Kuna haja kubwa ya Watanzania kujifunza English,huyu dereva teksi ametuaibisha

Kuna haja kubwa ya Watanzania kujifunza English,huyu dereva teksi ametuaibisha

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304
Kuna rafik yangu hajui kiswahili ameingia Tanzania leo kuja kutalii, ametoka marekani akaenda kwanza Entebe Uganda, kisha Nairobi Kenya leo kafika Dar.

sasa kanipigia simu ananiuliza nimwambie maana ya ten book wameshindwa kuelewana na dereva teksi,amemuuliza dereva teksi kwenda katikati ya mji ni kiasi gani dereva teksi hakajibu teni buku yani anaamanishi buku teni ( 10,000)
na amejiona yuko sahihi.

kuna haja ya kujua vizuri kiswahili na kiingereza pia ni muhimu sana kwa dunia ya sasa hivi kama wewe ni mfanyabiashara.

Amesikitisha sana dereva teksi hatuna budi kujua ata vitu muhimu muhimu.
 
Khaa! Bath hii pothti ungetuekea kwa kidhungu eti!
Chezea kingreza weyeee!
 
Hahahahahaaa... Nimeipenda bure hii..
 
Si mnakazania kiswahili eti "ni uzalendo?" Vumilieni ila eleweni kuwa NJE YA TANZANIA, MTANZANIA NI BUBU! Not even in Kenya!
 
Swala si kujua kiingereza bali kukikazania kiswahili kitumike duniani kote.
 
Huyu dereva alimjibu mteja wake kama alivyoulizwa. "Nikupay book ngapi".

Utani kando, labda kuanzia milioni na kutaja directions, vinginevyo madereva wengi hawashindwi kutamka ten thousands na wanaweza kuandika ili mawasiliano yawepo.
 
hapo ndipo siku zote napingana na nyerere na mfumo wa kutumia kiswahili ambacho kimetufanya kuishi kwa kujidharau kama siyo kudharauliwa even na majirani zetu
 
Unamshangaa dereva wa taxi ambaye hajui kizungu, mbona huwashangai wabunge wako ambao nao pia hawajui kizungu?
 
Uongo huo maana bei haitoi picha halisi ya gharama ya taxi kutoka airport to city centre, kichekesho chako ungekifanya kiendane na hali halisi
 
Uongo huo maana bei haitoi picha halisi ya gharama ya taxi kutoka airport to city centre, kichekesho chako ungekifanya kiendane na hali halisi

Mzungu kaja na Dar Express toka Nairobi. hii buku ten ni kutoka Ubungo terminal mpaka Sinza kwa Remmy. Huyu kaka hana rafiki wa hadhi ya ndege
 
Mkuu, najaribu kufikiria uhalisia wa scenario nzima.

1. Yaani Dreva tax ALIMUELEWA rafiki yako kwa lugha ya kiingereza ila kujibu ndio ikashindikana?!!!!!!

2. Kwa gharama za hapa Dar nadhani, hii "ten book" wether kutoka Ubungo hadi City Centre au niKutoka Airport hadi City centre ni ndogo(haiendani) HASA kama abiria kweli alikuwa 'mzungu'.
 
Jamaa atakua alikua anajoke ila anavyopenda kujisifu duh
 
ushauri wa bure kwa madereva wa taxi/wabunge make google translate your homepage now! Hii kitu inasaidia sana mfano i google translated "kuna haja kubwa ya watanzania kujifunza english" jibu hili hapa
there is a great need for Tanzanians to learn
english
Translate
Swahili>English
 
narudia tena na nina sisitiza ya kwamba si kila mzungu ni muingereza.
 
kuna haja ya kujua vizuri kiswahili na kiingereza pia ni muhimu sana kwa dunia ya sasa hivi kama wewe ni mfanyabiashara.

Mkuu mimi nitakinzana na wewe, na nina sababu kadha wa kadha zenye kunifanya nikinzane nawe lakini kwa sasa nitadokeza hii moja tu.

Unapoamua kutembelea nchi maarufu mathalani hizi ambazo zina umaarufu wa utalii kuna misamiati inakupasa ujifunze ikiwemo hii ya kuulizia bei ya usafiri kama wa taxi.

Ukiwa kama mtalii ingawaje dhumuni kuu ni kutembelea vivutio vya utalii, lakini katika kuifikia nia hiyo kuna mambo ya kitamaduni yahusuyo nchi uiendeayo yakupasa ujifunze.

Nimepata kufika Ethiopia na wakati fulani China na Thailand, raia wa huko ni aghalabu kuwasikia wakiongea Umombo na hata wakiongea basi ni zile sentensi za kubabaisha sana.

Kuna sentensi fupi fupi ilinipasa kujifunza au kutembea na vipeperushi vilivyo na translations za lugha hizo kwa ajili ya kuniongoza.
 
Back
Top Bottom