Kumtofautisha Rais Kikwete na wabunge wa CCM katika swala la katiba mpya ni kujidanganya!

Kumtofautisha Rais Kikwete na wabunge wa CCM katika swala la katiba mpya ni kujidanganya!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Mimi nawashauri viongozi wa vyama vya CHADEMA,NCCR na CUF wasiwe na matumaini kwamba Raisi Kikwete atawasikiliza na kwamba hatasaini muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba.

Raisi Kikwete ndie mwenyekiti wa CCM taifa na huu ni mkakati wa CCM kwahiyo wanachofanya wabunge wa CCM ni kutekeleza tu mkakati wa chama chao na hivyo Kikwete kutosaini itakuwa ni sawa na kuwasaliti wana CCM wenzake wakiwemo hao wabunge wa CCM waliopitisha muswaada huo.

Pia ifahamike kuwa serikali ya Kikwete imekuwa ikitegemea wabunge wa CCM kupitisha mambo yake ndani ya bunge na kwa maana hiyo si rahisi kwa Raisi Kikwete kuwaudhi wabunge ambao siku zote ndio tegemeo lake ndani ya bunge.

Atakachofanya Kikwete sana sana ni labda kuwaita wapinzani Ikulu kama ushahidi tu na kuwaridhisha licha ya kauli ya Wassira kwamba hatutawaita tena wapinzani Ikulu.Atakaa nao Ikulu wataongea lakini mwisho wa siku atasaini tu kama alivyowahi kufanya siku za nyuma juu ya swala hilo hilo la Katiba alipokutana na CHADEMA.

Raisi Kikwete siku zote ni mtu wa kuangalia upepo na huu muungano wa wapinzani juu ya katiba si wa kuupuza na hivyo ile kauli ya waziri Wassira haitafanyiwa kazi.Na pia naamini ile kauli ya Wassira ni kauli ya Kikwete.

Tusijdanganye,hakuna tofauti kati ya Kikwete na wabunge wa CCM katika swala la katiba.Kama ni kutosaini ni lazima Kikwete ashauriane na chama chake na si vinginevyo hata ikibidi kwa siri.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kwamba kikwete na Lusinde mbunge wa Mtera ni sawa sawa.
Hawana tofauti.
 
Kikwete na wabunge wake lao moja...sina imani naye ....

Labda ani "prove wrong" kwa hili.
 
Hapana Ninapishana na wewe, historia inaonyesha kuwa Rais Kikwete amekuwa akifanya maamuzi yake kwa kupitia washauri wake wa karibu kwa kujali maslahi ya kitaifa. Unakumbuka hoja ya Katiba mpya ililetwa na chama cha upinzani? na CCm walipinga kwa nguvu zote na kejeli hata kutumia wazee wake wakongwe kwenye hilo? lakini mwisho wake nini kilitokea? na nadhani kuwaita upinzani Ikulu si kuwabembeleza, bali ni kujenga ushawishi maana hiyon ndio demokrasia ili kupata kuungwa mkono, na kilichotokea alikubali ushauri wao. rasimu ya sasa kwa taarifa yako ilikuwa mezani kwa Rais kabla ya kurushwa hewani, na akaibariki, hakushindwa kuwadokezea na kuwashawishi kuondoa mambo fulani ambayo yeye angedhani yangeikwaza CCM. Aliamini kabisa kuwa anawaletea wananchi kitu chema na nina uhakika anajua angepingwa na baadhi ya makundi ndani ya CCM. Kwa hilo tayari anasisitiza wale wana-CCm wanaosimamia kutokuwapo kwa mabadiliko wajiandae kisaikolojia, nadhani hapo umenipata.
 
Huwezi kutenganisha matawi na shina kwenye mti mmoja.

Msimamo wa wabunge wa ccm ni msimamo wa chama ambacho kikwete ndiyo mwenyekiti.

