Kuna hatari ya kuwa na anuani ya makazi hewa kutokana na zoezi la anuani linaloendelea

Kuna hatari ya kuwa na anuani ya makazi hewa kutokana na zoezi la anuani linaloendelea

THE BROKER

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2014
Posts
743
Reaction score
915
Nimepigiwa simu na Baba Mzazi kutoka huko Moshi Kilimanjaro na kunieleza ya kwamba kuna hatari kubwa ya kuwepo kwa anwani hewa zitakazotokana na zoezi hili la urasimishaji wa anwani za makazi kama ifuatavyo:-

Kwamba, wahusika wanasajili makazi kwa maana ya "nyumba" ambapo Msingi unatafsiriwa kama nyumba hata kama ulishatelekezwa kwa miaka mingi iliyopita, boma/nyumba ambayo haiishi mtu yeyote pia inatambuliwa kama makazi hata kama wakazi wake wote wamefariki dunia au wamehama. Hata maghofu wanatambua kama makazi rasmi na kusajili.

Kutokana na makosa hayo mwisho wa siku tutakuwa na idadi kubwa ya anwani hewa kwenye makazi hewa ambayo hayapo na hayatakuja kuwepo.

Hivyo, naishauri serikali na wanaohusika kupitia tena upya kwenye eneo la kubainisha sifa za makazi yanayopaswa kusajiliwa ili tuepukane na janga la kuwa na anwani hewa kwenye makazi hewa.
 
Nimepigiwa simu na Baba Mzazi kutoka huko Moshi Kilimanjaro na kunieleza ya kwamba kuna hatari kubwa ya kuwepo kwa anwani hewa zitakazotakana na zoezi hili la urasimishaji wa anwani za makazi kama ifuatavyo:-

Kwamba, wahusika wanasajili makazi kwa maana ya "nyumba". Msingi unatafsiriwa kama nyumba hata kama ulishatelekezwa kwa miaka mingi iliyopita, boma/nyumba ambayo haiishi mtu yeyote pia inatambuliwa kama makazi hata kama wakazi wake wote wamefariki dunia au wamehama.

Kutokana na makosa hayo mwisho wa siku tutakuwa na idadi kubwa ya anwani hewa kwenye makazi hewa ambayo hayapo na hayatakuja kuwepo.

Hivyo, naishauri serikali na wanaohusika kupitia tena upya kwenye eneo la kubainisha sifa za makazi yanayopaswa kusajiliwa ili tuepukane na janga la kuwa na anwani hewa kwenye makazi hewa.
Ngoja tusubiri waje tuone wanasemaje
 
Hata pasipokaliwa na watu umuhimu wa anwani upo, sehemu ambayo watu wanaishi details za wanaoishi zinaingizwa ila sehemu ambayo hapaishi mtu ila yupo mmiliki taarifa itajazwa na maelezo hakuna jengo yataingizwa hata kama mmiliki wa awali amefariki hapawezi kukosa mrithi
 
Nafikiri bado kuna haja ya kufanyika review ya hilo zoezi kuondoa hayo mapungufu
 
Wanachofanya wao wakikuta kuna kiwanja, gofu au pagale hata kama watu walihama but wanatumia details kutoka Ardhi ili kujua mmiliki ni nani na kisha wanaingiza hizo taarifa kuwa na makazi ya nani na kisha kutoa hizo anuani za makazi. Kwahiyo hakuna anuani feki ipo siku hiyo sehemu itaendeleza na ndugu au mtu atakae nunua kwahiyo ukiparuka leo baadae itakuja kuwa vigumu ku fix anuani kwasababu hizi anuani zinaenda kimitaa.

Sent from my TECNO KB8 using JamiiForums mobile app
 
Nafikiri bado kuna haja ya kufanyika review ya hilo zoezi kuondoa hayo mapungufu
Hakuna upungufu hapo.Kila jengo na kiwanja tupu lazima vipate namba ya utambulisho.Ukiparuka siku wakija kuishi watu utaandikaje namba?Utairudia namba ipi na ulishazigawa kwa mfuatano?
 
