Kuna faida gani kuwatengea wanawake "Viti maalum" 110 vya ubunge?

Kuna faida gani kuwatengea wanawake "Viti maalum" 110 vya ubunge?

Ukute wabunge wenyewe ni wakina Wema Sepetu.
 
Mutajijua, HAPA KAZI TU. Kwani mulipo tupigia kura maana yake si munazikubari SERA zetu????? ndio hizo sasa zinafanya kazi.
 
Hao wakina mama ,,hasa wa ccm hua hawana cha maana zaidi ya kuwakanyaga watz maskini kwa kupitisha hoja za kishenzi na miswada kwa ajili ya wakubwa wao waliowaweka
 
Ikimbukwe kuwa Kipindi wanatengeneza hiyo sheria pale Dodoma hapakua na vyuo vikuu.
Na wote mnapaelewa dodoma palivyo, sijui mnatarajia wahwshimiwa wangeishije pale!!
Pungyzeni kulalamika au kuuliza kila swali linalowajieni vichwani mwenu, mambo mengine muwe mnajiongeza tu.
 
Hamna faida yeyote,tena mm nilikuwa najua viti maalum havizidi 10 bunge zima
 
Rasimu ya katiba chini ya mwenyekiti Jaji Joseph Sinde Warioba, walipendekeza kusiwe na viti maalum, bali kila jimbo la uchaguzi kuwe na mgombe me na ke......CCM wakaiba mchakato ule na matokeo yake majimbo yameongezeka na viti maalum vimeongezeko hivyo kuiongezea serikali mzigo wa kuhudumia kundi hili.

Mbaya zaidi viti maalum imekuwa takrima au bakshishi kwa pande zote mbili upinzani na tawala.

Mpaka tutakapobadili katiba au sheria hii mbovu ndipo tutaona hatua chanya na stahiki za maendeleo nchi hii.

Msimamo Wangu

Viti maalum vifutwe
 

Attachments

  • 1446895152649.jpg
    1446895152649.jpg
    41.8 KB · Views: 78
  • 1446895169279.jpg
    1446895169279.jpg
    39.5 KB · Views: 81
Ndio sehemu moja wapo vyama huungana na kuwageuka wananchi katika kufuja pesa za walipa kodi. . . . !!!

Endeleeni kushabikia vyama

Yaani kwenye maswala ya posho na kula hutasikia ukawa wakilalamika.
Hata posho ya send off bunge kuvunjwa mabilioni yameteketea kina Msigwa...Tundu Lissu kimyaaaa...
Na wakataka watumishi wa serikali wafutie seating allowance ya vikao wakati wao 'sleeping allowance' ndani ya kikao cha bunge + 'ndiyo allowance waka double.

Wabunge maslahi tu.
Maslahi matumbo na siasa uchwara.
Ukiwasubiri wakukomboe katika unyonge wako utasubiri sana
 
Ikimbukwe kuwa Kipindi wanatengeneza hiyo sheria pale Dodoma hapakua na vyuo vikuu.
Na wote mnapaelewa dodoma palivyo, sijui mnatarajia wahwshimiwa wangeishije pale!!
Pungyzeni kulalamika au kuuliza kila swali linalowajieni vichwani mwenu, mambo mengine muwe mnajiongeza tu.

Kwa hiyo hawa wabunge wa viti maalum ilikuwa ni kwaajili ya kukaliwa na wabunge wenzao na sio maslahi ya kitaifa eeh?
 
Siku zote sikuwahi kujua wala kufikiri kwamba idadi ya viti maalum vya wanawake bungeni inaweza kufikia hii, yaani viti 110, kwa ujinga wangu nilidhani ni chini ya viti 50.Lakini viti maalum 110, yaani karibu nusu ya wabunge wa kuchaguliwa ambayo namo bado kuna wanawake, kuingia akina mama wengine 110 kinamna ktk chombo nyeti cha kutunga sheria kama bunge naona kuna mushkeli mkubwa tena sana.Kwa hatua tuliyofikia ya kutoa haki na vigezo vilivyo sawa kwa jinsia zote katika hatua zote za kugombania nafasi za udiwani, ubunge na urais, sioni kama tuna haja tena ya kuwa na viti vingi vya upendeleo kiasi hiki.Nimejaribu kupekua na kupitia katiba za nchi wenzetu walio katika jumuiya ya madola ambayo na sisi ni mjumbe wa mabunge yake nimegundua kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee yenye kuwa na idadi kubwa ya viti vya upendeleo kwa wanawake ndani ya bunge.Fikiria mlolongo wa shida, matatizo na mdororo wa kiuchumi walionao watanzania lakini bado kuna wabunge 110 wanawake wamewekwa bungeni, wengine wakiwa wameingia tu kishikaji au kimahusiano binafsi kwa malipo ya kodi ya watanzania.Fikiria pia madeni ya waalimu, ukosefu wa dawa hospitalini, madeni ya wakandarasi, ukosefu wa maji na mengine mengi lakini bado kuna wabunge wanalipwa bila ya kuwa na jimbo wanaloliwakilisha, wanabaki ni wa kudandia dandia tu hoja za wenzao bungeni na kutetea vyama vyao ndani ya bunge.Nadhani wakati umefika sasa wa kuvipruni viti hivi na kubakiza viti 40 tu au kuvifuta kabisa na wanawake wanaotaka ubunge warudi kugombea kwenye majimbo yao badala ya kuvizia kutafuna kodi yetu huko bungeni bila kazi maalum. Binafsi sioni kama umuhimu wa wabunge hawa unalingana na mabilioni ya kodi yetu wanayotafuna. Kama Tanzania tumefikia hatua ya mwanamke kugombea urais akashika nafasi ya tatu mbele ya wagombea wanaume watano, na hata kumpata makamo wa Rais mwana mama bado tunadhaniaje wanawake ni wa kupewa upendeleo?
Wengine waliingia huki wakafanya kwrli kutetea wananchi. Nchi kama Norway wanasema 60% ya bodi za mashirika serikali ni wanawake. Tuwashirikishe tu wanaweza na tunawaanda viongozi wa Kitaifa km Mh Suluhu. Ukiacha Prof Tiba ni wanawake sifuri wametajwa kwe rushwa. Wanamajukumu ya kifamilia yanayowatoa kampeni acha mitusi wanayomiminiwa. Ref kesi ya Arusha 2011.
 
Tabia mbaya sana kutumia fedha zetu kukodi hawa wamama wa kupigia makofi hoja mfu huku wakiunga mkono 100% jambo wanalolilalamikia awali. Hivi viti nuksi kweli kweli.

Waliopo huko hata hawawasaidii wenzao lolote, sana sana wa chama cha kupiga makofi
 
Yaani kwenye maswala ya posho na kula hutasikia ukawa wakilalamika.
Hata posho ya send off bunge kuvunjwa mabilioni yameteketea kina Msigwa...Tundu Lissu kimyaaaa...
Na wakataka watumishi wa serikali wafutie seating allowance ya vikao wakati wao 'sleeping allowance' ndani ya kikao cha bunge + 'ndiyo allowance waka double.

Wabunge maslahi tu.
Maslahi matumbo na siasa uchwara.
Ukiwasubiri wakukomboe katika unyonge wako utasubiri sana


Ulishawahi kumuona mbunge wa upinzani amesinzia au kulala bungeni?
 
Ni mikataba ya kimataifa inayotaka at least theluthi moja ya wabunge wote wawe wanawake
 
Najiuliza tu Hivi kweli hiyo katiba mpya ingekuwa haina sula la serikali tatu kweli upinzani wangekuwa wanaipigania???
 
Back
Top Bottom