ni yapi?
 
Hahahaaaa Meku bana...haya basi naumizwa watu flani flani wakipigwa vijembe.

JK hatakiwi kuulizwa peke yake issue ya umeme kwa sababu there is plenty of blame to go around. Matatizo ya uhaba wa umeme hayajaanza leo. Ni ya muda mrefu sana. Nakumbuka kwenye mwanzoni mwa miaka ya 90 mzee Mwinyi akiwa raisi mgao wa umeme ulikuwepo.

Nakumbuka kwa uzuri kabisa kwa sababu kipindi hicho mimi nilikuwa naishi Chuo Kikuu (la hasha sikuwa mwanafunzi kwa hiyo msianze ku imagine umri wangu lol) na tulikuwa tunapata 'preferential treatment' kwa sababu chuo kikuu kilihesabika kuwa kama moja ya sehemu muhimu ambazo zilistahili kuwa na umeme muda wote na hivyo adha ya mgao hatukuwa tunaipata kama ilivyokuwa kwa wengine. Kwa waliokuwa wakiishi chuo kikuu enzi hizo kama wana kumbukumbu nzuri basi watakubaliana nami kuhusiana na hili.

Sasa kwa mtaji huo utaona kuwa hili tatizo la umeme limekuwa tatizo lililowashinda wengi sana na hivyo haitakuwa haki kumnyooshea kidole mtu mmoja tu na kusema wewe ndiyo sababu ya yote haya yahusianayo na huu umeme wa mgao. Lakini pia naelewa kuwa lawama au pongezi they come and go with the territory kwa hiyo itakuwa vigumu sana kwa Kikwete kama raisi kuepuka kubebeshwa lawama hapa.

Jambo la msingi ni wadau wote (kwa hapa namaanisha wananchi wote) kukuna vichwa vyetu na kuja na ufumbuzi wa tatizo. Tusikilizane na tusibezane. Sote ni wadau kwenye hili. Na kuanza kunyoosheana vidole hakutatatua tatizo. Hebu fikiria mwenyewe, ukianza kunyoosha vidole vya lawama utaanzia wapi na kuishia wapi na mwishowe manufaa yake yatakuwa ni yapi?
Msome vyema WOS mkuu na bila cherry picking just because you wanna back her up.Nimekupata hata hivyo inawezekana hujampata..
Haya matatizo hayana uhusiano wowote na vyama vya upinzani.CCM walikuwa na bado wana majority ya kufanya maamuzi ya muhimu kama kweli wako serious in solving this problem.Again,nilisema brush,nashukuru uko hapa kusaidia kwenye hilo.Kuna mchanganyiko usiomake sense hapa kwenye hoja yake ya awali.Ana imply kwamba rais anaoewa kwa maoni yake kuwa yeye si Mungu mwenye kuweza kuleta mvua.Hilo sikubali.

Kusema liliwashinda wengi haina mantiki.Sera za CCM ni zile zile.Hivyo halijawashinda wengi,labda useme limewashinda CCM..Nyani u know better than that mzee.

Na hivyo Nakubaliana na wewe kuwa ni lazima abebeshwe mzigo.Na ni lazima awe responsible.Kuja humu na kudai eti Rais asiulizwe kila swali ni uhuni wa kimawazo na upotofu wa kifikra nyakati hizi nyeti.People who are out of touch will bear such mindsets.Kuna wananchi wenye shida.Haiitaji kuwa na shida kuliona hilo.Wako wenye kuishi vizuri tu lakini wenye empathy na kuyaelewa matatizo ya wananchi wenye shida vyema.Hilo haliitaji miwani.

Na mkuu wangu narudia tena,huyu dada amefanya makosa makubwa sana kusema umeme ni just another tatizo.Hili ni tatizo la kimsingi na kuulizwa Mh Rais ni lazima aulizwe.Akikubali hilo tutakuwa msitari mmoja.However unaonekana umemesema zaidi na kama vile you have put words in her mouth.Sijali hilo kwa kuwa nilimweleza hapo awali kuwa atapata msaada.
Tuendelee na mjadala.
 
Msome vyema WOS mkuu na bila cherry picking just because you wanna back her up.Nimekupata hata hivyo inawezekana hujampata..

