Uchaguzi 2020 Kuna dalili zote kuwa endapo kutakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi, umoja wa Upinzani unaweza kuchukua nchi Oktoba 2020

Uchaguzi 2020 Kuna dalili zote kuwa endapo kutakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi, umoja wa Upinzani unaweza kuchukua nchi Oktoba 2020

M-mbabe

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2009
Posts
13,203
Reaction score
23,027
Wote ambao mmekuwa mkifutilia rallies za vyama vya upinzani (hapa "upinzani" strictly ninamaanisha ACT & Chadema) hapana shaka mtaafikiana nami kuwa mwamko wa wananchi ku support kambi hii ni mkubwa sana pamoja na uwepo wa vitisho kutoka vyombo vya dola. Imagine kusingekuwa na ukandamizaji huo sijui ingekuwaje.

Ni bahati mbaya sana tena sana kambi hii imeamua kuingia uchaguzini mwaka huu kabla ya kwanza kupigania Tume Huru ya Uchaguzi. Ni bahati mbaya sana kwa sababu japo watashinda kwa sehemu kubwa (>55% kwenye urais na >60% ubunge & madiwani), hawatatangazwa.

Wasijidanganye kabisa na mkakati wa eti "kulinda kura" baada ya polling. Wakifanya hivyo tutakuwa tumeamua kumkabidhi ziraili roho za akina Aquiline nyingine nyingi tu. Endapo "kulinda kura" ndiyo utakuwa msimamo, basi viongozi wa upinzani lazima watambue kuwa there'll be a huge price to pay, and dearly. Suala ni je upinzani umejipangaje ku mitigate hili tishio?

Those are only my 2 cents. Food for thought.

Usisahau kupitia video clip hii hapa chini ili uelewe context ya uzi wangu.

 
Hivi ndio vitu vinavyowafanya wapinzani tuwaone hamna maana, mnapiga kura na kuhesabu kabla ya uchaguzi, mnajitangazia na Matokeo, mwisho wa siku mnatafuta kulalamika hata mahali ambapo sipo baadaye mtasema mmenyang'anywa ushindi.
 
Hivi ndio vitu vinavyowafanya wapinzani tuwaone hamna maana, mnapiga kura na kuhesabu kabla ya uchaguzi, mnajitangazia na Matokeo, mwisho wa siku mnatafuta kulalamika hata mahali ambapo sipo baadaye mtasema mmenyang'anywa ushindi.
Ona MATAGA mwenzio hapo juu kawapa CCM 98%
 
1593772332328.png
 
yes, kwa kutumia mapolisi sawa.

Nimetembea kama mikoa minne, Mwanza, Mara, Kigoma na Iringa. Huko kote nimeongea na wananchi mbalimbali, nilichogundua ni kuwa bado wananchi wanataka kuona mabadiliko ya chama kilichoko madarakani.

Ni kama kilichotokea uchaguzi uliopita hawajakubaliana na chama kilichopo. Suala la kwamba wananchi wameichoka ccm, hilo wala halina mjadala, ila wanakosa uwanja wa kuonyesha hisia zao. Nilichojifunza ni kuwa watu hawana imani tena na tume ya uchaguzi.
 
Nimetembea kama mikoa minne, Mwanza, Mara, Kigoma na Iringa. Huko kote nimeongea na wananchi mbalimbali, nilichogundua ni kuwa bado wananchi wanataka kuona mabadiliko ya chama kilichoko madarakani. Ni kama kilichotokea uchaguzi uliopita hawajakubaliana na chama kilichopo. Suala la kwamba wananchi wameichoka ccm, hilo wala halina mjadala, ila wanakosa uwanja wa kuonyesha hisia zao. Nilichojifunza ni kuwa watu hawana imani tena na tume ya uchaguzi.
Mwanza ya wapi mkuu!!
 
Upinzani ni kweli upo lakini mbele ya Magufuli, hakuna upinzani!! Zingine ni hasira tu za Kwa nini upinzani hauwezi kushinda tena safari hii
 
Upinzani ni kweli upo lakini mbele ya Magufuli, hakuna upinzani!! Zingine ni hasira tu za Kwa nini upinzani hauwezi kushinda tena safari hii

Magufuli hajawahi kushindana kisiasa, na ndio maana hataki kuruhusu siasa za ushindani. Kwakuwa hayuko tayari kuruhusu mazingira ya ushindani, ww ndio unajua watu wanamkubali sana.
 
Back
Top Bottom