Ni ukweli uliyowazi kwamba ccm bado wapo usingizini na wanaiota ile kauli ya zidum fikra za mwekiti,

nakatika ndoto hiyo walipanga mkakati wakiamini kupitia bunge wataipitisha kwa nguvu ya wingi/rubertamp siyo ubora wa

hoja-japo ni ya hovyo lakini walilenga kwenye wingi wao na kusahau kabisa kwamba lile sio bunge la chama kimoja na

pale mjengoni kunavichwa-upinzani ambavyo hujenga hoja na katu haviburuziki-ukitaka kuviburuza vinakuachia bunge

nakupeleka kesi kwa raia/watanzania. Ni mtihani ambao hawakuutarajia na lazima inampasua kichwa kikwete.
 
Hapana Ninapishana na wewe, historia inaonyesha kuwa Rais Kikwete amekuwa akifanya maamuzi yake kwa kupitia washauri wake wa karibu kwa kujali maslahi ya kitaifa. Unakumbuka hoja ya Katiba mpya ililetwa na chama cha upinzani? na CCm walipinga kwa nguvu zote na kejeli hata kutumia wazee wake wakongwe kwenye hilo? lakini mwisho wake nini kilitokea? na nadhani kuwaita upinzani Ikulu si kuwabembeleza, bali ni kujenga ushawishi maana hiyon ndio demokrasia ili kupata kuungwa mkono, na kilichotokea alikubali ushauri wao. rasimu ya sasa kwa taarifa yako ilikuwa mezani kwa Rais kabla ya kurushwa hewani, na akaibariki, hakushindwa kuwadokezea na kuwashawishi kuondoa mambo fulani ambayo yeye angedhani yangeikwaza CCM. Aliamini kabisa kuwa anawaletea wananchi kitu chema na nina uhakika anajua angepingwa na baadhi ya makundi ndani ya CCM. Kwa hilo tayari anasisitiza wale wana-CCm wanaosimamia kutokuwapo kwa mabadiliko wajiandae kisaikolojia, nadhani hapo umenipata.
Profesa mpaka muswada kupelekwa Bungeni haukupitia kwenye kikao cha baraza la mawaziri ambacho Mh. Kikwete ndiye mwenyekiti?..........kitakachotokea Mh.Kikwete atasaini huo mswada kuwa sheria na CCM itatumia pesa nyingi sana na kufanya mikutano ya hadhara kutetea kile walichopitisha ndani ya Bunge kama walivyowahi kufanya kwa bajeti ya Meghji
 
Last edited by a moderator:
Hapana Ninapishana na wewe, historia inaonyesha kuwa Rais Kikwete amekuwa akifanya maamuzi yake kwa kupitia washauri wake wa karibu kwa kujali maslahi ya kitaifa. Unakumbuka hoja ya Katiba mpya ililetwa na chama cha upinzani? na CCm walipinga kwa nguvu zote na kejeli hata kutumia wazee wake wakongwe kwenye hilo? lakini mwisho wake nini kilitokea? na nadhani kuwaita upinzani Ikulu si kuwabembeleza, bali ni kujenga ushawishi maana hiyon ndio demokrasia ili kupata kuungwa mkono, na kilichotokea alikubali ushauri wao. rasimu ya sasa kwa taarifa yako ilikuwa mezani kwa Rais kabla ya kurushwa hewani, na akaibariki, hakushindwa kuwadokezea na kuwashawishi kuondoa mambo fulani ambayo yeye angedhani yangeikwaza CCM. Aliamini kabisa kuwa anawaletea wananchi kitu chema na nina uhakika anajua angepingwa na baadhi ya makundi ndani ya CCM. Kwa hilo tayari anasisitiza wale wana-CCm wanaosimamia kutokuwapo kwa mabadiliko wajiandae kisaikolojia, nadhani hapo umenipata.
Hivi unakumbuka kauli za Werema kuhusu katiba mpya?Na unadhani Werema kama mshauri wa Raisi alimshauri nini Kikwete kuhusu katiba?