Nakuhakikishia Mkuu NN kanipata bila chenga kabisa! Msome pia Mwanafalsafa1. Wewe ndio umemiss my point by far nahani umesoma ukiwa biased kuhusu uelewa wangu.Hint: read pia between the lines utanielewa vizuri.


Na mkuu wangu narudia tena,huyu dada amefanya makosa makubwa sana kusema umeme ni just another tatizo.Hili ni tatizo la kimsingi na kuulizwa Mh Rais ni lazima aulizwe.Akikubali hilo tutakuwa msitari mmoja
.
Nakuhakikishia tena kwa mara nyingine sijakosea.Lakini kisomi wanasema " everybody is enttled to their opinion" kwa msingi huo u could be right kuona nimekosea.


However unaonekana umemesema zaidi na kama vile you have put words in her mouth.Sijali hilo kwa kuwa nilimweleza hapo awali kuwa atapata msaada.

He has not, and i dont want to believe that he has put words in my mouth.

Tuendelee na mjadala.

Na kukutoa wasiwasi kuhusu uelewa wangu nakuomba soma post yangu namba 9 utanielewa.

Thanks!
 
Jmushi,
My compliments and respect to you as well!




Siwezi kujali bali nimekusahihisha pale nilipoona nawe umekosea hivyo nawe take it easy!
Sis WOS,
Ukitaka niijibu thread yako msitari kwa msitari ninaweza kufanya hivyo.However nafahamu kuwa wewe ni mwelewa na kama hujaelewa najuwa utafanya hivyo, its just a matter of time.

Kama heading yako inasema rais asitegemewe kupata majibu ya kila tatizo umekosea dada.Kwasababu baada ya kuingia ndani na kusoma contents,nimesoma kuwa "Kila tatizo" ni pamoja na la umeme.Nikasema kuwa suala la umeme si just "Kila tatizo" Ni issue ambayo ilitakiwa ifungiwe mkanda.Yani hata kama kila wizara ikapunguziwa pesa kwenye bajeti ama hata matumizi yakapunguzwa ili kuwekeza kwenye nishati ya umeme toshelezi.

Bila umeme nchi ambayo inategemea wawekezaji na ambayo ni lazima izalishe ie viwanda ili kupata maendeleo,hilo litakuwa ndoto ya mchana kweupe.Na kusema kuwa tatizo hilo viongozi wengi wamelikuta huku ukiwachanganya na wale wa upinzani ni even kosa kubwa zaidi.Ni kosa kubwa kwasababu CCM walikuwa na bado wana majority ya kutosha bungeni kufanya maamuzi ya msingi kusolve hii issue.Unakumbuka maamuzi ya DOWANS etc.

Nilipokwambia kuhusu katiba,nilimaanisha kuwa kama ni kweli rais hataki aulizwe kila swali,basi angesimamia mabadiliko ya katiba ili uwajibishwaji uwepo.Hivi sasa katiba tuliyonayo,mwananchi mimi ninayeelewa katiba na kufahamu kuwa ana nguvu kubwa kupita kiasi,basi nitamwajibisha yeye kwa kuwa nimeosioma katiba hiyo na nimegundua kuwa ana nguvu kubwa kiasi cha kwamba kila swali ama tatizo ni lazima aulizwe.

However hata kama hutaki aulizwe,nimekupa mfano wa US ambapo rais anaulizwa almost everything.Some you might even think its silly!Ni wajibu wake kushirikiana na wasaidizi wake kupata data za kutosha kumwezesha kuyajibu hayo.Kazi ya kuongoza taifa masikini kamTZ ni ngumu sana,narudia hilo.

Uongozi wa Taifa letu si ufalme.Na kwahiyo he must be aware of that,kwamba akili yake inatakiwa ichemke all the time.Ama unataka aendelee kusafiri tu?

Tuendelee na mjadala,nashukuru pia you didnt take it personal.Because doing so is taking it out of context.
 
Na kukutoa wasiwasi kuhusu uelewa wangu nakuomba soma post yangu namba 9 utanielewa.

