Kumtegemea Rais kupata majibu ya kila tatizo la nchi ni sawa?

Mkuu naona woman of substance ameweka maswali yote haya. Nadhani hakuyandika kwa style hii akiamini kuwa hapa JF watu wanajua ni nini kinaendelea.

Mkuu
Asante kuwatafunia wale waliozoea kutafuniwa kila kitu.Unajua Mkuu tunasikia kiwango cha elimu kimeshuka sana Tanzania.Moja wapo ya sababu ni kwa vile wanafunzi wengi wa ngazi zote wanapenda sana DESA. Wanataka mwalimu awape kila kitu, awaandikie notes na handouts. Library na vyanzo vingine vya maarifa ni kama kituo chapolisi! Hawataki kujisomea, kufikiri wala kutafiti.Hawataki kusumbua akili hata kidogo kusoma kitu na kuelewa kilichomo.Na ndio maana kuna usemi mbaya unaosema ' if you want to hide something from M-bongo,put it in writing/book"! watu wamezoea kusoma magazeti ya udaku tu. Ukimpa gazeti lolote makini atakuambia hajaona cha kusoma humo.

Huyu mwenzetu aliyesema hajaona swali wala usimshangae hata kidogo maana kawakilisha wengine wengi tu.
 
Urais ni taasisi; na kama taasisi inakuwa haina majibu (muda mfupi na muda mrefu) ya kutosheleza ktk kutatua matatizo ya wananchi wake; kwangu mimi hili ninaliona kuwa ni janga kubwa sana.
 
Suala la umeme kumtupia raisi pekee kwa kweli si sawa hila kuna lawama kadhaa ambazo azimuepuki particularly uzembe wake kwenye kusimamia maslahi (luck of information regarding his subordinates perforamance and political bureacy iliyojaa chini hivi ni vikwazo vya maendeleo mengi kwetu), uwajibikaji katika serikali yake ni aibu tupu kutumia lugha ya kistaarabu.

Akiwa kama nahodha indirectly he is to blame kwa kuwa yeye ndio mteuzi wa wazembe wengi na vilaza wengi kwenye serikali yake, na hii issue ya umeme kwa kweli wasomi wote waliojaa Tanzania awawezi shindwa tatua. Tatizo ni kwamba inaonekana suala la umeme ni mtaji wa mafisadi hapo ndio kuna mbinu za kutenga hela na kuzipoteza kwa namna ya lobbying na uanichi mwingine waujuao wao.

Kuna mfano mmoja wapo jamaa walilipata li mashine kubwa la umeme kuliko hilo la Dowans na wazungu walio negotiate nao wakasema hawataki malipo ya hata senti mpaka after five years; ndio wao watakao liendesha for that period na kugawana profit. After five years lilipiwe liwe mali yetu. Hapo tena ndyo yakaja yale mambo ya unamjua nani serikalini biashara ikaingia nyani haraka sana kisa watu wenyewe waliokuwa mstari wa mbele ni watanzania wakaida na sisi watoto wa mafisadi wala wadosi.

Hapo kweli tutafika hizi siasa za bongo ni uchwara mtupu si ajabu wengine wanaona bora kwanza kuweka life perspective sawa kulikoni kubangaizana na hawa useless individuals (wanasiasa wabongo). Hatari namna hii.
 
Reactions: LAT

Hapo penye bold naona kuna mtego.Hata mimi ningekuwa yeye ningesita! There is no free lunch.. unless its the cheese on the mouse trap.Nayo pia siyo bure, panya anahatari kulipa na maisha yake.
 
Hapo penye bold naona kuna mtego.Hata mimi ningekuwa yeye ningesita! There is no free lunch.. unless its the cheese on the mouse trap.Nayo pia siyo bure, panya anahatari kulipa na maisha yake.
There's no trap whatsoever jamaa walitaka serikali igharimu kulileta huko wao ndio ndio watakao li set up na kuzalisha umeme mpaka wazawa walizoee bila ya hela ya malipo ya mtambo, trust me that negotiation was not done by dump people watu walipiga chini hela za kulipa wanasheria wakizungu waweke mkataba hila serikali yetu ndio tatizo. Apparently wazawa weusi hawastahili dili kubwa; hizi ni za akina rostam na manji sijui na wapuuzi gani wengine.

Wajirekebishe waone mambo au wawasikilize watu halafu tuone kama umeme ni tatizo la hivyooo.
 


Umejibu vyema sana kaka .Mfumo wa utawala Tanzania umekuwa centralized na Rais ana aamini kwamba ana final say juu ya kila jambo .Yuko juu ya kila kitu .Kama nchi ingalikuwa na utawaala wa kusambaa wa ukweli hakika tungalikuwa mbali na pasingalikuwa na upuuzi huu .Viongozi wote wateule wanawajibika kwa Rais na si kwa Nchi na wananchi .Ndiyo maana kuna ushenzi kibao na tunalia na Rais tu hakuna wa zaidi .
 
Wiki hii tumeshuhudia matatizo ya mafuta. Yale ya umeme tumeanishwa kuwa ni ya mungu.
Hapa ndipo suala la kutegemea serikali linapoingia,haiwezekani kila mtu akaagiza mafuta itakuwa ni vurugu tupu. Anayepaswa kuratibu mipnago ni Rais ambaye ni mkuu wa serikali na nchi.

Hatujamsikia Rais na tumewasikia watu wake baada ya shinikizo bungeni. Kama si Rais wa kutupa majibu ni kwa vipi tudhani tunaweza kutoa suluhisho?
Endapo wananchi wataamua kutafuta suluhu bila kumtegemea mkuu wa nchi tutafika pabaya.
Ni kwa maana hiyo nasema yapo tunyoweza kutoa majibu na yapo yanayomtegemea mkuu wa nchi vinginevyo rais anawajibu gani ?
 
Raisi leo anafikia mahali anasema hata Mwalimu Nyerere, Mwinyi & Mkapa wameongoza nchi na wameshindwa kumaliza matatizo sembuse yeye...Yaani kila siku ni visingizio na malalamishi kibao, watendaji wanamuangusha (japo anaendelea kuwakumbatia), Kudura za Mwenyezi Mungu kuleta mvua (Steigler Gorge imelala miaka 20 sasa) na excuses nyingine nyiiiingi!! Nyerere alishasema Magogoni si mahali pa kupakimbilia, ni mzigo...sasa kama yeye alipakimbilia ndo matokeo yake haya sasa!! Imetosha sasa...Raisi aache kujiweka kuwa naye ni victim na afanye kazi!!!

Obama ameingia madarakani amekuta nchi imeshatikiswa kiuchumi kwa kiasi kikubwa lakini huwezi kumsikia anamsingizia G. W. Bush hata siku moja...anagangamala kivyake na wananchi watamsulubisha 2012 bila kujali kuwa matatizo yalianza wakati wa utawala wa nani!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…