Na je unakumbuka kauli ya mshauri mwingine wa Raisi kuhusu katiba mpya?Huyu si mwingine bali ni aliyekuwa waziri wa sheria na katiba kwa wakati ule mama Kombani.

Hao wote walitoa kauli za kupinga kuanza kwa mchakato wa katiba mpya na sasa unadhani walimshauri nini Raisi juu ya kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya?

Hapa jibu ni moja tu nalo ni kuwa Raisi mwenyewe na washauri wake wakuu walikuwa wanapinga wazo la kuanzisha mchakato wa kuanzisha katiba mpya ili kilichowasukuma kukubali kuanzisha mchakato huo ni shinikizo(pressure) kutoka kwa makundi mbalimbali ya kijamii,wanasiasa na wananchi kwa ujumla.

Hili liko wazi hata mtoto wa shule ya msingi anajua hivyo.Acheni kupotosha watu!
 
Hapana Ninapishana na wewe, historia inaonyesha kuwa Rais Kikwete amekuwa akifanya maamuzi yake kwa kupitia washauri wake wa karibu kwa kujali maslahi ya kitaifa. Unakumbuka hoja ya Katiba mpya ililetwa na chama cha upinzani? na CCm walipinga kwa nguvu zote na kejeli hata kutumia wazee wake wakongwe kwenye hilo? lakini mwisho wake nini kilitokea? na nadhani kuwaita upinzani Ikulu si kuwabembeleza, bali ni kujenga ushawishi maana hiyon ndio demokrasia ili kupata kuungwa mkono, na kilichotokea alikubali ushauri wao. rasimu ya sasa kwa taarifa yako ilikuwa mezani kwa Rais kabla ya kurushwa hewani, na akaibariki, hakushindwa kuwadokezea na kuwashawishi kuondoa mambo fulani ambayo yeye angedhani yangeikwaza CCM. Aliamini kabisa kuwa anawaletea wananchi kitu chema na nina uhakika anajua angepingwa na baadhi ya makundi ndani ya CCM. Kwa hilo tayari anasisitiza wale wana-CCm wanaosimamia kutokuwapo kwa mabadiliko wajiandae kisaikolojia, nadhani hapo umenipata.

Kukubali mabadiliko ya katiba lilikuwa ni jambo ambalo Kikwete asingeweza kulizuia. Ile ni kama upepo wa vyama vingi ulipovuma...Tanzania hata ingekataa ingejikuta inabaki peke yake. Mambo mengine haya ni kuangalia na wenzetu wanafanya nini. Sasa linapoamuliwa lifanyike, na jinsi linavyofanyika ndipo utata unapojitokeza.
 
ulitaka kikwete afanane na wabunge wa cuf au chadema fikiri kwanza kabula hujapost bavicha ni janga lataifa.
 
Unakosea sana. Kumbuka hata wazo la katiba mpya CCM hawakuwa nalo lakini ni JK aliyewaburuza baada ya yeye naye kubanwa na shinikizo la umma. Hata hapo tulipofika bado JK ana uwezo wa kuwaburaza CCM wenzake akielewa hoja ni nini na kama kweli dhana ya katiba anaielewa na kuikubali. Ni muhimu sana JK aendelee kushinikizwa ili aendelee kujitoa mhanga kwa ajili ya nchi na kuachana na maslahi finyu ya chama chake. Katiba Mpya ni jambo pekee alilobaki nalo katika kuweka alama ya kudumu ya utawala wake. Likimponyoka hili basi tena atasaulika mapema sana baada ya utawala wake kwisha.​
 
Kwani ni lini CHADEMA wamemtambua JK kama ni Rais wa Tanzania? Au wana maana Rais Dr Slaa? mniweke wazi hapo wakuu
 