Thanks!
Nimekusoma na nimekupata vyema sana tu kuwa you are partially wrong.Ngoja nisubiri wachangiaji wengine.I am standing by my points tho, kwamba you are wrong kutaka ku conclude kuwa kulitakiwa kuwepo ushirikiano wa vyama ili kuweza kuliondoa tatizo la umeme.Nikakupa mfano kuwa vyama vingi vimeanza tu recently.Na kwa hivyo kublame kutokushirikiana kwa vyma ni upotofu.Na wengi wa wapinzani walikuwa CCM before.Sera za CCM hazijaweza kutuondolea tatizo tulilonalo.Ni kwamba hawajawa serious.Hawahitaji ushirikiano wa upinzani kama wana agenda ya kutosheleza.

Nimekusoma vyema tu,nimeshangazwa na wewe kusapoti kauli ya "Mimi si Mungu ninyeshe mvua" Umesoma wewe dada,naamini hivyo.Tafadhali.
 
WoS,
Nishati ni nyenzo muhimu sana katika maendeleo ya nchi. Nchi zote zilizopiga hatua zinalichukulia suala la nishati kama usalama wa taifa.
Tangu tatizo lilipoanza unaweza nchi imeathirika sana kiuchumi. Kama tungelikuwa na idara za uchumi na takwimu independently tungeona data za kutisha sana. TRA peke yake wanapoteza mabilioni , pesa zinazohitajika kuendesha serikali na kukabili nakisi inayozibwa na wafadhili.

Maisha ya wananchi yamebadilika sana kijamii na kiuchumi kuanzia inflation, employment n.k. Uwekezaji unaopigiwa debe sasa umekwama, nani atawekeza mahali pasipo na nishati ya uhakika? Tunaona makampuni yanakimbilia nchi jirani n.k. Kwa muktadha huu suala la nishati huwezi kulitenga na usalama wa taifa kiuchumi na ni hapo linaangukia mikononi mwa Rais na serikali yake.

Katiba iliyopo Rais ana mamlaka yote kuliko chombo kingine. Mfano, alipotakiwa kuwawajibisha walioshiriki kuhujumu nishati ,kwa mamlaka yake aliwaacha wastaafu na wengine hawakuchukuliwa hatua. Kumbuka yeye ndiye mwenyekiti wa baraza la mawaziri linaloidhinisha miradi mikubwa kama ya nishati na yeye ndiye anayeidhinisha malipo au madeni ya nchi. Inaweza kuwa siye anayesaini lakini afanyaye hivyo ana baraka zake zote. Hili linajibu swali la awali kuwa nani alaumiwe kwa tatizo.

Alipochaguliwa alijua tatizo na alikuwa na majibu ambayo wananchi wanayataka(rejea ilani ya uchaguzi). Hakuchaguliwa kutueleza chanzo cha tatizo bali suluhisho. Inapotokea nchi yenye upepo, natural gas, coal na wind inaingia gizani na jibu la Rais ni kumlaumu mungu inasikitisha. Yaani kwa mamlaka na uwezo wake wote aliopewa na katiba anashindwa kutumia rasilimali za mungu badala yake anakimbilia kumlaumu !hapo kuna tatizo, tena kubwa.

Ushirikiano wanaotoa wapinzani haupokelewi. Wanaposema wezi na wahujumu wa nishati wafikishwe mbele ya sheria na ikiwezekana wafilisiwe, serikali na rais wanatumia siasa kuwakejeli.
Kwa nchi za wenzetu mawazo ya wapinzani huchukuliwa na kufanyiwa kazi,hapa kwetu hilo litahatarisha uwepo wa baadhi ya watu mjengoni Dodoma, hivyo ni bora kuwakabili wapinzani na si kutatua matatizo ya umeme.
Mikataba ya nishati inapofanywa siri ili kuwalinda wahalifu tutarajie wapinzani wafanye nini zaidi? Ndio, ushirikiano unahitajika lakini hakuna utayari wa kushirikiana kama Rais alivyomkejeli Mnyika na waziri wake kumkejeli Mbowe.

