Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2012
Posts
15,892
Reaction score
16,476
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu JamiiForums.

Ndugu zangu Watanzania;

Kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa. Familia masikini/fukara kuuza nyumba yao ya pekee ni pigo kubwa sana kwa watoto wadogo.

Ninaandika haya nikijua fika ya kwamba hakuna idadi ya mali au pesa kinachoweza kulingana na uhai wa mwanadamu. Unakumbuka ajali ya MV Bukoba? Unakumbuka ajali ya MV Spice kule Zanzibar?

Ni Watanzania wangapi walikufa katika ajali zile? Hivi wakati wa majanga yale uliwahi kusikia hata siku moja Watanzania wanalalamika kuhusiana na thamani ya zile meli?

Unajua gharama ya vyombo vile ni mamilioni ya pesa ngapi za Kitanzania? Licha ya kuwa ni pesa nyingi sana zilitumika katika kununua/kuunda vyombo vile Watanzania bado wakawa wanalilia roho za binadamu wenzao kwa maana kwamba hakuna cha kufananisha na uhai wa mwanadamu.

Hiyo ndio asili ya huruma ambayo Mungu ametupa sisi wanandamu. Familia zetu hizi masikini, mali tunazipata kwa tabu sana, ujenzi wa kuungaunga nyumba moja unajenga kwa kudunduliza miaka zaidi ya 9.

Baada ya ujenzi kukamilika, mnaishi miaka yenu 3, alafu ghafla mnasikia baba yenu mzazi anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya ini au figo zote zimefeli anapaswa kupelekwa India kwa matibabu zaidi.

Ndugu wanajitahidi kuchangisha kwa jamaa na rafiki zao hapa na pale kiasi hakifikii pesa sahihi inajohitajika kuweza kukidhi gharama za matibabu hivyo wanaamua kuuza mali zao za thamani walizonazo kumpeleka baba yao nje ya nchi (India) kwa matibabu zaidi.

Matokeo yake baba anakufa, mzee wa miaka 69, na mali zote mmeuza. Unaikuta familia iliyotoka kupanga chumba na sembule kisha wakajikwamua kujenga wanarudi tena katika nyumba za kupanga na maisha ya kuomba omba.

Nimemua kuleta mada hii hapa baada ya kukutana na kijana mmoja jina lake ni ****** ambaye nilikuwa ninakaa nao Keko Juu mwaka 2011 ambaye baba yao alifariki mwaka 2014 kwa ugonjwa wa saratani ya kibofu cha mkojo.

Inasemekana kwamba mzee yule wa miaka 66 hakuwa na matumaini ya kupona, kulingana na taarifa ambazo mmoja wa ndugu yao wa karibu (baba mdogo) alipewa na daktari katika hospitali moja maarufu tu hapa Dar.

Kwa kuwa familia bado ilikuwa inampenda na kumthamini mzee wao wakaona ni bora wauze hata nyumba waliokuwa wanajenga huko Toa Ngoma njia ya Kongowe ili wampeleke baba yao huko India. Matokeo yake ndio kama haya. Wamepoteza vyote, baba pamoja na nyumba.

Mama ndio hivyo tena biashara za kuungaunga za akina mama lishe, dada zake wawili walizaa tu hapo nyumbani yaaani nilipoonana na huyu kijana (ni agemate na mimi) machozi yalitaka kunitoka.

Basi tu kwa kuwa na mimi mwenyewe ni Taxi Driver mlala hoi sina cha kumpa zaidi ya kusimuliana story za zamani tulipokuwa tunacheza mpira (cha ndimu) wote na kwenda kuogelea baharini kule Kurasini tulikuwa tunapaita ZAMCARGO au SAVA.

Ndugu zangu, kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike tusizidishe umasikini katika familia.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
Kuna magonjwa sawa unaweza kutumia busara Kama cancer

Ila ushawahi kujiuliza why wanapambana hvyo kumuweka hai mpendwa wao!!!

Kumpoteza mtu kusikie kwa wenzako tu

Pesa sio kila kitu

Kipimo kizuri cha uzi huu ni kusubiria mtu wako wa karibu sana yamfike.

Katika kitu ambacho binadamu au pengine wanyama wote tumejaliwa na kinatutenganisha na mimea ni kitu kinaitwa HOPE/MATUMAINI

Tumaini ulilonalo wewe unapambana mpk mwisho hata mambo yakiwa magumu kiasi gani ndo matumaini hayo hayo yanafanya hio unayoita "busara" isitumike

Kuwa na kitu "to hold on to". Wewe sio unayeamua kuwa atakufa au hafi lakini at least uweze kusema nilifanya kila lililo ndani ya uwezo wangu kuokoa maisha ya babaangu ila Mungu alimpenda zaidi.

