Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 8,870
- 14,258
Kikosi kidogo cha askari wa Ukraine hivi karibuni kilifanikiwa kuvuka mto Dnipro oblast ya Kherson kutoka upande wa Magharibi na kuingia Mashariki ambako ndiko ziliko ngome za jeshi la Urusi tangu walipoamua kuachia eneo hilo la mashariki ambalo halina umuhimu kwao kiulinzi.
Kikosi hicho mwanzoni kilikuwa tukio kubwa kwa jeshi la Ukraine linalokaribia kushindwa vita na habari zake kutajwa sana na raisi Zelensky wa nchi hiyo.
Ili kuendelea kuwepo eneo hilo inabidi waendelee kupata nyongeza ya mahitaji yao kila mara kama vile chakula,maji na mafuta kwa ajili ya majenereta. Kila aina ya msaada wanaohitja kuwafikia huwa unapigwa na kuzamishwa na jeshi la Urusi.
Kama kwamba Urusi iliwaachia wafike eneo hilo kwa makusudi wamejikuta wamezingirwa kutokea pande zote na kuishiwa na mahitaji huku adui akipiga maeneo yote yanayowazunguka na kushindwa kusonga mbele huku wakiwa hawana namna yoyote ya kurudi walikotokea.
Imebidi wakati mwengine watoe gharama zao kwenda kusaka mahitaji kwa kificho kwenye vijiji vya jirani.
Katika malalamiko yao wanasema karibu wote waliofika eneo hilo ni askari walioingizwa jeshini siku za karibuni na wangependa wapate msaada kutoka askari wenye uzoefu zaidi wa vita kuliko wao na ambao hawawaoni.
Wanashangaa kuona viongozi wa juu wa Ukraine wakiendelea kutangaza habari zao kama ni ushujaa lakini makamanda wao wameshindwa kabisa kuwapa msaada wala kuwaokoa.
Kutokana na hali hiyo wamepata fikra kuwa katika hatua hii jiliyofikiwa ya vita hakuna mawasiliano tena baina ya makamanda wa ngazi za jini na majenerali wa kivita ili kumpa taarifa kamili raisi Zelensky juu ya hali waliyonayo.
Kikosi hicho mwanzoni kilikuwa tukio kubwa kwa jeshi la Ukraine linalokaribia kushindwa vita na habari zake kutajwa sana na raisi Zelensky wa nchi hiyo.
Ili kuendelea kuwepo eneo hilo inabidi waendelee kupata nyongeza ya mahitaji yao kila mara kama vile chakula,maji na mafuta kwa ajili ya majenereta. Kila aina ya msaada wanaohitja kuwafikia huwa unapigwa na kuzamishwa na jeshi la Urusi.
Kama kwamba Urusi iliwaachia wafike eneo hilo kwa makusudi wamejikuta wamezingirwa kutokea pande zote na kuishiwa na mahitaji huku adui akipiga maeneo yote yanayowazunguka na kushindwa kusonga mbele huku wakiwa hawana namna yoyote ya kurudi walikotokea.
Imebidi wakati mwengine watoe gharama zao kwenda kusaka mahitaji kwa kificho kwenye vijiji vya jirani.
Katika malalamiko yao wanasema karibu wote waliofika eneo hilo ni askari walioingizwa jeshini siku za karibuni na wangependa wapate msaada kutoka askari wenye uzoefu zaidi wa vita kuliko wao na ambao hawawaoni.
Wanashangaa kuona viongozi wa juu wa Ukraine wakiendelea kutangaza habari zao kama ni ushujaa lakini makamanda wao wameshindwa kabisa kuwapa msaada wala kuwaokoa.
Kutokana na hali hiyo wamepata fikra kuwa katika hatua hii jiliyofikiwa ya vita hakuna mawasiliano tena baina ya makamanda wa ngazi za jini na majenerali wa kivita ili kumpa taarifa kamili raisi Zelensky juu ya hali waliyonayo.