Lazima tukiri kuwa hapa tulipo ingawa bado tupo porini, vyama vya siasa kama Chadema vimesaidia sana kupaza sauti na kuamsha CCM. Sakata la Jairo na Ngeleja limeungwa mkono na CCM kwa hofu ya upinzani kulifanya ajenda. Ni kweli safari yetu hasa ya vyama vya upinzani ni ndefu lakini tuwashukuru kwa kile kidogo wanachokifanya kwa uchache wao chini ya ubabe wa bunge la CCM na spika wake.

Rais wa nchi hapaswi kulalamika au kutoa visingizio kwa kushindwa kutatua tatizo. Hakuchaguliwa kuwa kiongozi wa kidini anayetukumbusha kazi ya mwenyezi mungu. Amechaguliwa kutatua matatizo ya wananchi kwa kushirikiana na wenzake.
Kama Kenya kuna ukame na umeme upo, kwanini tumlaumu Mwenyezi mungu kwa ututusa wetu?
Katiba yetu inampa mamlaka yote na anabeba dhima kubwa ya kututatulia matatizo kwa heshima aliyopewa. Heshima inaambatana na kuwajibika na majukumu sio ving'ora, kwa hili la umeme hana jinsi ya kukwepa lawama na kushindwa kwake. Ni failure ya Rais kiuchumi, kisiasa na kijamii bila kumsingizia mwenyezi mungu.
 
WoS,
Nishati ni nyenzo muhimu sana katika maendeleo ya nchi. Nchi zote zilizopiga hatua zinalichukulia suala la nishati kama usalama wa taifa.
Tangu tatizo lilipoanza unaweza nchi imeathirika sana kiuchumi. Kama tungelikuwa na idara za uchumi na takwimu independently tungeona data za kutisha sana. TRA peke yake wanapoteza mabilioni , pesa zinazohitajika kuendesha serikali na kukabili nakisi inayozibwa na wafadhili.

Maisha ya wananchi yamebadilika sana kijamii na kiuchumi kuanzia inflation, employment n.k. Uwekezaji unaopigiwa debe sasa umekwama, nani atawekeza mahali pasipo na nishati ya uhakika? Tunaona makampuni yanakimbilia nchi jirani n.k. Kwa muktadha huu suala la nishati huwezi kulitenga na usalama wa taifa kiuchumi na ni hapo linaangukia mikononi mwa Rais na serikali yake.

Katiba iliyopo Rais ana mamlaka yote kuliko chombo kingine. Mfano, alipotakiwa kuwawajibisha walioshiriki kuhujumu nishati ,kwa mamlaka yake aliwaacha wastaafu na wengine hawakuchukuliwa hatua. Kumbuka yeye ndiye mwenyekiti wa baraza la mawaziri linaloidhinisha miradi mikubwa kama ya nishati na yeye ndiye anayeidhinisha malipo au madeni ya nchi. Inaweza kuwa siye anayesaini lakini afanyaye hivyo ana baraka zake zote. Hili linajibu swali la awali kuwa nani alaumiwe kwa tatizo.

Alipochaguliwa alijua tatizo na alikuwa na majibu ambayo wananchi wanayataka(rejea ilani ya uchaguzi). Hakuchaguliwa kutueleza chanzo cha tatizo bali suluhisho. Inapotokea nchi yenye upepo, natural gas, coal na wind inaingia gizani na jibu la Rais ni kumlaumu mungu inasikitisha. Yaani kwa mamlaka na uwezo wake wote aliopewa na katiba anashindwa kutumia rasilimali za mungu badala yake anakimbilia kumlaumu !hapo kuna tatizo, tena kubwa.

Ushirikiano wanaotoa wapinzani haupokelewi. Wanaposema wezi na wahujumu wa nishati wafikishwe mbele ya sheria na ikiwezekana wafilisiwe, serikali na rais wanatumia siasa kuwakejeli.
Kwa nchi za wenzetu mawazo ya wapinzani huchukuliwa na kufanyiwa kazi,hapa kwetu hilo litahatarisha uwepo wa baadhi ya watu mjengoni Dodoma, hivyo ni bora kuwakabili wapinzani na si kutatua matatizo ya umeme.
Mikataba ya nishati inapofanywa siri ili kuwalinda wahalifu tutarajie wapinzani wafanye nini zaidi? Ndio, ushirikiano unahitajika lakini hakuna utayari wa kushirikiana kama Rais alivyomkejeli Mnyika na waziri wake kumkejeli Mbowe.