Wahusika hawana habari kwenye mambo ya msingi kazi kuimba tu "anaupiga mwingi"
 
Huku kwetu mitaa wameipa majina ya watu ,
wengine ni mateja.

Wametoa majina bila kushirikisha wanainchi..
Nyie watu vipi lakini?

Hivi kwann wasiweke majina ya mashujaa wetu au majina ya mikoa?
Mfano
Mtaa wa Arusha,
Mtaa wa Tanga.
Mtaa wa Mwanza nk.

Mfano,
Mtaa wa Mkwawa.
Mtaa wa Kinjekitile Ngwale.
Mtaa wa Mirambo.
Mtaa wa Mwinyigumba.
Mtaa wa Kimweri.
Nk?

Mitaa mnaipa majina ya wajumbe wa nyumba kumi na majina ya mateja.

Nyie watu hovyo kabisa.
 
Huku kwetu mitaa wameipa majina ya watu ,
wengine ni mateja.

Wametoa majina bila kushirikisha wanainchi..
Nyie watu vipi lakini?

Hivi kwann wasiweke majina ya mashujaa wetu au majina ya mikoa?
Mfano
Mtaa wa Arusha,
Mtaa wa Tanga.
Mtaa wa Mwanza nk.

Mfano,
Mtaa wa Mkwawa.
Mtaa wa Kinjekitile Ngwale.
Mtaa wa Mirambo.
Mtaa wa Mwinyigumba.
Mtaa wa Kimweri.
Nk?

Mitaa mnaipa majina ya wajumbe wa nyumba kumi na majina ya mateja.

Nyie watu hovyo kabisa.
Zoezi la urasimishaji wa CCM hili.. Majina ya mitaa inatakiwa wapendekeze wananchi. Kwa sababbu hayo majina tayari yapo ila yalikuwa hayajaandikwa tu kwenye makaratasi
 
Zoezi la urasimishaji wa CCM hili.. Majina ya mitaa inatakiwa wapendekeze wananchi. Kwa sababbu hayo majina tayari yapo ila yalikuwa hayajaandikwa tu kwenye makaratasi

Alafu juzi kati kuna jambo limenichanganya kidogo.Mimi nimepanga sehemu frem ya biashara lkn cha kushangaza wamechukua information zangu kama mpangaji na kujaza kwenye system, But nkawauliza endapo nikahama au nikaacha kabisa biashara inakuwaje mwenyewe hakua na majibu ya kueleweka alikua anajiuma uma hii imekaaje wadau?
 
Alafu juzi kati kuna jambo limenichanganya kidogo.Mimi nimepanga sehemu frem ya biashara lkn cha kushangaza wamechukua information zangu kama mpangaji na kujaza kwenye system, But nkawauliza endapo nikahama au nikaacha kabisa biashara inakuwaje mwenyewe hakua na majibu ya kueleweka alikua anajiuma uma hii imekaaje wadau?
Hayo ni makosa ya wazi kabisa, coz hapo wewe ni mpitaji kwa nini wasichukue za mwenye nyumba? Ndio makosa kama haya tunataka yarekebishweee
 
Hawa wanaoandikisha makazi Tunawatambuaje jamani? Wengine huku majumbani wanakuja bila vitambulisho wala mjumbe halafu wanahitaji Data zetu..
 
Mleta màda ndio akili mdogo. Kila kitu kinaandikishwa ndio maana ya anuani za makazi kila kitu kinakuwa na anauani hadi open space. Mtu akifia kwenye pagare hapo polis watakuwa directed sawasawa na eneo hilo, maana hata lisipokuwa na watu haliwezi kuwa hivyo milele na hata likikaa hivyo milele address lazima liwe nayo. Haya tu assume wameruka mapagare kesho likinunuliwa atakaejenga hapo atapewa namba ipi?

Zoezi hili lime clone kutoka nchi zilizoishafanya haya mambo, hakuna jipya, jipya ni wewe unaeshangaa mambo yakiokuwepo tangu Yesu hajazaliwa.
 
Back
Top Bottom