Mimi nimeshafuatilia kwa karibu sana mchakato wa Katiba mpya. Kila chama kina mkakati wake, CCM wana mkakati wao na CHADEMA nao wana mkakati wao, CUF na NCCR wanapelekwa kama majuha. CHADEMA hawana wangekuwa na jipya kwenye mchakatohuu wangeanza kususia pale walipoitwa kwenda kunywa chai Ikulu. Tutambue kuwa siyo watakaloliomba kwa Rais kikwete ili lionekane jema sharti alikubali, la hasha, wao wana mkakati wao na CCM wana mkakati wao.
 
ulitaka kikwete afanane na wabunge wa cuf au chadema fikiri kwanza kabula hujapost bavicha ni janga lataifa.
Tumia akili!Swala la katiba ni zaida ya vyama na ndio maana leo hata wapinzani wanaungana juu ya swala hili.

Wewe kwa akili zako unadhani ni makosa Raisi kuungana na wapinzani linapokuja swala la katiba kama tungekuwa na mkuu wa nchi makini?!

Hii nchi wala katiba si mali ya CCM!
 
Unakosea sana. Kumbuka hata wazo la katiba mpya CCM hawakuwa nalo lakini ni JK aliyewaburuza baada ya yeye naye kubanwa na shinikizo la umma. Hata hapo tulipofika bado JK ana uwezo wa kuwaburaza CCM wenzake akielewa hoja ni nini na kama kweli dhana ya katiba anaielewa na kuikubali. Ni muhimu sana JK aendelee kushinikizwa ili aendelee kujitoa mhanga kwa ajili ya nchi na kuachana na maslahi finyu ya chama chake. Katiba Mpya ni jambo pekee alilobaki nalo katika kuweka alama ya kudumu ya utawala wake. Likimponyoka hili basi tena atasaulika mapema sana baada ya utawala wake kwisha.​
Ndio maana nikasema Jk huwa anaangalia upepo unakwendaje.
 
ulitaka kikwete afanane na wabunge wa cuf au chadema fikiri kwanza kabula hujapost bavicha ni janga lataifa.
 
Mimi nimeshafuatilia kwa karibu sana mchakato wa Katiba mpya. Kila chama kina mkakati wake, CCM wana mkakati wao na CHADEMA nao wana mkakati wao, CUF na NCCR wanapelekwa kama majuha. CHADEMA hawana wangekuwa na jipya kwenye mchakatohuu wangeanza kususia pale walipoitwa kwenda kunywa chai Ikulu. Tutambue kuwa siyo watakaloliomba kwa Rais kikwete ili lionekane jema sharti alikubali, la hasha, wao wana mkakati wao na CCM wana mkakati wao.

thatha

Tuwekee hiyo misimamo ilituijadili.......
 
Unakosea sana. Kumbuka hata wazo la katiba mpya CCM hawakuwa nalo lakini ni JK aliyewaburuza baada ya yeye naye kubanwa na shinikizo la umma. Hata hapo tulipofika bado JK ana uwezo wa kuwaburaza CCM wenzake akielewa hoja ni nini na kama kweli dhana ya katiba anaielewa na kuikubali. Ni muhimu sana JK aendelee kushinikizwa ili aendelee kujitoa mhanga kwa ajili ya nchi na kuachana na maslahi finyu ya chama chake. Katiba Mpya ni jambo pekee alilobaki nalo katika kuweka alama ya kudumu ya utawala wake. Likimponyoka hili basi tena atasaulika mapema sana baada ya utawala wake kwisha.​

Ni upunguani kwa Dr Kama wewe kudhani kuwa Rais anaweza kushinikizwa kwa kila jambo. vinginevyo hakuna umuhimu wa kuwa na Rais
 
ulitaka kikwete afanane na wabunge wa cuf au chadema fikiri kwanza kabula hujapost bavicha ni janga lataifa.

kati kati

Tunataka kikwete afanye swala la katiba kwa maslahi ya Taifa siyo vyama vya siasa hususani ccm

Katiba nizaidi ya cdm, cuf, nccr nk na ni zaidi ya ccm.

huo ndiyo mtazamo wetu.
 
Back
Top Bottom