Lazima tukiri kuwa hapa tulipo ingawa bado tupo porini, vyama vya siasa kama Chadema vimesaidia sana kupaza sauti na kuamsha CCM. Sakata la Jairo na Ngeleja limeungwa mkono na CCM kwa hofu ya upinzani kulifanya ajenda. Ni kweli safari yetu hasa ya vyama vya upinzani ni ndefu lakini tuwashukuru kwa kile kidogo wanachokifanya kwa uchache wao chini ya ubabe wa bunge la CCM na spika wake.

Rais wa nchi hapaswi kulalamika au kutoa visingizio kwa kushindwa kutatua tatizo. Hakuchaguliwa kuwa kiongozi wa kidini anayetukumbusha kazi ya mwenyezi mungu. Amechaguliwa kutatua matatizo ya wananchi kwa kushirikiana na wenzake.
Kama Kenya kuna ukame na umeme upo, kwanini tumlaumu Mwenyezi mungu kwa ututusa wetu?
Katiba yetu inampa mamlaka yote na anabeba dhima kubwa ya kututatulia matatizo kwa heshima aliyopewa. Heshima inaambatana na kuwajibika na majukumu sio ving'ora, kwa hili la umeme hana jinsi ya kukwepa lawama na kushindwa kwake. Ni failure ya Rais kiuchumi, kisiasa na kijamii bila kumsingizia mwenyezi mungu.

Ndugu yangu Nguruvi3
Heshima kwako sana mkuu!
Umelenga kwenye moyo haswaa!

Hata mimi nakubaliana nawe kuwa suala la umeme ni nyeti na siyo tatizo la kawaida.Linalenga kwenye usalama wa nchi kwa maana halisi. Kukosekana umeme kunahatarisha maisha ya watanzania.

Je rais wetu hawezi kuchukua hatua za dharura ikibidi hata kupunguza vifungu vya bajeti za wizara na kuelekeza nyenzo zote kuhakikisha tunapata umeme tunusuru uchumi na mengi yaliyomo hatarini?

Rais kasema tumpe mapendekezo ya jinsi gani kutatua tatizo. Nadhani moja ya pendekezo ni hili!
 
Hata mimi nakubaliana nawe kuwa suala la umeme ni nyeti na siyo tatizo la kawaida.Linalenga kwenye usalama wa nchi kwa maana halisi. Kukosekana umeme kunahatarisha maisha ya watanzania.
Je rais wetu hawezi kuchukua hatua za dharura ikibidi hata kupunguza vifungu vya bajeti za wizara na kuelekeza nyenzo zote kuhakikisha tunapata umeme tunusuru uchumi na mengi yaliyomo hatarini?
Rais kasema tumpe mapendekezo ya jinsi gani kutatua tatizo. Nadhani moja ya pendekezo ni hili!

WoS, Rais anapewa mamlaka na katiba kutangaza hali ya dharura, na vitu kama presidential decree. Nguvu hizo zinamwezesha yeye kuchukua hatua za dharura kwa manufaa ya nchi, ikiwa ni pamoja na kuelekeza resource bila ruhusa ya mamlaka nyingine ikibidi. Kwahiyo tatizo sio pesa au nyenzo nyingine ila kitu kinaitwa political will.

Suala la umeme limekuwa la kisiasa zaidi kuliko utaalamu ndio maana kuna mwingiliano wa kamati za bunge, wizara n.k. Hakuna anayejua nani mwenye kauli zaidi ya mwingine. Kibaya zaidi wataalamu wamewekwa pembeni ili siasa ikidhi matakwa ya wahitaji.
Richmond ilingia kwa nguvu za siasa na sio wataalam. Na kibaya zaidi wanasiasa wanaofanya hivyo 'wanamamlaka' yasiyo rasimi ndani ya serikali lakini yenye nguvu sana.Hawa ndio wanoifunga serikali na Rais mikono ya kuchukua hatua za dharura, wakilinda masilahi yao. Sidhani Dowans a.k.a Symbion au IPTL wangependa mgao upungue!!

