Kuna anayeijua kampuni ya Salvation farm?

Kuna anayeijua kampuni ya Salvation farm?

Ilivyokua mwaka wa mwisho chuo semister ya pili niliwekeza au niseme niliingia nao mkataba wa kulima nikatoa 2600000 kwa ajili ya kulima heka mbili za tikiti maji nikitegemea faida sasa mpaka saivi naona kimya nimejaribu kufatilia kwa wafanyakazi kwa kuwapigia simu wanasema walipata hasara na mkurugenzi hapo Tz ko wamekua wakinizungusha kipindi naingia mkataba niligongesha form zao kwa mwanasheria nmeenda kwake yeye anasema niende mahakamani hapa sielewi ndio nauliza Kuna mtu labda amewekeza ili tujue jinsi ya kudai

Hiyo kampuni walifilisika
So wakawa wanawazungusha wateja wake kwa kutumia pesa za wateja wapya kuwalipa wa zamani
But so far, imekufa na hawana hayo mashamba waliyosema wanayo.. mm nilikomaa nao nikasema tawapeleka takukuru
Ilikuwa December 2021 nilichukua kama wiki moja hivi kupewa mazao
Na ni baada ya kuwa naenda kushinda ofisini kwao kila siku
 
Ni kampuni inayojihusisha na kilimo makao makuu yapo mbinga Ruvuma unaweza ukaeapa pesa wakakulimia mnaingia mkataba sasa nilikua nauliza Kuna mtu anaijua au ameisha fanya hivyo mm Ni mmoja wapo ambae nmewekeza
Wewe ndugu usishiriki wizi..hawa Salvation wamepotea na mitaji ya watu..mimi ni mhanga 5M....wamekula...wamepotea...Walikua na ofisi yao pale mabibo...wanefunga...
Kuna kundi la watsap tumo wawekezaji wote....jamaa mara wanasema alikimbilia Mozambique...huyu anaitwa Dismas...

In short ni wizi tu...usishawishi watu wapoteze hela

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Salvation Farm walikuwa wanajitangaza kwenye redio Yao INAITWA Salvation Fm , hii redio Naamini Bado ipo pale Mbinga
 
Back
Top Bottom