Tatizo ni kama utaanza kujuta baadae(hujasema kama jamaa yako anajutia hatua hiyo) kama unajuta basi hukutumia " busara"

Anaweza kuwa karudi nyuma sana kimaisha lakini akawa na amani mno moyoni kwa jinsi alivyompambania mzazi wake. Na unaweza ukatumia "busara" kwamba huyu anakufa tu yanini tuhangaike halafu ukabaki na machungu na majuto makubwa sana rohoni hata hiyo nyumba haiwezi kutafuta machungu hayo. Ukabaki na maswali tu kwamba "what if" ninge ninge kibao

Kifo kisikieni tu kwa wengine. Ungekua ni uwezo wetu kila mtu angezuia ndugu/mpendwa asife kwa gharama yoyote ile

RIP to the fallen
 
Dah! Ila bwana mjeshi nawe huwa unatuchosha na salamu zako kama umefika mjini leo asee, na hiyo hitimisho pia.
Siwezi kuacha kusalimia watu kwa maana ndio desturi njema kwetu sisi watanzania/waafrika.

Kuhusiana na uzalendo ndio usinipime kabisa mkuu. Tunaweza tukagombana tena nikakuweka kabisa katika IGNORE LIST yangu. Ninakukumbusha tena;

ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE.
 
Yah lazima busara itumike. Kuna magonjwa mengine kwa kweli hayatibiki mf mtu ana kansa au hivi hata ufanyaje hawezi pona Ila pia. Mzazi akiwa critical lazima mtu ufanye lolote si kumwacha tu coz atakufa. Mf unaweza ukauza nyumba ukanunua Figo mtu akaendelea kusivive na kujijenga upya.
 
Ni kweli yanatokea miongoni mwetu kwa makubwa mno. Ila kama ulivyotangulia kusema ni lazima busara itumike. Na Busara yenye tija ndio kumrudia Mwenyezi Mungu pekee.

Katika vitabu na mafundisho ya Dini zetu pameelekezwa namna bora ya kumsahili Mwenyezimguu ili awalinde na awafungulie wale yote wanaoguza mgonjwa waweze kupata tiba sahihi bila kupoteza muda na rasilimali pesa.
 
Katika kitu ambacho binadamu au pengine wanyama wote tumejaliwa na kinatutenganisha na mimea ni kitu kinaitwa HOPE/MATUMAINI

Tumaini ulilonalo wewe unapambana mpk mwisho hata mambo yakiwa magumu kiasi gani ndo matumaini hayo hayo yanafanya hio unayoita "busara" isitumike

Kuwa na kitu "to hold on to". Wewe sio unayeamua kuwa atakufa au hafi lakini at least uweze kusema nilifanya kila lililo ndani ya uwezo wangu kuokoa maisha ya babaangu ila Mungu alimpenda zaidi.

Tatizo ni kama utaanza kujuta baadae(hujasema kama jamaa yako anajutia hatua hiyo) kama unajuta basi hukutumia " busara"

Anaweza kuwa karudi nyuma sana kimaisha lakini akawa na amani mno moyoni kwa jinsi alivyompambania mzazi wake. Na unaweza ukatumia "busara" kwamba huyu anakufa tu yanini tuhangaike halafu ukabaki na machungu na majuto makubwa sana rohoni hata hiyo nyumba haiwezi kutafuta machungu hayo. Ukabaki na maswali tu kwamba "what if" ninge ninge kibao

Kifo kisikieni tu kwa wengine. Ungekua ni uwezo wetu kila mtu angezuia ndugu/mpendwa asife kwa gharama yoyote ile

RIP to the fallen

Kwenye kuuguza msikilize Daktari kwa makini hapo utafanya maamuzi sahihi. Hakuna Daktari mwenye hekima na busara atakuambia huyu mgonjwa wako hatibiki tena Bali atakupa ishara utumie akili zako.

Kwa mfano unaambiwa hii cancer ni stage four tumaini la kupona dogo sana lakini mnaweza kwenda kujaribu India, kama pesa ipo ya kutosha beba mgonjwa nenda India lakini kama ni kuuza nyumba ambayo ni hifadhi ya familia achana na hiyo safari.

Rafiki yangu mmoja alikuwa diagnosed obstructive azoospermia(at the of 32years) ili apate mtoto anatakiwa afanye IVF,at that time jamaa alikuwa ana fight kuanzisha company ili awe na economic freedom. Mkewe akawa ana force watumie pesa ya mtaji kufanya IVF,for three wanashindana mwisho ndoa ikavunjika jamaa akatafuta single mother mwenye mtoto wa 1year akamuoa na kumu adopt mtoto. Daima hisia zisiongeze uhalisia.
 
Back
Top Bottom