Rais anapoomba mawazo ni dalili nyingine ya kushindwa kazi. Hivi mwanakijiji anayewania mhogo wa siku au yule mama aliyebeba ndoo ya maji km 5, au mfanyakazi anayekata mbuga kutoka ubungo kwenda posta kwa mguu,kweli anaweza kuwa na wazo la kumpa mheshimiwa. Hawa wana mizigo mizito inayowasubiri.

Mbowe ametoa ushauri iundwe kamati ya wataalamu wanaoweza kuja na solution. Kumbuka pia tuna wasomi waliobobea katika uchumi, nishati, biashara n.k kutoka katika rasilimali watu na academicians. Rais hajawatumia hawa.
Kamati za bunge, shirikisho la wenye viwanda, wawekezaji kila mara wamekuwa na ushauri. Jambo la kusikitisha ni kuwa ushauri na maoni yao yanapofika mezani kwa mheshimiwa hukutana na nguvu kubwa ya kisiasa na huwekwa pembeni.

Rais anatakiwa atoke mbele, atangaze hali ya dharura, akutane na wadau wa sekta ya nishati, wanataaluma,wanasiasa makini na wafanyabiashara wenye nia njema walizungumze tatizo na kupata ufumbuzi wa muda mfupi na muda mrefu.
Atafanikiwa tu endapo atakubali kuweka siasa pembeni, kuacha wapambe na kuwa tayari kuchukua maamuzi magumu.

Kazi ya Rais ni ku mobilise resources ili zitoe majibu ya matatizo, inapofika mahali yeye hawezi kutumia resources zote kama human resource,natural resource, political and executive power anasubiri kusikia kutoka mitaani inasikitisha!!
Majibu ya tatizo yapo, shida inakuwa nani wa ku mobilize resource za kiutaalamu, kiutendaji ili zitoe majibu? Kama kumfukuza Jairo ilisubiri Rais akiwa nje, na kwa mwendo wa safari za nje nani anaweza kusimamia zoezi la umeme lenye nguvu za kisiasa na kiushawishi kama si yeye.
 
Hamna mshikamano kwenye jamii ya sasa. Dikteta na muwongo mkubwa Kikwete anadai kwenye mahojiano yake na BBC eti mwenye idea ya solution aljitokeze Serikali yake ipo tayari kusikiliza. Lakini ukweli ni kwamba kina Mufuruki wanaowakilisha sekta binafsi wamepiga kelele wee kuonyesha umuhimu wa Serikali kuwajumuisha wadau mbalimbali kwenye jamii kutafuta suluhisho la dharura la tatizo la umeme lakini hakuna dalili kuwa hilo limefanyika.
 
Haipo sawa hiyo! Majibu menyewe hayana logic, anayetegemewa atoe majibu naye hajui nini chakusema! Tz yetu noma!
 
Kibaya zaidi wataalamu wamewekwa pembeni ili siasa ikidhi matakwa ya wahitaji.
This is the saddest fact....nadhani viongozi wetu wafike mahali waone aibu!


Kumbuka pia tuna wasomi waliobobea katika uchumi, nishati, biashara n.k kutoka katika rasilimali watu na academicians. Rais hajawatumia hawa.
Kamati za bunge, shirikisho la wenye viwanda, wawekezaji kila mara wamekuwa na ushauri. Jambo la kusikitisha ni kuwa ushauri na maoni yao yanapofika mezani kwa mheshimiwa hukutana na nguvu kubwa ya kisiasa na huwekwa pembeni.

Hili nalo neno! Nakumbuka hata hapa JF kuna mada iliwahi kuanzishwa na tukampata Eng.Nsiande mwana JF mwenzetu akatoa insights nzuri sana kama mtaalamu ndani ya TANESCO kuonyesha kwamba kuna zaidi ya yanayozungumzwa na wanasiasa.Sasa Mh.Rais anataka muujiza gani tena kama hataki kutuma wataalam au hata kusikiliza ushauri unaotolewa na wadau mbalimbali?

