Kumtukana Rais Samia hadharani ni uhaini

Aisee, wewe ni mnoma sana a.k.a mdedile. Yaani mpaka umewakopi vigogo hao watatu? Unataka hao vigogo wawashughulikie barabara

Nadhani kuna tofauti kati ya kumsema mtu vibaya na kumtukana. Mtu anaweza kusemwa vibaya labda kutokana na tabia au mwenendo wake usioridhisha. Hata katika hali ya kawaida kama umefanya jambo la ovyo lazima tu utasemwa vibaya. Hii ni familia yetu. Kama baba au mama amefanya jambo lisilo na afya kwa ustawi wa familia, wanafamilia wana haki ya kutoa yao ya moyoni.

Hao unaodhani wanasitahili kushughulikiwa na mamlaka tajwa ni wanafamilia. Wanayo haki ya kusema na pia kusikilizwa kwani naamini hata baba au mama hukosea. Wao pia ni binadamu. Cha msingi na cha sekondari viongozi wetu wasishupaze shingo pale wananchi wanapowakosoa kwenye raslimali za nchi kwani uongozi ni dhamana tu ya muda. Tanzania ni yetu sote. Hakuna Mwenye hatimiliki ya nchi. Kila mmoja wetu ana haki ya kulinda na kutetea raslimali za nchi pale anapogundua kuna hujuma zinaenda kufanywa.

"Nani aliyesema kwamba rais hawezi kusemwa vibaya?"
 
Kuuza bandari na loliondo ndio uhaini,tena nchi nyingine unanyongwa...hao uliowatag hawana lolote la kufanya mana nao ni mazuzu kama wewe
 
nani amemtukana asiye na adabu huyo? zaidi ya Mange aliyeleta allegations na matusi ya nguoni, hakuna mwingine. halafu, katafute mwanasheria akufafanulie kwenye Penal code nini maana ya treason.
 
Hebu tupe mfano wa matusi unayodai ya kumtukana Rais!! Mimi ninachojua ni kwamba tusi kubwa kwa Rais ni kumsifu wakati alichokifanya kinahitaji lawama wala si sifa!! Hilo mni tusi kubwa sana!! ni kumfanya yeye kuwa ni mjinga!! Mfano: Ukikutana na mtu amebeba makopo kisha unamsifu kuwa amependeza wakati siyo ni kwamba unamkebehi!! Wewe ndiwe tukutuhumu kwa kumkebehi rais!! mnampotosha badala ya kumwambia ukweli!! Mnamfanya rais awe kwenye mstari mmoja na sultan Mangungo aliyeuza nchi yake kwa bei ambayo wala haikutajwa!! Ndivyo mkataba wa bandari ulivyo!! Unachukuwa bandari zetu jumla bila kutaja sisi tutapata nini!! Wanaomlaumu rais katika hili ndio wanaompenda!!
 
Mbona wakati anatukanwa Magufuli hatukuona ukiandika hivyo,hivi unajaua maana ya uhaini au unasumbuliwa tu na uchawa., weka na namba yako ya simu basi huenda wakakukumbuka.
 

Sema kumtukana rais ni uhaini
 
Kwani Samia ni Mungu? Kama hataki kutukanwa aachie ngazi akalee wajukuu.
 
Hebu mkuu kuwa straight.
Tutajir wanaomtukana rais na aina ya matusi wanayomtukana ili nasi tuanze kuwazomea popote pale
 
China imetupa mbali sana.

Tukisema tuwe kama china wanasiasa wengi watafilisika na kunyongwa pia.
 
ameomba kazi yote akubali wenye mali wanataka kusikia maendeleo kama wanaibiwa lazima watoe hisia akiona kelele aondoke afike mtu anayekubali yote
 
Una maana ya mama wa kambo anayetaka kuuza nchi yetu kwa waarabu?
 

Maneno mangine si tusi bali ni jina la kitendo kilichotendeka /fanyika.
Kwa hiyo mjinga, mpumbavu na mengine yanayofanana na hayo ni majina anayostahili kuhitwa mtu aliyefanya vitu vya jinsi hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…