Hawa wasanii Wa bongo wanashida gani? Je; Wanatanguliza maisha ya anasa au ni nini?
Umaarufu wao unafaida gani kama pesa ya kujitibia tu hawana?
Kuna watu wanaleta hoja dhaifu kwamba makampuni wanayo ya promote eti yawe yanawajibika kuwatibia;
Hivi Hamtambui kwamba kuna mikataba, tena baadhi ya wasanii hulipwa pesa zote, lakini huzitapanya kwa anasa?
Umaarufu wao unawasaidia nini kama hawawezi kujitibia?
kweli mkuuTatizo lao hela wanapata sema hawana utamaduni wa kutunza fedha....wao wakipata hela ni kuwafukunyua wadada tu hela yote wana invest chini huko!
Huku wakijua kesho watapata hela tena kwenye Dili lingine wakati hawajui kuwa maisha siyo Kila siku utaterezaaa tu lazima Ipo siku utapigika
Ova
Duuh hili nalo neno... Maana majuto ukisema kuhusu mikataba yake anapewa hela ndio lakini hawezi iweka eti akiba kesho anaweza patwa na matatzo.. Yeye anapiga anajua kesho dili nyingne yajaaa..!! So tusiwalaumu sana.. Pia gharama za nje ni kubwaa sana mfano gharama Mil 10 jumla kuipata majuto binafsi si mchezo.. Sanaa yetu INATENGENEZA MASKINI WENYE MAJINA MAKUBWAA...Kama Wanasiasa Na Wizi Na ma posho Yao yote wakiumwa hawawezi kujitibu ije kuwa wasanii?
Lissu hapa limetembezwa bakuli hatareee
Ndugai huko Kila kitu Serikal
Akina Sitta kule Germany Kila kitu ilikuwa Serikal
Sasa kati ya Wasanii Na Wanasiasa Nani alipaswa kuwa Na hela za kujitibia?
Hela wanapata sana tu sema matumizi YaoTatizo lao ndilo la wengi wetu, hatupendi kusoma, kuandika na kuwa imara na makini kwenye mikataba, iwe ya chumba, vyumba, nyumba, ardhi au rasilimali na maliasili ya nchi...
Sisi tunadharau sana mikataba, hata ile kusema basi nimlipe mwanasheria bobezi laki 2 kwenye huu mkataba wa milioni tunakuwa wabahili..
Wasanii karibu wote wameingizwa kingi kwenye mikataba tu, hawawatumii wanasheria husika wala ile kuhangaika ile mikataba iwe na "clauses" nyingi za kuwasaidia...Ujinga wao faida kwa matapeli..
kweli kabisa mkuuTatizo lao ndilo la wengi wetu, hatupendi kusoma, kuandika na kuwa imara na makini kwenye mikataba, iwe ya chumba, vyumba, nyumba, ardhi au rasilimali na maliasili ya nchi...
Sisi tunadharau sana mikataba, hata ile kusema basi nimlipe mwanasheria bobezi laki 2 kwenye huu mkataba wa milioni tunakuwa wabahili..
Wasanii karibu wote wameingizwa kingi kwenye mikataba tu, hawawatumii wanasheria husika wala ile kuhangaika ile mikataba iwe na "clauses" nyingi za kuwasaidia...Ujinga wao faida kwa matapeli..
Wachangiwe na ccm tuuNilifikiri kuchangia Matibabu ya mtu ni hiari sikujua kwamba unalazimishwa!