Rais anatakiwa atoke mbele, atangaze hali ya dharura, akutane na wadau wa sekta ya nishati, wanataaluma,wanasiasa makini na wafanyabiashara wenye nia njema walizungumze tatizo na kupata ufumbuzi wa muda mfupi na muda mrefu.
Atafanikiwa tu endapo atakubali kuweka siasa pembeni, kuacha wapambe na kuwa tayari kuchukua maamuzi magumu.

Laiti kama angesikia na kuchukua hatua za dharura maana wananchi sasa tumechoka na tunapoteza subira.



Hamna mshikamano kwenye jamii ya sasa. Dikteta na muwongo mkubwa Kikwete anadai kwenye mahojiano yake na BBC eti mwenye idea ya solution aljitokeze Serikali yake ipo tayari kusikiliza. Lakini ukweli ni kwamba kina Mufuruki wanaowakilisha sekta binafsi wamepiga kelele wee kuonyesha umuhimu wa Serikali kuwajumuisha wadau mbalimbali kwenye jamii kutafuta suluhisho la dharura la tatizo la umeme lakini hakuna dalili kuwa hilo limefanyika.

Sijui kama hajawasikiliza wadau hawa wenye uelewa mpana wa tatizo, anataka nani tena amshauri!

WoS,

OUr Dear leader has no clue about nothing!

MHH! Yangu macho na masikio tu...... sina la kusema
 
I beg to differ on this talk that we need Katiba first.

It seems recently with the talk of New Katiba being on way, we have resorted to point fingers at Katiba and claim that nothing can be done without Katiba mpya.

A new Katiba can never bring significant competency on an individual, rather it will be a tool sort of to rid of someone in power, but has nothing to do with Maendeleo.

The claims that we need new Katiba so that we can rid poverty, bureaucracy and corruption have no difference with Kikwete claiming he is not the creator and government can not make rain!

THe only thing Katiba will do is to create checks and balances in which we have such opportunity to do checks and balances with our current Katiba, but we choose (CCM, Opposition and Wananchi) not to use the means available currently to bring discipline and fiscal responsibility.

The CAG report for the last 3 years, demonstrates an extreme misuse of government funds, budget and taxes. How can a new Katiba fix that problem if we know that misuse has penalties, from civil to criminal charges and the only problem is decision making to reprimand those who are abusing an d mismanage these funds?

A new President and new Katiba will not bring Umeme or rid Umasikini if we the people are not committed to rid Umasikini and demand Umeme. No changes will take place if we continue to elect inneficient representatives and rather than openly air our voices of no confidence, we are easily manipulated through cheap politics and we dust off our wounds and move forward singing hewala, Mungu atatujalia na ni Mapenzi yyake.

There is no way, if Tanzanians were sane enough that people would have passed out and collapse sobbing about resignation of Rostum. It is an insult to hear a massive turnout in the rally in Mbeya led by Nape, Sitta and Mwakyembe while people are suffering and live unde abject poverty.

We must have been Jujurized somewhere that we are turning our cheeks to CCM and scraundel politicians who have been unable to deliver development and prosperity to us.

May be we ought to go back to the same God who has tighten the rain showers for his mercy so that he can shower us with not only rains to fill our hydro electric dams and our farms, but rain us with wisdom and confidence to fight for what is just and right for us as a nation and as his Children.
 
Hata sijaona swali hapo zaidi ya maelezo mareeeeefu yaliyopindapinda kama Mizengo

Kama tuna sheria kwanini isitumike sheria ku deal na Jairo?

Kama mtu ametoa rushwa, au kama mtu anakausanya fedha kwa ajili ya kutoa rushwa, kama mtu amekuwa akifanya ujanja wa kutumia mlungula kuwahonga wabunge ili wapitishe bajeti yake, kwanini rais asubiriwe na sio sheria zilizopo?

Kwanini tutegemee mtu aamue jambo wakati kuna system in place ku deal na mambo kama hayo?

Kwanini David Jairo asikamatwe na Takukuru na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria?

Mkuu naona woman of substance ameweka maswali yote haya. Nadhani hakuyandika kwa style hii akiamini kuwa hapa JF watu wanajua ni nini kinaendelea.
 
Back
Top Bottom